Sunday, September 29, 2019

DKT. SALIM ATUNUKIWA NISHANI YA JUU YA URAFIKI YA JAMHURI YA WATU WA CHINA

Dodoma, 29 Septemba 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

DKT. SALIM ATUNUKIWA NISHANI YA JUU YA URAFIKI YA JAMHURI YA WATU WA CHINA

Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mheshimiwa Xi Jinping, leo asubuhi tarehe 29 Septemba 2019 amemtunukia Waziri Mkuu Mstaafu Mheshimiwa. Dk. Salim Ahmed Salim, Nishani ya Juu ya Urafiki ya Jamhuri ya Watu wa China ikiwa ni sehemu ya matukio ya maadhimisho ya miaka 70 tangu kuanzishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China iliyofanyika jijini Beijing.  Mheshimiwa Dkt. Salim anakuwa mwafrika wa kwanza kupewa heshima na tuzo hiyo ya juu katika historia ya China.

Nishani hiyo ilipokelewa na Bi. Maryam Salim, Binti ya Dk. Salim Ahmed Salim ambaye pia ni Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Dunia nchini Albania kwa niaba ya Baba yake kutokana na kushindwa kuhudhuria kwa sababu za kiafya. Katika tukio hilo, Serikali ya Tanzania iliwakilisha na Balozi wa Tanzania nchini China Mheshimiwa Mbelwa Kairuki.

Hafla hiyo kubwa ya kitaifa ya kukabidhi nishani ilihudhuriwa na viongozi waandamizi wa Chama na Serikali ya China akiwemo Makamu wa Rais Mheshimiwa Wang Qishan, Waziri Mkuu Mheshimiwa Li Keqiang, Spika wa Bunge Mheshimiwa Li Zhanshu na Wajumbe wote wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China na Baraza la Taifa.

Mbali na Dk.Salim,  wengine waliotunukiwa Nishani ya Urafiki ni pamoja na Kiongozi wa Chama cha Kikoministi cha Cuba Jenerali Raul Castro, Dada wa Mfalme wa Thailand Maha Chakri Sirindhorn, Kiongozi wa Jumuiya ya Urafiki ya China na Urusi Ndugu Galina Kulikova, Waziri Mkuu Mstaafu wa Ufaransa Jean-Pierre Raffarin na Bi  Isabel Crook  kutoka Canada.

Vilevile  Rais Xi alitoa Nishani  ya Jamhuri na Nishani ya Heshima ya Taifa kwa raia 36 wa China kwa kutambua mchango wao mkubwa katika maendeleo ya Taifa la China kupitia kazi zao katika fani mbalimbali.

Nishani ya Juu ya Urafiki ya Taifa la China imetolewa kwa Dkt. Salim  kutokana na mchango wake wa kuiwezesha Jamhuri ya Watu wa China kuwa Mwanachama wa Umoja wa Mataifa mwaka 1971 alipokuwa Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.  Aidha, mchango wa Dk. Salim katika kuimarisha mahusiano kati ya China na Tanzania wakati aliposhikilia nyadhifa mbalimbali umetajwa kama sababu ya kutunukiwa Nishani hiyo. Vilevile, mchango wa Dk.Salim katika kujenga mahusiano kati ya China na Afrika akiwa na nafasi ya Katibu Mkuu wa OAU umetajwa kuwa sababu nyingine ya kutunukiwa Nishani.

Tukio la Kutoa Nishani limetangazwa moja kwa moja na Televisheni zote za Jamhuri ya Watu wa China na kushuhudiwa na watu zaidi ya Milioni 500.

Kwa mujibu wa maelezo ya Balozi wa Tanzania nchini China Ndugu Mbelwa Kairuki Kupitia tukio la leo, mamilioni ya Wachina hususan vijana wamepata fursa ya kufahamu nafasi na mchango wa Tanzania na Bara la Afrika katika historia ya taifa lao. Aidha, tukio la leo limeifanya Tanzania kufahamika kwa watu wengi zaidi nchini China kupitia tukio mara moja. Hatua hiyo itaamsha udadisi na hamasa miongoni mwa Wachina wengi wa kizazi kipya kutaka kuifahamu zaidi Tanzania. Hali hii yaweza kujitafsiri katika fursa kubwa ya kukua kwa utalii, biashara na wawekezaji ikizingatiwa kuwa  wananchi wa China hutoa mwitikio mkubwa kwa nchi ambazo husemwa vizuri na kuthaminiwa na Serikali yao.

