Wednesday, November 26, 2014

Watanzania kupata punguzo la asilimia 40 kwa matibabu katika Hospitali ya Irani iliyoko Dubai


Konseli Mkuu, Bw. Omar Mjenga wa Konseli Kuu ya Dubai kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Irani iliyopo Dubai (Iranian Hospital Dubai),  wakiweka saini makubaliano ya pamoja ambayo yatatoa punguzo la asilimia 40 ya matibabu kwa Mtanzania yeyote yule atakayetibiwa katika hospitali hiyo.  Makubaliano hayo yamewekwa saini katika hospitali ya Irani iliyopo Dubai, maeneo ya Jumeirah. 
Konseli Mkuu Omar Mjenga wa Tanzania, Dubai pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Irani, Dubai wakionyesha makubaliano mara baada ya kumaliza kutiliana saini.

Tuesday, November 25, 2014

Rais Kikwete apokea salamu za kheri toka kwa Rais Obama

Balozi wa Tanzania nchini Marekani Mh. Liberata Mulamula akiwasilisha kwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete salamu za kumtakia afya njema kutoka kwa Rais wa Marekani Barack Obama leo jijini Baltimore, Maryland, Marekani.

Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiongea kwa furaha na ujumbe kutoka Ubalozi wa Tanzania ulioko jijini Washington DC uliomtembelea kumjulia hali na kuwasilisha salamu maalumu za pole za Rais Barack Obama jijini Baltimore, Maryland.  
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi Liberata Mulamula na ujumbe wake wa maafosa waandamizi wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani baada ya kupokea salamu maalumu za kumtakia kheri ya afya njema kutoka kwa Rais Barack Obama wa Marekani leo jijini Baltimore, Maryland, Marekani.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiongea na Balozi Liberata Mulamula na ujumbe wake wa maafosa waandamizi wa ubalozi wa Tanzania nchini Marekani baada ya kupokea salamu maalumu za kumtakia kheri ya afya njema kutoka kwa Rais Barack Obama wa Marekani leo jijini Baltimore, Maryland, Marekani.
Rais Prof. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mulamula na Maafisa Waandamizi wa Ubalozi Tanzania, nchini Marekani (Picha na Freddy Maro)

Friday, November 21, 2014

Waziri Membe azindua Chama cha Urafiki wa Tanzania na China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa hotuba ya uzinduzi wa  Chama cha Urafiki wa Tanzania na China. Hafla ya uzinduzi huo ilifanyika Jijini Dar es Salaam na kuhuduhuriwa na Mwenyekiti wa Chama hicho ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim, Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Yongqing na Viongozi wengine.
Mhe. Membe akihutubia.
Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Yongqing akihutubia wakati wa hafla hiyo. 
Mwenyekiti wa Chama hicho Mhe. Salim nae akizungumza wakati wa hafla hiyo
Mhe. Membe kwa kushirikiana na Balozi Lu Yongqing wakizindua Chama hicho kwa mara nyingine.
Waziri Membe, Balozi Lu na Dkt. Salim pamoja na wageni waalikwa wakati wa hafla hiyo.
Waziri Membe pamoja na Wageni waalikwa wakiinua glasi juu kutakiana heri

