Tuesday, December 20, 2022

DKT. TAX AONGOZA MAMIA YA WAOMBOLEZAJI KATIKA MAZISHI YA BALOZI MUSHY

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax ameungana na familia, ndugu, jamaa na mamia ya waombolezaji katika mazishi ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Austria, Balozi Celestine J. Mushy yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro.  

Akitoa Salamu za pole kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Tax amesema Serikali inatambua mchango wa Marehemu Balozi Mushy katika sekta  ya Diplomasia nchini na kwamba itauenzi na kusimamia yale yote aliyokuwa anayaamini katika kukuza na kuimarisha Diplomasia nchini.

Amesema marehemu ametoa mchango mkubwa katika kukuza diplomasia na kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na nchi mbalimbali na Mashirika ya Kimataifa.

Dkt. Tax amesema marehemu Balozi Mushy alikuwa Balozi wa kwanza kuhudumu katika Ubalozi mpya wa Tanzania nchini Austria, hivyo katika nafasi hiyo, aliweza kutekeleza vyema majukumu yake na kuimarisha uhusiano kati  ya Tanzania na Austria na aliweza kutafuta na kuibua fursa za biashara na uwekezaji zilizopo nchini humo.

Ameongeza kusema Balozi Mushy aliweza kukuza na kuimarisha uhusiano kati ya Tanzania na Mashirika ya Umoja wa Mataifa yaliyopo Vienna, Austria, tangu ateuliwe kuwa Balozi wa Tanzania nchini Austria na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna.

“Kama ilivyo kwa Familia, Serikali, Watanzania na Dunia kwa ujumla tumepokea kwa mshtuko, simanzi na masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Balozi Celestine Mushy. Mshtuko, simanzi na masikitiko yetu unatokana na ukweli kwamba kifo cha Balozi Mushy kimekuwa cha ghafla mno. Taifa bado lilikuwa linamhitaji sana,” alisema Dkt. Tax

Dkt. Tax amesema Wizara imeguswa na kifo cha Balozi Mushy kwani katika uhai wake alikuwa na mchango mkubwa kwa nchi katika maeneo mbalimbali. 

Amesema Serikali imepoteza Kiongozi mnyenyekevu, mwenye upendo kwa watu wote, mchapakazi hodari, aliyejitoa kwa yeyote aliyehitaji msaada wake, na aliyekuwa na mchango mkubwa kwa Wizara na Taifa kwa ujumla.  

Wakati huo huo, Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete aliyehudhuria mazishi ya Balozi Mushy amemuongelea marehemu kama mchapa kazi, mwenye weledi mkubwa na ambaye ameifanyia makubwa Tanzania.

“Nilimfahamu Balozi Mushy kama kijana hodari tangu alipoajiriwa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa mwaka 1999, alikuwa kijana hodari, mchapa kazi na mwenye weledi. Ni kutokana na utendaji wake huo mzuri alipelekwa kama Afisa katika Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa New York, Marekani.

Amesema Balozi Mushy alikuwa mbobezi na mahiri wa masuala ya diplomasia, lakini pia alikuwa mzalendo na alikuwa tayari kujitoa kwa ajili ya Tanzania na kuongeza kuwa hata alipoteuliwa na Rais Samia kuwa Balozi wa Tanzania Austria na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi ya Umoja wa Mataifa, Vienna niliona kuwa Mhe Rais amelenga mtu sahihi

Viongozi wengine walioungana na familia katika mazishi ya Balozi Mushy ni Naibu Waziri, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Katibu Mkuu, Balozi Joseph Sokoine, Menejimenti ya Wizara, mabalozi mbalimbali wanaoiwakilisha Tanzania Nje ya Nchi wakiongozwa na Amidi Mkuu na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza Mhe. Dkt. Asha Rose Migiro, Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo, Balozi wa Tanzania nchini Italia, Mhe. Mahamoud Thabit Kombo, Balozi wa Tanzania nchini Misri, Mhe. Dkt. Emmanuel Nchimbi, Majaji, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo Nje, Ulinzi na Usalama Mhe. Vita Kawawa pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Shaka Hamdu Shaka.

Januari, 2022 Marehemu Balozi Mushy aliteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa Balozi wa Tanzania nchini Austria na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Ofisi za Umoja wa Mataifa Vienna.

