Friday, October 11, 2024

BALOZI SHELUKINDO AFUNGA MAFUNZO


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akifunga mafunzo ya siku nne (4) ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara hiyo yaliyofanyika jijini Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba 2024

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo leo tarehe 11 Oktoba 2024 amefunga rasmi mafunzo ya siku nne (4) ya mawasiliano ya kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara hiyo yaliyofanyika jijini Dodoma.

Mafunzo hayo yaliyotolewa na timu ya Mabalozi Wastaafu sita (6) akiwemo Balozi Bertha Semu-Somi, Balozi Mohammed Maundi, Balozi Begum Taji, Balozi Peter Kalaghe, Balozi Tuvako Manongi na Balozi Mohamed Hamza yalijikita katika kujenga ubunifu na uelewa katika mawasiliano ya kidiplomasia na mafunzo ya nadharia na vitendo ya uandishi wa taarifa za kidiplomasia.
Katibu wa Mabalozi Wastaafu, Balozi Bertha Semu Somi akifafanua jambo kwenye hafla ya kufunga mafunzo ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yaliyofanyika jijini Dodoma.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bi. Chiku Kiguhe katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, akimkaribisha Katibu Mkuu Balozi Dkt. Samwel Shelukindo kwenye hafla ya kufunga mafunzo ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara hiyo yaliyofanyika jijini Dodoma.
Afisa Mambo ya Nje Bi. Symphrosa Chacha akitoa neno la shukrani kwa waandaaji na wawezeshaji wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kidiplomasia
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo na Katibu wa Mabalozi Wastaafu, Balozi Bertha Semu Somi wakijadili jambo
Mafunzo ya kiendelea

PRELIMINARY STATEMENT BY HIS EXCELLENCY DR. AMANI ABEID KARUME, FORMER PRESIDENT OF ZANZIBAR AND HEAD OF THE SADC ELECTORAL OBSERVATION MISSION (SEOM) TO THE PRESIDENTIAL, LEGISLATIVE AND PROVINCIAL ELECTIONS IN THE REPUBLIC OF MOZAMBIQUE












 

MISHENI YA SADC YATOA TAARIFA YA AWALI KUHUSU UCHAGUZI MKUU NCHINI MSUMBIJI


Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya SADC ya Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume, leo tarehe 11 Oktoba 2024 ametangaza Taarifa ya Awali kuhusu Uchaguzi wa Rais na Wabunge kufuatia uchaguzi uliofanyika nchini humo tarehe 9 Oktoba 2024.

 

Katika hotuba yake, Mhe. Dkt. Karume amesema kuwa uchaguzi nchini Msumbiji kwa kiasi kikubwa umezingatia kanuni na miongozo ya uchaguzi wa kidemokrasia ya SADC, inayosisitiza katika haki, uhuru, usawa, na uwazi.

 

Amesema katika kutekeleza jukumu lake, misheni hiyo iliangalia masuala mbalimbali muhimu kabla na wakati wa uchaguzi, ikiwemo hali ya siasa na usalama nchini humo, usimamizi wa uchaguzi, ripoti za vyombo vya habari kuhusu uchaguzi, na uwakilishi wa jinsia, ambayo yote yametekelezwa kwa kiasi kikubwa.

 

Aidha, Misheni hiyo imeshuhudia nchi hiyo ikiwa katika hali ya amani na utulivu katika kipindi chote cha kabla na wakati wa uchaguzi, ambapo kampeni, mikutano ya hadhara  na mchakato wa upigaji kura vilifanyika kwa amani, licha ya changamoto za kiusalama katika baadhi ya maeneo, hususan katika jimbo la Cabo Delgado.

 

Pia Mhe. Dkt. Karume ametumia nafasi hiyo kuwashukuru wananchi wa Msumbiji kwa kuonyesha ukomavu wa kisiasa na uvumilivu katika kipindi chote cha uchaguzi, akiwataka washindani wa kisiasa kufuata taratibu za kisheria endapo kutatokea migogoro yoyote kuhusu uchaguzi.

