Thursday, April 5, 2018

Waziri Mahiga akutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Shelisheli na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ugiriki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Shelisheli Mhe. Balozi Barry J. J. Faure (kushoto), mazungumzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Mkutano wa Wizara tarehe 05 Aprili,2018, Dar es Salaam. Mhe. Faure yuko hapa nchi kwa ziara ya siku mbili (2) ambapo aliwasili tarehe 03 Machi,2018 na anatarajiwa kuondoka tarehe 05 Aprili,2018 

Pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kukuza zaidi mahusiano kati ya Tanzania na Shelisheli hasa katika maeneo ya vita dhidi ya madawa ya kulevya, usafirishaji haramu wa binadamu na katika sekta ya nishati.
Aidha, katika ziara hiyo Mhe. Faure aliambatana Mwanasheria Mkuu Bw. Frank Ally, na Kamishina Mkuu wa Polisi Bw. Krishnan Labonte wa nchi hiyo.
Ujumbe ulioambatana na Balozi Faure kutoka kulia ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali wa nchi hiyo Bw. Frank Ally, Kamishina Mkuu wa Polisi wa nchi hiyo Bw. Krishnan Labonte wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Mhe. Balozi Grace Mujuma (wa kwanza kushoto), Katibu wa Waziri Bw. Murobi Magabilo (wa kwanza kulia), pamoja na Afisa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Isack Isanzu nao wakifuatilia mazungumzo hayo
Dkt. Mahiga akiagana na Balozi Faure mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
Mhe. Mahiga na mgeni wake Balozi Faure, wakiwa katika picha ya pamoja




 Waziri Mahiga akutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ugiriki



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.) akutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Ugiriki Mhe. Terens Quicq (kushoto), mazungumzo hayo yalifanyika katika ukumbi wa Mkutano wa Wizara tarehe 05 Aprili,2018, Dar es Salaam. Mhe. Quicq aliwasili hapa nchini tarehe 04 Aprili,2018 

Pamoja na mambo mengine mazungumzo yalijikita katika kukuza zaidi mahusiano kati ya Tanzania na Ugiriki hasa katika biashara na Uwekezaji katika maeneo ya viwanda vya kuzalisha madawa ya binadamu na wanyama,nishati na utalii.
Ujumbe uliongozana na Mhe. Quicq, kutoka kulia ni Balozi wa Ugiriki nchini Tanzania mwenye makazi yake nchini Kenya, Mhe. Balozi Konstantinos Moatsos(Kulia), Balozi wa Heshima Bw.William K. Ferentinos(katikati) na Bi. Maya Solomou kutoka Ubalozi wakifuatilia mazungumzo hayo.

Mazungumzo yakiendelea
Dkt. Mahiga akiagana na Mhe. Quicq mara baada ya kumaliza mazungumzo yao.
 Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo .

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.