Balozi Mushy alifariki dunia Desemba 12, 2022 katika ajali ya gari iliyotokea Mkata wilayani Handeni mkoa wa Tanga baada ya gari alilokuwa akisafiria kugongana na lori la mizigo na kuungua moto akiwa ndani.

Baadhi ya Viongozi mbalimbali waandamizi wa Serikali wakifuatilia ibada ya mazishi ya Marehemu Balozi Celestine Mushy wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro. Katikati ni Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akitoa salamu za Serikali katika mazishi ya aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Austria, Balozi Celestine  Mushy yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro 

Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Kikwete akitoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Balozi Celestine Mushy

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Shaka Hamdu Shaka akitoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Balozi Celestine Mushy

Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola akitoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu Balozi Mushy

Mwakilishi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa (DMC) katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Hellen Maduhu akieleza alivyomfahamu Marehemu Celestine Mushy

Sehemu ya Uongozi wa Wizara ukifuatilia ibada ya mazishi ya Marehemu Balozi Celestine Mushy nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Viongozi wa Dini wakiendelea na ibada ya mazishi ya Marehemu Balozi Celestine Mushy nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Mjane na Watoto wa Marehemu Balozi Mushy wakifuatilia ibada ya mazishi ya Marehemu Balozi Celestine Mushy nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika picha ya pamoja mbele ya jeneza lililohifadhi mwili wa Marehemu Balozi Celestine Mushy nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Baadhi ya Mabalozi katika picha ya pamoja mbele ya jeneza lililohifadhi mwili wa Marehemu Balozi Celestine Mushy nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiweka udongo katika kaburi la Marehemu Balozi Celestine Mushy wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiweka udongo katika kaburi la Marehemu Balozi Celestine Mushy wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Joseph Sokoine akiweka udongo katika kaburi la Marehemu Balozi Celestine Mushy wakati wa mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake katika Kijiji cha Sambarai, Tarafa ya Kibosho, Mkoni Kilimanjaro



Monday, December 19, 2022

WABUNGE WA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI (EALA) WAAPA RASMI

 

Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) akiapa kuwa Mjumbe wa Baraza la Maamuzi la Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo Jijini Arusha

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akiapa kuwa Mjumbe wa Baraza la Maamuzi la Bunge la Afrika Mashariki (EALA) leo Jijini Arusha


Dkt. Shogo Richard Mlozi akiapishwa kuwa Mbunge wa bunge la EALA

Mhe. Dkt. Abdullah Makame akiapishwa kuwa Mbunge wa bunge la EALA

Mhe. Dkt. Ngwaru Jumanne Maghembe akiapa kuwa Mbunge wa bunge la EALA

Mhe. Angela Charles Kizigha akiapa kuwa Mbunge wa bunge la EALA
Sehemu ya Wabunge wa Bunge la EALA








CONSULTANCY OPPORTUNITIES AT THE AFRICAN DEVELOPMENT BANK




 

VACANCY ANNOUNCEMENT



 

Sunday, December 18, 2022

WAJASIRIAMALI WAASWA KUONGEZA UBUNIFU, UBORA WA BIDHAA

Wajasiriamali Wadogo na wa kati wamehimizwa kuendelea kuongeza ubunifu na ubora wa huduma na bidhaa wanazozalisha ili kujiweka kwenye nafasi nzuri ya ushindani katika soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (African Continental Free Trade Area - AfCFTA). 

Rai hiyo imetolewa na Waziri anayesimamia Masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Magode wa Uganda kwenye hafla ya kufunga Maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati, maarufu Juakali yaliyofanyika katika viwanja vya Uhuru vya Kololo jijini Kampala, Uganda. 

Amesema pamoja na kazi nzuri inayoendelea kufanywa na wajasiriamali, wasiridhike na hatua ya mafanikio waliyoifikia bali waendelee kuongeza ubunifu na ubora zaidi wa huduma na bidhaa wanazozalisha ili kujiweka katika nafasi nzuri ya ushindani hasa katika nyakati hizi za soko huria. 

Waziri Magode amesema Serikali za Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Jumuiya hiyo wanaendelea kutengeneza mazingira wezeshi zaidi kwa wafanyabiashara ili waweze kuendesha shughuli zao kwa uhuru na kwa faida zaidi. 

