Thursday, February 29, 2024

WAZIRI MKUU WA ETHIOPIA ATUA NCHINI KWA ZIARA YA KITAIFA YA SIKU TATU

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Shirikisho la Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali amewasili nchini leo tarehe 29 Februari 2024 kuanza ziara yake ya  kitaifa ya siku tatu.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Mhe. Waziri Mkuu Abiy amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba.

Mhe. Dkt. Abiy atapokelewa rasmi na mwenyeji wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 01 Machi 2024.

Pamoja na mambo mengine ziara ya Waziri Mkuu Abiy inalenga kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Ethiopia katika maeneo ya kimkakati ikiwemo usafirishaji kwa njia ya anga, nishati, kilimo na mifugo, biashara na uwekezaji na Ushirikiano katika sekta za elimu, uhamiaji, na ulinzi na usalama 

Ziara hiyo ambayo itakamilika tarehe 02 Machi 2024 inafanyika kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Matukio katika picha:

Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali akishuka kwenye ndege katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) jijini Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba (Mb.) akisalimiana na Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali mara baada ya kuwasili Tanzania kwa ziara ya Kitaifa ya siku tatu.

Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Shamrashamra wakati wa mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.

Shamrashamra wakati wa mapokezi ya Waziri Mkuu wa Ethiopia, Mhe. Dkt. Abiy Ahmed Ali nchini Tanzania katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam.



Wednesday, February 28, 2024

TANZANIA NA URUSI KUIMARISHA DIPLOMASIA YA UCHUMI



Tanzania na Urusi zimesisitiza kuendelea kuimarisha diplomasia ya uchumi kwa maslahi ya pande zote kupitia ushirikiano wa kidiplomasia ulioanzishwa tangu mwaka 1961.

Msisitizo huo umetolewa katika mazungumzo kati ya Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb) na Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan yaliyofanyika katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam Februari 28, 2024. 

Mazungumzo ya viongozi hao yalijikita katika ufuatiliaji wa masuala ya uchumi, biashara, uwekezaji na masuala ya kibinadamu yaliyojadiliwa wakati wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali Urusi – Afrika uliofanyika nchini Urusi mwaka 2023.

Aidha, wamejadili juu ya utaratibu mpya wa kuanzishwa kwa mkutano wa kwanza wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Urusi na Afrika unaotarajiwa kufanyika nchini Urusi mwezi Oktoba mwaka 2024 ambao utaishirikisha Sekretarieti ya Umoja wa Afrika kama sehemu ya marafiki waalikwa wa Urusi.

Kadhalika, mkutano huo utaongeza nafasi kwa Nchi za Afrika kujadili utekelezaji wa masuala mbalimbali yaliyokubaliwa na Serikali zao katika nyakati tofauti, sambamba na kuongeza maeneo mapya ya ushirikiano katika sekta za kimkakati.

Akiainisha maeneo ya kimkakati, Mhe. Mbarouk ameeleza kuwa Tanzania ina nia ya dhati ya kuimarisha sekta ya utalii, hivyo ni wakati sahihi wa kuangalia namna bora ya kuhuisha mifumo mbalimbali inayowezesha kuongeza idadi ya watalii na huduma nyingine za kitalii.

Naye Mhe. Avetisyan ameeleza kuwa Urusi imejipanga kuendeleza ushirikiano katika sekta ya utalii kwa kutoa mafunzo kwa kampuni za kitalii na watoa huduma za hoteli ambazo zitaenda sambamba na utangazaji wa filamu ya “Tanzania the Royal Tour”.

Pia Mhe. Balozi  Andrey Avetisyan ameeleza kuwa Urusi inaunga mkono jitihada za kutangaza utalii ambapo inafanya utaratibu kuliwezesha Shirika la Utangazaji la Urusi la “Russia Today” kuja nchini kuandaa makala za runinga zitakazorushwa nchini Urusi kwa lengo la kuendelea kuhamasisha utalii na utamaduni kwa pande zote mbili.

Vilevile viongozi hao wamejadili juu ya umuhimu wa ushirikiano katika sekta ya elimu pamoja na kuendelea kutoa hamasa kufuatia fursa za ufadhili za masomo ya muda mrefu na mfupi zinazotolewa na Serikali ya Urusi kwa Watanzania


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) akizungumza na Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan alipomtembelea katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam tarehe 28 Februari, 2024.

Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini, Mhe. Andrey Avetisyan akieleza juu ya masuala mbalimbali ya ufuatiliaji yaliyojadiliwa wakati wa mkutano wa Urusi - Afrika uliofanyika jijini Moscow, Urusi mwaka 2023.