Waziri Membe akijadiliana jambo na Dkt. Salim
Hafla ikiendelea

WAZIRI MEMBE AWAASA WAHITIMU WA KIU KUTII SHERIA ZA NCHI

 Brass Band ya Jeshi la Magereza ikiwaongoza Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU), Kampasi ya Dar es Salaam , Rais Mstaafu, Mhe. Ali Hassan Mwinyi, mgeni rasmi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe, Maafisa, Wahadhiri,Wahitimu pamoja na Wageni Waalikwa kuingia katika Viwanja vya Chuo Kikuu  hicho katika sherehe za Mahafali ya Kumi na Moja ya chuo hicho yaliyofanyika tarehe 21.11.2014.
  Mhe. Membe (mwenye joho la bluu) akiongozana na baadhi ya Wahadhiri kuingia katika viwanja yalikofanyika mahafali ya kumi na moja ya chuo kikuu cha Kimataifa cha Kampala Kampasi Dar es Salaam huko Gongo la Mboto.
 Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi  (mwenye kofia ya njano) akiwa pamoja na mgeni rasmi  Mhe. Membe (wa pili kutoka kushoto) wakiwa wamesimama kwa heshima ya Wimbo wa Taifa kama ishara ya kuanza kwa mahafali hayo ya kumi na moja.
 Shekhe Dr.Badruh H.Sseguja akifungua kwa sala Mahafali ya Kumi na Moja ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 21.11.2014
  Mchungaji Ogah Ogbole akifungua kwa sala mahafali ya kumi na moja ya Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 21.11.2014
 Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala Profesa Mohamed Ndaula akitoa hotuba ya ufunguzi wa  mahafali hayo ya kumi na moja ya chuo hicho Jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya wahitimu wa fani mbalimbali wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala Kampasi ya Dar es Salaam wakiwa wamekaa kwa utulivu tayari kabisa kwa ajili ya sherehe za mahafali ya kumi na moja ya chuo hicho ambapo jumla ya wanafunzi 902 walihitimu masomo yao.
 Baadhi ya wakuu wa idara mbalimbali za Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala wakiingia katika viwanja vya chuo hicho Kampasi ya Dar es Salaam tayari kwa mahafali ya kumi na moja ya chuo hicho.
 Mkuu wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala Mheshimiwa Ally Hassan Mwinyi akiwahutubia wahitimu wa mahafali hayo ya kumi na moja.
   Mgeni rasmi, Mhe. Bernard Membe akiwahutubia wahitimu wa mahafali hayo ya kumi na moja ambapo aliwaasa kwenda kufanya kazi kwa bidii na kutii sheria za nchi.
 Baadhi ya wahitimu wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala wakinyanyua kofia zao juu mara baada ya kutunukiwa shahada zao katika mahafali yao ya kumi na moja ya chuo hicho.
 Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria mahafali hayo wakifuatilia hatua kwa hatua kile kinachoendelea katika sherehe hizo.
 Mkuu wa chuo kikuu cha kimataifa cha Kampala akitunuku shahada kwa wahitimu wa mahafali hayo.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa Awamu ya Pili, Mhe. Ally Hassan Mwinyi ( mwenye joho la njano) akiwa pamoja na mgeni rasmi, Mhe. Membe pamoja na meza kuu wakiwa wamesimama kwa heshima ya wimbo wa taifa kama ishara ya kufunga mahafali hayo ya kumi na moja.


 Mgeni rasmi akizungumza na waandishi wa habari baada ya mahafali hayo.

PICHA NA Reuben Mchome
======================================

Membe Mgeni Rasmi Mahafali KIU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe, amesema elimu imekomboa wanawake nchini Tanzania kwa kuwapa uwezo wa kushiriki sawa sawa na wanaume kwenye fursa za kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Mhe. Membe, ambaye alikuwa akihutubia kwenye mahafali ya 11 ya Chuo Kikuu cha Kampala (KIU), Jijini Dar es Salaam leo, aliwataka wanawake kutumia kikamilifu fursa za elimu ya juu ili wajitegemee kiuchumi na kuondokana kabisa na unyanyasaji wa kijinsia.

Alielezea kuridhishwa na uwezo ulioonyeshwa na wahitimu wa kike katika chuo hicho. Kati ya wahitimu 902 waliotunukiwa Shahada na Stashahada na Mkuu wa Chuo Kikuu hicho, Rais Mstaafu, Ali Hassan Mwinyi, 423 ni wanawake.

Mhe. Membe aliwataka wahitimu hao watumie elimu yao vizuri katika kuiendeleza jamii na taifa, kufanya kazi kwa bidii na kutii sheria za nchi.

Tuesday, November 18, 2014

PRESS RELEASE

Sultan of Oman, His Majesty Qaboos bin Said Al Said

PRESS RELEASE

His Excellency Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Majesty Qaboos bin Said Al Said, Sultan of the Sultanate of Oman on the occasion of the 44th Anniversary of the Sultanate of Oman National Day.

The message reads as follows;
“His Majesty, Qaboos bin Said,
Sultan of the Sultanate of Oman
MUSCAT,
Your Majesty,

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, I would like to sincerely convey my warm congratulations to you, Your Majesty and through you, to the Government and the people of Oman on celebrating the 44th Anniversary of the National Day.

The Sultanate of Oman and the United Republic of Tanzania have enjoyed cordial and brotherly bilateral relations over the years. As you commemorate this joyous occasion of your National Day, I wish to take this opportunity to reiterate my Government’s desire and commitment to further enhance the traditional bond of friendship and cooperation existing between our two countries for our mutual benefits.

