Thursday, September 30, 2021

UFAFANUZI KUHUSU MAGARI YA MIZIGO YA TANZANIA YALIYOKWAMA NCHINI MALAWI


 

TANGAZO LA NAFASI YA KAZI KATIKA KAMISHENI YA UMOJA WA AFRIKA


 

WAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS WA MAKAMPUNI YA THE PULA GROUP JIJINI DAR

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Makampuni ya The Pula Group Dkt. Mary Stith katika ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam

Kampuni ya The Pula Group ni Kampuni ya Kimarekani inayojishughulisha na uchimbaji wa madini ya risasi (graphite) hapa nchini ambayo ni moja ya malighafi muhimu katika uzalishaji wa betri. Pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili masuala mbalimbali muhimu katika kutangaza fursa kwa lengo la kuvutia wawekezaji wengi zaidi katika sekta hiyo. 

Akizungumza baada ya mkutano huo Dkt. Mary ameeleza sambamba na kumshirikisha Waziri Mulamula kuhusu mchango na nafasi ya Kampuni yake katika kutangaza fursa za uwekezaji zinazopatikana nchini hasa kwenye sekta ya madini pia ametumia fursa hiyo kujifunza na kupata uzoefu wa masuala mengi kuhusu Wanawake na Uongozi kutoka kwa Waziri Mulamula.

“Wakati huu ambao Dunia inakabiliana na adhari za madiliko ya Tabianchi, mahitaji ya madini ya ghraphite ambayo ni muhimu katika uzalishaji wa nishati ya umeme yameendelea kuongezeka Duniani kwa sababu ni rafiki kwa mazingira, nafarijika kuona Tanzania ikiwa na kiasi kikubwa cha hifadhi ya madini haya yenye viwango vya kimataifa” Amesema Dkt. Mary. 

Aidha Waziri Mulamula kwa upande wake amemwakikishia Dkt. Mary kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya uongozi madhubuti wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji nchini sambamba na kudumisha ulinzi na usalama. 

Kampuni ya The Pula Group ilianza kuendesha shughuli za utafutaji na uchimbaji wa madini ya graphite nchini mwaka 2014. 


Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula amekutana na kufanyamazungumzo na Balozi Mteule Prof. Adelardus Kilangi katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam. Prof. Adelardus Kilangi aliteuliwa kuwa Balozi Septemba 12, 2021.


Katika tukio jingine Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula ameshiriki Sherehe ya Maadhimisho ya Miaka 60 ya Peace Corps Tanzania yaliyofanyika kwenye viunga vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam. Maadhimisho hayo yaliongozwa na kauli mbiu “Miaka Sitini ya Huduma na Urafiki”. 

Akizungumza katika Maadhimisho hayo Waziri Mulamula ameeleza kuwa Tanzania ina thamini sana jitihada na mchango wa Marekani katika maendeleo ya Kijamii na Kiuchumi kwenye maeneo mabalimbali hapa nchini ikiwemo; afya, elimu, miundombinu, maji, teknolojia ya habari na mawasiliano, kuimarisha demokrasia, haki za binadamu, utawala wa sheria na utawala bora.

Waziri Mulamula aliongeza kusema wakati huu ambao nchi hizi mbili zinasherekea Maadhimisho ya Miaka Sitini ya Huduma na Urafiki, ni fursa nyingine ya kutafakari mafanikio yaliyopatikana kutokana na ushirikiano wetu ambayo ni chachu katika kudumisha na kuimarisha ushirikiano wa karibu zaidi baina ya Nchi hizi mbili rafiki. Aidha, Waziri Mulamula amewashukuru Raia wa Marekani ambao kwa muda mrefu wamejitolea kufanya kazi bila kuchoka katika maeneo mbalimbali ya vijijini nchini wakishirikiana na Washirika wa ndani ikiwemo kufundisha hesabu na sayansi katika shule za upili, wakufunzi wa walimu katika teknolojia ya habari na mawasiliano na sekta ya afya.

“Nitumie fursa hii kusisitiza kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Marekani na itaendelea kufanya kazi kwa ukaribu na Peace Corps Tanzania katika kuleta maendeleo endelevu kwa Nchi yetu”. Alisema Waziri Mulamula.

Peace Corps Tanzania ni Taasisi ya Kimarekani inayochangia nguvu kazi katika shughuli 

mbalimbali za maendeleo ya Kijamii na Uchumi kwa kujitolea. Kazi na majukumu ya Peace Corps Tanzaniayanaongozwa na Mkataba uliosainiwa kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Marekani Januari 9, 1979.