Maafisa kutoka Ubalozi wa Urusi walioambatana na Mhe. Avetisyan wakifatilia mazungumzo.

Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo.

Mazungumzo yakiendelea

Balozi Mbarouk akiagana na Mhe. Avetisyan.

 

Monday, February 26, 2024

WIZARA YAAHIDI KUBORESHA,KUIMARISHA MICHEZO

Ikiwa ni saa kadhaa baada ya kumalizika kwa mashindano ya mbio zilizojipatia umaarufu kuliko mbio za nyikani, "Kili Marathon 2024", Uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, ukiongozwa na Katibu Mkuu wake Balozi Dkt. Samwel Shelukindo umewapongeza wanariadha wa Wizara walioshiriki mbio hizo na kuahidi kuboresha mazingira ya michezo wizarani.

Akiongea na wanamichezo hao jana mjini Moshi, baada ya kumalizika kwa mashindano ya Kili Marathon 2024, Dkt. Shelukindo alisema  kuwa michezo ni afya, hivyo watumishi wanapaswa kujituma kufanya mazoezi mara kwa mara siyo tu kwa ajili ya kuimarisha afya zao bali kuwawezesha pia kushiriki michezo mbalimbali ndani na Nje ya nchi.

"Natambua kuwa ndani ya Wizara yetu kuna watumishi wenye vipaji tofauti, nawasihi pamoja na ufinyu wa muda mlionao mjitahidi kufanya mazoezi ili muweze kumudu ushindani wa michezo mbalimbali na kuipaisha Wizara yetu ndani na Nje," alisema Dkt. Shelukindo

Kwa upande wake, Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi aliwapa hamasa wanamichezo ya kuongeza idadi ya michezo wizarani ili kupanua wigo wa watumish kushiriki na kuitaja michezo hiyo kuwa ni pamoja na mpira wa kikapu, mpira wa tenesi, michezo ya Jadi na ndondi.

Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara, Balozi Said Shaibu Mussa aliwataka wanamichezo wa Wizara kuendelea kujituma kwa bidii na kuwa na nidhamu ya mazoezi ili kuwawezesha kushinda michezo wanayoshiriki na kuipeperusha bendera ya Wizara vizuri kwenye kila mashindano wanayoshiriki ikiwa pamoja na kuwahimiza kuandaa bonanza za michezo yatakayoshirikisha wadau tofauti ili kuimarisha mahusiano, kukuza diplomasia ya michezo hatimaye kutangaza Wizara.

Awali akiongea katika kikao cha Viongozi na wanamichezo, Mwenyekiti wa Klabu ya Michezo Wizarani (Nje sports Club), Bw. Ismail  Hamidu Abdallah aliushukuru Uongozi wa Wizara kwa kuwawezesha na kuwapa motisha wakati wote wanaposhiriki katika michezo mbalimbali.

"Tunawashukuru Viongozi wetu kwa kutuwezesha wanamichezo, kwa kweli kwa ushirikiano tunaoupata kutoka kwenu tunaahidi kuendelea kujituma kwa bidii katika michezo na kuipaisha vyema bendera ya Wizara," amesema Bw. Ismail

Wanamichezo wa Wizara wamegawanyika katika michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, mpira wa pete kwa wanawake, volleyball, mchezo wa kuvuta kamba pamoja na riadha.

Mwenyekiti wa Klabu ya Michezo Wizarani (Nje sports Club), Bw. Ismail  Hamidu Abdallah akizungumza wakati wa kikao kilichowakutanaisha Viongozi wa Wizara na wanamichezo wake, mjini Moshi jana jioni


Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaibu Mussa akizungumza wakati wa kikao baina ya viongozi wa Wizara na wanamichezo jana, mjini Moshi. Kulia (mwenye Tshirt nyeusi) ni Katibu Mkuu Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akifuatiwa na Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi. Wengine ni wanamichezo wa Wizara. 

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Wizarani, Bi. Ester Masigo akizungumza wakati wa kikao




Sunday, February 25, 2024

NJE JOGGING YASHIRIKI KILI MARATHON, KUNYAKUA MEDALI 20

Timu ya riadha ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki - Nje Jogging imeshiriki mashindano ya Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) na kujinyakulia medali 20 leo Februari 25, 2024 Moshi, Kilimanjaro.

Timu hiyo yenye jumla ya wanariadha 30 imeongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Said Shaibu Mussa. 

Katika mbio hizo, wanariadha 10 wameshiriki mbio za Kilometa tano (05) – (Fun run) na wengine 20 wameshiriki mbio za umbali wa kilometa 21 (Tigo half Marathon) ambazo pia Balozi Shelukindo alishiriki.

