Monday, July 28, 2014

Watanzania waishio Comoro waandaa futari kwa kushirikiana na Ubalozi

Baadhi ya Watanzania wanaoishi Visiwani Comoro wakiwa katika picha ya pamoja na Bw. Ali Mwadini (wa pili kutoka kushoto), Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania, Comoro ambaye alimwakilisha Mhe. Balozi Chabaka Kilumanga wakati wa  futari ya pamoja iliyoandaliwa na Watanzania hao kwa kushirikiana na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Moroni. 
Jumuiya ya Watanzania waishio Comoro wakipata futari ya pamoja.


 WATANZANIA WANAOISHI VISIWANI COMORO WAANDAA FUTARI YA PAMOJA KWA KUSHIRIKIANA NA UBALOZI

Jamii ya Watanzania wanaoishi Visiwani Comoro wameandaa futari ya pamoja, kwa kushirikiana na Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mjini Moroni. Lengo la futari hiyo lilikuwa ni kuwakutanisha Watanzania wanaoishi Comoro, hususan katika kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ili wajumuike pamoja. 

Wakizunguza wakati wa hafla hiyo, Watanzania hao walielezea kufurahishwa na kufarijika kwao kutokana na kitendo cha Serikali ya Tanzania kufungua Ubalozi nchini Comoro. Walieleza pia utayari wao wa kushirikiana na Ubalozi ili kuhamasisha maendeleo yao na ya nchi kwa ujumla.

Akizungumza katika halfa hiyo kwa niaba ya Mhe. Balozi Chabaka Kilumanga, Bw. Ali Mwadini wa Ubalozi wa Tanzania Moroni, aliwashukuru Watanzania hao kwa kupata wazo zuri la kuandaa futari na kuushirikisha Ubalozi.

Aidha, aliwasihi waendelee na umoja huo kwa kusaidiana na kuwa raia wema kwa kutii sheria za nchi wanapoishi. Aliwakumbusha pia kufika Ubalozini na kujisajili kwa wale ambao bado walikuwa hawajafanya hivyo. Vile vile, aliwahimiza kushiriki katika Kongamano la Watanzania Wanaoishi Ughaibuni linalotarajiwa kufanyika Jijini Dar es Salaam tarehe 14 na 15 Agosti 2014.




PRESS RELEASE

H.E. Joko Widodo, Indonesian president-elect


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency Joko Widodo, president elect of the Republic of Indonesia.

The message reads as follows;

“His Excellency Joko Widodo,
 The President,
 Jakarta,
 REPUBLIC OF INDONESIA.


Your Excellency,

It is with great pleasure that I take this opportunity to convey to you, on behalf of the Government and people’s of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf warm greetings and congratulations upon your election as the President of the Republic of Indonesia following the general election held on 9th July 214.  

 The government and the people of the United Republic of Tanzania are confident that under your able leadership, the Government and people of the Republic of Indonesia will score remarkable achievements in the years ahead.
The Government of the United Republic of Tanzania assures Your Excellency its commitment to work with the Government of the Republic of Indonesia to further promote the close ties of friendship and co-operation which so happily exist between our two countries.

Please accept, Your Excellency, my best wishes for your personal good health and peace and prosperity for the people of the Republic of Indonesia”.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam.
28th July 2014




Naibu Waziri akutana na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki



Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (Mb.)  akisalimiana na Mkurugenzi wa Shirika la Kimatifa la Nguvu za Atomiki,  Bw. Yukiya Amano alipofika Wizarani kwa ajili ya mazungumzo kuhusu ushirikiano kati ya Shirika lake na Serikali ya Tanzania. Bw. Amano yupo nchini kwa ziara ya kikazi.
Mhe. Mahadhi akizungumza na Bw. Amano
Mhe. January Makamba (wa kwanza kushoto), Naibu Waziri wa Mawasiliano,  Sayansi na Teknolojia pamoja na Wajumbe wengine akiwemo Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Modest Mero (wa pili kulia) na Msaidizi wa Mhe. Maalim, Bw. Adam Isara (kulia) wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Maalim na Bw. Amano (hawapo pichani). 
Bw. Amano akimweleza jambo Mhe. Maalim wakati wa mazungumzo yao.
Baadhi ya Wajumbe kutoka Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia wakifuatilia mazungumzo.
Wajumbe wengine.
Mkurugenzi Msaidizi kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Japhet Mwaisupule na Bi. Ramla Khamis, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo.


