Thursday, February 28, 2019

Watumishi wa Mambo ya Nje wahimizwa kuzingatia sheria za utumishi wa umma


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizungumza kwenye kikao cha pili na Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hawapo pichani) Pamoja na mambo mengine amewataka Watumishi hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii, weledi na kuzingatia sheria, kanuni, taratibu na miongozo iliyopo. Kikao hicho kilifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano  wa Wizara uliopo Chuo Kikuu cha Dodoma hivi karibuni
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bibi Savera Kazaura akizungumza wakati wa kikao hicho
Sehemu ya Watumishi wa Wizara wakiwemo Wakuu wa Idara 
Balozi Mteule, Dkt. Mpoki Ulusubisya akitoa mada kuhusu afya kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hawapo pichani) wakati wa kikao kati yao na Katibu Mkuu wa Wizara. Pamoja na mambo mengine aliwashauri Watumishi kuwa na utratibu wa kupima afya zao mara kwa mara.
Sehemu ya Watumishi wa Wizara wakiwemo Wakuu wa Idara na Vitengo wakifuatilia mada
Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara

Sehemu nyingine ya Wakuu wa Idara na Vitengo

Wakuu wa Vitengo akifuatilia mkutano

Wakurugenzi wakiwa kwenye mkutano

Mkutano ukiendelea

Sehemu ya Watumishi wakifuatilia mkutano

Watumishi wakiwa kwenye mkutano

Mkutano ukiendelea

Sehemu nyingine ya Watumishi wakati wa mkutano

Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye mkutano na Katibu Mkuu.






Prof. Kabudi akutana na viongozi mbalimbali wakati wa kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la UN

Waziri wa Katiba na Sheria ambaye pia ni Kiongozi wa Ujumbe wa Tanzania katika Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (wa tatu kushoto) akizungumza na Kamishna wa Haki za Biandamu, Bi. Michelle Bachelet (mwenye miwani kulia) kuhusu masuala ya haki za binadamu. Wakati wa mazungumzo yao, Bi. Bachelet aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kupambana na rushwa, kupigia hatua za maendeleo ya kiuchumi, kuendelea kuwahifadhii wakimbizi na ushiriki katika ulinzi wa amani barani Afrika. Kwa upande wake, Prof. Kabudi alisema Tanzania itaendeea kulinda Haki za Binadamu kwa wananchi wote na kuahidi kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Kamishna huyo.
Mhe. Prof. Kabudi na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Bi. Michelet.
Mhe. Prof. Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Hassan Shire, Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi isiyo ya kiserikali ya Defenddeffenders mara baada ya mazungumzo kati yao. Pamoja na mambo mengine mazungumzo yao yalijikita kwenye masuala yanayohusu haki za binadamu ambapo, Mhe. Prof. Kabudi aliishauri taasisi hiyo ambayo inajishughulisha na masuala ya haki za binadamu  kujikita katika kufanya tafiti ili kuandaa taarifa za uhakika kuhusu nchi za Afrika ikiwemo Tanzania zinavyotekeleza haki za binadamu. 
Mhe. Prof. Kabudi ( wa tatu kushoto) na ujumbe wake wakiwa katika picha ya pamoja na Bw. Shire (wa nne kulia) na mjumbe aliyeongozana naye Bw. Nicolas Agostini (wa pili kulia) 

