Tuesday, February 28, 2023

BALOZI SHELUKINDO ASISITIZA UMUHIMU WA KUFANYA KAZI KWA USHIRIKIANO


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akipokea maua mara baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023. Balozi Shelukindo aliapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuushika wadhifa huo tarehe 27 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Balozi Fatma Rajab wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Alex Mfungo wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Balozi Naimi Aziz wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.


Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Balozi Caesar Waitara wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkaguzi Mkuu wa Ndani, Bw. Japhary Kachenje wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. Haji Janabi wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bi. Talha Waziri wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akimkaribisha Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Samwel Shelukindo ajitambulishe kwa menejimenti ya Wizara wakati wa hafla ya mapokezi iliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo (kushoto) akiongoza kikao cha Menejimenti kilichofanyika kwa lengo la kujitambulisha katika ofisi za Wizara jijini Dododma tarehe 28 Februari 2023. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Balozi Fatma Rajab. 

Mkurugenzi Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bw. Alex Mfungo na Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango, Bw. Haji Janabi wakifatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Mkurugenzi Idara ya Afrika, Balozi Naimi Aziz akijitambulisha kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo katika hafla ya mapokezi yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.


Mkurugenzi wa Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Caesar Waitara (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Noel Kaganda wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.

Kutoka kulia ni Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Swalehe Chondoma na Bw. Haji Janabi wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.


Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati, Bw. Leonce Bilauri na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji wakifuatilia kikao cha utambulisho cha Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrka Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo.

Sehemu nyingine ya wajumbe wa managementi wakifuatilia kikao.

Kutoka kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama, Bw. Amani Mwatonoka na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika, Bi. Salma Baraka wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dododma tarehe 28 Februari 2023.

Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Dkt. Isaac Kalumu  na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Bi. Talha Waziri wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dododma tarehe 28 Februari 2023.

Mwakilishi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Ally Kondo (Kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Uratibu wa Biashara za Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi, Bw., Francis Berege wakifuatilia kikao cha utambulisho wa Katibu Mkuu kilichofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo akiwasili katika ofisi za Wizara  jijini Dodoma tarehe 28 Februari 2023.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo (kulia) akisalimiana na sehemu ya madereva walioshiriki hafla ya mapokezi katika ofisi za Wizara jiji Dodoma tarehe 28 Februari 2023

Picha ya Pamoja






TANZANIA KUANZA SAFARI ZA NDEGE MOJA KWA MOJA HADI SAUDI ARABIA

Tanzania inategemea kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja hadi Saudi Arabia ambapo safari ya kwanza kati ya Dar es Salaam na Jeddah inatarajiwa kuanza tarehe 26 Machi 2023.

Hayo yamebainishwa katika mazungumzo ya Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia Mhe. Ali Mwadini na Meneja Mkuu wa Masoko, Kanda ya Kati wa Shirika la Ndege la Saudi Arabia Bw. Abdulrahman Alabdulwahab na kujadili maandalizi ya uzinduzi wa safari za ndege za moja kwa moja kati ya Tanzania na Saudi Arabia. 

Katika mazungumzo yao viongozi hao pia walijadili mikakati ya kutangaza vivutio vya utalii vya Tanzania ili kuongeza idadi ya watalii na kurahisisha usafirishaji wa bidhaa za Tanzania hususan nyama na matunda. 

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. Ali Mwadini na Meneja Mkuu wa Masoko, Kanda ya Kati wa Shirika la Ndege la Saudi Arabia Bw. Abdulrahman Alabdulwahab wakikabidhiana zawadi baada ya kumaliza mazungumzo yao katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia

Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. Ali Mwadini akijadiliana jambo na Meneja Mkuu wa Masoko, Kanda ya Kati wa Shirika la Ndege la Saudi Arabia Bw. Abdulrahman Alabdulwahab katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia



Monday, February 27, 2023

EU YARIDHISHWA NA UBORESHWAJI WA HAKI ZA BINADAMU, UTAWALA BORA NCHINI

 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akichangia jambo wakati wa majadiliano ya kisiasa kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya. Majadiliano hayo yamefanyika leo Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Umaoja wa Ulaya nchini, Mhe. Manfredo Fanti akitoa mchango wake wakati wa majadiliano ya kisiasa kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya. Majadiliano hayo yamefanyika leo Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax pamoja na Balozi wa Umaoja wa Ulaya nchini, Mhe. Manfredo Fanti wakionesha makubaliano waliyosaini baada ya majadiliano ya kisiasa kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yaliyofanyika leo Jijini Dar es Salaam

