Wednesday, September 30, 2015

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA


 
Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 

    
20 KIVUKONI FRONT,P.O. BOX 9000,
       11466 DAR ES SALAAM, 
                                    Tanzania.


Taarifa zaidi ya Mahujaji kutoka Tanzania huko Saudi Arabia

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa masikitiko makubwa imepokea majina mengine mawili ya  Mahujaji kutoka Tanzania waliofariki dunia kufuatia tukio la mkanyagano wa Mahujaji lililotokea eneo la Mina, Makkah tarehe 24 Septemba, 2015 na kupelekea vifo vya Watanzania kufuatia tukio hilo kufikia watu saba (7) hadi sasa.

Majina ya Mahujaji hao ni Bw. Athumani Mateso Chaulana na Bw. Ahmed Said Bawazir ambao kupitia picha zao wametambulika kuwa wamefariki dunia.

Aidha, Wizara imepokea majina mapya 19 ya Mahujaji kutoka Tanzania ambao bado hawajaonekana. Itakumbukuwa kuwa tarehe 29 Septemba, 2015 Wizara ilitoa taarifa za kupatikana kwa majina 18 ya Mahujaji wa Tanzania ambao ni kati ya 50  ambao bado hawajaonekana. Kupatikana kwa majina hayo kunafanya idadi ya Mahujaji waliopotea na majina yao kutambulika kufikia 37.

Orodha ya majina mapya 19 ya Mahujaji wa Tanzania ambao mpaka sasa bado hawajaonekana ni kama ifuatavyo:-

1.  Juma Bajuka
2.  Masoud Juma
3.  Issa Amir Faki
4.  Juma Jecha Dabu
5.  Nassor Mohammed Hemed
6.  Mohamed Awadh Namongo
7.  Juma Bakula
8.  Said Habib
9.  Hamis Juma Shamte
10.              Khadija Hamad
11.              Rahma Salim
12.              Hadija Abdallah Sefu
13.              Farida Khamis
14.              Laila Manunga
15.              Bi. Hawa Amrani Khamis
16.              Saida Awadhi
17.              Maimuna Seleman Ruwaly
18.              Jalia Kassim Mashule
19.              Nuru Omar Karama

Mbali na taarifa za kupatikana kwa majina hayo, Wizara imepokea taarifa ya kuonekana Mahujaji saba wakiwa hai. Mahujaji hao ni:-

1.  Ali Abdulrahman (Abidina)
2.  Abdallah Hassan Pande
3.  Suleiman Ali Kidogoli
4.  Mohammed Salum
5.  Mwadini Hassan
6.  Habiba Ramadhan Ali (Maulana)
7.  Ramadhan Muhsin

Ubalozi kwa kushirikiana na Tanzania Hajj Mission na Vikundi vya Mahujaji unaendelea na juhudi za kuwatambua Mahujaji wengine wa Tanzania ambao hawajaonekana kwa kutembelea katika hospitali zilizohifadhi maiti na kulaza majeruhi wa ajali hiyo ikiwa ni pamoja na kuhakiki picha za mahujaji waliofariki ili kubaini Mahujaji kutoka Tanzania.

Wizara inapenda kufafanua kuwa, orodha inayotolewa si kamili kwa maana kwamba inaweza kuongezeka kwa vile baadhi ya majina ya Mahujaji yaliwayowasilishwa Ubalozini na ndugu wa mahujaji waliopotea hayamo katika orodha hii. Pia Ubalozi unaendelea kuwasiliana na vikundi vilivyopeleka Mahujaji ili kuweza kupata taarifa kamili na sahihi ya jumla ya Mahujaji wote ambao hawaonekani.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam
30 Septemba, 2015


Mkurugenzi wa Asia na Australasia na Balozi wa India wajadili maandalizi ya India- Africa Summit

Mkurugenzi wa Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Mbelwa Kairuki (kulia) akiwa katika mazungumzo na Balozi wa India nchini, Mhe. Sandeep Arya. Mazungumzo yao yalihusu pamoja na mambo mengine, ushiriki wa Serikali ya Tanzania katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Kiafrika na India utakaofanyika jijini New Delhi, India tarehe 26 - 29 Oktoba 2015.

Mazungumzo kati ya Balozi wa India na Balozi Kairuki yanaendelea. Wengine katika picha, kulia ni Bw. Emmanuel Luangisa, Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na kushoto ni Afisa wa Ubalozi wa India wakifuatilia mazungumzo hayo.