Akizungumza mara baaada ya kushiriki mbio hizo, Balozi Shelukindo amesema Wizara imeshiriki ili kuunga mkono Kili Marathon ambayo ni moja ya jukwaa la kuutangaza Mlima Kilimanjaro na Tanzania, lakini pia kutangaza majukumu ya Wizara katika mbio hizo. Kadhalika, Dkt. Shelukindo amewasihi waandaaji wa Kili Marathon kwa wakati ujao kuhakikisha kuwa wanashirikiana na Balozi za Tanzania Nje ya nchi ili kuitangaza Kili Marathon zaidi Duniani na kuifanya kuwa bora zaidi ya sasa.

“……………Kilimanjaro ni moja kati ya vivutio vya urithi wa dunia, hivyo kupitia mashindano ya mbio za Kilimanjaro International Marathon tutaweza kutangaza zaidi Kilimanjaro duniani,” alisema Dkt. Shelukindo.

“Tumefurahi kwa kweli kwa kuwa mbio hizi zimefanyika katika mazingira salama, hivyo natoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuweka mazingira salama hapa nchini ambayo yamewawezesha washiriki kutoka mataifa mbalimbali ulimwenguni kushiriki. 

Kadhalika, Balozi Shelukindo amewaasa vijana hususan watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki pamoja na majukumu waliyonayo wajikite katika kufanya mazoezi kwa wingi na nidhamu ili kuwawezesha kushiriki kwa wingi katika michezo ya aina hiyo na mingine na kushinda medali mbalimbali.

Mgeni rasmi katika mbio hizo, Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro amewapongeza waandaaji wa mbio hizo ambazo zimechangia kwa kiasi kikubwa kuboresha michezo nchini pamoja na kuibua vipaji vipya vya riadha kwa kila mwaka.

"Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na waandaaji wa mbio hizi, pamoja na wadhamini wakuu na wadau wengine wa michezo katika kuhakikisha mbio hizi zilizoanzishwa zaidi ya miaka 20 iliyopita zinakuwa endelevu kwa manufaa ya maendeleo ya michezo nchini", amesema.

Katika mbio hizo, Augustino Sulle (Tanzania) ameshinda kilomita 42 kwa wanaume akitumia saa 02:21:06, mbele ya Abraham Kosgei (Kenya) ambaye alitumia saa 02:22:02. Kwa upande wa wanawake, Natalia Sulle (Tanzania) alikuwa mshindi wa kwanza ambapo alitumia Saa 02:51:23, akimtangulia Mtanzania mwenzake Neema Sanka aliyetumia saa 02:51:47, akifuatiwa na Vailet Kidasi katika nafasi ya tatu baada ya kukimbia kwa saa 03:01:03 na hivyo kukamilisha ushindi wa Watanzania kwa nafasi zote tatu za kwanza kwa umbali wa kilomita 42.

Kwa upande wa wanaume mbio za Tigo Half Marathon, Faraj Damas (Tanzania) aliibuka mshindi baada ya kutumia saa 01:16:40, akifuatiwa na Peter Mwangi (Kenya) aliyetumia saa 01:23:44, huku Mtanzania Kennedy Abel akishika nafasi ya tatu baada ya kukimbia mbio hizo kwa muda wa saa 01:24:22.

Kwa upande wa wanawake, wariadha wa Tanzania walitawala mbio hizo za Tigo Half Marathon ambapo Failuna Matanga (Tanzania) aliibuka mshindi baada ya kutumia saa 01:16:40 akifuatiwa na Neema Kisuda (Tanzania) katika nafasi ya pili baada ya kukimbia kwa saa 01:16:54, na nafasi ya tatu ilichukuliwa na Neema Mbua (Tanzania) baada ya kukimbia kwa saa 01:17:07.

Mbio za mwaka huu zimeshirikisha zaidi ya mataifa 56 na idadi ya wanariadha ikiwa ni zaidi ya 10,000 kutoka ndani na nje ya nchi walishiriki katika mbio hizo. Aidha, mbio hizo zilijumuisha mbio za Kilimanjaro premium lager 42km, 21km Tigo Half marathon na Gee Soseji 5km fun run. Mbio hizo zimeongeza umaarufu wa mbio hizo, katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Wanariadha wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki - Nje Jogging ikiongozwa na Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi wakiwa tayari kushiriki mashindano ya Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) kipengele cha (fun run) Moshi, Kilimanjaro



Sehemu ya washiriki wa timu ya riadha ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki - Nje Jogging wakimaliza mbio za Km 5 katika kipengele cha (fun run) Kilimanjaro International Marathon 2024 Moshi, Kilimanjaro



Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi katika picha baada ya kumaliza  mbio za Km 5 katika kipengele cha (fun run) Kilimanjaro International Marathon 2024 Moshi, Kilimanjaro

Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro katika picha ya pamoja na washiriki wa mbio za Kimataifa za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) kipengele cha (fun run) Moshi, Kilimanjaro



Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akzingumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza mbio za za Kimataifa za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) Moshi, Kilimanjaro

Wanariadha wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki - Nje Jogging ikiongozwa na Katibu Mkuu, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo wakiwa tayari kuanza rasmi mashindano ya Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) kipengele cha (Tigo Half Marathon Km 21) Moshi, Kilimanjaro

Baadhi ya wanariadha wakiwa katika picha ya pamoja na medali zao baada ya kushiriki Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) kipengele cha (Tigo Half Marathon Km 21) Moshi, Kilimanjaro



Saturday, February 24, 2024

INDIA YATANGAZA NEEMA KWA ZAO LA MBAAZI NCHINI


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akifurahia jambo na Waziri wa Biashara na Viwanda wa India Mhe. Piyush Goyal walipokutana kwa mazungumzo jijini New Delhi. 

India imeridhia Tanzania kuuza kiasi cha mbaazi inachoweza nchini humo kuanzia sasa hadi Machi 2025.

Makubaliano hayo yamefikiwa leo tarehe 24 Februari 2024 wakati wa mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba(Mb.) na Mwenyeji wake Waziri wa Biashara na Viwanda wa nchini humo Mhe. Piyush Goyal yaliyofanyika jijini New Delhi. 

Kadhalika, katika mazungumzo hayo viongozi hao wamekubaliana kufanyika kwa Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Biashara mwezi Aprili 2024 ili kuweka mikakati ya pamoja ya kukuza biashara baina ya Tanzania na India. 

Awali kabla ya kufikiwa kwa makubaliano haya India iliridhia Tanzania kuuza kiasi cha tani laki mbili pekee za mbaazi kwa mwaka.

Waziri Makamba alikuwa nchini India kushiriki Mkutano wa Raisina 2024 sambamba na kufuatilia utekelezaji wa makubaliano yaliyofikiwa wakati wa ziara ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyoifanya nchini humo mwezi Oktoba 2023.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akisalimiana na Waziri wa Biashara na Viwanda wa India Mhe. Piyush Goyal walipokutana kwa mazungumzo ofisini kwake jijini New Delhi. 
Mazungumzo yakiendelea
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiwa na Waziri wa Biashara na Viwanda wa India Mhe. Piyush Goyal baada ya mazungumzo yaliyofanyika Ofisini kwake jijini New Delhi. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akiwa katika Wizara ya Viwanda na Biashara, India. Wakwanza kulia ni Balozi wa Tanzania nchini humo Mhe. Anisa Mbega.

NJE JOGGING MGUU SAWA KILI MARATHON 2024

Ikiwa imebakia siku moja kufanyika kwa mbio za kimataifa  za Kilimanjaro (Kilimanjaro International Marathon 2024) Timu ya riadha ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki -Nje Jogging - imeendelea na maandalizi ya kushiriki mbio hizo zinazotarajiwa kufanyika Tarehe 25 Februari 2024 Moshi, Kilimanjaro.

Wanariadha hao wameweka kambi ya siku tatu mjini Moshi wakijifua na hatua za maandalizi ya mbio hizo. Kadhalika, Makatibu Wakuu wa Wizara wanatarajiwa kuungana na timu hiyo katika mbio hizo kesho.

Viongozi hao ni Katibu Mkuu, Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Said Shaibu Mussa.

Mbio za Kilimanjaro International Marathon 2024 zitafanyika katika Chuo cha Usharika Moshi (MoCU) ambapo zimeandaliwa na Kampuni ya Kilimanjaro Marathon na kuratibiwa kitaifa na Kampuni ya Executive Solutions.

Baadhi ya wanariadha wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifanya mazoezi ya riadha, Moshi - Kilimanjaro

Baadhi ya wanariadha wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifanya mazoezi ya riadha, Moshi - Kilimanjaro


Friday, February 23, 2024

TANZANIA, JAPAN KUIMARISHA USHIRIKIANO

Tanzania imeahidi kuendelea kushirikiana na Japan kuimarisha na kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia uliodumu kwa miaka 63 kwa maslahi ya pande zote mbili.

Ahadi hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.) wakati aliposhiriki katika hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwa Mfalme wa 126 wa Japan Mhe. Emperor Naruhito ambaye ametimiza miaka 64 tarehe 22 Februari, 2024 jijini Dar es Salaam. 

