Tuesday, January 31, 2023

UBALOZI WA UFARANSA WAFUNGUA OFISI NDOGO JIJINI DODOMA


Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipowasili eneo la Kilimani jijini Dodoma kwa ajili ya kufungua rasmi Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika makao makuu tarehe 31 Januari 2023

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa na Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui wakati nyimbo za Taifa za Tanzania na Ufaransa zikipigwa  alipowasili eneo la Kilimani jijini Dodoma kwa ajili ya kufungua rasmi Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika makao makuu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa na  Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akizindua rasmi Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika eneo la Kilimani jijini Dodoma 



Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akizungmza wakati wa uzinduzi rasmi wa Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika eneo la Kilimani jijini Dodomaakisikilizwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax  na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rose Senyamule wa (kwanza kushoto) 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa jijinii Dodoma 

Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi wa ofisii ya Uwakilishi ya Ubalozi wa ufaransa wakifuatilia tukio hilo

Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax baada ya kukamilika kwa hafla ya uzinduzi wa  Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa jijini Dodoma  tarehe 31 Januari 2023

 




 


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) ameupongeza Ubalozi wa Ufaransa nchini kwa kufungua Ofisi Ndogo ya Uwakilishi jijini Dodoma na kuzihamasisha Balozi nyingine kuendelea kuitikia wito wa kuhamia Makao Makuu ya Nchi.

Akizungumza katika ufunguzi wa Ofisi hiyo, Mhe. Dkt. Tax amesema anaupongeza ubalozi huo kwa kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alioutoa mwanzoni mwa mwaka 2023 wa kuwasihi Mabalozi kuhamia Makao Makuu ya Serikali jijini Dodoma.

“Tuko hapa kwa ajili ya kufungua Ofisi ndogo za Uwakilishi za Ubalozi wa Ufaransa nchini, baada ya Serikali kuhamia rasmi Dodoma, ofisi hii ni ya tatu baada ya zile za Ujerumani na China, niwapongeze sana kwa uamuzi wenu huu, mmeiunga mkono Serikali katika kuhamia kwake hapa Dodoma’, alisema Dkt. Tax.

Dkt. Tax ameuhakikishia na kuuahidi Ubalozi huo kuwa, Serikali itatoa msaada wowote watakaouhitaji ili kuiwezesha ofisi hiyo kufanya kazi zake kwa ufanisi na kwamba Serikali itaendelea kushirikiana nao katika kuhakikisha ndoto ya kuwa na ubalozi kamili inakamilika.

Amesema  hatua ya kufunguliwa kwa Ofisi hiyo ni muhimu katika kuimarisha uhusiano na urafiki uliopo baina ya Tanzania na Ufaransa  na kwamba ina dhamira ya kuupeleka uhusiano huo katika ngazi nyingine.

Ameeleza kuwa tayari Serikali imewapatia viwanja na hati Balozi zote na Taasisi za Kimatifa zenye uwakilishi nchini na kuongeza kuwa Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika jiji la Dodoma ili kuhakikisha Jiji hili linakuwa na miundombinu na huduma bora za kijamii zinazotosheleza mahitaji ya wakazi wake wote.

Ameongeza kusema ana imani kuwa wito wa Serikali wa kuhamia makao makuu ya nchi utaenziwa na kuungwa mkono na Balozi na Mashirika ya Kimataifa na kuihakikishia jumuiya ya wanadiplomasia nchini kuwa Serikali itatoa msaada wowote utakaohitajika ili kurahisisha uhamiaji wao jijini Dodoma.

Naye Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui amesema Ufaransa imefungua Ofisi yake jijini Dodoma ikiwa ni hatua za kuunga mkono uamuzi wa Serikali ya Tanzania wa kuhamishia Makao Makuu yake jijini humo, lakini pia kurahisisha huduma mbalimbali za kibalozi kwa wananchi wa Dodoma na mikoa jirani.