“Katika ngazi ya Jumuiya Nchi Wanachama kwa kushirikiana na Sekretarieti na wadau wengine sote tumekubaliana na tunaahidi kuendelea kuweka mazingira wezeshi ya uendeshaji ya biashara yatakayowezesha Wafanyabishara wadogo, kati, wa kubwa sio tu kunufaika na soko la Afrika Mashariki bali soko kubwa la Afrika katika mpango wa AfCFTA”.  Mhe. Waziri Magode

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki anayesimamia musuala ya Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala Mhandisi Steven Mlote ametoa rai kwa Jumuiya kuendelea kuenzi na kutumia lugha ya Kiswahili katika kuendesha biashara kwa kuwa ndiyo lugha pekee itayako wezesha kuunganisha wafanyabiasha wengi zaidi katika jumuiya na kurahisisha ufanyaji wa biashara. 

Amesema Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki imepokea mapendekezo ya wajasiriamali ya kuomba maonesho hayo yafanyike walau mara mbili kwa mwaka kutokana na umuhimu wake na kwamba mapendekezo hayo yataafikishwa katika ngazi husika kwa mashauriano na maamuzi zaidi.

Sherehe za kufunga maonesho hayo ziliambatana na shughuli mbalimbali ikiwemo ugawaji wa zawadi kwa washiriki, vyeti vya ushiriki na burudani mbalimbali. 

Aidha, Jamhuri ya Burundi imepewa dhamana ya kuandaa maonesho yajayo ya 23 ya Afrika Mshariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati yanayotarajiwa kufanyika mwakani 2023.
Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki anayesimamia musuala ya Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala Mhandisi Steven Mlote akikabidhi cheti kwa mshiriki wa maonesho kutoka Jamhuri ya Congo kwa kufanya vizuri katika ngazi ya kitaifa.
Waziri anayesimamia Masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Magode wa Uganda akihutubia kwenye sherehe za kufunga Maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati, maarufu Juakali yaliyofanyika katika viwanja vya Uhuru vya Kololo jijini Kampala, Uganda.
Picha ya pamoja na Meza Kuu na Wajasiriamali waliopata vyeti na tuzo za kufanya vizuri zaidi kwenye Maonesho ya 22 ya Juakali yaliyofanyika katika viwanja vya Uhuru vya Kololo jijini Kampala, Uganda.
Waziri anayesimamia Masuala ya Afrika Mashariki Mhe. James Magode wa Uganda na Naibu Katibu Mkuu wa Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki anayesimamia musuala ya Mipango, Miundombinu, Fedha na Utawala Mhandisi Steven Mlote wakikabidhi tuzo kwa mshiriki mdogo zaidi wa manoesho kutoka nchini Burundi.
Kikundi cha ngoma kutoka nchini Burundi kikisherehesha kwenye sherehe ya kufunga Maonesho ya 22 ya Juakali iliyofanyika katika viwanja vya Uhuru vya Kololo jijini Kampala, Uganda.

Thursday, December 15, 2022

BALOZI SIRRO AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO KWA RAIS WA ZIMBABWE

Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa, Ikulu Zimbabwe.

Julai 20, 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alimteua aliyekuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro kuwa Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe.

Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa, Ikulu Zimbabwe

Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Emmerson Mnangagwa akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. Simon Sirro Ikulu Zimbabwe baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho

Picha ya pamoja 



Tuesday, December 13, 2022

AFRIKA MASHARIKI WAHIMIZWA KUTUMIA BIDHAA ZA NDANI

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma (kulia) akiangalia bidhaa za mjasiriamali kwenye maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati maarufu Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma ametoa wito kwa wananchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kujivunia na kutumia bidhaa zinazozalishwa katika Jumuiya ili kuijenga Afrika Mashariki yenye uchumi stahimilivu na maendeleo endelevu. 

Waziri Riziki Pembe Juma ameeleza hayo alipokuwa akizungumza kwenye sherehe za SIKU YA TANZANIA (TANZANIA DAY) katika maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati maarufu kama “Juakali”, yanayoendelea katika viwanja vya Uhuru vya Kololo Jijini Kampala, Uganda. 