Majadiliano ya kisiasa kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yakiendelea Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme akichangia mjadala wa kisiasa kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya Jijini Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Kasiga akiongoza majadiliano ya kisiasa kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya Jijini Dar es Salaam

Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika Nchi za Jumuiya ya Ulaya wakitambulishwa 

Picha ya pamoja 



VACANCY ANNOUNCEMENT


 

Sunday, February 26, 2023

DKT. TAX APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI WA ZAMBIA, BRAZIL NA VATICAN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amepokea nakala za Hati za Utambulisho za mabalozi wateule wa nchi za Zambia, Brazil na Vatican.

Mhe. Waziri Tax amepokea nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Zambia nchini, Mhe. Mathew Jere, Balozi mteule wa Brazil nchini, Mhe. Gustavo Martins Nogueira na Balozi Mteule wa Vatican Nchini, Mhe. Askofu Mkuu Angelo Accattino leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na mabalozi hao kwa nyakati tofauti Waziri Tax amewahakikishia ushirikiano kutoka Serikalini wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao ya kibalozi hapa nchini. Pia Waziri Tax ametoa rai kwa mabalozi hao kuendeleza na kudumisha ushirikiano uliopo baina ya Tanzania na nchi zao.

“Tanzania na Zambia tumekuwa marafiki na ndugu wa muda mrefu, Serikali ya Tanzania itaendelea kushirikiana na Serikali ya Zambia katika sekta za biashara na uwekezaji kwa maslahi mapana ya pande zote mbili,” alisema Dkt. Tax  

Balozi mteule wa Zambia nchini, Mhe. Mathew Jere ameahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya Zambia na Tanzania katika sekta za biashara na uwekezaji, usafirishaji, pamoja na nishati.  

Kwa upande wake Balozi Mteule wa Brazil, Mhe. Gustavo Martins Nogueira ameahidi kuwa Brazil itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mapya ya kimkakati kwa manufaa ya mataifa yote mawili hususan kilimo, biashara na uwekezaji.

Naye Balozi wa Vatican nchini, mhe. Askofu Mkuu Angelo Accattino ameahidi kuendeleza kuimarisha ushirikiano mzuri uliopo baina ya Vatican na Tanzania. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea  nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Zambia nchini, Mhe. Mathew Jere katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea  nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa  Brazil nchini,  Mhe. Gustavo Martins Nogueira katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea  nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa  Vatican nchini, Mhe. Askofu Mkuu Angelo Accattino leo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Friday, February 24, 2023

SERIKALI YAWAHAKIKISHIA WAFANYABIASHARA MAZINGIRA SALAMA YA BIASHARA

Serikali imewahakikishia wafanyabiashara kutoka Nchi za Umoja wa Ulaya (EU) kuwa mazingira ya biashara na uwekezaji nchini ni salama, bora na rafiki.

Rai hiyo imetolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi alipofunga Jukwaa la Biashara kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya lililofanyika jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 23 – 24 Februari 2023. 

Dkt. Mwinyi alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imekusudia kuweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji kwa ajili ya kuvutia wawekezaji wengi kuja kuwekeza nchini.

“EU imekuwa mwekezaji mkubwa nchini Tanzania na imechangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la ufanyaji biashara kati yake na Tanzania, lengo la serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania ni kukuza na kuendeleza sekta binafsi yenye nguvu, hivyo natoa rai kwenu kuwekeza kwa wingi kwani mazingira ni bora na salama,” alisisitiza Dkt. Mwinyi

Rais Mwinyi aliongeza kuwa Serikali imejikita katika kukuza uwekezaji kupitia sekta za kilimo, uchumi wa buluu, madini, usafirishaji, miundombinu, utalii na nyingine nyingi na kuwasihi wafanyabiashara wapatao 400 kutoka EU kuchangamkia fursa za biashara na uwekezaji zinazopatikana nchini. 

“Napenda kuwahakikishia kuwa Serikali imejidhatiti kuweka mazingira yenye ushindani ya biashara na uwekezaji ikiwa ni mkakati wa kuendelea kuimarisha mazingira ya uwekezaji na biashara na kuhakikisha yanakuwa rafiki kwa wawekezaji,” aliongeza Rais Mwinyi.

