Saturday, September 16, 2023

NAIBU WAZIRI BYABATO AKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA BIASHARA WA JAMAICA

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith walipokuta pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 16 Septemba 2023

 

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith walipokuta pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 16 Septemba 2023

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith walipokuta pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 16 Septemba 2023

 
Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) katika picha na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 16 Septemba 2023

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) amekutana na kuzungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara wa Jamaica Mhe. Kamina John Smith pembezoni mwa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China unaofanyika jijini Havana nchini Cuba.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wameelezea kuridhishwa kwao na hali ya uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Jamaica na kuahidi kuendelea kushirikiana zaidi ili kuimarisha uhusiano huo.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Byabato amemuelezea Mhe. Smith kuwa Tanzania inaridhishwa na uhusiano mzuri uliopo na kuongeza kuwa kuna haja ya kuhakikisha uhusiano huo wa kidplomasia unaimarishwa na kufikia hatua ya juu.

Amemuhakikishia utayari wa Serikali ya Tanzania kuanzisha Tume ya Kudumu ya Pamoja (JPC) na Jamaica katika maeneo yatakayozinufaisha pande zote mbili.

Pia amemuelezea nia ya Tanzania kupanua wigo wa maeneo ya ushirikiano na kuingiza sekta za uchumi wa buluu, biashara na uwekezaji.

Akizungumza katika kikao hicho Mhe. Smith alisema pamoja na uhusiano mzuri uliopo kati yake na Tanzania, Jamaica inaiomba Tanzania kuiunga mkono katika nafasi mbili inazogombea kimataifa katika Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Bahari (IMO) na Kamati ya Urithi wa Dunia iliyo chini ya UNESCO.

DKT. MWINYI AHUTUBIA MKUTANO WA NCHI ZA KUNDI LA G77+CHINA

 






Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan jijini Havana Cuba tarehe 15 Septemba 2023


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China akizungumza jijini Havana Cuba tarehe 15 Septemba 2023

 



 


Washiriki wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China katika picha ya pamoja jijini Havana Cuba tarehe 15 Septemba 2023


Washiriki wa Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundi la G77+ China katika picha ya pamoja jijini Havana Cuba tarehe 15 Septemba 2023




Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amehutubia Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Kundo la G77+ China akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

 

Akihutubia katika Mkutano huo, Dkt. Mwinyi amesema Sayansi, Teknolojia na Ubunifu ni nguzo muhimu kwa nchi zinazoendelea kujiletea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza kuwa nchi hizo zinaweza kuendelea kiuchumi kupitia maendeleo katika sekta muhimu za kilimo, nishati, elimu, afya, madini, maendeleo ya muindombinu, maji na mazingira.

Mhe. Rais Dkt. Mwinyi amekumbusha namna nchi zinazoendelea zilivyoathirika na janga la maradhi ya UVIKO-19, bidhaa kupanda bei, mizozo ya kisiasa na athari za mabadiliko ya tabia nchi na kuongeza kuwa baadhi ya changamoto zilisababisha kupanda kwa gharama za maisha na kudhoofisha jitahada za kujikwamua kiuchumi.

 

Mhe. Dkt. Mwinyi alikumbushia namna nchi zilizoendelea zilivyobanwa na teknolojia ya kutengeneza chanjo na kunyimwa msaada wa kiteknolojia ili zitengeneze chanjo zao na kusababisha kampuni za kutengeneza dawa za mataifa tajiri kupata faida kubwa kwa kuziuzia nchi zinazoendelea chanjo ya UVIKO-19.å

Mhe.Dkt. Mwinyi amezitanabaisha nchi za kundi la G77+China kuchukua changamoto hizo kama somo na zisibweteke kusubiri msaada kutoka mataifa yaliyoendelea. 

 

Mkutano huo unaofanyika jijini Havana nchini Cuba tarehe 15-16 Septemba 2023 unayakutanisha mataifa yanayoendelea unajadili changamoto zinazoikabili dunia baada ya kuathirika na janga la UVIKO-19 na migogoro inayoendelea duniani na vikwazo mbalimbali vya kiuchumi.  

 

Mkutano huo umejikita kutafuta namna bora ya kujenga ustahimilivu kupitia maendeleo ya sayansi na teknolojia na ubunifu ili kundi la G77+China liweze kufikia malengo yake kwa pamoja.