Amesema wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha uhusiano kwa manufaa ya pande zote mbili na kuahidi kuwa Ufaransa kupitia Shirika lake la Maendeleo la AFD itaendelea kushirikiana na Serikali katika jitihada zake za kuboresha na kuinua maisha ya wananchi wa Tanzania kupitia Sekta za Maji, Nishati, Afya, Kilimo na Elimu kwa Tanzania Bara na Zanzibar

Kufunguliwa kwa Ofisi hizo kunafanya Dodoma kuwa na ofisi tatu za Ubalozi baada ya zile za Ujerumani na China. Ofisi hizo ambazo zipo eneo la Kilimani jijini Dodoma zitatoa huduma mbalimbali kwa Serikali na wananchi wote kwa ujumla na zinajumuisha pia Ofisi za Shirika la Msaada la Ufaransa la Agence Francaise de Development (AFD).

 



TANZANIA INASHIRIKIANA NA COMESA KUPITIA AfCFTA- BALOZI MBAROUK

Naibu Waziri Mmambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akijibu swali bungeni jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023


Tanzania inaendelea kushirikiana na nchi zinazounda Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) kupitia utekelezaji Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) na pia kupitia Utatu unaoundwa na nchi za COMESA, Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Momba, Mhe. Condester Michael Sichalwe aliyetaka kujua kwa nini Tanzania haioni haja ya kujiunga tena na COMESA.

Amesema Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi 19 zilizokuwa waanzilishi wa Jumuiya ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) mwaka 1994. Hata hivyo, Tanzania ilijitoa katika COMESA mwaka 2000 kwa sababu ilikuwa ni mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambapo baadhi ya nchi za jumuiya hizo pia ni wanachama wa COMESA.

Ameongeza kusema Tanzania pia ilijitoa COMESA baada ya kujiridhisha kuwa nchi haitaathirika kiuchumi kwa kuwa bado ni mwanachama wa EAC na SADC na kwamba lengo ni kulipunguzia taifa gharama hasa michango ya uanachama kwenye Jumuiya hizo.

Pia amesema kitendo cha Bunge cha kuridhia kwa Mkataba wa kuanzisha Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA) hapo mwezi Septemba 2021, kunaifanya Tanzania kuendelea kushirikiana na nchi za COMESA.

“Ikumbukwe kuwa mwaka 2008 nchi za COMESA, EAC na SADC zilikubaliana kuanzisha Utatu na hivyo Tanzania inaendelea kushirikiana na COMESA kupitia Utatu huo wa COMESA–EAC-SADC,” alisema Mhe. Mbarouk.

 


FURSA ZA UTAFITI NCHINI JAPAN


 

TANZANIA NA FINLAND ZAAHIDI KUIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA BIASHARA

Serikali za Tanzania na Finland zimeahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta zenye maslahi mapana ya kiuchumi kwa wananchi wa nchi hizi mbili ikiwemo biashara, utalii na uwekezaji.

Ahadi hiyo imetolewa katika mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä walipokutana katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023.

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii, teknolojia ya habari na mawasiliano, usafirishaji, afya, kilimo, madini, nishati, elimu, mazingira na tafiti ili kupitia sekta hizo wananchi hususan wa Tanzania wanufaike kiuchumi na kijamii.

Dkt. Tax ameeleza kuwa amefurahishwa na ziara ya Mhe. Mika Lintilä na ujumbe wake nchini ikiwemo ujumbe wa wafanyabiashara alioambatana nao kutoka katika sekta za msingi kwa maendeleo ya pande zote mbili.

“Tanzania na Finland zina ushirikiano wa kihistoria ulioasisiwa kati ya nchi hizo mara baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1962. Tupo tayari kuendelea kushirikiana na Finland katika kujenga uchumi wa kidigitali ili kuyafikia mapinduzi ya viwanda” alisema Dkt. Tax.

Vile vile, ametumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya Finland kwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa 19 wa Nchi za Nordic na Afrika uliofanyika mwezi Juni 2022. Pia ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kushiriki kwenye majukwaa mbalimbali ili kuwasilisha mchango wake katika masuala ya kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake, Mhe. Mika Lintilä ameeleza kuwa Umoja wa Ulaya umetenga fedha kiasi cha Euro Billioni 300 kwa ajili ya kushirikiana na nchi zinazoendelea na zile za Kusini mwa Jangwa la Sahara katika sekta za maendeleo.

Vile vile, ameongeza kuwa tarehe 23 na 24 Februari 2023 kampuni za biashara zipatazo 40 kutoka Finland zitashiriki katika Jukwaa la Wafanyabiashara wa Tanzania na Umoja wa Ulaya litakalofanyika jijini Dar es Salaam.