Awali Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) nchini, Mhe. Manfredo Fanti alisema Tanzania imejitahidi kuboresha mazingira, kuimarisha mahusiano ya nje na kuondoa vikwazo mbalimbali hivyo ni wakati muafaka kwa EU kufanya biashara na Tanzania kwakuwa mazingira ni mazuri na yanaridhisha.

“Mfano kitendo cha Benki ya Uwekezaji ya Umoja wa Ulaya (EIB) kurejea Tanzania na kufanya uwekezaji mkubwa wenye thamani ya Euro milioni zaidi ya 500 ni kutokana na Serikali kuboresha mazingira ya bishara na uwekezaji,” alisema Balozi Fanti   

Balozi Fanti amewasihi wafanyabiashara wa Tanzania kupenda kukuza ujuzi ili waweze kuendeleza na kukuza biashara zao pamoja na uchumi wa Taifa kwa ujumla.

“EU kwa umoja wetu tutaendelea kuimarisha nguvu zetu kwa pamoja ili kuhakikisha tunaendelea kuwekeza na kukuza biashara kati yetu na Tanzania kwa maslahi ya mataifa yote,” alisema Balozi Fanti.

Kwa upande wake Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Kazi Uchumi na Uwekezaji Zanzibar, Mhe. Mudrick Ramadhan Soraga amesema Tanzania na Nchi za Umoja wa Ulaya zimekuwa na ushirikiano imara na wa muda mrefu na kwamba ushirikiano huo umesaidia kuendelea kushirikiana katika sekta mbalimbali za maendeleo kwa maslahi ya mataifa yote mawili.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi akihutubia wakati wa kufunga rasmi Jukwaa la Biashara kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya lililofanyika jijini Dar es salaam kuanzia tarehe 23 – 24 Februari 2023  

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akifuatilia Hotuba ya ufunguzi wa Jukwaa  la Biashara kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya lililofanyika Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Anthony Mavunde.   

Sehemu ya viongozi mbalimbali wakifuatilia Hotuba ya ufunguzi wa Jukwaa  la Biashara kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya lililofanyika Jijini Dar es Salaam

Baadhi ya Mabalozi wa Tanzania katika nchi za Umoja wa Ulaya  wakifuatilia Hotuba ya ufunguzi wa Jukwaa  la Biashara kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya lililofungwa Jijini Dar es Salaam


Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Grace Martin akichangia jambo wakati wa Jukwaa  la Biashara kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya lililofungwa leo Jijini Dar es Salaam 

VACANCY ANNOUNCEMENT



 

VACANCY ANNOUNCEMENT


 

DKT. TAX AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA 43 WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa  43 wa Kawaida wa  Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) uliofanyika jijini Bujumbura, Burundi tarehe 23 Februari 2023.

 

Mhe. Dkt. Tax ambaye ameshiriki Mkutano huo kwa mara ya kwanza tangu kuteuliwa kwake kwenye wadhifa huo, ameungana na Mawaziri wenzake wanaosimamia masuala ya Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda katika Jumuiya hiyo kupitia, kujadili na kupitisha mapendekezo ya agenda mbalimbali zinazolenga kuboresha utendaji wa Jumuiya kwa manufaa ya Nchi Wanachama.

 

Miongoni mwa agenda zilizojadiliwa na kupitishwa na Baraza hilo ni pamoja na ripoti ya utekelezaji wa maazimio mbalimbali yaliyofikiwa na Baraza hilo kwenye vikao vilivyopita; taarifa kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, taarifa ya utekelezaji wa program mbalimbali katika sekta za miundombinu, forodha na biashara, utalii na ajira;  taarifa ya mwaka ya ukaguzi wa hesabu za jumuiya kuanzia mwezi Januari hadi Juni 2022 na ripoti ya kamati ya utawala na fedha.pamoja na kupitia na kupitisha ratiba ya shughuli za Jumuiya kwa kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Juni 2023.

 

Kadhalika masuala mengine yaliyojadiliwa ni umuhimu wa kukitangaza Kiswahili  duniani kwa kuanzisha vituo vya utamaduni wa lugha hiyo katika Balozi za Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki; na kutoa mwelekeo wa kuanza kutumika kwa lugha ya Kifaransa na Kiswahili katika uendeshaji wa shughuli  rasmi za Jumuiya. 

