Tuesday, September 8, 2015

Mfalme Letsie III wa Lesotho, atua nchini kwa ziara

 Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb.), akisalimiana na Mfalme Letsie III wa Lesotho, muda mfupi baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, kabla ya kuelekea Jijini Arusha kuhudhuria Mkutano wa Kilele wa Dunia kuhusu Uimarishaji wa chakula (Global Summit on Food Fortification, na kuanza ziara ya siku tatu kuanzia leo 08 hadi 11 Septemba 2015.
Mfalme Letsie III wa Lesotho, akisalimiana na Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Balozi Radhia Msuya, muda mfupi baada ya Mfalme huyo kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
 Mfalme Letsie III wa Lesotho, akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala, muda mfupi baada ya Mfalme huyo kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
 Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb), akiwa ameongozana na mgeni wake, Mfalme Letsie III wa Lesotho, wakielekea chumba cha mapumziko, kabla ya kuelekea Jijini Arusha kuanza ziara ya siku mbili kuanzia leo 08 hadi 11 Septemba 2015.
Mhe. Bernard Membe (Mb), akifanya mazungumzo na Mfalme Letsie III wa Lesotho, kabla ya kuelekea Jijini Arusha kuhudhuria Mkutano wa Kilele wa Dunia kuhusu uimarishaji wa chakula (Global Summit on Food Fortification).
Mhe. Bernard Membe (Mb.), akiagana na mgeni wake, Mfalme Letsie III wa Lesotho.
===============================
PICHA NA REUBEN MCHOME.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.