Friday, September 13, 2019

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI INDIA WASHIRIKI KONGAMANO LA BIASHARA NA UWEKEZAJI JIJINI CHENNAI

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akihutubia wakati wa Kongamano la kuvutia Biashara, Uwekezaji na Utalii lililofanyika katika hoteli ya Westin Jijini Chennai katika Jimbo la Tamil Nadu hivi karibuni. Kongamano hilo limeandaliwa na Shirikisho la Viwanda nchini India [Confederation of Indian Industry (CII) ambapo jumla ya wafanyabiasha 110 walihudhuria.
Kongamano likiendelea
Mhe. Balozi Luvanda (wa pili kulia) akiwa na Viongozi walioshriki Kongamano la kuvutia biashara, uwekezaji na utalii lililofanyika jijini Chennai nchini India
Meza kuu

========================================================================

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda amewakaribisha wafanyabiashara ba wawekezaji kutoka India kuja kuwekeza nchini kwani Tanzania imefanya mabadiliko makubwa katika sera zake za  kukuza biashara na kuvutia wawekezaji kutoka nje ikiwemo kuanzishwa kwa Wizara mahsusi inayosimamia masuala ya Uwekezaji.

Mhe. Balozi Luvanda ametoa rai hiyo wakati akihutubia Kongamano la kuvutia Biashara, Uwekezaji na Utalii lililofanyika katika hoteli ya Westin Jijini Chennai katika Jimbo la Tamil Nadu tarehe hivi karibuni. Kongamano hilo liliandaliwa na Shirikisho la Viwanda nchini India [Confederation of Indian Industry [CII] ambapo jumla ya wafanyabiasha 110 walihudhuria.

Mhe. Balozi Luvanda alieleza kuwa, kwa kiasi kikubwa mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji nchini Tanzania yameboreshwa ikiwa ni pamoja na Serikali kufanyia kazi changamoto mbalimbali zilizokuwepo kwa wawekezaji na wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi. Jitihada hizo zinafanywa na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli za kuiwezesha Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati na viwanda ifikapo mwaka 2025.

Mhe. Balozi Luvanda alitumia fursa hiyo kuwaomba wafanyabiashara hao kuongeza ushirikiano na Tanzania katika  sekta ya biashara na utalii, hasa ikizingatiwa kuwa zaidi ya watalii milioni 20 wanaotembelea nchi mbalimbali duniani kwa mwaka wanatokea India, ikilinganishwa na watalii milioni 1.5 wanaoingia nchini Tanzania kwa mwaka.  
Pia ametoa wito kwa wafanyabiashara hao kutumia fursa ya kuanza safari za moja kwa moja za ndege za Shirika la Ndege la “Air Tanzania” kutoka Dar es Salaam kwenda Mumbai kuongeza idadi ya  watalii  wa India kutembelea Tanzania na kwa wawekezaji wake kuja kuwekeza katika hoteli na fukwe za Tanzania.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.