Rais Magufuli akutana na Makamu Rais Mtendaji wa JICA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa katika mazungumzo na Makamu wa Rais Mtendaji Mwandamizi wa Shirika la Kimataifa la Ushirikiano la Japan (JICA), Bw. Kazuhiko Koshikawa (wa tatu Kushoto) na ujumbe wake walipokutana  Ikulu jijini Dar es salaa leo Februari 28, 2019. Wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Damas Ndumbaro (Mb).
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimpa zawadi ya picha ya kuchora ya wanyama wakuu watano (Big Five)  Makamu wa Rais Mtendaji Mwandamizi wa Shirika la Kimataifa la Ushirikiano la Japan (JICA), Bw. Kazuhiko Koshikawa alipokutana na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaa leo Februari 28, 2019.
Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.  Dkt. Damas Ndumbaro (Mb).
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli akimpa zawadi ya kinyago cha UJAMAA  Makamu wa Rais Mtendaji Mwandamizi wa Shirika la Kimataifa la Ushirikiano la Japan (JICA), Bw. Kazuhiko Koshikawa alipokutana na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es Salaam leo Februari 28, 2019.
Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb)
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli katika picha ya pamoja na  Makamu wa Rais Mtendaji Mwandamizi wa Shirika la Kimataifa la Ushirikiano la Japan (JICA), Bw. Kazuhiko Koshikawa (wa tatu Kushoto) na ujumbe wake baada ya kukukutana na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Februari 28, 2019. Wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb).
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiagana na Makamu wa Rais Mtendaji Mwandamizi wa Shirika la Kimataifa la Ushirikiano la Japan (JICA) Bw. Kazuhiko Koshikawa (wa tatu Kushoto) na ujumbe wake baada ya kukukutana na kufanya naye mazungumzo Ikulu jijini Dar es salaam leo Februari 28, 2019. Wa pili kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb).


Wednesday, February 27, 2019

Serikali ya Awamu ya Tano kuendelea kulinda na kutetea Haki za Binadamu-Prof. Kabudi aliambia Baraza la Haki za Binadamu la UN


Waziri wa katiba na Sheria, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi akihutubia Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika jijini Geneva nchini Uswisi
Mhe. Prof. Kabudi alipata fursa pia ya kuzungumza na Kundi la Mabalozi kutoka nchi za Afrika waliopo Geneva kama anavyoonekana pichani
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi (wa nne kulia) akiwa katika picha  ya pamoja na baadhi ya maafisa wa Tanzania mara baada ya kuhutubia kikao hicho cha Baraza la Haki za Bianadamu kinachofanyika Geneva, Uswisi.

=====================================================


Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi amesema Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kutekeleza wajibu wake wa kukuza na kulinda haki za binadamu na ustawi wa jamii kama kipaumbele chake na  itaendelea kushirikiana na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuhakikisha haki za binadamu nchini na duniani kote zinadumishwa.

Prof. Kabudi amesema hayo jana alipohutubia Kikao cha 40 cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kinachofanyika jijini Geneva nchini Uswisi. Prof. Kabudi amesema Serikali ya Tanzania imelenga pamoja na mambo mengine kuimarisha haki za binadamu, utawala bora na utii wa sheria nchini na kuondoa ukatili dhidi ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu. 


Serikali imelenga kuimarisha haki za binadamu, utawala bora, utii wa sheria na kuondoa ukatili dhidi ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu, kwa sasa tunatekeleza mpango mkakati wa kitaifa wa kuondoa ukatili dhidi ya wanawake na watoto wa mwaka 2017/18 - 2021/22, lengo likiwa ni kulinda na kudumisha haki za wanawake, watoto na watu wenye ulemavu,” alisema Prof. Kabudi.

Amesema Serikali pia inazingatia suala la kuwapatia haki kwa haraka wananchi wasio na uwezo kwa kutolea maamuzi kwa haraka mashauri yanayowahusu watu wasio na uwezo na kuwapatia msaada wa kisheria kupitia utekelezaji wa Sheria ya Msaada wa Kisheria ya mwaka 2017 ili wananchi hao waweze kupata haki zao kwa wakati. 

Aidha, Prof. Kabudi amelihakikishia Baraza hilo kuwa Serikali inatambua kazi kubwa inayofanywa na vyombo vya habari nchini na imeendelea kuhakikisha uhuru wa vyombo hivyo unalindwa huku jumla ya vituo vya redio 152, televisheni 34, magazeti 172  nchini kote yamesajiliwa na kuongeza kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira stahiki yatakayowezesha vyombo vya habari kufanya kazi zao kwa uhuru.

Ameongeza kuwa Serikali imedhamiria kuleta ustawi wa jamii kwa kutekeleza mipango mbalimbali ya maendeleo ikiongozwa na Dira ya Maendeleo ya Taifa ya mwaka 2025 na kunadi kuwa Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha kuwa haki ya kupata elimu, afya na maji zinawafikia wananchi wote. 

“Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha kuwa haki ya kupata elimu, afya na maji zinawafikia wananchi wote na kuongeza kuwa Serikali inatumia zaidi ya Shilingi Bilioni 23 kwa mwezi kutoa elimu pasipo malipo na hivyo kuongeza udahili wa watoto wanaojiunga darasa la kwanza kwa asilimia 35.2 na asilimia 20.1 kwa wanaojiunga na kidato cha kwanza,” alisema. 

Prof. Kabudi pia amesema Serikali imedhamiria kufikisha huduma za afya karibu na watanzania wote ambapo imeongeza bajeti ya afya kutoka Shilingi bilioni 31 mwaka 2015/2016 hadi Shilingi bilioni 269 mwaka 2017/2018 na kuongeza kuwa Serikali inatekeleza mikakati ya kujenga vituo vya afya ambapo hadi sasa imejenga vituo 304, na nyumba za watumishi wa afya 578 zimejengwa nchini kote.

Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa ni chombo cha Umoja wa Mataifa chenye jukumu la kukuza na kulinda haki za binadamu duniani kote na kushughulikia uvunjwaji wa haki za binadamu unaotokea katika nchi wanachama wa umoja huo na kushauri hatua za kuchukuliwa ili kuboresha haki za binadamu duniani. 

Baraza hilo pamoja na mambo mengine linatarajia kupokea taarifa mbalimbali kuhusu haki za binadamu duniani na kutoa nafasi kwa viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa kutoa maelezo yao kuhusu utekelezaji wa wajibu wao wa kulinda na kukuza haki za biandamu katika nchi zao.


Tuesday, February 26, 2019

Finland yaipongeza Tanzania vita dhidi ya Rushwa.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Finland yaipongeza Tanzania vita dhidi ya Rushwa.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Timo Soini.amepongeza jitihada zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli za kupambana na rushwa na kusimamia uwajibikaji.

Pongezi hizo alizitoa wakati alipofanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga ambaye yupo nchini Finland kwa ziara ya kikazi ya siku mbili tarehe 25 na 26 Februari 2019.

Kwenye mazungumzo yao, Mawaziri hao wamesisitiza umuhimu wa Tanzania na Finland kuboresha ushirikiano kwenye sekta mbalimbali zikiwemo za biashara, uwekezaji, mafunzo ya ufundi, ajira kupitia sekta ya misitu, ushirikiano katika majukwaa ya kimataifa kwa kuzingatia usawa, pamoja na kuwajengea uwezo wanawake na watoto.

Aidha, Mhe. Soini  alitoa shukrani zake za dhati kwa Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kuhifadhi wakimbizi na mchango mkubwa katika usuluhishi wa migogoro inayozikabili baadhi ya nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu. Hivyo, walikubaliana kuendelea kushirikiana katika kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiusalama ikiwa ni pamoja na biashara ya madawa ya kulevya, biashara haramu ya kusafirisha binadamu, na matishio ya ugaidi.

Kabla ya mazungumzo hayo, Mhe. Balozi Mahiga alikutana na kufanya mazungumzo na Bw. Sampo Suihko, Mkurugenzi Mkuu wa Chuo cha OMNIA Espoo ambaye alieleza utayari wa Taasisi yake wa kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kubadilishana uzoefu wa kutoa mafunzo ya elimu ya ufundi yanayoendana na soko la ajira.

Mhe. Mahiga pia alifanya mazungumzo na Mhe. Matti Ahtisaari, Rais Mstaafu wa Finland na Mwanzilishi wa Taasisi ya Utatuzi wa Migogoro. Mhe. Ahtisaari aliipongeza Tanzania kwa kazi nzuri inayofanya katika utatuzi wa migogoro kwenye nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu na kusihi kuendeleza jitihada hizo kwa ustawi wa Dunia nzima.

Vilevile, Dkt. Mahiga alifanya mazungumzo na Bw. Jukka Kallio, Makamu wa Rais wa Helsinki. Katika mazungumzo hayo, uongozi wa Bandari ya Vuosaari umeahidi kushirikiana na uongozi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania katika kuboresha mifumo ya kidigitali (Digitalization) itakayoongeza ufanisi wa Bandari ya Dar es Salaam.