 

Kaulimbiu ya Mkutani inasema, “Changamoto za Maendeleo: Nafasi ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu”.

Friday, September 15, 2023

TANZANIA ITAENDELEA KUHESHIMU MISINGI YA MTANGAMANO, DKT. BITEKO

Tanzania imeahidi kuwa itaendelea kuheshimu na kusimamia misingi ya mtangamano wa bara la Afrika kama ilivyofundishwa na kuachwa na waasisi wa Taifa hili, ili kufikia Afrika yenye ustawi na umoja.

Hayo yameelezwa leo Septemba 15, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati anafungua Kikao cha Umoja wa Afrika cha Nne cha Kamati Maalumu ya Kitaalam kuhusu Uchukuzi, Miundombinu ya Kikanda na ya Bara, na Nishati kinachofanyika mjini Zanzibar.

Dkt. Biteko aliwambia wajumbe wa kikao hicho ambacho kinalenga kutoa mapendekezo ya kisera na miongozo ya kimkakati katika uendelezaji wa sekta ya miundombinu barani Afrika kuwa, Tanzania ipo katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya miundombinu ambayo msingi wake ni kuimarisha mtangamano baina ya Tanzania na nchi inazopakana nazo, Afrika na dunia kwa ujumla.

Miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa yenye urefu wa kilomita 1,800 inayounganisha Bandari ya Dar es Salaam na nchi jirani za Uganda, Burundi, Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki lenye urefu wa kilomita 1,400 linalounganisha Tanzania na Uganda, Mradi wa Bwawa la Kuzalisha umeme wa Maji la Julius Nyerere litakalozalisha megawati 2,115 kwa ajili ya matumizi ya Tanzania na nchi jirani na kufufua shirika la ndege ambalo kwa sasa lina ndege 12 zinazoiunganisha Tanzania na nchi zisizopungua 9 za Afrika.

Dkt. Biteko alisisitiza umuhimu wa nchi za Afrika kushirikiana ili kufikia matarajio ya mamilioni ya Waafrika ya kuwa na miundombinu ya uhakika. Kufanikisha hilo, Dkt. Biteko alitoa wito kwa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, washirika wake na wabia wa maendeleo kuimarisha juhudi za utafutaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi ya miundombinu ambayo ni muhimu katika kuimarisha biashara, kuongeza ajira na kukuza uchumi barani Afrika. 

Awali, wakati wa uzinduzi wa ripoti ya miaka 10 ya utekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Miundombinu Barani Afrika (PIDA), wajumbe waliainisha masuala mbalimbali ya kuzingatia ili awamu ya pili ya mpango huo, uweze kufanikiwa. Masuala hayo ni pamoja na kuwa na sera zinazoendana na mabadiliko ya dunia, kushirikisha sekta binafsi katika ujenzi wa miundombinu na kupeana taarifa muhimu ili kufanikisha uandaaji na utekelezaji wa miradi ya kipaumbele ya miundombinu.

Kufanyika kwa mkutano huo nchini ni jitihada za Serikali ya awamu ya sita kupitia Ubalozi wake nchini Ethiopia, chini ya uongozi wa Balozi Innocent Shiyo za kukuza diplomasia ya uchumi na utalii wa mikutano. 

Wajumbe takribani 400 kutoka barani Afrika; washirika wa maendeleo, kama Benki ya Maendeleo ya Afrika, Exim Bank; Kamisheni ya Uchumi ya Afrika; watafiti na wanazuoni wa fani mbalimbali duniani wameshiriki mkutano huo.