Aidha Balozi Kairuki ameeleza kwamba maadhimisho ya miaka 70 ya Jamhuri ya Watu wa China mwaka huu yanaambatana na maadhimisho ya miaka 55 ya urafiki na udugu kati ya China na Tanzania kufuatia kuanzishwa kwa mahusiano rasmi ya kidiplomasia mwaka 1964. Uhusiano wa China na Tanzania uliotokana na uhusiano mzuri wa waasisi wa mataifa haya mawili, Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Hayati Mao Tsetung. Uhusiano huo umeendelezwa na viongozi wa pande zote mbili ambao umekuwa ukiimarika siku hadi siku. Uhusiano huu umekwenda mbali zaidi ya uhusiano kati ya Serikali na Serikali na kushamiri kwa uhusiano wa watu kwa watu.

Ni kwasababu hiyo, katika maadhimisho ya miaka 70 ya Taifa la China, Jumuiya ya Urafiki wa watu wa China na Tanzania ni miongoni mwa Jumuiya za mataifa 17 yenye urafiki wa majira yote na China walioalikwa  kushiriki kwenye maadhimisho hayo na tarehe 1 Oktoba 2019 watakuwa na gwaride lao maalum. Katika jumuiya hizo 17, Kutoka Barani Afrika ni Tanzania na Zambia ndio watahudhuria.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Bi. Maryam Salim mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salim akiwa na Rais wa Jamhuri ya Watu wa China, Mhe. Xi Jinping mara baada ya kupokea tuzo kwa nimba ya Baba yake.


 Bi. Maryam Salim mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Salim Ahmed Salimakiwa na Balozi wa Tanzania nchini China, Mhe. Mbelwa Kairuki mara baada ya kupokea nishani kwa nimba ya baba yake.

Saturday, September 28, 2019

TAMASHA LA JAMAFEST LAMALIZIKA KWA MAFANIKIO

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akitoa hotuba ya kufunga rasmi Tamasha la Nne la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki (JAMAFEST ) lililofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 21 hadi 28 Septemba 2019. Tamasha hilo la aina yake lilizishirikisha nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwemo Burundi, Rwanda, Kenya, Uganda na Tanzania. Wakati wa Tamasha hilo vikundi mbalimbali vya sanaa na utamaduni kutoka nchi hizo vilishiriki. Katika hotuba yake Mhe. Balozi Iddi alitoa rai wadau wa sanaa na utamaduni kujikita kwenye ubunifu kwa ajili ya kukuza uchumi kupitia sanaa. Tamasha la JAMAFEST ambalo hufanyika kila baada ya miaka miwili limepangwa kufanyika mwaka 2021 nchini Burundi
Mhe. Balozi Iddi akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bw. Christopher Bazivamo alipowasili kwenye Tamasha la JAMAFEST
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akifuatilia hotuba ya Mhe. Balozi Iddi (hayupo pichani)

Sehemu ya wageni waalikwa wakiwemo viongozi wa dini wakiwa kwenye sherehe za ufungaji wa Tamasha la JAMAFEST
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa

Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akipata maelezo kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Aloyce Nzuki kuhusu Banda la Maonesho la Wizara hiyo  alipotembelea mabanda mbalimbali ya maonesho yaliyofanyika wakati wa Tamasha la JAMAFEST
Mhe. Balozi Iddi akipata maelezo kwenye Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii
Mhe. Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akimsikiliza mmoja wa washiriki wa maonesho alipotembelea Banda la Wizara ya Maliasili na Utalii
Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye banda la Zanzibar
Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye Banda la Rwanda

 

Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye banda la Burundi

Mhe. Balozi Iddi akiwa kwenye banda la Uganda

Msanii Mrisho Mpoto akitumbuiza wakati wa sherehe za kuhitimisha Tamasha la JAMAFEST
Wasanii kwenye JAMAFEST

Watoto kutoka Dodoma wakitumbuiza

PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI AHUTUBIA KATIKA MKUTANO MKUU WA 74 WA BARAZA LA UMOJA WA MATAIFA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akihutubia katika Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akihutubia katika Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika ukumbi wa Umoja wa Mataifa muda muchache kabla ya hutubia katika Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jijini New York, Marekani. Kulia ni Waziri wa Afya wa Zanzibar Mhe. Hamad Rashid Mohamed akifuati na Waziri wa nchi,Ofisi ya Makamu wa pili wa Rais zanzibar, Mhe. Mohammed Aboud Mohammed na nyuma ya Prof. Kabudi ni Balozi Ali Abeid Amani Karume. 

