Friday, December 29, 2017

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Uturuki nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea Nakala za Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Mteule wa Jamhuri ya Uturuki nchini, Mhe.Ali Dovutoglu. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Desemba 2017.
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Dovitoglu ambapo alimuhakikishia kumpa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yake pamoja na kumpongeza kwa kuteuliwa kwake kwa awamu nyingine kuiwakilisha Jamhuri ya Uturuki nchini.

Waziri Mahiga akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini, Mhe. Song Geum - Young alipomtembelea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 29 Desemba 2017.
Mazungumzo yao yalijikita katika kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia uliopo baina ya mataifa hayo, kuanzisha maeneo mapya ya ushirikiano sambamba na hali halisi ya utekelezaji wa  miradi ya maendeleo inayotekeleza kwa ushirikiano baina ya Tanzania na Korea.

Mhe. Waziri Mahiga akielekezana jambo na Mhe. Song Geum-Young.
Mhe.Waziri Mahiga akiagana na Mhe Song Geum-Young.



Thursday, December 21, 2017

Dkt. Mahiga ahutubia Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China

Wziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Mkuu wa Chuo cha Mambo ya Nje cha China kabla ya wawili hao hawajaelekea kwenye ukumbi kuhutubia wanafunzi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augastine Mahiga akihutubia wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China. Dkt. Mahiga alieleza ushirikiano wa Tanzania na China ulipoanza hadi leo na kuwasihi wanafunzi hao waangalie namna y kuuimarisha kutokana na nafasi zao.

Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China wakisikiliza Hotuba ya Dkt. Mahiga. Wanafunzi hao ambao walikuwa wadadisi sana walifurahi sana kutokana na elimu ya siku moja waliopata kutoka kwa Mbobezi wa masuala ya Diplomasia.

Dkt. Mahiga akiendelea na hotuba yake huku Mkuu wa Chuo akisikiliza kwa makini. Mkuu huyo alikiri kuwa kutokana na hotuba hiyo amejifunza vitu vingi sana.

Ujumbe uliomsindikiza Waziri Mahiga, kutoka kulia ni Bw. Benedict Msuya, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje, Bw. Gerald Mbwafu, Katibu wa Waziri na Kanali Remigius Ng'umbi, Mwambata Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.

Mstari wa Mbele kutoka kushoto ni Kamishna msaidizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Malmeltha Mtagwaba, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Thomas Kashililah, Naibu Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Vwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchweishaija, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha wa Zanzibar, Bw. Khams Omar na Balozi wa Tnzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki wakifuatilia hotuba hiyo.

Mmoja wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mambo ya Nje cha China akiuliza sawali kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga.

Picha ya Pamoja.


 Ziara katika kampuni ya magari ya Foton Motors Group


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisikiliza maelezo kutoka kwa mmoja wa viongozi wa kampuni ya Foton Motors Group kabla ya kuanza kutembelea kampuni hiyo kujionea shughuli zake.

Baadhi ya aina ya magari yanayotengenezwa na kampuni ya Foton Motors Group.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa ndani ya moja ya magari yanayotengenezwa na kampuni ya Foton Motors Group.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa ndani ya karakana ya Foton Motors Group kuangalia shughuli za uzalishaji wa magari zinavyofanyika.

Baada ya kuona shughuli za kampuni hiyo, Waziri Mahiga alifanya mazungumzo rasmi na viongozi wa kampuni hiyo ambapo walimuomba awasaidie ili waweze kuwekeza nchini Tanzania. Kampuni hiyo inataka kufungua kiwanda cha kuunganisha magari yao kwa lengo la kuuza Tnzania na soko la Afrika. Walisema kampuni yao inatengeneza magari ya aina yote makubwa, madogo, mabasi na malori ndio inayoongoza kwa mauzo nchini China kwa kipindi cha miaka 13 sasa.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akipokea zawadi ya mfano wa moja ya magari yanayotengenezwa na kampuni ya Foton Motors Group.

Mazungumzo na Makamu wa Rais wa Kampuni ya China Merchant

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiwa katika mazungumzo na Makamu wa Rais wa Kampuni ya China Merchant inayowekeza kwenye mradi wa Bandari ya Bagamoyo. Makamu wa Rais huyo pamoja na mambo mengine alielezea kufurahishwa kwake na uamuzi wa Serikali kuidhinisha rasmi utekelezaji wa mradi huo.

Tuesday, December 19, 2017

China yaunga mkono juhudi za Rais Magufuli.



 Na Mwandishi Maalum, Beijing

China imeahidi kushirikiana na Tanzania kikamilifu katika miradi ya kipaumbele ambayo Serikali ya AwamuyaTano imepanga kuitekeleza ili kufikia azma yake ya uchumi wa viwanda ifikapo 2020 na baadaye uchumi wa Kati ifikapo 2025.