“Wakati tukiadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa kwa Mfalme wa 126 wa Japan, pia tunapata fursa ya kusherekea kukua kwa maendeleo ya ushirikiano kati ya Tanzania na Japan katika sekta mbalimbali,” alisema Balozi Mbarouk

Balozi Mbarouk aliongeza kuwa kwa miaka mingi Japan imekuwa ikifadhili maendeleo ya kijamii na kiuchumi nchini Tanzania kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) ambapo maendeleo ya miradi muhimu yameanzishwa. 

“Mwaka jana tumeadhimisha miaka 30 ya ushirikiano tangu kuanzishwa kwa Mkutano wa Kimataifa wa Tokyo kuhusu Maendeleo ya Afrika (TICAD) mwaka 1993. Ushirikiano wetu umekuza sekta za kilimo, miundombinu, nishati, usafirishaji, afya, elimu kwa ufadhili wa masomo ya muda mfupi na mrefu, pamoja na ufadhili wa miradi 383 ya maendeleo katika sekta ya elimu, afya na maji kwa baadhi ya mikoa ya Tanzania, tunaishukuru Japan kwa jitihada hizo ambazo zimechangia kuongeza maarifa na ujuzi kwenye jamii yetu” alisema Balozi Mbarouk 

Kadhalika, Balozi Mbarouk ameongeza kuwa biashara kati ya Tanzania na Japan imeendelea kuongezeka kutoka Dola za Kimaraekani milioni 30.9 mwaka 2021 hadi kufika Dola za Kimarekani milioni 89.1 mwaka 2022 na katika kipindi hicho, Tanzania iliagiza bidhaa zenye thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 469 hadi Dola za Kimarekani 521.6, na Kampuni za Japan zilizowekeza nchini Tanzania hadi kufika mwezi Augusti 2023 zimewekeza mtaji wenye thamani ya Dola za Kimarekani 7.58 na kutoa mamia ya ajira.

Kwa upande wake Balozi wa Japan nchini, Mhe. Yasushi Misawa alisema kuwa ushirikiano wa Japan na Tanzania ni wa kihistoria na umekuwa imara wakati wote na Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania kijamii, kisiasa na kiuchumi kwa manufaa ya pande zote mbili.

“Tunapoadhimisha siku hii muhimu ya Mfalme wa 126 Mhe. Emperor Naruhito tunakumbuka pia miaka 63 ya uhusiano kati ya Japan na Tanzania. Aidha, Balozi Misawa aliongeza kuwa Japan itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kukuza na kuendeleza ushirikiano wa miradi ya maendeleo kwa maslahi ya pande zote mbili,” alisema Balozi Misawa.

Balozi Misawa aliongeza kuwa hivi karibuni Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) imesaidia kufadhili baadhi ya miradi ya maendelo nchini Tanzania ikiwemo ujenzi wa barabara ya juu ya Mfugale (Mfugale Flyover) katika makutano ya barabara ya Tanzara, ujezi wa barabara mpya ya Bagamoyo na daraja la Gerezani. JICA pia imefadhili ujezi wa barabara ya Iringa – Shinyanga pamoja na miradi mingine mingi ikiwemo ya kujenga kituo cha kupoozea umeme cha Kinyerezi II.

Kadhalika, Balozi Misiwa ameongeza kuwa tangu mwaka 1989 Japan imekuwa ikitekeleza miradi mbalimbali Tanzania bara na Zanzibar ambapo miradi 400 yenye thamani ya Dola za Kimarekani milioni 30 imetekelezwa. Mwaka 2023 Ubalozi wa Japan ulikubali kufadhili shule nne za Sekondari na Msingi katika mikoa ya Dar es Salaam, Mbeya na Zanzibar.

Tanzania na Japan zinashirikiana katika sekta mbalimbali ikiwa ni pamoja na afya, biashara, viwanda, uwekezaji na utalii ambapo kwa pamoja zimekubaliana kuendeleza ushirikiano huo ili kuleta tija katika utekelezaji wa diplomasia ya uchumi wa pande zote mbili.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akitoa hotuba ya ufunguzi katika hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwa Mfalme wa 126 wa Japan Mhe. Emperor Naruhito ambaye ametimiza miaka 64 tarehe 22 Februari, 2024 jijini Dar es Salaam 

Balozi wa Japan nchini, Mhe. Yasushi Misawa akizungumza katika hafla ya kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwa Mfalme wa 126 wa Japan Mhe. Emperor Naruhito ambaye ametimiza miaka 64 tarehe 22 Februari, 2024 jijini Dar es Salaam