Balozi wa India nchini, Mhe.Sandeep  Arya akiagana na Balozi Kairuki mara baada ya kukamilisha mazunguzmo yao yaliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Tanzania yazindua rasmi Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu

Mratibu wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Bw. Alvaro Rodriguez, akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa Malengo ya  Maendeleo Endelevu  (SDGs), Naibu Katibu Mtendaji, Ofisi ya Rais, Tume ya Mipango, Bw. Paul Kessy (kushoto) na Kamishna wa Mipango wa Zanzibar, Bw. Ahmed Makame (kulia). Uzinduzi huo  rasmi uliofanyika  hapa nchini katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam unafuatia uzinduzi uliofanywa na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Mataifa Mjini New York, Marekani tarehe 25/09/2015. Malengo hayo 17 ya miaka 15 yamerithi Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) yaliyomaliza utekelezaji wake mwaka huu.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya MAmbo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya akiwa pamoja na baadhi ya wadau wa maendeleo kutoka Mashirika ya Kimataifa na Balozi mbalimbali zilizopo nchini waliohudhuria uzinduzi wa Malengo ya Maendeleo Endelevu ( SDGs) iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam.
Mmoja wa wawakilishi wa vijana akiuliza swali kuhusu utekelezaji wa Malengo hayo hapa nchini
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani (UNFPA), Dkt. Natalia Kanem akifafanua jambo katika kipindi cha maswali na majibu.
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Bi. Joyce Mends-Cole naye akijibu moja ya swali lililoulizwa wakati wa uzinduzi wa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Simba Yahya (wa pili kushoto) akiwa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (kulia), Kamishna wa Mipango wa Zanzibar, Bw. Ahmed Makame ( wa pili kulia) na Balozi wa  Ireland nchini , Mhe. Fionnuala Gilsenan (kushoto)  kwa pamoja wakifunua pazia maalum kuashiria uzinduzi rasmi wa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu  ( SDGs).
Wakishangilia baada ya kuzindua rasmi Malengo hayo hapa nchini.
Shamra shamra za uzinduzi zikiendelea. 
Mabalozi, Viongozi wa Serikali, Waandishi wa Habari na baadhi ya wanafunzi kutoka Shule ya Msingi Uhuru Mchangayiko  wakiwa kwenye picha ya pamoja huku wakiinua juu vibao vilivyoandikwa Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu  ( SDGs). Malengo hayo ni pamoja na Kuondokana na Umaskini;Kuondokana na Njaa; Kuondokana na Magonjwa; Kutunza na kuhifadhi Mazingira; Elimu Bora; Usawa wa Kijinsia na kuwawezesha wanawake na wasichana; Huduma Bora za Jamii ikiwemo upatikanaji wa maji safi na salama;kukuza uchumi na kuongeza ajira; kupambana na mabadiliko ya tabianchi na upatikanaji wa nishati endelevu.
Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Uhuru Mchangayiko walioshiriki kutengeneza tangazo maalum la kuelimisha jamii kuhusu Malengo 17 ya Maendeleo Endelevu  ( SDGs).
Meza kuu katika picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Picha na Reginald Philip

Taarifa kwa Vyombo vya Habari


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
 
Simu: 255-22-2114615, 211906-12
Barua pepe: nje@nje.go.tz
Barua pepe: gcu@nje.go.tz

Nukushi: 255-22-2116600

              

 

 
20 KIVUKONI FRONT,
P.O. BOX 9000,
      11466 DAR ES SALAAM, 
                                    Tanzania.


Taarifa za kupatikana kwa majina 18 ya Mahujaji kutoka Tanzania waliopotea huko Saudi Arabia

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imepokea majina 18 ya Mahujaji kutoka Tanzania ambao hadi sasa hawaonekani kufuatia tukio la mkanyagano wa Mahujaji lililotokea eneo la Mina, Makkah tarehe 24 Septemba, 2015 na kusababisha vifo vya watu 769 na wengine 934 kujeruhiwa.

Itakumbukwa kuwa tarehe 28 Septemba, 2015 Wizara ilitoa taarifa kuwa Mahujaji wa Tanzania wapatao 50 bado hawajaonekana huku wengine watano wakiwa wamefariki dunia.