Picha na Reginald Philip

Friday, July 25, 2014

PRESS STATEMENT

PRESS STATEMEMNT

In a Press Conference held on 14th July, 2014, the Minister for Foreign Affairs and International Co-operation, Hon. Bernard Membe, on behalf of the Government of the United Republic of Tanzania called on Israel and Hamas to ceasefire immediately, adding that The United Nations Security Council should step in to restore harmony in the Middle East.

The Government of the United Republic of Tanzania wishes to reiterate this position and further condemns the ongoing killings of innocent civilians among them elderly, women and children in Gaza.

The Government of the United Republic of Tanzania calls upon the International Community to continue supporting diplomatic efforts to end the conflict peacefully.  Core to the solution of this conflict is availing the people of Palestine the right to self-determination through the establishment of an independent Palestinian state.

The Government of the United Republic of Tanzania therefore maintains its support to the two-state solution with Palestine and Israel co-existing in harmony and ensuring security of the State of Israel.

                      Issued by: The Permanent Secretary,

Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam


25th July 2014 

Thursday, July 24, 2014

Wizara yamuaga Balozi wa Norway nchini


Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akisoma hotuba kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernad K. Membe (Mb.) kwa ajili ya kumuaga Balozi wa Norway nchini, Mhe. Ingunn Klepsvik ambaye amemaliza muda wake wa kazi. Hafla hiyo fupi ya chakula cha mchana ilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, Dar es Salaam.
Balozi Mushy akimkabidhi Balozi Klepsvik zawadi ya picha ya kuchora ya Twiga  kama ukumbusho wake kwa Tanzania
Balozi Klepsvik naye akizungumza machache wakati wa hafla hiyo.
Mkuu wa Mabalozi  ambaye pia ni Balozi wa DRC hapa nchini, Mhe. Juma Halfan Mpango (kushoto) pamoja na Balozi Mushy na Balozi Klepsvik wakati wa hafla hiyo.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bibi Victoria Mwakasege akiwakaribisha wageni waalikwa wakati wa hafla ya kumuaga Balozi Klepsvik.

Tanzania na Sri Lanka kuimarisha ushirikiano

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sri Lanka, Mhe. Prof. G.L. Peiris walipokutana mjini Colombo, Sri  Lanka wakati wa ziara ya Mhe. Membe nchini humo hivi karibuni. Wakati wa ziara hiyo  Mhe. Membe kwa niaba ya Serikali ya Tanzania alisaini mikataba mitatu ikiwemo ule wa Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Sri Lanka, Mkataba wa Ushirikiano katika masuala ya Siasa na Mkataba wa Makubaliano katika Maendeleo na Utafiti wa Kilimo endelevu cha Minazi.
Mhe. Membe na Ujumbe wake (kushoto) wakati wa mazungumzo na Mhe. Peiris na Ujumbe wake (kulia)
Mhe. Membe na Mhe. Peiris wakisaini Mkataba wa kuanzisha Tume ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na Sri Lanka.
Mhe. Membe na Mhe. Peiris wakibadilishana Mkataba mara baada ya kuusaini.
Mhe. Membe na Waziri wa Kilimo wa Sri Lanka wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Maendeleo na Utafiti wa Kilimo endelevu cha Minazi.
Mhe. Membe na Mhe. Prof. Peiris wakizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano waliyokubaliana.
Wajumbe kutoka Tanzania na Sri Lanka pamoja na Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mhe. Membe na Mhe. Peiris (hawapo pichani)

Monday, July 21, 2014

Waziri Membe ashiriki futari nyumbani kwa Balozi Mdogo Mhe. Omary Mjenga

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Membe (Mb.) akiwa na Balozi Mdogo wa Tanzania Dubai Mhe. Omary Mjenga wakisubiri muda wa futari mjini Dubai leo. Mhe. Membe alikuwa njiani kuelekea Colombo, Sri Lanka kwenye Mkutano wa Jumuiya ya Madola.
Mhe. Membe pamoja na Mhe. Mjenga, wakiwa katika mazungumzo kwenye ukumbi wa mazungumzo (majlis) nyumbani kwa Balozi Mdogo
Waziri Membe akiwa akiwa na Balozi Mdogo Mhe. Omary Mjenga kwenye futari.



Friday, July 18, 2014

PRESS RELEASE


Rt. Hon. Dato' Sri Mohammad NajibTun Abdul Razak

PRESS RELEASE

H.E. Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a condolence message to Rt. Hon. Dato' Sri Mohammad NajibTun Abdul Razak, Prime Minister of Malaysia following the loss of lives due to the crash of a Malaysian airliner on Thursday 17th July 2014. The message reads as follows:

“Rt. Hon Dato' Sri Mohammad Najib Tun Abdul Razak,
The Prime Minister of Malaysia,
Kuala Lumpur.
Malaysia

I have learnt with great shock and sorrow the sad news of the loss of so many lives due to the crash of a Malaysian airliner on its way from Amsterdam to Kuala Lumpur that occurred on Ukrainian territory on Thursday 17th July 2014.