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akisoma hotuba ya ufunguzi wa Kikao cha Umoja wa Afrika cha Nne cha Kamati Maalumu ya Kitaalam kuhusu Uchukuzi, Miundombinu ya Kikanda na ya Bara, na Nishati kinachofanyika mjini Zanzibar
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko na wajumbe wengine katika meza kuu wakiimba Wimbo wa Taifa wakati wa ufunguzi wa Kikao cha Umoja wa Afrika cha Nne cha Kamati Maalumu ya Kitaalam kuhusu Uchukuzi, Miundombinu ya Kikanda na ya Bara, na Nishati kinachofanyika mjini Zanzibar

Wajumbe wakiimba Wimbo wa Taifa ambao ni pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Innocent Shiyo (wa tatu kushoto na Balozi wa Tanzania, Jamhuri ya Sudan, Mhe. Silima Kombo Haji (wa pili kushoto)

Kamishina wa Miundombinu na Nishati wa Umoja wa Afrika, Bibi Amani Abou-Zeid akihutubia Kikao cha Umoja wa Afrika cha Nne cha Kamati Maalumu ya Kitaalam kuhusu Uchukuzi, Miundombinu ya Kikanda na ya Bara, na Nishati kinachofanyika mjini Zanzibar


Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Erick Ngilangwa na Bi. Maria Ndumbalo wakifuatilia kwa makini hotuba za ufunguzi


Wajumbe wakisikiliza hotuba za ufunguzi

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akiagana na baadhi ya wajumbe wanaoshiriki Kikao cha Umoja wa Afrika cha Nne cha Kamati Maalumu ya Kitaalam kuhusu Uchukuzi, Miundombinu ya Kikanda na ya Bara, na Nishati baada ya kufungua kikao hicho




TANZANIA ,CUBA ZAKUBALIANA KUSHIRIKIANA ELIMU YA JUU NA KUFUNDISHA KISWAHILI NCHINI CUBA

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Waziri wa Elimu ya Juu wa Cuba Mhe. Dkt. Walter Garcia wakisaini hati ya makubaliano ya ushirikiano kati ya Tanzania na Cuba kupitia elimu ya juu

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato na Waziri wa Elimu ya Juu wa Cuba Mhe. Dkt. Walter Garcia wakionesha hati ya makubaliano ya ushirikiano waliyosaini kati ya Tanzania na Cuba kupitia elimu ya juu

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam Prof. William Anangisye na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Havana Prof. Miriam Garcia wakionesha Hati ya Makubaliano waliyosaini ya ushirikiano kati ya vyuo hivyo katika hafla ya uzinduzi wa Ubalozi wa Tanzania jijini Havana nchini Cuba tarehe 14 Septemba 2023






Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Cuba zimesaini Hati za Makubaliano ya kushirikiana kupitia elimu ya juu, kubadilsihana wakufunzi na wanafunzi na kufundisha lugha ya kiswahili nchini Cuba na kutengeneza kamusi ya kiswahili na kihispaniola.

Makubaliano hayo yamesainiwa wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Cuba iliyofanyika jijini Havana na kushuhudiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa.

Makubaliano hayo yamesainiwa na Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato kwa niaba ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na Waziri wa Elimu ya Juu wa Cuba Mhe. Dkt. Walter Garcia.

Makubaliano mengine yaliyosainiwa ni kati ya Chuo Kikuu cha Dar es Salam kilichowasilishwa na Makamu Mkuu wa chuo hicho Prof. William Anangisye na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Havana Prof. Miriam Garcia

Katika makubaliano hayo Tanzania na Cuba zimekubaliana kushirikiana katika masuala ya kubadilishana ujuzi na uzoefu kupitia wahadhiri, wanafunzi, masuala ya utafiti, sayansi, teknolojia, kufundisha lugha ya Kiswahili katika Chuo Kikuu cha Havana na kutengeneza kamusi ya lugha ya Kiswahili na Kispaniola ili kusambaza matumizi ya kugha ya kiswahili nchini Cuba na nchi nyingine zinazozungumza lugha ya kispaniola.

Akizungumza katika hafla ya utuaji saini makubaliano hayo Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humphrey Polepole amesema Ubalozi wa Tanzania Havana unajivunia kusainiwa kwa makubaliano hayo ambayo yanatoa mwongozo maalum wa jinsi ya kutekeleza mpango wa kufundisha lugha ya Kiswahili nchini humo.

"Haya ni mafanikio makubwa kwetu, Ubalozi wa Tanzania Havana unajivunia kusainiwa kwa makubaliano haya, sasa yatatoa mwongozo   maalum utakaowezesha taasisi husika za elimu ya juu kutekeleza kikamilifu mpango wa kusambaza na kueneza lugha ya Kiswahili  nchini Cuba," alisema Mhe. Balozi Polepole.