Katika kuhamasisha uwekezaji wa viwanda nchini, Mhe. Waziri Mahiga alifanya mazungumzo na Jumuiya ya Wafanyabiashara (Business Finland) na Makampuni makubwa ya kibiashara nchini humo. Wafanyabiasha hao walipongeza jitihada zinazoendelea kufanyika nchini Tanzania katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji na  waliahidi kuwekeza na kushawishi makampuni mengine kuona umuhimu wa kuwekeza nchini Tanzania.

Mhe. Waziri anahitimisha ziara hiyo kwa kufanya mazungumzo na Bi. Anne-Mari Virolainen, Waziri wa Biashara na Maendeleo wa Finland; Bw. Mauri Pekkarinen, Naibu Spika wa Bunge la Finland, Bw. Juhan Damski, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi  ya Utabiri wa Hali ya Hewa ya nchini Finland na baadaye kuzungumza na Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge la Finland.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
26 Februari 2019

Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland, Mhe. Timo Soini (kulia) akimkaribisha ofisini kwake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga. Dkt. Mahiga yupo nchini Finland kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.

Waziri Mahiga na ujumbe wake (kushoto) ukiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Finland na ujumbe wake.


Friday, February 22, 2019

Tanzania na Ufaransa ushirikiano wazidi kuimarika

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania na Ufaransa ushirikiano wazidi kuimarika

Tanzania na Ufaransa  zimeahidi kuimarisha ushirikiano wa kimaendeleo; kuongeza uwekezaji na biashara; na kutafuta ufumbuzi wa migogoro inayozikabili nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu, Ukanda wa Bahari ya Hindi na changamoto nyingine za kiusalama katika maeneo hayo.

Ahadi hiyo ilitolewa na Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi hizo jijini Paris leo walipokutana kwa ajili ya mazungumzo. Mhe. Dkt. Augustine Mahiga, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki yupo nchini Ufaransa kwa ziara ya kikazi siku siku mbili 21 na 22 Februari 2019 kufuatia mwaliko wa Waziri wa Ulaya na Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mhe. Jean- Yves Le Drian ambaye ameahidi pia kufanya ziara ya kikazi nchini Tanzania hivi karibuni.
Kabla ya mazungumzo hayo, Mheshimiwa Balozi Mahiga alikutana na kufanya mazungumzo na kundi la Maseneta wa Ufaransa ambao ni marafiki wa Tanzania wakiongozwa na Seneta Ronan Dantec ambaye ni Mwenyekiti wa Maseneta hao. Maseneta hao walipendekeza kuanzishwa kwa ushirikiano dada kati ya jiji la Paris na Dodoma. Ushirikiano huo ujikite zaidi katika matumizi bora ya ardhi, mipango miji na kutekeleza miradi mbalimbali ya kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi.

Vilevile, Maseneta hao wameelezea dhamira  yao ya kutaka kushirikiana na Serikali ya Tanzania kuibua vipaji vya mchezo wa mpira wa miguu katika shule mbalimbali nchini.

Wakati huo huo, Mhe. Mahiga alifanya mazungumzo na Bibi Marie Audouard, Naibu Mshauri wa Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa anayeshughulikia masuala ya Afrika. Katika mazungumzo yao, Bibi Audouard aliainisha maeneo ya kipaumbele ya Mhe. Rais Emmanuel Macron katika mahusiano yake na nchi za Afrika. Vipaumbele hivyo ni pamoja na kuimarisha zaidi mahusiano na nchi zinazoongea lugha ya kiingereza na kireno; kuendelea kushirikiana katika usuluhishi wa migogoro ya kikanda na kimataifa; kuhamasisha sekta binafsi ya Ufaransa kwenda kuwekeza Afrika; na  kubadilishana uzoefu katika nyanja za utamaduni hasa kwa vijana.
Viongozi wengine aliofanya nao mazungumzo Mhe. Waziri ni pamoja na Bibi Audrey Azoulay, Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO; na Bw. Bertrand Walckenaer, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Ufaransa (AFD).
Katika mazungumzo na Mkurugenzi wa UNESCO, Waziri Mahiga alilishukuru Shirika hilo kwa kuwa mshirika wa Tanzania kwa miaka mingi kwenye masuala ya elimu, sayansi na utamaduni na kuahidi kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana katika masuala mbalimbali yanayohusu elimu, sayansi na utamaduni.
Kwa upande wa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa AFD, Mkurugenzi huyo alieleza kuwa, kutokana na ushirikiano mzuri uliopo wameongeza mara mbili kiwango cha fedha za maendeleo nchini Tanzania ambazo zitatumika kufadhili miradi katika sekta za uchukuzi, nishati, maji safi na taka, kilimo, afya na mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Waziri anahitimisha ziara yake leo kwa kukutana na Jumuiya ya Wawekezaji na wafanyabiashara wa Ufaransa (MEDEF) na Bi. Luise Mushikiwabo, Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya nchi zinazozungumza Kifaransa (IOF).