Wakati huo huo, Waziri Lintilä amekutana na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ambapo viongozi hao wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uwekezaji ili kukuza uwiano wa biashara kati ya nchi hizi mbili ambao bado ni mdogo.

Pia Dkt. Kijaji ameongeza kuwa, Tanzania itaendelea  kuongeza samani ya bidhaa zake kama mbao, chakula na madini ili kuziwezesha kuingia katika soko la kimataifa ikiwemo Finland.

Waziri Lintilä yupo nchini kwa ziara ya siku nne (4) ambapo ameambatana na kundi la wafanyabiashara wapatao 18 kutoka katika sekta mbalimbali za kiuchumi ili kujionea maeneo mbalimbali ya uwekezaji  na biashara.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (kati)akizungumza na Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä (hayupo pichani)  katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bw. Albert Philip.

Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä (kulia) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (hayupo pichani) katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023. Pembeni ya Mhe. Lintilä ni Balozi wa Finland nchini, Mhe. Theresa Zitting.

Mazungumzo yakiendelea.

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisalimiana na Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023. 

Dkt. Tax akimkabidhi zawadi Mhe.Mika Lintilä


Monday, January 30, 2023

DIPLOMATIC CORPS IN TANZANIA REMINDED TO OBSERVE THE VIENNA CONVENTION

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (katikati), Naibu Waziri Mhe. Balozi  Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Balozi Fatma Rajab (kulia) wakiwa kwenye Mkutano na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab  akizungumza wakatika wa Mkutano kwenye Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza  kwenye Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya Mabalozi wa Wakifuatilia Mkutano 
Sehemu ya Mabalozi wa Wakifuatilia Mkutano 
Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini ukiendelea jijini Dodoma
Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini ukiendelea jijini Dodoma
Balozi wa Rwanda hapa nchini Mhe. Meja Jenerali Charles Karamba akichangia jambo  kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma. 
Balozi wa Ujerumani hapa nchini Mhe. Regine Hess akichangia jambo  kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma
Sehemu ya Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Balozi wa Rwanda hapa nchini Kanali Mstaafu Fredy Mwesigye akichangia jambo  kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma. 
Sehemu ya Mabalozi wa Wakifuatilia Mkutano 
Mwakilishi wa Ubalozi wa Marekani hapa nchini akichangia jambo kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma
Meza Kuu wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini mara baada ya Mkutano baina  yao, Wizara na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Meza Kuu wakiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini mara baada ya Mkutano baina yao, Wizara na Mabalozi wanaoziwakilisha Nchi zao hapa nchini uliofanyika jijini Dodoma
Meza Kuu wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza  na Waandishi wa Habari mara baada ya  Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akifafanua jambo kwenye Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.





 

Sunday, January 29, 2023

WAZIRI WA MASUALA YA UCHUMI WA FINLAND AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

Waziri wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä amewasili nchini kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 29 Januari hadi tarehe 1 Februari 2023. 

Lengo la ziara hiyo ni kujadili masuala yenye maslahi kwa Tanzania na Finland ili kuimarisha ushirikiano wa pande mbili kupitia Programu ya sasa ya Ushirikiano wa Maendeleo na biashara na kukuza ushirikiano wa kibiashara katika sekta ya biashara na uwekezaji.

Mhe. Lintilă akiwa nchini anatarajia kukutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Dkt. Stergomena Tax, Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Pindi Chana, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Nnauye, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Prof. Adolf F. Mkenda.

Viongozi wengine ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa, Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe,  Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC); Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Shirika la Umerne Tanzania (TANESCO).

Waziri wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kwa ziara ya kikazi ya siku tatu kuanzia tarehe 29 Januari hadi tarehe 1 Februari 2023

Waziri wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä akimsikilza Balozi wa Finland Nchini, Mhe. Zitting Maria Theresa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä akimsikilza Balozi wa Finland Nchini, Mhe. Zitting Maria Theresa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Masuala ya Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Tapani Lintilä akiteta jambo na Balozi wa Finland Nchini, Mhe. Zitting Maria Theresa baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam


Friday, January 27, 2023

TANZANIA, INDIA KUFUNGUA FURSA MPYA ZA BIASHARA

Tanzania na India zimeonesha dhamira ya kufanya kazi kwa karibu katika kutafuta njia bora za kufungua fursa mpya za biashara na uwekezaji kwa maslahi ya pande zote mbili. 