Maadhimisho hayo pamoja na washiriki wengine yalihudhuriwa na Mhe. Dr. Donald Wright Balozi wa Marekani nchini Tanzania na Bi. Stephanie Joseph de Goes Mkurugenzi Mkazi wa Peace Corps Tanzania

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Peace Corps Tanzaniayaliyofanyika kwenye viunga vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Dr. Donald Wright alipowasili kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Peace Corps Tanzania yaliyofanyika kwenye viunga vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Balozi Mteule Prof. Adelardus Kilangi akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Balozi Mteule Prof. Adelardus Kilangi akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kufanya mazungumzo na Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula na Balozi Mteule Prof. Adelardus Kilangi wakiwa katika mazungumzo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (katikati), Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Dr. Donald Wright (kulia) na Mkurugenzi Mkazi wa Peace Corps Tanzania Bi. Stephanie Joseph de Goes (kushoto) wakiwa wamesimama wakati Wimbo wa Taifa la Tanzania na Marekani unaimbwa. 
Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Dr. Donald Wright akizungumza kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Peace Corps Tanzania yaliyofanyika kwenye viunga vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkaazi wa Peace Corps Tanzania Bi. Stephanie Joseph de Goes akizungumza kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Peace Corps Tanzania yaliyofanyika kwenye viunga vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula, Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mhe. Dr. Donald Wright na Mkurugenzi Mkazi wa Peace Corps Tanzania Bi. Stephanie Joseph de Goes wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi wa Marekani na Peace Corps Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula na Rais wa Makampuni ya The Pula Group Dkt. Mary Stith wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika kwenye Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Rais wa Makampuni ya The Pula Group”Dkt. Mary Stith yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Muzungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akizungumza kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Peace Corps Tanzaniayaliyofanyika kwenye viunga vya Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam.

Tuesday, September 28, 2021

WAZIRI MULAMULA AZINDUA MASHINDANO YA KIMATAIFA YA BAISKELI TANZANIA JIJINI DAR


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) leo Septemba 28, 2021 amezindua Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania (Tanzania International Cycle Tour) jijini Dar es Salaam. Mashindano haya ambayo yatafanyika sambamba na Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania yanalenga kutambua mchango wa Tanzania katika kupigania Ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika na kusherekea mafanikio yaliyofikiwa na Tanzania katika demokrasia, amani na utulivu wakisiasa tokea kupata Uhuru kiasi cha kuwa mfano wa kuigwa katika barani Afrika.

Akizungumza katika ufunguzi wa mashindano hayo Waziri Mulamula ameeleza imani yake kuwa kupitia mashindano hayo yakipekee ujumbe wa Mshikamano na Umoja ambao unabeba dhana nzima ya Maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru utawafikia watu wengi zaidi. Aidha ametumia nafasi hiyo kutoa Wito kwa Taasisi zingine kutoka Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki kuiga jambo lililofanywa na waandaaji wa Shindano hili ambao ni Taasisi ya Afrika Mashariki Fest na Taasisi ya Utalii wa Utamaduni Butiama. 

“Tunaamini pia baada ya mashindano haya mtakuwa mabalozi wazuri wa Tanzania kwa kuwa mkiwa huko njiani wakati wa mashindano mnaenda kujionea mabaliko makubwa ya maendeleo kijamii na kiuchumi na mafanikio makubwa yaliyofikiwa na Nchi yetu katika nyanja mbalimbali” alieleza Waziri Mulamula


Mheshimiwa Tabia Maulid Mwita Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar akizungumza katika ufunguzi huo amesema, amefarijika sana namna vijana kutoka nchini, Jumuiya Afrika Mashariki na nchi nyingine nje ya Jumuiya walivyohamasika kushiriki katika Mashindano haya. Aliendelea kueleza hiki ni kielelezo tosha kuwa vijana wanatambua na kudhamini uhuru wao sambamba na kudhamini jitihada zinazofanywa na Serikali yao katika kuleta maendeleo. 

Kwa upande wake Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Taasisi ya Utalii wa Utamaduni Butiama Bw. Godfrey Madaraka Nyerere ameeleza kuwa pamoja na mambo mengine mashindano haya yanaenda kuionesha dunia hatua kubwa ya maendeleo iliyofikiwa nchini katika ujenzi wa miundiumbinu ya uchukuzi hivyo kuleta mchango mkubwa katika kutangaza Utalii sambamba na kuvutia Uwekezaji kutoka Nje. 