 

Pia ametoa wito kwa wadau mbalimbali kuendelea kuwa watulivu na wavumilivu wakati mamlaka za usimamizi wa uchaguzi zikikamilisha matokeo ya uchaguzi kabla ya kutangazwa rasmi, akiwaomba kuendelea kuhamasisha amani, uvumilivu, na utulivu kupitia majukwaa mbalimbali katika kipindi cha baada ya uchaguzi.

 

Kulingana na Misingi na Miongozo ya SADC inayosimamia uchaguzi wa kidemokrasia iliyorekebishwa mwaka 2021, misheni hiyo itatoa taarifa ya mwisho kuhusu uchaguzi siku 30 baada ya kutolewa kwa taarifa ya awali.

 

Misheni ya SADC, iliyozinduliwa rasmi tarehe 3 Oktoba 2024, ilipeleka waangalizi 52 katika majimbo yote 11 ya Msumbiji ili kuangalia uchaguzi.

 

Mhe. Dkt. Karume aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi, na Usalama, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuongoza misheni hiyo.


Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya SADC ya Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume, akitangaza Taarifa ya Awali ya Misheni hiyo kuhusu Uchaguzi wa Rais na Wabunge kufuatia uchaguzi uliofanyika nchini Msumbiji tarehe 9 Oktoba 2024
Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Elias Magosi akishiriki Mkutano wakati Mkuu wa Misheni na Rais Mstaafu wa Zanzibar, Mhe. Dkt. Karume akitangaza kwa waandishi wa habari Taarifa ya Awali ya Uangalizi kuhusu uchaguzi Mkuu wa Msumbiji uliofanyika tarehe 09 Oktoba 2024
Wajumbe wa Troika kutoka Tanzania ambao ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu Mussa (kulia) na Mshauri wa Rais masuala ya Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Sofia Mjema (kushoto) wakifuatilia taarifa ya awali ya SADC kuhusu uangalizi wa uchaguzi nchini Msumbiji
Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji, Mhe. Phaustine Kasike akishiriki mkutano wa uwasilishwaji wa Taarifa ya Awali ya SADC ya Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu nchini Msumbiji
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Talha Waziri akishiriki mkutano wa uwasilishwaji wa Taarifa ya Awali ya Misheni ya Uangalizi ya SADC kuhusu uchaguzi mkuu nchini Msumbiji
Sehemu ya wadau mbalimbali walioshiriki mkutano
Sehemu nyingine ya wadau
Mkutano ukiendelea
Mkutano ukiendelea
Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya SADC ya  Uangalizi wa Uchaguzi Mkuu nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mtendaji wa SADC na Wakuu wa Misheni za Kimataifa za Uangalizi wa Uchaguzi nchini Msumbiji mara baada ya kukamilisha mkutano wa pamoja wa kutoa taarifa zao za awali za uangalizi wa uchaguzi nchini humo. Kutoka kulia ni Mhe. Elias Magosi, Katibu Mtendaji wa SADC, Mkuu wa Misheni ya Uangalizi kutoka Umoja wa Afrika (AU-EOM) na Makamu wa Rais Mstaafu wa  Angola, Mhe. Bornito de Sousa Baltazar Diogo, ,  Mkuu wa Misheni ya Uangaliz ya Jumuiya ya Madola na Waziri Mkuu Mstaafu wa Saint Lucia, Mhe. Kenny Anthony, Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Jumuiya ya Nchi zinazozungumza Kireno na Waziri wa Mambo ya Nje mstaafu wa Ureno, Mhe. João Gomes Cravinho na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi ya Jukwaa la Uchaguzi la SADC, Jaji Dkt. Manuel Pereira da Silva 











































 

Thursday, October 10, 2024

MKUU WA MISHENI YA UANGALIZI WA UCHAGUZI YA SADC NCHINI MSUMBIJI ASHUHUDIA ZOEZI LA UPIGAJI KURA NCHINI MSUMBIJI

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume alitembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.

