Wednesday, November 10, 2021

BALOZI SOKOINE AKUTANA NA KATIBU MKUU WIZARA YA MAMBO YA NJE WA SLOVENIA

 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akizungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Slovenia Balozi Jozef  Drofenik walipokutana katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Slovenia Balozi Jozef Drofenik akizungumza alipokutana na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Mazungumzo kati ya Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Slovenia Balozi  Jozef Drofenik yakiendelea .



Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Slovenia Balozi Jozef Drofenik (kushoto) na  Mkurugenzi wa Huduma za Kisheria na Manunuzi ya Umma Wizara ya Mambo ya Nje ya Slovenia Bw. Gregor Pelicon walipokutana katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine akiwa na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Slovenia Balozi Jozef Drofenik walipokutana katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.  

   


 

 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine amekutana kwa mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Slovenia Balozi  JOZEF DROFENIK katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamekubaliana kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania na Slovenia ambao umekuwepo kwa miaka mingi kwa maslahi ya nchi zote mbili.

Akizungumza katika kikao hicho Balozi Sokoine ameihakikishia Slovenia kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kufanya kazi kwa karibu na Serikali ya nchi hiyo na kuahidi kuongeza ushirikiano kwa ajili ya kukuza na kuimarisha uhusiano wa kirafiki uliopo baina ya nchi hizo. Balozi Sokoine ametumia nafasi hiyo kuwaita na kuwaalika wawekezaji, wafanya biashara na watalii kutoka nchini humo kuja Tanzania ili kutumia fursa mbalimbali za uwekezaji na utalii zinazopatikana nchini.

Naye Balozi  Jozef Drofenik kutoka Jamhuri ya Slovenia ameihakikishia Serikali ya Tanzania utayari wa nchi yake kuendelea kushirikiana na Tanzania na kufanya kazi kwa pamoja na kuialika kushiriki katika Jukwaa la Slovenia na nchi za Afrika litakalofanyika mwakani  ambalo amesema ni nchi chache za Afrika hualikwa kushiriki . Balozi Jozef Drofenik  amewakaribisha Watanzania kwenda Slovenia na maandiko ya miradi mbalimbali ili kuwekeza nchini humo na kuongeza kuwa watakuwa tayari kuwapokea na kufanya nao kazi kwa pamoja. 

Viongozi hao wamekubaliana kuangalia namna ya kuendelea kuimarisha  ushirikiano wa nchi zao na kuona kama Slovenia itakuwa tayari kushirikiana na Tanzania katika maeneo ya biashara, uwekezaji na uchumi, utalii, utengenezaji dawa, elimu, kilimo, uhandisii wa misitu ili kuhifadhi misitu , sayansi na teknolojia , uchumi wa buluu ili kuwa na uvuvi endelevu na matumizi bora ya rasilimali za majini na eneo la mafuta na gesi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.