Please accept, Your Majesty, my most sincere congratulations and best wishes for the continued good health and happiness, and for the friendly people of the Sultanate of Oman, further progress and prosperity”.

ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM.
18th NOVEMBER, 2014



Monday, November 17, 2014

Waziri Membe afungua Mkutano wa Kimataifa kuhusu Sayansi ya Jamii

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akitoa hotuba ya ufunguzi wa   Mkutano wa Kimataifa wa siku mbili kuhusu Sauti ya Kwanza ya Sayansi ya Jamii. Mkutano  huo ambao unafanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani  chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam unawashirikisha Wajumbe kutoka  Tanzania, Kenya, Uganda, Ghana, Nigeria na Canada. Katika hotuba yake Mhe. Membe alisisitiza umuhimu wa Wasomi na Wanazuoni kujikita katika Tafiti za Kisayansi ili kuja na majibu yatakayoisaidia nchi kuondokana na umaskini, utunzaji wa mazingira na masuala mengine ya manufaa kwa nchi.
Mhe. Membe akikaribishwa na Prof. Florence Luoga ambaye ni Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Dar es Salaam mara baada ya kuwasili kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani kwa ajili ya ufunguzi rasmi wa Mkutano wa Kimataifa wa siku mbili kuhusu Sauti ya Kwanza ya Sayansi ya Jamii  ulioandaliwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. 
Mhe. Membe akikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa mkutano huo
JUU NA CHINI: Ni sehemu ya Wajumbe wakifuatilia mkutano huo kuhusu masuala ya Sayansi ya Jamii.
Mhe. Membe akiendelea na hotuba yake ya ufunguzi huku wajumbe wakimsikiliza.
Sehemu ya wajumbe wakifurahia jambo wakati Mhe. Membe (hayupo pichani) akitoa hatuba ya ufunguzi.
Mhe. Membe akisindikizwa kwenda kupiga picha ya pamoja na Maprofesa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam waliokuwepo kwenye mkutano huo
Mhe. Membe (wa tatu kulia waliokaa) katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe wa mkutano kuhusu masuala
Waziri Membe akifurahia jambo na mmoja wa Wajumbe wanaoshiriki mkutano huo.
Mhe. Membe akihojiwa na Wanahabari kuhusu mkutano huo.

Picha na Reuben Mchome

Saturday, November 15, 2014

Waziri wa Uchukuzi akutana na Konseli Mkuu wa Tanzania, Dubai

Waziri wa Uchukuzi Mhe. Harrisson Mwakyembe (Mb.), amekutana na kufanya mazungumzo ofisini kwa Bw. Omar Mjenga, Konseli Mkuu wa Tanzania, Dubai.

 Konseli Mkuu amemueleza Mhe. Mwakyembe kuhusu mazungumzo yake pamoja na Mhe. Gaith  Alghaith, Mtendaji Ma wa Shirika la Ndege la FlyDubai, kuhusu mpango wa shirika hilo kuingia makubaliano ya ushirikiano pamoja na shirika la Ndege la Tanzania(Air Tanzania) ambako Flydubai watatoa ndege tano zitakazochukua njia za ndani (domestic routes) na zile za kikanda (regional routes).

Ushirikiano huu utasaidia kufufua njia zote za ATC na kuiwezesha ATC kuanza kupata mapato.
Njia za kikanda ni pamoja na Kinshasa, Lubumbashi, Goma, Kigali, Bunjumbura, Entebe, Nairobi, Sychelles, Moroni, Madagascar, Mauritius, Maputo, Lilongwe, Lusaka, Joharnessburg, na Harare.

Friday, November 14, 2014

Waziri Membe akutana na Mabalozi wa Misri na Sudan nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Balozi wa Misri hapa nchini, Mhe. Hossam Moharram alipofika Wizarani kwa mazungumzo kuhusu kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizi mbili.
Mhe. Membe akifafanua jambo wakati wa mazungumzo yake na Balozi Moharram. Wengine pichani ni Maafisa kutoka Ubalozi wa Misri.


......Waziri Membe na Balozi wa Sudan

Waziri Membe akisalimiana na Balozi wa Sudan hapa nchini, Mhe. Dkt. Yassir Mohamed Ali alipokutana nae kwa mazungumzo Wizarani.

Picha na Reuben Mchome