Wednesday, January 11, 2023

BALOZI FATMA ATETA NA BALOZI WA ALGERIA

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Ahmed Djellal katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Januari 2023. 

Pamoja na mambo mengine, viongozi hao walijadili kuhusu masuala mbalimbali ya kuimarisha uhusiano wa kihistoria uliopo baina ya Tanzania na Algeria kwa maslahi mapana ya pande zote mbili.

Kwa upande wake Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Ahmed Djellal aliongea kuhusu masuala mbalimbali ya ushirikiano baina ya Algeria na Tanzania hususani diplomasia ya kimataifa, kukuza na kuimarisha biashara, uwekezaji na utalii baina ya nchi zetu mbili.

“katika mazungumzo yetu leo, tumekubaliana kuendelea kuimarisha diplomasia baina ya mataifa yetu kwa maslahi mapana ya nchi zetu na kwa maendeleo ya wananchi wetu,” amesema Balozi Djellal .

Balozi Fatma amesema kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana na Algeria katika sekta mbalimbali kama vile za nishati, elimu, afya na miundombinu kwa maendeleo ya mataifa yote mawili.

Algeria ilifungua Ubalozi wake nchini Tanzania mwaka 1964 ikiwa ni miongoni mwa nchi za mwanzo kabisa kufungua ubalozi hapa nchini. Mwaka 1981 nchi hizi mbili zilianzisha Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) ambayo imechangia kuimarisha na kukuza ushirikiano wake na Tanzania.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akimsikiliza Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Ahmed Djellal walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Januari 2023

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika picha ya pamoja na Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Ahmed Djellal baada ya kumaliza mazungumzo yao katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika picha ya pamoja na Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Ahmed Djellal baada ya kumaliza mazungumzo yao katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Afisa Mambo ya Nje Wizarani Bi. Khadija Othman. 

Balozi wa Algeria nchini, Mhe. Ahmed Djellal akiagana na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.