Tuesday, February 14, 2023

MKUTANO WA MAJADILIANO YA KIMKAKATI YA NGAZI YA JUU KATI YA SERIKALI NA WADAU WA MAENDELEO WAFANYIKA

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Sterrgomena Tax wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023.

 Washiriki wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo katika meza kuu wakati wa mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023.


Washiriki wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo wakifuatilia mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023.

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki balozi Joseph Sokoine (wa pili kulia) akifuatilia Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo  uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023.

Washiriki wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo wakifuatilia mkutano huo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akifuatilia Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023.

Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023 ukiendelea.

Baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023 katika picha ya pamoja.

Meneja ratiba wa Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakti ya Ngazi ya Juu kati ya Serikali na Wadau wa Maendeleo uliofanyika jijini Dar es Salam tarehe 14 Februari, 2023 bi Ellen Maduhu akimkaribisha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk kuzungumza katika mkutano huo.



Mkutano wa Majadiliano ya Kimkakati ya Ngazi ya Juu ulioshirikisha watendaji wakuu wa Serikali na wadau wa maendeleo wafanyika jijini dar es Salaam.

Akimwakilisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax , Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amewahakikishia wadau wa maendeleo ushirikiano kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutekeleza kwa pamoja mipango ya maendeleo.

Balozi Mbarouk amesema kufanyika kwa kikao hicho kunadhihirisha ushirikiano wa muda mrefu uliopo kati Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na wadau wa maendeleo na Taasisi za Umoja wa Mataifa.

“Uwepo wenu hapa katika kikao hiki unadhihirisha ushirikiano usliopo kati ya Tanzania na wadau wa maendeleo, Sio kwamba uwepo wenu unachochea ubia wetu na kuimarisha nia yenu ya kuhakikisha tunatekeleza kikamilifu Mpango wa Tatu wa Taifa wa Maendeleo ambao umelenga kutekeleza malengo Endelevu ya Milenia ya Umoja wa Mataifa na makubaliano ya Addis Ababa ya kuchangia maendeleo na mabadiliko ya tabia nchi,” alisema Balozi Mbarouk

Mkutano huo ulihudhuriwa na Mawaziri na Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Zanzibar, Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa yenye uwakilishi wao hapa nchini, wadau wa maendeleo , sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikal.

 

 


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.