Majina ya baadhi ya Mahujaji wa Tanzania ambao mpaka sasa bado hawajaonekana ni kama ifuatavyo:-

1. Abdul Iddi Hussein
2. Awadh Saleh Magram
3. Burhani Nzori Matata
4. Yussuf Ismail Yusuf
5. Saleh Mussa Said
6. Adam Abdul Adam
7. Archelaus Antory Rutayulungwa
8. Farida Khatun Abdulghani
9. Rashida Adam Abdul
10. Hamida Ilyas Ibrahim
11. Rehema Ausi Rubaga
12. Faiza Ahmed Omar
13. Khadija Abdulkhalik Said
14. Shabinabanu Ismail Dinmohamed
15. Salama Rajabu Mwamba
16. Johari Mkesafiri Mwijage
17. Alwiya Sharrif Salehe Abdallah
18. Hafsa Sharrif Saleh Abdallah

Mbali na taarifa za kupatikana kwa majina hayo, Wizara imepokea taarifa ya kutambuliwa kwa mwili wa hujaji mmoja wa Tanzania anayeitwa Hadija Shekali Mohammed wa kikundi cha Ahlu Daawa.

Aidha, Serikali ya Saudi Arabia imetoa picha za maiti za Mahujaji waliokufa Makkah ambao wamehifadhiwa katika vyumba vya kuhifadhia maiti kwa ajili ya utambuzi. Hivyo, Ubalozi wa Tanzania nchini humo kwa kushirikiana na Tanzania Hajj Mission pamoja na vikundi vya Mahujaji unaendelea na zoezi la kuzihakiki picha hizo ili kubaini kama zinalingana na sura za Mahujaji wetu waliopotea.

Vilevile, Mamlaka ya Serikali ya Saudi Arabia imesema kuwa imechukua alama za vidole za Mahujaji waliokufa ili wazilinganishe na zile walizozichukua Uwanja wa Ndege wakati Mahujaji hao wakiingia nchini humo. Wizara inaamini kuwa taarifa za alama za vidole zitakapotolewa zitasaidia sana kuwatambua Mahujaji wetu.

Pamoja na jitihada zote hizo, Ubalozi pia unaendelea na juhudi za kuwatambua Mahujaji wengine wa Tanzania ambao hawajaonekana kwa kutembelea katika hospitali zilizohifadhi maiti na kulaza majeruhi wa ajali hiyo.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali kwa Umma,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam

29 Septemba, 2015

President Kikwete Addresses the United Nations General Assembly

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania Addresses the 70th Session of the United Nations General Assembly Tuesday September 29, 2015, United Nations, New York

http://gadebate.un.org/70/united-republic-tanzania

Ambassador Liberata Mulamula, Hon. Sophia Simba and Super Model Flaviana Matata of Tanzania congratulating President Kikwete after his address at the United Nations General Assembly.


STATEMENT BY HIS EXCELLENCY DR. JAKAYA MRISHO KIKWETE, PRESIDENT OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA, AT THE GENERAL DEBATE OF THE SEVENTIETH SESSION OF THE UNITED NATIONS GENERAL ASSEMBLY, NEW YORK, 29 SEPTEMBER 2015
Theme:  “The United Nations at 70: the road ahead for peace, security and human rights