Makubaliano yaliyosainiwa ni kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Cuba ambapo Chuo Kikuu cha Havana kilikubaliana na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kushirikiana katika masuala ya utafiti, sayansi na Teknolojia na kufanya kazi kwa pamoja ili kutunga Kamusi ya Kiswahili na Kihispaniola.

 

Makubaliano mengine yaliyosainiwa ni kati ya Wizara ya Elimu Sayansi na Teknojia na Wizara ya Elimu ya Juu ya nchini Cuba ambayo yatawezesha ubadilishanaji wa wanafunzi, wahadhiri na watafiti katika eneo la sayansi na teknolojia ili kuwawezesha wahusika kubadilishana ujuzi na uzoefu katika maeneo hayo na hivyo kuleta tija na ufanisi kwa pande zote mbili.


 



DKT. MWINYI AZINDUA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI CUBA


 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.  Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba wakizindua Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Havana nchini Cuba katika hafla iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.  Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa wakikata utepe wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Cuba iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.  Dkt. Hussein Ali Mwinyi akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano nchini Cuba kwa ajili ya kuzindua  Ubalozi huo katika hafla iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023 kulia kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humphrey Polepole na kushoto ni Mke wa Mhe. Dkt. Mwinyi Mama Mariam Mwinyi

 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Havana nchini Cuba wakati wa hafla ya uzinduzi wa ubalozi huo iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.  Dkt. Hussein Ali Mwinyi akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa akizungumza wakati wa hafla ya kuzindua Ubalozi wa Tanzania nchini Cuba iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano nchini Cuba iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023



 

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.  Dkt. Hussein Ali Mwinyi amezindua Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Havana katika hafla iliyofanyika jijini Havana tarehe 14 Septemba 2023.

 

Akizungumza katika uzinduzi wa Ubalozi huo Mhe. Rais Dkt. Mwinyi amesema kufunguliwa kwa Ubalozi huo mwaka 2019 kunaonesha nia ya Tanzania ya kuendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Cuba na kujibu kitendo cha Cuba ilipofungua Ubalozi wake nchini mwaka 1962.

 

 

“kufunguliwa kwa Ubalozi huu mwaka 2019 kunaonesha nia ya Tanzania ya kuendelea kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia uliopo kati ya Tanzania na Cuba na kujibu kitendo cha Cuba ilipofungua Ubalozi wake nchini mwaka 1962,” alisema Dkt. Mwinyi.

 

Amesema kufunguliwa kwa ubalozi huo mwaka 2019 kunarahisisha uratibu wa shughuli za nchi zetu katika kuimarisha ushirikiano wa maendeleo ya kijamii na kuwaletea maendeleo wananchi wa nchi hizo.

 

 

Dkt. Mwinyi ameishukuru Wizara ya Mambo ya Nje ya Cuba na Serikali ya Jamhuri ya Cuba kwa ushirikiano mkubwa ambao imekua ikiupatia Ubalozi wa Tanzania Havana tangu ulipoanzishwa mwaka 2019 hadi wakati huu kitu ambacho kimeuwezesha Ubalozi huo kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

 

“Kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania namshukuru Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba, Wizara ya Mambo ya Nje ya Cuba na Serikali ya Jamhuri ya Cuba kwa ushirikiano mkubwa ambao imekua ikiupatia Ubalozi huu tangu mwaka 2019 ulipofunguliwa, kitendo hicho kimeuwezesha Ubalozi wetu kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi,” alisema Dkt. Mwinyi.

 

Akiongea katika hafla ya uzinduzi wa Ubalozi huo Makamu wa Rais wa Cuba Mhe. Salvador Valdes Mesa amesema Serikali ya Jamhuri ya Cuba inauthamini uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Tanzania na itaendelea kufanya hivyo kwani uhusiano uliopo ni wa kindugu na wa kihistoria na kufanya hivyo ni kuwaenzi waanzilishi wa mataifa hayo.

 

“Mhe. Rais na Wananchi wote wa Tanzania, Serikali ya Cuba inauthamini uhusiano na ushirikiano uliopo kati yake na Tanzania na itaendelea kuuthmini, uhusiano wetu ni wa Kindugu na wa kihistoria na kufanya hivi ni kuwaenzi waanzilishi wa mataifa yetu,” alisema Mhe. Mesa

 

Mhe Mesa amesema Serikali ya Cuba inaipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uamuzi wake wa kufungua Ubalozi nchini Cuba na kuahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania na kuuwezesha Ubalozi huo kufanya kazi na kufikia malengo ya kuanzishwa kwake.