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (Mb.)  amesema kufunguliwa kwa soko la parachichi nchini India mwaka 2022 ni miongoni mwa mifano ya hatua zilizochukuliwa za kuimarisha biashara kati ya Tanzania na India. 

Balozi Mbarouk amesema hayo wakati wa sherehe za maadhimisho ya miaka 74 ya Jamhuri ya India zilizofanyika tarehe 26 Januari 2023 katika Ofisi za Ubalozi wa India Jijini Dar es Salaam.

“India ni mshirika wa tatu kwa ukubwa wa kibiashara na Tanzania na imekuwa miongoni mwa wawekezaji watano bora kwa kuwekeza Dola za Kimarekani bilioni 4.58 kwa mwaka 2021/22. Usawa wa kibiashara katika mwaka huo ulikuwa sawa na miradi 630 ya uwekezaji yenye thamani ya Dola za Kimarekani bilioni 3.68 iliyozalisha ajira mpya 60,000,” alisema Balozi Mbarouk

Balozi Mbarouk aliongeza kuwa wawekezaji wa India wameonesha nia ya kuwekezaka nchini Tanzania katika sekta mbalimbali kama vile madini, utalii, viwanda, kilimo, usindikaji wa mazao ya kilimo, nishati, usafirishaji, ujenzi, huduma za fedha na maendeleo ya rasilimali watu umekuwa ukiongezeka kwa kasi. 

“Sekta nyingine wawekezaji wa India walizowekeza nchini Tanzania ni pamoja na afya, elimu, maji, teknolojia ya Habari na mawasiliano. Mfano, Mwezi Juni 2022 tulishuhudia kampuni sita kutoka India zikisaini kandarasi ya uchimbaji wa visima vya maji katika miji 28 vyenye thamani ya Dola za Kimarekani Milioni 500, kukamilika kwa mradi huo kutawawezesha watanzania milioni sita (6) kupata maji safi na salama,” aliongeza Balozi Mbarouk

Amesema Tanzania itaendelea kushirikiana na India katika kuendeleza na kuimarisha misingi ya ushirikiano iliyowekwa na waasisi wa Mataifa yetu mawili, Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Hayati Mahatma Gandhi. “tutaendelea kutafuta maeneo mapya yenye fursa za kushirikiana ili kuimarisha zaidi ushirikiano wetu wa kijamii, kiuchumi na kisiasa,” aliongeza Balozi Mbarouk.

Kwa upande wake Balozi wa India nchini, Mhe. Binaya Srikanta Pradhan amesema India imekuwa na uhusiano mzuri na Tanzania ambapo uhusiano huo umekuwa ni chachu ya maendeleo kwa mataifa yote mawili. 

Balozi Pradhan alisema kuwa katika kipindi cha baada ya uhuru, uhusiano kati ya India na Tanzania umestawi na kuchochea misingi ya kuongezeka kwa uhusiano wa kibiashara na uwekezaji kwa pande zote mbili.

“Tunaendelea kuimarisha ushirikiano katika kuhakikisha nchi hizi mbili zinakua kiuchumi, hivyo ushirikiano wa India na Tanzania ni muhimu katika kukuza uchumi na kuhakikisha maendeleo yanaimarika,” alisema Balozi Pradhan

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akihutubia sherehe za maadhimisho ya 74 ya Jamhuri ya India jana jioni katika Ofisi za Ubalozi wa India Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akihutubia sherehe za maadhimisho ya 74 ya Jamhuri ya India jana jioni katika Ofisi za Ubalozi wa India Jijini Dar es Salaam


Balozi wa India nchini, Mhe. Binaya Srikanta Pradhan akihutubia sherehe za maadhimisho ya 74 ya Jamhuri ya India jana jioni katika Ofisi za Ubalozi wa India Jijini Dar es Salaam

Balozi wa India nchini, Mhe. Binaya Srikanta Pradhan akihutubia sherehe za maadhimisho ya 74 ya Jamhuri ya India jana jioni katika Ofisi za Ubalozi wa India Jijini Dar es Salaam

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk katika picha ya pamoja na kiongozi wa Mabalozi nchini ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comoro nchini, Mhe. Dkt. Ahmada El Badaoui Mohamed pamoja na Balozi wa India nchini, Mhe. Binaya Srikanta Pradhan  



Wednesday, January 25, 2023

CFR WAASWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAKE YA MSINGI

Chuo cha Diplomasia (CFR) kimeaswa kutekeleza majukumu yake ya msingi ili kukifanya chuo hicho kuwa kituo mahiri cha diplomasia.

Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) alipotembelea chuo hicho kilichopo Jijini Dar es Salaam na kuzungumza na watumishi wake.

Dkt. Tax amekitaka chuo hicho kifanye tafiti mahsusi za kusaidia utatuzi wa changamoto mbalimbali kwenye jamii hususani za kistratejia na kiintelijensia na kusimamia kwa ukaribu utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa chuo hicho.

Amekitaka chuo kupanua wigo wa programu kutokana na ongezeko la wanafunzi ambao wanahitaji kujiunga na chuo hicho na kuandaa mpango wa kitaifa wa kutekeleza diplomasia ya uchumi. 

“Chuo kinapaswa kiongeze wigo wa mafunzo yake kama vile kutoa mafunzo ya strategia, kifanye tafiti mahsusi na kutoa ushauri kwa serikali na wadau wengine katika sehemu ya strategia na diplomasia,……….tafiti hizo zitachangia kuimarisha diplomasia na kuweka mikakati ya pamoja ya kukabili changamoto zinazoikabili Serikali katika eneo hilo,” alisisitiza Dkt. Tax

Aidha, Dkt. Tax ameongeza kuwa, kila mhadhiri na mtumishi chuoni hapo anapaswa kuzingatia maadili na sheria kwani maadili ni sehemu muhimu katika eneo la kazi na kuongeza kuwa kwa kufanya hivyo wataweza kutoa wahitimu wenye maadili na tabia njema ambayo ni sifa kwa chuo.

Dkt. Tax pia amewahahakishia watumishi wa Chuo hicho kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na chuo hicho katika kuhakikisha kinaboresha mazingira yake ili kiendelee kuzalisha wanadiplomasia wabobezi watakao endeleza sifa nzuri ya chuo hicho nchini, kitaifa na kimataifa.

Akizungumza katika kikao hicho Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Diplomasia, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi amesema chuo  hicho ni muhimu katika kutoa mafunzo ya uhusiano wa kidiplomasia na kuongeza kuwa kwa sasa chuo kinaendelea kuboresha muundo wake na mitaala ili kukifanya kuwa bora zaidi.

“Mhe. Waziri kwa sasa tuna jukumu la kukibadilisha chuo chetu kuwa taasisi ya kitaaluma na kimkakati, hii ni moja kati ya hatua za utekelezaji wa maelekezo ya viongozi wakuu,” alisema Balozi Mwinyi.

Awali Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Felix Wandwe alisema chuo kinaendelea kuandaa miundo mbalimbali ya kuboresha mazingira ya kufundishia na kuboresha mbinu za kuwanoa wanadiplomasia chuoni hapo.

Aidha, Dkt. Wandwe ameishukuru Serikali kwa kuendelea kukilea chuo hicho na kukiwezesha kuzalisha wanadiplomasia wazalendo wanaopeperusha vyema bendera ya Tanzania kitaifa na kimataifa. 

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Wangwe aiomba Serikali kukiwezesha chuo hicho kutatua changamoto ya wakufunzi wa masomo ya lugha za kigeni hususan Kireno na Kifaransa.  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akiongea na watumishi wa Chuo cha Diplomasia (hawapo pichani) Jijini Dar es Salaam  

Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Diplomasia, Balozi Ramadhani Muhongwa Mwinyi akizungumza  na watumishi wa Chuo cha Diplomasia (hawapo pichani) Jijini Dar es Salaam 

Kikao cha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na watumishi wa Chuo cha Diplomasia kikiendelea Jijini Dar es Salaam 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akikabidhi vitabu kwa Mwenyekiti wa Baraza la Chuo cha Diplomasia, Balozi Ramadhani Muhongwa Mwinyi na Kaimu Mkuu wa CFR, Dkt. Felix Wandwe

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akikagua mradi wa ujezi wa madarasa ya kufundishia katika Chuo cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa Chuo cha Diplomasia Jijini Dar es Salaam