“Nimepata fursa ya kutembelea baadhi ya mabanda ya maonesho na nimefurahishwa kuona bidhaa mbalimbali kutoka kwa wajasiriamali, kwa kweli bidhaa zilizopo zina ubora na ubunifu na zinavutia sana. Nitoe rai kwa wana Afrika Mashariki kutumia bidhaa hizi zinazozalishwa katika Jumuiya ili kuunga mkono juhudi za Serikali za kubadilisha sekta isiyo rasmi kuwa rasmi ili wananchi waweze kushiriki katika kuchangia maendeleo endelevu na pato la Jumuiya”. alisema Waziri Riziki Pembe Juma

Maadhimisho ya TANZANIA DAY yaliambatana na shughuli mbalimbali zilizofanywa na wajasiriamali wa Tanzania kwa lengo la kucherehesha maonesho na kuonesha utamaduni wa Tanzania pamoja na bidhaa mbalimbali zinazozalishwa nchini. Miongoni mwa shuguli zilizofanywa ni pamoja na maonesho ya mavazi ya asili, maonesho ya vito vya thamani na madini, vyakula vya asilia, ngoma za asili na muziki. 

Akizungumza na maelfu ya washiriki wa maonesho hayo Waziri Riziki Juma Pembe mbali na kutoa wito kwa wana Jumuiya kununua bidhaa za ndani alielezea hatua mbalimbali zinazo endelea chukuliwa na Serikali za Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kutatua changamoto zinazowakabili wajariamali, ambapo kwa upande wa Serikali ya Tanzania amezitaja hatua zilizochukuliwa kuwa ni pamoja na; kutoa mikopo yenye masharti nafuu, kuanzisha maeneo maaalum ya kufanyia biashara na kutoa elimu ya ujasiriamali.

“Serikali za Jumuiya ya Afrika Mashariki zinaendelea kuhakikisha wajasiriamali hawa hawaendelei kubaki wadogo bali wanapaswa kukua ili waweze kushiriki katika sekta rasmi kama wajasiriamali wakubwa. Vilevile kwa kushirikia na Sekretarieti ya Jumuiya tutahakikisha maonesho haya yanaendelea kufanyika kwa lengo la kuwapatia fursa wajasiriamali wa sekta hii ili waweze kutambua fursa zilizopo katika nchi zetu na kushiriki katika uzalishaji na maendeleo ya nchi zetu”. Alieleza Waziri Riziki Pembe Juma

Hii ni mara ya tano kwa Jamhuri ya Uganda kuwa mwenyeji wa maonesho haya tokea kuanzishwa kwake mwaka 1999.
Mkurugenzi anayesimamia masuala ya Diapora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi James Bwana akiangalia bidhaa za mjasiriamali kwenye maonesho ya 22 yaJuakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda

Meza Kuu wakiwa wamesimama wakati wimbo wa Taifa ukipigwa wakati wa maadhimisho ya SIKU YA TANZANIA kwenye maonesho ya 22 ya Juakali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Kampala, Uganda

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma akihutubia wakati wa maadhimisho ya SIKU YA TANZANIA kwenye maonesho ya 22 ya Juakali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Kampala, Uganda

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma akifurahia muziki wa asili pamoja na wajasiriamali iliokuwa ukipigwa wakati wa maadhimisho ya SIKU YA TANZANIA kwenye maonesho ya 22 ya Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda.

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma (kulia) akiangalia bidhaa za mjasiriamali kwenye maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati maarufu Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda.

Balozi wa Tanzania nchini Uganda Mhe. Aziz Mlima akitoa salaam kwa wajasiriamali wakati wa maadhimisho ya SIKU YA TANZANIA kwenye maonesho ya 22 ya Juakali ya Jumuiya ya Afrika Mashariki yanayofanyika jijini Kampala, Uganda

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma (kulia) akiangalia bidhaa za mjasiriamali kwenye maonesho ya 22 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Wajasiriamali Wadogo na Wakati maarufu Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda

Wajiriamali wa Tanzania wakiwa kwenye maonesho ya mavazi yaliyofanyika kwenye maonesho ya 22 ya Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Riziki Pembe Juma akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi na Watendaji wa Serikali na wajasiriamali`kwenye maonesho ya 22 ya Juakali yanayoendelea jijini Kampala, Uganda.