Hayo yalibainishwa leo jijini Beijing  na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming na baadaye kukaririwa tena na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipango (NDRC), Bw. Ning Jizhe walipofanya mazungumzo kwa nyakati tofauti na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga.

Katika mazungumzo hayo, Balozi Mahiga aliainisha na kufafanua namna Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Dkt. John Pombe Maguful iilivyokusudia kuwashirikisha wadau mbalimbali kwenye utekelezaji wa miradi ya kipaumbele ambayo inalenga kuchochea agenda ya uchumi wa viwanda. 

Miradi hiyo ni pamoja na kuendeleza nishati ya umeme ambapo Serikali imedhamiria kuzalisha umeme wa megawatts 5000 ifikapo mwaka 2020 ili kuharakisha utekelezaji wa agenda ya uchumi wa viwanda ambayo haitaweza kufanikiwa kama hakutakuwa na umeme wa kutosha na wauhakika.
Kutokana na uhalisia huo, Serikali imepanga kujenga kituo cha kuzalisha umeme wa megawatts 2100 kwenye mto Rufiji na kujenga njia za kusambaza umeme huo kutoka Rufiji, Chalinze hadi Dodoma na nyingine kutokaChalinze, Kilimanjaro hadi Arusha. 

Miradi mingine ni ujenzi wa mtandao wa usafiri wa reli na uboreshaji wa reli ya TAZARA, ujenzi wa bandari ya Bagamoyo na viwanja vya ndege ikiwa ni pamoja na kujenga jengo  la abiria katika Kiwanja cha ndege cha Mwanza.
Waziri Mahiga alisisitiza umuhimu wa miundombinu hiyo kuunganishwa ili iweze kuleta tija iliyokusudiwa katika uchumi. Aliongeza kuwa uchumi wa Tanzania unakua kwa wastani wa asilimia 7 kwa mwaka na uchumi wa nchi za jirani ambazo zinategemea bandari za Tanzania pia unakua, hivyo kuendeleza na kuunganisha miundombinu ya usafiri ni muhimu kwa ustawi wa uchumi wa nchi hizo na uchumi wa Tanzania.

Aidha, Waziri Mahiga alieleza namna Serikali inavyoendelea na zoezi la kuhamisha makao makuu ya Serikali kwenda Dodoma na kukaribisha makampuni ya China kushiriki kwenye uwekezaji wa miundombinu mbalimbali kwenye mji huo mpya wa makao makuu.

Baadhi ya miundombinu muhimu inayohitajika Mjini Dodoma ni upatikanaji wa maji safi ya na ya uhakika na kuiomba China ishiriki katika ujenzi wa Bwawa la Kidunda mkoani Morogoro. Bwawa hilo likijengwa na kukamilika litasaidia sio tu kusambaza maji ya uhakika mkoani Dodoma bali hata mkoa wa Dar Es Salaam ambao matumizi ya maji yanaongezeka kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu kila siku.

Waziri Mahiga aliahidi kuwa Serikali yake itakamilisha taratibu zilizosalia ili mradi wa Mchuchuma na Liganga uweze kuanza kwa kuwa mradi huo ni muhimu sana katika sera ya uchumi wa viwanda.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Biashara aliahidi kuwa Serikali ya China itafanyia kazi kwa haraka miradi yote iliyowasilishwa ili Tanzania iweze kutimiza malengo yake ya kuwaletea maendeleo wanachi. 

Aliongeza kuwa Serikali yake itaharakisha kufanya upembuzi yakinifu wa miradi hiyo kwa madhumuni ya kutimiza masharti ya kampuni za uwekezaji na taasisi zinazotoa fedha nchini China.

Aidha, alipongeza hatua ya Serikali ya Tanzania ya kuweka mikakati ya kuzalisha umeme wa megawatts 5000 ifikapo mwaka 2020. Hivyo, aliahidi kuwa atazishawishi kampuni za China zinazozalisha umeme wa jua, upepo na joto ardhi zijek uwekeza nchini ili lengo hilo litimie kwa haraka.

Wakati huo huo, Waziri Mahiga alikutana na watendaji wa makampuni mbalimbali ya uwekezaji yaliyodhamiria kuwekeza nchini kwenye sekta mbalimbali. Makampuni hayo yanataka kuwekeza kwenye uzalishaji wa Sukari, ujenzi wa kiwanda cha kusindika mihogo, uagizaji wa mihogo mikavu toka Tanzania kwa wastani wa tani laki 3 hadi 5 kwa mwaka na huduma za kitalii kama ujenzi wa mahoteli yenye hadhi ya nyota tano. 

Kampuni hizo zote zimeomba kukutanishwa na wadau husika ili wkamilishe taratibu zinazotakiwa waanze uwekezaji haraka iwezekanavyo.