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
22 Februari 2019

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akipokelewa na mwenyeji wake, Waziri wa Ulaya na Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mhe. Jean- Yves Le Drian jijini Paris. Dkt. Mahiga yupo nchini Ufaransa kwa ziara ya siku mbili tarehe 21 na 22 Februari 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri wa Ulaya na Mambo ya Nje wa Ufaransa, Mhe. Jean- Yves Le Drian




Thursday, February 21, 2019

Tanzania na Umoja wa Ulaya waazimia kuimarisha Uhusiano

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania na Umoja wa Ulaya waazimia kuimarisha Uhusiano

Tanzania na Umoja wa Ulaya (EU) wamekubaliana kuimarisha uhusiano na ushirikiano kwa kufanya majadiliano ya mara kwa mara yatakayojengwa katika misingi ya kuaminiana, usawa, uwazi na kuheshimiana ili kujenga uelewa wa pamoja katika maeneo mbali mbali yenye changamoto kwa manufaa  mapana ya watu wa pande zote mbili.

Makubaliano hayo yamefikiwa wakati wa mazungumzo kati ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb) na Mkurugenzi wa Idara ya Pembe ya Afrika na Afrika Mashariki, Huduma za Nje katika Umoja wa Ulaya, Bw. Patrick Simonnet wakati wa ziara yake iliyofanyika nchini kuanzia tarehe 17 hadi 20 Februari 2019.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Waziri aliushukuru Umoja wa Ulaya kwa misaada ambayo umekuwa ukiipatia Tanzania kwa ajili ya utekelezji wa miradi mbalimbali ya maendelea katika sekta za kilimo, nishati na ujenzi wa miundombinu ya barabara na viwanja vya ndege. “Umoja wa Ulaya ni mbia muhimu wa Tanzania katika shuguli za maendeleo tokea mahusiano rasmi ya kidiplomasia yalipoanzishwa mwaka 1975; baada ya kusainiwa kwa mkataba wa kwanza wa Rome baina ya kundi la nchi za Afrika, Caribbean na Pasifiki (ACP) na nchi wanachaama wa Umoja wa Ulaya”; alisema Mhe. Mahiga.

Viongozi hao walihitimisha mazungumzo yao kwa kuazimia kuendelea kuimarisha ushirikiano uliopo baina ya pande mbili hizi katika maeneo mbalimbali ikiwa ni pamoja na biashara, uwekezaji, ushirikiano wa maendeleo na usalama wa majini, hususan katika pwani ya Bahari ya Hindi. 
Aidha, walikubaliana kuimarisha ushirikiano katika nyanja za kimataiafa ikiwa ni pamoja na kusaidia juhudi za kudumisha na kuimarisha hali ya amani, usalama na utulivu katika eneo la Maziwa Makuu.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma.
21 Februari 2019


Tuesday, February 19, 2019

Wanadiaspora wa Saudia wapigwa msasa Uhamiaji mtandao

 Jumuiya ya Watanzania waishio Jeddah nchini Saudi Arabia “Tanzania Welfare Society” hivi karibuni ilifanya Mkutano wa pamoja wa wanajumuiya Watanzania na Wanadiaspora. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Mgaza.