 

Mhe. Dkt. Karume ambaye aliambatana na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, Mhe. Elias Magosi  na Mjumbe wa Troika kutoka Tanzania na Mshauri wa Rais masuala ya Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Sofia Mjema, alianza kwa kutembelea kituo cha kupigia kura katika Shule ya Sekondari ya Josima Machel ambapo pia ni kituo alichopigia kura Rais wa Msumbiji, Mhe. Filipe Nyusi.

 

Vituo vingine alivyotembelea ni katika Shule za Msingi za Fevereiro, Maxaquene, Maxaquene Khovo na Kitivo cha Elimu ya Michezo na Mazoezi.  

 

Mhe. Dkt. Karume pia alishuhudia ufungwaji wa vituo vya kupigia kura na zoezi la kuhesabu kura baadaye jioni.

 

Misheni ya Uangalizi ya SADC nchini Msumbiji imepeleka Waangalizi 52 katika majimbo yote 11 nchini humo ambayo ni Cabo Delgado, Gaza, Inhambane, Manica, Maputo City, Maputo, Niassa, Nampula Tete na Zambezia.

 

Mhe. Dkt. Karume aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuongoza Misheni hiyo.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akizungumza na mmoja mawakala wa vyama wanaosimamia zoezi la upigaji alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.


Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akizungumza na mmoja wa mawakala wa vyama wanaosimamia zoezi la upigaji alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo. Mhe. Dkt. Karume aliambatana na ujumbe wake akiwemo Katibu Mtendaji wa SADC, Mhe. Eliasi Magosi (mwenye kofia) na Mjumbe wa Troika kutoka Tanzania na Mshauri wa Rais masuala ya Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Sofia Mjema (mwenye kilemba)

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akizungumza na maafisa wanaosimamia zoezi la upigaji alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akizungumza na mmoja wa mawakala wa vyama wanaosimamia zoezi la upigaji alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akizungumza na maafisa wanaosimamia zoezi la upigaji alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akiangalia moja ya sanduku la kupigia kura alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akizungumza na mawakala wanaosimamia zoezi la upigaji kura alipotembelea vituo kadhaa vya kupigia kura katika jiji la Maputo kwa ajili ya kuangalia ufunguzi wa vituo hivyo, zoezi la upigaji kura na zoezi la kuhesabu kura kufuatia uchaguzi uliofanmyika tarehe 09 Oktoba, 2024 nchini humo.
Wananchi wakiwa wamejipanga mstari katika vituo vya kupigia kura jijini Maputo tayari kwa kupiga kura

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akishuhudia Afisa anayesimamia zoezi la upigaji akitoa maelezo kwa mpiga kura kabla ya kupiga kura
Mwananchi akipiga kura
Mwananchi akiwa katika chumba cha kupigia kura
Mwananchi akiwekwa alama ya wino mara baada ya kupiga kura
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Talha Waziri akimwonesha Mhe. Dkt. Karume taarifa  iliyotumwa kwa njia ya video  kutoka kwa waangalizi wa uchaguzi wa SADC waliopelekwa kwenye majimbo mbalimbali kuhusu namna uchaguzi unavyoendelea kwenye maeneo hayo

Rais Mstaafu wa Zanzibar na Mkuu wa Misheni ya Uangalizi wa Uchaguzi ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC –SEOM) nchini Msumbiji, Mhe. Dkt. Amani Abeid Karume akishuhudia zoezi la kuhesabu kura
Zoezi la kuhesabu kura likiendelea





















































 

Wednesday, October 9, 2024

NAIBU WAZIRI CHUMI ASISITIZA WELEDI NA UWAJIBIKAJI

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi (Mb.) amewasisitiza Maafisa Mambo ya Nje Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuongeza uchapakazi na weledi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Hayo yamejili wakati wa hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya siku nne (4) ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara hiyo yanayoendelea katika Hotel ya St. Gaspar jijini Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba, 2024.

Akiongea katika ufunguzi huo Mhe. Chumi ameeleza furaha yake kuwaona Mabalozi Wastaafu wakiendelea kushirikiana na Wizara na kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo watumishi wa Wizara kila wanapohitajika au kuombwa kufanya hivyo.