Waziri Mahiga aliwahakikishia wawekezaji hao kuwa uamuzi wao wa kuwekeza Tanzania hawataujutia kwa kuwa Tanzania ni nchi tulivu na yenye amani, ina rasilimali nyingi na soko kubwa kutokana na kuwa mwanachama wa SADC na EAC.

Matukio yanayojiri katika ziara ya kikazi ya Balozi Mahiga nchini China

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea jambo wakati alipokuwa katika mazungumzo rasmi na Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming jijini Beijing.
Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming akisisitiza jambo alipokuwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt.Augustine Mahiga leo jijini Beijing.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kulia) akiwa na ujumbe wake aliongozana nao katika ziara ya kikazi nchini China. Kutoka kushoto ni Mwambata Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China, Kanali Remigius Ng'umbi anayefuata ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Dkt. Thomas Kashililah na Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki.

Wajumbe wa pande mbili za China na Tanzania wakiwa katika mazungumzo.

Wajumbe wengine wa Tanzania wakifuatilia mazungumzo. Kutoka kulia ni Kamishna Msaidizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango, Bi. Malmeltha Mutagwaba, Naibu Katibu Mkuu wa Biashara na Uwekezaji kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchweishaija na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango kutoka Serikali ya Zanzibar, Bw. Khamis Omar 

Balozi Mahiga akitoa zawadi ya picha kwa Naibu Waziri wa Biashara wa China, Mhe. Qian Keming.

Mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipango ya China
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Mipngo ya China, Bw. Ning Jizhe alipowasili ofisini kwake kwa ajili ya kufanya mazungumzo.

Ujumbe wa Tanzania na China wakijadiliana namna nchi zao zitakavyoweza kushirikiano katika masuala ya uchumi, uwekezaji n biashara.

Bw. Jing Jizhe akionesha utayari wa nchi yake wa kushirikiana na Tanzania katika masuala ya maendeleo ya kiuchumi.
 Mazungumzo na wafanyakazi wa Ubalozi
Balozi Mahiga na ujumbe wake wakiwa katika mazungumzo na wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania nchini China.

Balozi Mahiga akiwa na katika mazungumzo na mmoja wa wawekezaji aliyedhmiria kuwekeza Tanzania.

Mwekezaji mwingine akisalimiana na Balozi Mahiga kabla ya kuanza kwa mazungumzo yao.

Waziri Mahiga akiwa katika mazungumzo na aliyekuwa Balozi wa China nchini Tanzania, Dkt, Lu Youqing

Mhe. Balozi, Dkt. Ramadhani Dau awasilisha Hati za Utambulisho kwa Mtukufu Mfalme wa Cambodia

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Malaysia anayewakilisha pia nchini Cambodia, Mhe. Dkt. Ramadhani Kitwana Dau (kushoto) akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mfalme wa Cambodia, Mtukufu Preah Bat Samdech Preah Boromneath NORDOM SIHAMON. Makabidhiano hayo yalifanyika tarehe 28 Novemba 2017 Jijini Phnom Pen, Cambodia.
Mhe. Balozi Dkt. Dau (wa pili kushoto) akiwa katika mazungumzo na Mtukufu Mfalme mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho. Wanaoshuhudia kulia ni maafisa wa Serikali ya Cambodia na kushoto ni Afisa wa Ubalozi wa Tanzania.

Mazungumzo yao yalijikita katika kuendeleza na kuimarisha uhusiano wa Kidiplomasia uliopo baina ya mataifa hayo ambao ulianzishwa rasmi mwaka 1995. Pia kuimarisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uwekezaji. Vilevile Mtukufu Mfalme aliahidi kumpa ushirikiano Mhe. Balozi Dkt. Dau katika utekelezaji wa majukumu yake.



Mhe. Balozi Dkt. Dau akimtambulisha Afisa wa Ubalozi wa Tanzania, Bw. Khatib Makenga aliyeambatana naye katika hafla ya  makabidhiano ya Hati za Utambulisho

Mhe. Balozi Dkt. Dau akipokelewa mara baada ya kuwasili jijini Phnom Penh, Cambodia. 