Your Excellency, Mr. Mogens Lykketoft, President of the General Assembly;
Your Excellency, Mr. Ban Ki-moon, United Nations Secretary-General;
Excellencies Heads of State and Government;
Distinguished Delegates;
Ladies and Gentlemen;
I join those who spoke before me in congratulating you, on your well-deserved election to preside over the 70th Session of the General Assembly. Your election is a fitting tribute to your distinguished political career, having served as a Finance Minister, Foreign Minister and recently as Speaker of the Danish Parliament. It is also a reflection of the high regard this august Assembly has for your great country, Denmark. I would like to assure you of my country’s full support and cooperation in discharging your duties and responsibilities.
Mr. President;
I wish to pay glowing tribute to your predecessor Hon. Sam Kahamba Kutesa, Minister for Foreign Affairs of the Republic of Uganda for the outstanding manner in which he steered the affairs of the sixty-ninth session of the Assembly. Indeed, this great son of the African soil has done us proud. A deserving word of appreciation also goes to our illustrious Secretary-General His Excellency Ban Ki Moon and his staff, for their dedicated service and efforts in promoting the ideals and principles of the Charter of the United Nations.
Mr. President;
I also commend you, your predecessor and the Secretary General for the excellent work which has culminated into the adoption of the Post 2015 Development Agenda and the 17 Sustainable Development Goals (SDGs) with their 169 targets. We sincerely hope that there will be reliable mechanisms of ensuring availability of means of implementation and follow-up. It was failure to have such mechanisms which was responsible for the short falls in the implementation of the MDGs.
Mr. President;
My delegation welcomes the theme designated for this general debate, namely “The United Nations at 70: the road ahead for peace, security and human rights”.  Indeed, at 70 years the United Nations has not only withstood the test of time but has evolved and become a stronger organization. I am glad we all agree that a lot has been achieved in the past 7 decades. Equally, we agreed that not everything that the founding fathers envisaged the UN would do has been done satisfactorily.
The United Nations has succeeded to prevent another world war but challenges of preserving world peace and security remain. Interstate and intrastate conflicts and wars are many and on the increase. Terrorism has become a serious global threat. There are still too many people who live under conditions of abject poverty, squalor and depravation in a world of unprecedented wealth.
The Partnership Between UN and Regional Organization
Mr. President;
Unlike 70 years ago, today there is better understanding, cooperation and partnership between countries and organizations in preserving peace and security.  It is easier today for the world to come together for a course of peace than it was before.
As a matter of fact most of the conflicts we are witnessing today are being handled, first and foremost, by   regional and sub-regional organizations. The UN, therefore,   must seek to forge strategic partnership with these organizations. By taking advantage of the knowledge these organizations have of the history and nature of the crises, the key players and culture of the people, it would be easier to manage and resolve the conflicts. Where and when appropriate, the   United Nations should invest in strengthening the capacity of these organizations and their member states, in anticipating, detecting, preventing, managing and resolving conflicts. I am of the view that this capacity is urgently needed in Africa.
The Security Council Reform
Mr. President;
We highly commend the President of the Sixty-ninth session of the General Assembly and the Chair of the Intergovernmental Negotiations (IGN) on reform of the Security Council, for efforts made. It is the wish of member states to see an acceleration of the negatiation process during this 70th Session. For the UN Security Council to remain what it was 70 years ago is incomprehensible and, to say, the least, unacceptable. It is high time the demands of the majority of the membership of the United Nations are heard and heeded too. 
We must be mindful of the fact that the credibility of the UN depends on a more agile, representative and responsive Security Council. Let all of us muster political will and accomplish this long overdue task, for the sake of our Organization.  In the mean time we must continue to support the Revitalization of the work of the General Assembly.
Peace Keeping Operation
Mr. President;
Peace keeping operations remain one of the most dependable instruments of promoting world peace and security. I believe it will remain so for many years to come. I am told there are about 125,000 men and women deployed in 16 peacekeeping missions across the world. Tanzania is proud to have contributed 1,322 of these gallant people who often times serve under challenging conditions. Sometimes they are compelled to serve in places where there is little or no peace to keep. Tanzania stands ready to contribute more whenever requested to do so.
Combating Terrorism
Mr. President;
We can not talk about security challenges of today without mentioning terrorism. This is the security challenge that the United Nations and the entire international community must remain vigilant in the coming decade. While reiterating our strongest condemnation of terrorism, in all its forms and manifestations, we believe there is an urgent need to bolster efforts at all levels for fighting the scourge. Collectively, we must aspire to improve our preparedness, collaboration and response to the threat we face.

Global Epidemics
Mr. President;
The Ebola outbreak in West Africa last year is a stark reminder of how dangerous epidemics can be and how vulnerable we are as nations and people. More than 11,000 people lost their lives including citizens of the US and Spain and about 28,000 were infected. The economies of Liberia, Guinea and Sierra Leone were devastated. Economic activities and services almost ground to a halt thus causing gigantic losses to the economies of the three countries. The World Bank estimates that they lost about USD 2.2 billion of their GDP as a result. There were about 7,000 children who lost their parents and about half a million people who became food insecure. More than 5 million children lost valuable schooling and skills-development time.  It requires mammoth recovery efforts to get these economies and societies back to where they were before the outbreak. Unfortunately, many countries in Africa also, suffered irrespective of how far a country is from the three affected countries. The tourist industry has been affected the most.
Mr. President;
The biggest lesson from the handling of this Ebola outbreak in West Africa is that the world needs to be better prepared to prevent and respond to epidemics in future. This was not the case unfortunately. It is in this regard that, we should all commend the Secretary General for the wise decision he took of establishing a High Level Panel on Global Health Crises to come up with recommendations about how the world can respond better to public health emergencies of global concern in future.
I was given the honour of chairing the panel. It is premature for me to report anything substantive now to this august Assembly. We will complete our work in December, 2015 and I am sure our report will be brought before this Assembly for information and action. We look forward to your support.      
US/Cuba Relations
Mr. President;