Wanajumuiya walipata fursa ya kujadiliana mambo mbalimbali yakiwemo uwekezaji na uchumi, ajira nchini Saudi Arabia, masomo nchini Saudi Arabia. Aidha, wanajumuiya walipata maelezo kuhusu matumizi ya mfumo mpya uhamiaji mtandao “e-immigration” ambapo walifahamishwa na kutakiwa kuanza rasmi kuomba pasi mpya za kusafiria za ki-electronic, hati za dharura za kusafiria za ki-electronic.  Pia wanajumuiya walitakiwa kuwahamasisha wageni kutembelea Tanzania kwa shughuli za utalii, uwekezaji na biashara, na pia sasa wanaweza kuomba viza za kuingia Tanzania kwa njia ya mtandao “e-visa”. 

Wanajumuiya walisisitizwa kuwa na umoja na uzalendo kwa Tanzania. Walitakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha wanachangia maendeleo ya Tanzania

Kutoka Kushoto  Afisa Utawala wa Konseli Kuu ya Jeddah Ali Mohamed, Makamu wa Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania waishio Jeddah, Bw. Salim Ali Shatri, Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Hemedi Mgaza akihutubia, kujibu maswali na kutoa ufafanuzi, mwisho kulia ni Mweka Hazina wa Jumuiya ya Watanzania ya Jeddah, Bw. Abdallah Faris.
Watanzania na Wanadiaspora wa Jeddah wakiwa mkutanoni.
Watanzania na Wanadiaspora wa Jeddah wakisikiliza hotuba katika hoteli ya Trident Jeddah.

Watanzania na Wanadiaspora wa Jeddah wakipata chakula
Wanajumuiya wakipata chakula

Friday, February 15, 2019

Re-advertisement for the post of Director of Internal Oversight



PRESS RELEASE

Re-advertisement for the post of Director of Internal Oversight 

The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received a note from the Secretariat of the Organization for the Prohibition of Chemical Weapons (OPCW) expressing that, it has extended closing date for the post of Director, Office of Internal Oversight, D-2 from 6th February 2019 to 20th February 2019.

Interested candidates are advised to make applications online through the Organization’s website www.opcw.org

Female applicants are highly encouraged.



Issued by;
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dodoma.
15th February 2019.

Naibu Waziri atembelea Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Damas Daniel Ndumbaro (Mb.) akizungumza na Watumishi wa Ofisi ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Zanzibar alipofanya ziara kwenye Ofisi hiyo ikiwa ni miongoni mwa ziara zake za kuzitembelea Taasisi za Wizara zilizopo nje ya Dodoma. Katika mkutano wake na Watumishi hao, Mhe. Naibu Waziri aliwataka  kuanzisha mazungumzo ya pamoja kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Wizara katika vikao vitakavyofanyika kwa zamu baina ya Zanzibar na Dodoma ili kukuza ufanisi wa Wizara kwa ujumla. Wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar, Balozi Mohammed H. Hamza. Ziara hiyo imefanyika tarehe 15 Februari 2019.
Balozi Hamza akizungumza na kumkaribisha Mhe. Dkt. Ndumbaro kwenye Ofisi za Mambo ya Nje Zanzibar ambapo pia alimweleza mafanikio ya Ofisi hiyo yaliyopatikana katika utekelezaji wa majukumu ya kuratibu masuala ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa upande wa Zanzibar.
Bw. Suleiman M. Mohammed, ambaye ni Mhasibu kwenye Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar akizungumza wakati wa ziara ya Naibu Waziri
Mhe. Dkt. Ndumbaro akimsikiliza Bw. Iddi Seif Bakari, Afisa Mambo ya Nje alipokuwa akieleza changamoto mbalimbali zinazowakabili Watumishi kwenye Ofisi hiyo
Bi. Asia Hamdani, Afisa Tawala kwenye Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar nae akizungumza kwenye mkutano kati ya Watumishi wa Ofisi hiyo na Mhe. Naibu Waziri
Mtumishi mwingine ambaye ni Afisa Mambo ya Nje kwenye Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar, Bw. Salim R. Haji akichangia jambao wakati wa mkutano kati ya Watumishi wa Ofisi ya Mambo ya Nje Zanzibar na Naibu Waziri.