 

Awali akizungumza na Waandishi wa Habari Mwenyekiti kutoka Jamhuri ya Burundi ambaye pia ni Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Ezekiel Nibigira amesema kuwa Burundi kama mwenyekiti inaona fahari kuandaa Mkutano wa aina hiyo ambapo pia aliwakaribisha Mawaziri wenzake na washiriki wa Mkutano  huo nchini humo na kueleza kuwa nchi hiyo imeendelea kuwa na amani na utulivu wakati wote.

                                                                                           

Mkutano huo ambao umefanyika kwa siku tano , ulitanguliwa na vikao vya Wataalam na Makatibu Wakuu kutoka nchi wanachama viilivyofanyika kuanzia tarehe 19 hadi 22 Februari 2023.

 

Mbali na Mhe. Dkt. Tax ujumbe wa Tanzania pia uliwajumuisha Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya, Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Geophrey Pinda,  Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine, Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Jilly Maleko,  Naibu Makatibu Wakuu akiwemo Bibi.  Amina Khamis Shaaban   Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango na Maafisa Waandamizi kutoka Serikalini.

 

Miongoni mwa majukumu ya Baraza la Mawaziri la Jumuiya ni kutunga sera za Jumuiya, kufuatilia na kufanya mapitio ya mara kwa mara juu ya utekelezaji wa program mbalimbali za Jumuiya kwa maslahi mapana ya Nchi Wanachama.

 

Jumuiya ya Afrika Mashariki ambayo inaundwa na nchi saba za Tanzania, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imeendelea kuhakikisha wananchi katika nchi hizo wananufaika na Jumuiya hiyo hususan katika nyanja za biashara, ulinzi na usalama, viwanda, kilimo, miundombinu na huduma za kijamii.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (katikati) akichangia jambo wakati wa Mkutano wa 43 wa Kawaida wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliomalizika hivi karibuni jijini Bujumbura, Burundi. Mhe. Dkt. Tax aliongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano huo.

Mhe. Dkt. Tax akiwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (kushoto)na Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya (kulia) wakati wa Mkutano wa 43 wa Kawaida wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
 


Mwenyekiti wa Mkutano wa 43 wa Kawaida wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambaye pia ni Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki nchini Burundi, Mhe. Balozi Ezekiel Nibigira akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano huo. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Peter Mathuki.
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Geophrey Pinda (kulia) akishiriki Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Wengine ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha, Bibi Amina Khamis Shaaban
Sehemu ya ujumbe wa Burundi wakishiriki mkutano
Ujumbe wa Uganda na Sudan Kusin katika mkutano
Ujumbe wa Kenya katika mkutano
Ujumbe kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wakishiriki Mkutano

Ujumbe wa Rwanda katika Mkutano
Mkutano ukiendelea
Awali Mhe. Dkt. Tax aliongoza ujumbe wa Tanzania katika kikao cha kupokea na kujadili taarifa ya nchi kuhusu Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri. Pichani Mhe. Dkt. Tax akizungumza wakati wa kikao hicho kilichomshirikisha pia Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (kulia) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine (kushoto)
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Geophrey Pinda akichangia jambo wakati wa kikao cha kupokea na kujadili taarifa ya nchi kuhusu Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri. Pichani Mawaziri. Kulia ni Balozi Sokoine
Balozi wa Tanzania nchini Burundi, Mhe. Dkt. Jilly Maleko akishiriki kikao cha kupokea na kujadili taarifa ya nchi kilichofanyika kabla ya kuanza Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri.
Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi akifafanua jambo kuhusu agenda za Mkutano kwa Waheshimiwa Mawaziri (hawapo pichani) wakati wa kikao cha kupokea na kujadili taarifa ya nchi kuhusu Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri. Kulia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Mhe. Mhandisi Godfrey Kasekenya na katikati ni Mhe. Balozi Maleko
Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa Ndani wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Japhary Kachenje akishiriki kikao cha kupokea na kujadili taarifa ya nchi kabla ya Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri.

Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Haji Janabi akishiriki kikao cha kupokea na kujadili taarifa ya nchi kuhusu Mkutano wa 43 wa Baraza la Mawaziri.

Kikao kikiendelea