Mafunzo hayo yanalenga pamoja na masuala mengine kuwajengea uwezo watumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa ufasaha kwa kuwa wao ni kiungo muhimu katika kutekeleza jukumu la msingi la Wizara la kuratibu masuala ya kikanda na kimataifa kwa niaba ya Serikali.

"Katika mafunzo haya ya mawasiliano ya kidiplomasia mtajifunza kukusanya taarifa, kuchambua taarifa na kutunza siri za serikali kwa maslahi ya taifa, hivyo natarajia yatakuwa chachu katika kuongeza ufanisi na uwajibikaji’’, alisema Mhe. Chumi.

Mabalozi hawa ni watumishi waliomaliza muda wa utumishi wa umma lakini wameiishi na kuitekeleza diplomasia kwa vitendo, hivyo ni vema mkawa makini kufuatilia na kuyapokea mafunzo mnayopewa kwa umakini. Pia akaongeza kuwa naye ni zao lililotengenezwa na Mabalozi wanaotoa mafunzo hayo na akawashukuru kwa malezi yao na kwa kuendelea kuisaidia wizara na Serikali kwa ujumla.

Ameeleza pia mafunzo hayo yatainua utendaji wa Wizara kwa kuwa idadi kubwa ya watumishi wapya watapata fursa ya kupata ujuzi zaidi wa namna ya kutekeleza Sera ya Mambo ya Nje inayotilia msisitizo wa utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Naye Katibu wa Mabalozi Wastaafu, Balozi Bertha Semu Somi ameeleza kuwa jukumu hilo la kuwajengea uwezo watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwao ni fahari kwa kuwa ni kielelezo kuwa bado wanamchango katika kuendelea kusaidia Serikali.

“Serikali iliwekeza katika kutujengea uwezo wa kutekeleza kwa ufasaha majukumu ya kidiplomasia hivyo, nasi tunapata nafasi ya kurejesha kile kilichowekezwa kwetu kwa vijana ambao wanarithishwa jukumu hili muhimu kwa maslahi ya nchi’’ alisema Balozi Somi.

Pia ameeleza maafisa wanaonesha umakini kwa kuwa katika siku ya pili kila Afisa amefanya wasilisho ya yale yaliyotangulia kufundishwa ambapo ametoa mrejesho mzuri kwa Mabalozi wanaofundisha katika kufahamu nini kimepungua na nini kiongezwe katika kuyaboresha mafunzo hayo.

Maafisa wanaohudhuria mafunzo wamesisitizwa kujiongezea weledi kwa kusoma sera, sheria na miongozo mbalimbali na pia wasome nyaraka kama Sera ya Mambo ya Nje, Diara ya Maendeleo ya Taifa, Ilani ya Chama cha Mapinduzi, Mkataba wa Vienna, Kanuni za Utumishi wa Mambo ya Nje, na miongozo mingine ya kikanda na kimataifa.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi (Mb.) akifungua mafunzo ya siku nne (4) ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara hiyo yanayofanyika katika Hotel ya St. Gaspar jijini Dodoma kuanzia tarehe 8 hadi 11 Oktoba 2024.
Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bi. Chiku Kiguhe akimkaribisha Naibu Waziri Mhe. Cosato Chumi kwenye ufunguzi wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara hiyo yanayofanyika katika Hotel ya St. Gaspar jijini Dodoma.
Mfunzo yakiendelea
Mafunzo yakiendelea
Picha ya pamoja

Hafla ya ikiendelea
Katibu wa Mabalozi Wastaafu, Balozi Bertha Semu Somi akisisitiza jambo kwenye ufunguzi wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yanayofanyika katika Hotel ya St. Gaspar jijini Dodoma.
Balozi Peter Kalaghe akifuatilia mafunzo Maafisa Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifuatilia hafla ya ufunguzi wa mafunzo ya Mawasiliano ya Kidiplomasia kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yanayofanyika katika Hotel ya St. Gaspar jijini Dodoma.