Ukumbi wa mikutano wa Umoja wa Mataifa kunaofanyika Mkutano wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliopo New York,Marekani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (mwenye tai nyekundu katikati) akiwa katika  picha ya pamoja na baadhi ya viongozi muda mfupi baada ya kumaliza kuhutubia katika Mkutano Mkuu wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa,New York Marekani.

Baadhi ya viongozi na watumishi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa New York,Marekani wakiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) muda mfupi baada ya kumaliza kuhutubia katika mkutano mkuu wa 74 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, New York,Marekani.



Thursday, September 26, 2019

PROF. KABUDI AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MKURUGENZI MKUU WA WHO NEW YORK MAREKANI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa pamoja na Dkt. Tedross Adhamon Ghebreyesus,Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) kulia ni Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa Balozi Modest Mero. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwa katika mazungumzo na Dkt. Tedross Adhamon Ghebreyesus,Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO).Mazungumzo hayo yamefanyika New York, Marekani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiagana na  Dkt. Tedross Adhamon Ghebreyesus,Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) mara baada ya kumaliza mazungumzo walipokutana Jijini New York Nchini Marekani.


Wednesday, September 25, 2019

PROF. PALAMAGAMBA JOHN KABUDI KATIKA PICHA YA PAMOJA NA RAIS WA MAREKANI DONALD TRUMP NA MKEWE

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Marekani Donald Trump na Mkewe Melania. Prof. Palamagamba John Kabudi yuko New York Marekani kuhudhuria mutano wa 74 wa Baraza la Umoja wa Mataifa.

TANZANIA KUNUFAIKA NA DOLA ZA KIMAREKANI MILIONI 120 KUPAMBANA NA SELI MUNDU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ubalozi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioko New York Marekani.

Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir akimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Hayupo Pichani) wakati wa mazungumzo yao yaliyofanyika katika Ubalozi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioko New York Marekani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika kikao na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir. Mazungumzo hayo yamefanyika katika Ubalozi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioko New York Marekani.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika  
Ubalozi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioko New York Marekani.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika  Ubalozi wa kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulioko New York Marekani 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.

MAREKANI KUTOA DOLA ZA MAREKANI MILIONI 120 KUPANDA NA UGONJWA WA SELI MUNDU (SICKLE CELL)

Tanzania ni miongoni mwa baadhi ya Nchi zinazotarajiwa kunufaika na kiasi cha dola za Kimarekani milioni 120 zilizotengwa na Serikali ya Marekani kwa ajili ya utafiti wa kupambana na ugonjwa wa  seli mundi (sickle cell).

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi jijini New York Nchini Marekani.

Admiral Brett ameutaja mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi kama mwanzo mpya wa ushirikiano baina ya Tanzania na Marekani na kuongeza kuwa Nchi yake ina nyenzo zote ikiwemo teknolojia ya kuoambana na maradhi ya seli mundu ili kuboresha Maisha ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa katika siku za hivi karibuni Tanzania imekuwa ikipiga hatua chanya katika kuimarisha masuala mbalimbali ya afya za wananchi wake na kwamba ni azma ya Marekani kuona kuwa ugonjwa wa seli mundo unapata tiba.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amesema utafiti na hatimae tiba ya maradhi hayo ya seli mundu kwa kiasi kikubwa itainufaisha Tanzania kutokana na kushika nafasi ya tatu katika Bara la Afrika na ya nne duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wa seli Mundu.

Ameongeza kuwa Tanzania na Marekani zitashirikiana katika kufundisha na kujengeana uwezo wa namna ya kupambana na maradhi ya seli mundu lakini pia kutafuta fedha zitakazowezesha upatikanaji wa dawa ya seli mundu kutokana na ukweli kuwa dawa za ugonjwa huo kwa Tanzania ni miongoni mwa dawa muhimu yaani essential drugs ili iweze kuwafikia wananchi wengi na kwa bei nafuu.