Thursday, December 14, 2017

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ampokea Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Mgeni wake Rais wa Msumbiji Mhe.Filipe Nyusi wakipita kwenye gadi ya heshima iliyoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakati Rais huyo akiwasili katika uwanja wa ndege wa mjini Dodoma

Vikundi vya ngoma za jadi vikisherehesha katika shughuli za mapokezi ya Rais wa Msumbiji Mhe.Filipe Nyusi katika uwanja wa ndege wa mjini Dodoma


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na mgeni wake Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Nyusi wakati akimpokea mjini Dodoma. Rais Nyusi amewasili leo mjini Dodoma kwa ziara ya kikazi ya siku moja na kupokelewa na mwenyeji wake Rais Magufuli, kabla ya kuelekea Ofisini kwa mazungumzo. Katika mazungumzo yao wamejadili na kukubaliana masuala mbalimbali ya kukuza na kuendeleza ushirikiano uliodumu kwa muda mrefu baina ya Mataifa haya mawili (Tanzani na Msumbiji). Aidha Rais Magufuli na Rais Nyusi wamekubaliana kuanzisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ya kiuchumi ikiwemo katika sekta ya gesi usafiri wa anga na miundombinu.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe.Balozi Dkt. Augustine Mahiga akisalimiana na Rais wa Msumbiji Mhe.Filipe Nyusi alipowasili uwanja wa ndege wa mjini Dodoma kwa ziara ya kikazi ya siku moja


        Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.               Dkt.  John Pombe Magufuli  akiwa na Mgeni wake Rais wa Msumbiji Mhe.Filipe Nyusi katika Ikulu ndogo ya Mjini Dodoma kabla ya kuanza mazungumzo yao

Wednesday, December 13, 2017

TANZANIA'S POSITION ON THE STATUS OF JERUSALEM



TANZIA


TANZIA

Marehemu Mama Badriya Kiondo
Familia za Bw. Kiondo wa Kwaminchi Tanga na Bw. Ramadhan Haji wa Betras, Zanzibar wanasikitika kutangaza kifo cha Mtoto wao mpendwa, Bi. Badriya Ramadhan Kiondo aliyekuwa Mkuu wa Utawala na Fedha katika Ubalozi wa Tanzania nchini India kilichotokea tarehe 11 Desemba, 2017 katika Hospitali ya Apollo mjini New Delhi, India. 

Mwili wa Marehemu Mama Kiondo unatarajiwa kuwasili nchini Alhamisi tarehe 14 Desemba, 2017 saa 8.45 mchana kwa Ndege ya Shirika la Emirates. Aidha, mazishi yatafanyika katika Makaburi ya Kisutu Jijini Dar es Salaam Ijumaa tarehe 15 Desemba, 2017 saa 10.00 jioni.

Msiba wa Marehemu Mama Kiondo upo nyumbani kwa mumewe Bw. Frank Mwamkai Kiondo maeneo ya Ada Estate, Na. 73, Kinondoni, Barabara ya Ali Hassan Mwinyi karibu na Ubalozi wa Ufaransa.

Habari ziwafikie ndugu, jamaa na marafiki wote wa familia hizi popote pale walipo.


Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina



RATIBA YA MAZISHI YA MAREHEMU BI. BADRIYA RAMADHAN KIONDO




Tuesday, December 12, 2017

Waziri Mahiga awaasa Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne (4) la Jumuiya ya Afrika Mashariki kuwa Wazalendo na kusimamia maslahi ya Jumuiya.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga(katikati) akiongea katika kikao cha uongozi wa Wizara hiyo na Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne (4) la Jumuiya ya Afrika Mashariki, kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam, tarehe 12 Disemba 2017. Pembeni yake kushoto ni Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba na kulia ni Mwenyekiti wa Wabunge wateule wa Bunge la Afika Mashariki, Mhe. Abdullah Makame.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akiongea katika kikao hicho ambapo aliwakaribisha Waheshimiwa Wabunge wateule pamoja na kuwaeleza kuwa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ipo tayari kuwapa ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao. Pembeni yake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Ramadhan Muombwa Mwinyi.

Mwenyekiti wa Wabunge Wateule wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe.Dkt. Abdullah Makame akiushukuru uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kikao kizuri cha utangulizi kabla ya kuanza kwa Bunge hilo na pia akaahidi kuwa wataenda kuliwakilisha Taifa vizuri sambamba na kusimamia maslahi ya Jumuiya kwa maendeleo na ustawi wa wananchi wake.

Sehemu ya Waheshimiwa Wabunge Wateule wa Bunge la Afrika Mashariki wakifuatilia maelekezo yaliyokuwa yakitolewa na Mhe. Waziri Mahiga (hayupo pichani)

Sehemu nyingine ya Waheshimiwa Wabunge wakifuatilia kikao hicho.
Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia kikao hicho. Kutoka kulia  Bw. Eliabi Chodota, Bw. Bernard Haule na Bw.Joachim Otaru.



Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Stephen Mbundi akitoa ufafanuzi kuhusiana na taratibu na miongozo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Waheshima Wabunge Wateule. 

Mhe. Waziri na  Naibu Waziri  wakiwa katika picha ya pamoja na Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Picha ya pamoja uongozi wa Wizara  na Wabunge Wateule wa Tanzania kwenye Bunge la nne la Jumuiya ya Afrika Mashariki.