The crash is an immense tragedy not only for the loved ones of those who perished but also for all the people of Malaysia and their friends. As a country, our thoughts and prayers are with the people of Malaysia in this time of grief.

On behalf of the Government and the people of the United Republic of Tanzania, and indeed on my own behalf, I offer you our sincere condolences, support and solidarity.

Please accept, Your Excellency the assurances of my highest consideration”.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam

18th July, 2014

Naibu Katibu Mkuu amuaga Balozi wa Israel nchini

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Gil Haskel, Balozi wa Israel nchini Tanzania ambaye alifika Wizarani kwa lengo la kuaga baada ya kumaliza muda wake. Kwenye mazungumzo yao, Balozi Gamaha ameishukuru Serikali ya Israel kwa ushirikiano mzuri na Serikali ya Tanzania hususan kwenye upande wa kujengea uwezo wa Watanzania kwenye masuala ya Kilimo cha Umwagiliaji. Kwa upande wake Balozi Haskel ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano mkubwa alioupata katika kipindi chake. Pia ameahidi kuendeleza ushirikiano huo hata katika wadhifa wake mpya akiwa nchini kwake, ambapo atakua Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Israel.

Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati,  Balozi Simba Yahya (kushoto) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bi. Mindi Kasiga (kulia) na Bw. Leonce Bilauri, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia na kunukuu mazungumzo kati ya Naibu Kaibu Mkuu na Balozi wa Israel nchini.

Picha na Reginald Philip

Thursday, July 17, 2014

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Hungary nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho za Mhe. Sander Kocsis, Balozi wa Hungary nchini Tanzania mwenye makazi Nairobi, Kenya. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam hivi karibuni.
Balozi Kocsis akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Balozi Kocsis akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) mara baada ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais.
Balozi Kocsis akisalimiana na Balozi Joseph Sokoine, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Kocsis.

Mhe. Rais katika picha ya pamoja na Balozi Kocsis, Waziri Membe na Mhe. Mark Mwandosya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum.
Balozi Kocsis akisikiliza wimbo wa taifa lake uliopigwa na bendi ya polisi (haipo pichani) kwa heshima yake. Wengine katika picha ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohhamed Maharage Juma (kulia) na Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo (kushoto)
ASP Kulwa akiongoza Bendi ya Polisi wakati wa mapokezi ya Balozi Kocsis (hayupo pichani)

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Shelisheli nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hatiza Utambulisho za Mhe. Claude Morel, Balozi wa Shelisheli hapa nchini mwenye makazi yake nchini Afrika Kusini. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 15 Julai, 2014.
Balozi Morel akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Morel, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) huku Prof. Mark Mwandosya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum akishuhudia.
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Morel.
Mhe. Balozi Morel (katikati) akisikiliza wimbo wa taifa lake mara baada ya kuwasili Ikulu. Wengine katika picha ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohamed Maharage Juma (Kulia) naBw. Shaaban Gurumo, Mnikulu. 
Bendi ya Polisi ikiongozwa na ASP Kulwa wakiwa kazini

Wednesday, July 16, 2014

Mhe. Rais apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa New Zealand hapa nchini


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Richard Stuart Mann, Balozi wa New Zealand hapa nchini mwenye makazi yake Afrika Kusini. Hafla hiyo fupi ilifanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 15 Julai, 2014.

Balozi Mann akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) mara baada ya Balozi huyo kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais Kikwete, wakwanza kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Kazi maalum Mhe. Prof. Mark J. Mwandosya (Mb.)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Richard Stuart Mann
Balozi Richard Stuart Mann akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Balozi Mann akisikiliza Wimbo wa Taifa lake ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Juma Maharage na wakwanza kushoto ni Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo


Picha na Reginald Philip



Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho za Balozi wa Ujerumani nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mhe. Egon Kochanke, Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, jijini Dar es Salaam tarehe 15 Julai, 2014.
Balozi Kochanke akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya kuwasili Ikulu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na Mhe. Egon Kochanke
Picha ya pamoja
Balozi Kochanke akisikiliza Wimbo wa Taifa lake ukipigwa kwa heshima yake mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkurugenzi na Mkuu wa Itifaki, Balozi Mohammed Juma Maharage na kushoto ni Mnikulu, Bw. Shaaban Gurumo

Picha na Reginald Philip