Tanzania welcomes the historic and momentous decision taken by the United States of America and the Republic of Cuba to restore diplomatic relations and reopen embassies of the two countries in Washington D.C. and Havana.  We join the people of Cuba and the United States in celebrating this landmark achievement.  
We commend President Barack Obama and President Raul Castro for their bold and courageous leadership. The two leaders and countries have proved to all of us, the power of dialogue in finding solutions, even to deep rooted difference and long standing conflicts. We extend best wishes to our US and Cuban friends as they open a new chapter in their bilateral relations. We hope and appeal to the United States to lift the economic embargo which has condemned the people of Cuba to untold socio-economic hardships, poverty and misery for the last 50 years.
Palestine
Mr. President;
In the same vein, it is our wish that Israel and Palestine would resume the dialogue so that their long standing conflict can be resolved peacefully. It is high time the pain and suffering endured by the people of Palestine over the many decades was put to an end. Also, it is about time the people of Israel lived peacefully and harmoniously with their neighbours.
It is regrettable that we are celebrating seventy years of the founding of the United Nations this conflict remains unresolved. Tanzania subscribes and supports the two states solution, with the state of Israel and a sovereign, contiguous and viable state of Palestine living side by side, in peace, security, harmony, mutual recognition, trust and cooperation. We believe it is possible and achievable. We must double our efforts.
The Question of Western Sahara
Mr. President;
         Another outstanding matter which this organisation has to ensure that it does not continue to be left unresolved is the issue of Western Sahara. The lack of movement on the side of the United Nations to implement its decisions on the matter is both regrettable and incomprehensible.  The people of Saharawi have waited for far too long to get the opportunity to determine their fate and future. Let this esteemed Organisation of ours muster political will and pluck up courage to do what it had long decided to do. At seventy years the United Nations is old enough and has accumulated a lot of wisdom and experience to put this matter to rest. Please do it.
A Farewell Message
Mr. President;
On September 20th, 2006, I stood on this very podium, for the first time and addressed this august Assembly as the newly elected fourth President of my dear country: the United Republic of Tanzania.  Today, I am standing here to bid farewell to you all as I am about to leave office at the completion of my two term mandate, as provided for in the Tanzania Constitution.
I thank all of you for the invaluable support and cooperation extended to me, my administration and my country in the past ten years that we have worked together.  Kindly be assured that I will always value each and every one’s contribution. I feel proud to have had the opportunity to work with all of you in promoting the ideals of the United Nations and contributed to the pursuit of world peace, security, stability and development.
As I take leave of you, I would like to assure you that Tanzania shall remain a faithful member and an unwavering supporter of the United Nations’ Organisation.  I am confident that you will find in my successor, a likeable and dependable friend and ally. Please accord him or her the necessary support and cooperation in fulfilling his or her duties and responsibilities.
Conclusion
Mr. President;
The road ahead for peace, security and development remains challenging but worthy the journey. It requires our renewed resolve and reaffirmation of our commitment to the ideals, values and principles laid down by the founding fathers of the United Nations seven decades ago in San Francisco.  All nations, individually and collectively, should endeavour to promote them as we have been doing in the last seventy years. It can be done, play your part.

I thank you.

Hon. Nandi-Ndaitwah Netumbo, Deputy Prime Minister and Minister of Foreign Affairs of the Republic of Namibia congratulating President Kikwete at the UN, New York.
H.E. Wilson Masilingi, Ambassador of the United Republic of Tanzania to the United States of America. 
Ambassador Samwel Shelukindo, Head of Department of Africa, Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation

Eva Ng'itu, Foreign Service Officer responsible for Common Wealth
Justin Kisoka, Foreign Service Officer at the Tanzania Permanent Mission to the United Nations responsible for fith committee