Amezitaja Nchi zilizo na idadi ya watoto wengi wanaozaliwa na ugonjwa wa seli mundu ambapo kwa Afrika Tanzania ni ya tatu baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Nigeria nay a nne duniani baada ya India.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
New York,Marekani
25 Septemba 2019

Tuesday, September 24, 2019

MATUKIO MBALIMBALI KATIKA TAMASHA LA JAMAFEST LINALOENDELEA JIJINI DAR ES SALAAM

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Eliabi Chodota akitoa mchango wake wakati wa warsha kuhusu namna utamaduni unavyochangia uchumi na maendeleo ya nchi za kanda ya Afrika Mashariki na namna ya kutangaza utalii kupitia sanaa na utamaduni iliyofanyika sambasamba na Tamasha la Sanaa na Utamaduni la Jumuiya ya Afrika Mashariki maarufu kama JAMAFEST linaloendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Tamasha hilo ambalo lilifunguliwa rasmi na Makamu wa Rais tarehe 22 Septemba 2019 linatarajiwa kumalizika tarehe 28 Septemab 2019. 
Watoa mada na wachangiaji wakiwa kwenye warsha hiyo iliyojadili kwa kina masuala ya mila na tamaduni zinavyoweza kuchangia uchumi wa nchi za Afrika Mashariki
Sehemu ya washiriki wa warsha 
Washiriki wakifuatilia mada zilizowasilishwa kwenye warsha hiyo
Sehemu nyingine ya washiriki
Wanafunzi nao wakishriki warsha hiyo iliyojadili masuala kuhusu Utamaduni
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Dkt. Harrison Mwakyembe akipata maelezo kutoka kwa washiriki wa maonesho ya bidhaa zinazotengenezwa kwa mikono wakati wa tamasha la JAMAFEST linaloendelea kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam
Washiriki wa maonesho ya bidhaa mbalimbali za utamaduni wakiwa kwenye mabanda yao wakati wa Tamasha la JAMAFEST 2019
Sanaa za Utamaduni kama zinavyoonekana kwenye  Tamasha la JAMAFEST
Vinyago katika banda mojawapo la Tanzania
Sanaa za maonesho kama zinavyoonekana

PROF. KABUDI AMUWAKILISHA RAIS DKT. JOHN POMBE MAGUFULI UNGA


  Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi akifuatilia Mkutano wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu upatikanaji wa huduma za afya kwa wote ambao unafanyika sambamba na mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York, Marekani.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb) akiwa katika Mkutano wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu upatikanaji wa huduma za afya kwa wote ambao unafanyika sambamba na mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York, Marekani.


 Baadhi ya wajumbe wanaoshiriki katika Mkutano wa viongozi wa ngazi ya juu kuhusu upatikanaji wa huduma za afya kwa wote ambao unafanyika sambamba na mkutano wa 74 wa Baraza kuu la Umoja wa Mataifa New York, Marekani. Katika Mkutano huo Tanzania inawakilishwa na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb)


NAIBU WAZIRI DKT DAMAS NDUMBARO AMUAGA BALOZI WA QATAR NCHINI TANZANIA

Balozi wa Qatar nchini Tanzania,Balozi Abdulla Jassim Al-Madadadi akibadilishana nyaraka na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro wakati alipomtembelea Naibu Waziri kwa lengo la kumuaga katika ofisi ndogo za Wizara zilizopo Jijini Dar es Salaam
Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Damas Ndumbaro akiongea na Balozi wa Qatar nchini Tanzania, Balozi Abdulla Jassim Al-Madadadi ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi wakati alipowasili katika ofisi ndogo za Wizara zilizopo Jijini Dar es Salaam ambapo pamoja na mambo mengine, mazungumzo hayo yalilenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya Tanzania na Qatar.  




NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI AMUAGA BALOZI WA QATAR NCHINI TANZANIA.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro amemuaga Balozi wa Qatar hapa nchini Mhe. Balozi Abdulla Jassim Al-Madadadi ambaye amemaliza muda wake, na kuahidiana kudumisha mahusiano ya kidiplomasia na biashara.

Akiongea wakati wa hafla ya kumuaga Balozi wa Qaatar ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi nchini, Dkt. Ndumbaro amemshukuru Balozi Al-Madadadi kwa kumaliza muda wake wa uwakilishi vizuri na kumpongeza kwa kazi nzuri aliyoifanya ya kudumisha mahusiano kati ya Tanzania na Rwanda katika kipindi chake cha uwakilishi. 

Nae Balozi wa Qatar amemwambia Dkt. Ndumbaro kuwa "Nchi za Tanzania na Qatar zitaendelea kudumisha siyo tu mahusiano ya kidiplomasia bali kushirikiana katika sekta ya biashara na kukuza uchumi wa nchi zote mbili" 

Mhe. Balozi ameeleza kufurahishwa na uhusiano mzuri uliopo baina ya nchi yake na Tanzania na kupongeza hatua mbalimbali ambazo Rais wa Jamhuri ya Muungano Dkt. John Pombe Magufuli ameendelea kuzichukua katika kuimarisha mahusiano hayo.