Katika hafla hiyo ya ufunguzi wa Mashindano pamoja na washiriki wengine yalihudhuriwa na Mhe. Tabia Maulid Mwita Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mabalozi na Wanadiplomasia kutoka Nchi Wanachama wa Afrika Mashariki wanaoziwakilisha Nchi zao hapa nchini, Bw. Kisembo Ronex Tendo Mtendaji Mkuu wa Afrika Mashariki Fest kutoka nchini Uganda na Bw. Godfrey Madaraka Nyerere Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Taasisi ya Utalii wa Utamaduni Butiama.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akihutubia kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akifuatilia ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisisitiza jambo kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akihutubia kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mheshimiwa Tabia Maulid Mwita (Mb) akihutubia kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Taasisi ya Utalii wa Utamaduni Butiama Bw. Godfrey Madaraka akizungumza kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam
Wimbo wa Taifa ukipigwa kabla ya ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Afrika Mashariki Fest kutoka nchini Uganda Bw. Kisembo Ronex Tendo akizungumza kwenye ufunguzi wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mheshimiwa Balozi Liberata Mulamula (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya waandaaji wa Mashindano ya Kimataifa ya Baiskeli Tanzania.

WATAALAMU WAKUTANA KUJADILI MRADI WA KUFUA UMEME MURONGO/KIKAGATI

 Na Mwandishi Wetu, Bukoba

Timu ya wataalamu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekutana na kujadiLi utekelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Murongo/Kikagati uliopo katika mto Kagera mpakani mwa Tanzania na Uganda.

Mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu ngazi ya Wataalamu kuhusu mradi wa kufua umeme wa Murongo/Kikagati umefanyika Mjini Bukoba kuanzia tarehe 28 – 30 Septemba, 2021 ambapo pamoja na mambo mengine, wataalamu wamepata fursa ya kujadili mambo mbalimbali kuhusu utekelezaji wa mradi huo.

Inategemewa kuwa mara baada ya kukamilika kwa mradi huo, utazalisha megawatts 14, na kila nchi itapata megawatts saba. Aidha, Mkutano wa Kitaifa wa Mkatibu Wakuu kwa ngazi ya Wataalamu, utafuatiwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 01 Oktoba 2021.  

Akiongelea kuhusu Mkutano wa Kitaifa wa Mkatibu Wakuu Ngazi ya Wataalamu, Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Kijamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota amesema lengo la Mkutano huo ni kujadili mambo mbalimbali ikiwa ni mafanikio na changamoto zinazo ukabili mradi kwa sasa. Aidha, Mkutano wa ngazi ya Wataalamu ni utekelezaji wa maagizo ya Mkutano wa 13 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Nishati la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika mwezi Novemba 2018.

Ujenzi wa Mradi huo ni makubaliano ya nchi mbili za Tanzania na Uganda ya matumizi bora ya maji ya mto Kagera ambao upo mpakani mwa nchi hizo. Mradi huo unatekelezwa/kujengwa na Kampuni binafsi ya Kikagati Power Company Limited (KPCL).

Awali ujenzi wa mradi huo wenye gharama ya dola milioni 95 ulianza Mei 2018 na sasa unatarajiwa kukamilika Oktoba 2021.

Kaimu Mkurugenzi wa Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Kijamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akiwasilisha mada katika mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu, ngazi ya Wataalamu kuhusu Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kikagati leo Mjini Bukoba


Kamishna Msaidizi wa Umeme na Nishati Jadidifu kutoka Wizara ya Nishati, Mhandisi Edward Ishengoma akieleza jambo kwa Wataalamu wakati wa mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu ngazi ya Wataalamu kuhusu Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kikagati leo Mjini Bukoba


Mhandisi Neema Rushema kutoka Wizara ya Nishati akiongea na Wataalamu katika Mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu ngazi ya Wataalamu kuhusu Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kikagati


Mhandisi Mgeta Sabe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akifafanua jambo katika Mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu ngazi ya Wataalamu kuhusu Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kikagati

Sehemu ya Wajumbe wakifuatilia Mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu ngazi ya Wataalamu kuhusu Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kikagati ukiendelea 


Mkutano wa Kitaifa wa Makatibu Wakuu ngazi ya Wataalamu kuhusu Mradi wa kufua Umeme wa Murongo/Kikagati ukiendelea