 

Akizungumza awali Balozi wa Tanzania nchini Cuba Mhe. Humphrey Polepole amesema Tanzania itaendelea kuimarisha uhusiano wake na Cuba uhusiano ambao ni wa kindugu na hasa ikizingatiwa kuwa Cuba ilikuwa miongoni mwa nchi za kwanza kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia na Tanzania.

 

Amesema Tanzania imeendelea kushirikiana na Cuba katika sekta ya Afya na elimu ambapo wamekuwa wakibadilishana wataalamu kuanzia miaka ya 1960 hadi nyakati hizi kwa ajili ya kusaidia jamii za kitanzania katika eneo hilo.

 

 

Uzinduzi wa Ubalozi huo wa Tanzania Havana  uliofunguliwa mwaka 2019 ulihudhuriwa na Jumuiya ya Wanadiplomasia mbalimbali walioko jijini Havana.

 

 


Thursday, September 14, 2023

BALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI AZUNGUMZA NA ALIYEKUWA MWAKILISHI MKAZI WA UNDP MALAWI

Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na aliyekuwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Malawi, Bw. Shigeki Komatsubara ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi nchini humo mara baada ya mazungumzo baina yao yaliyofanyika katika Ubalozi wa Tanzania, Lilongwe hivi karibuni
===================================================================

Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola amekutana kwa mazungumzo na aliyekuwa Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Malawi, Bw. Shigeki Komatsubara ambaye amemaliza muda wake wa uwakilishi nchini humo.

 

 

Lengo la mazungumzo yao ambayo yalifanyika katika Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Lilongwe hivi karibuni, lilikuwa ni kumuaga Bw. Komatsubara na kujadili ushirikiano kwenye maeneo mbalimbali.

 


Katika mazungumzo yao, Balozi Kayola alimshukuru Mwakilishi huyo Mkazi kwa kufika kumuaga rasmi na kumtakia kila la kheri anapokwenda kuwa Mwakilishi Mkazi wa UNDP nchini Tanzania. Vile vile, alimpongeza Bw. Komatsubara kwa kumaliza muda wa uwakilishi nchini Malawi kwa mafanikio na kuahidi kuendelea kushirikiana nae anapotekeleza majukumu yake nchini Tanzania.

 


Kadhalika Mhe. Balozi alimweleza Mwakilishi Mkazi kuwa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) ni moja ya mashirika muhimu ya maendeleo yanayothaminiwa sana na Serikali ya Tanzania, hivyo anategemea kuendelea kufanya kazi na kushirikiana nae ili kusaidia Tanzania kufikia malengo ya maendeleo. Alimueleza kuwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, anaendelea kuleta mabadiliko chanya kwenye sekta zote muhimu nchini na matokeo yake yanaonekana.

 


Bw. Komatsubara aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kuweka mipango ya Taifa inayoakisi mabadiliko ya dunia na kuipongeza Serikali kwa kuimarisha mikakati ya maendeleo kwa ajili ya kuboresha maisha ya Watanzania.

 


Pia alimshukuru Balozi Kayola kwa kutenga muda kuzungumza nae na aliahidi kuendelea kushirikiana na Ubalozi hata atakapokuwa nchini Tanzania. Aidha, ameuomba Ubalozi umpe ushirikiano mrithi wake hapa Malawi, Bi. Fenella Frost. 

 


Sunday, September 10, 2023

UBALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI WATUMIA SIKU YA AFRIKA KUTANGAZA FURSA NA UTAMADUNI WA TANZANIA


Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mhe. Agnes Kayola (mwenye nguo yenye nakshi za bendera ya Tanzania) akimshuhudia Waziri wa Viwanda na Biashara wa Malawi, Mhe. Simplex Chithyola akionja chakula cha kitanzania wakati wa maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika yaliyofanyika jijini Lilongwe tarehe 09 Septemba 2023. Ubalozi wa Tanzania umeshiriki maadhimisho hayo kwa kutangaza fursa za uwekezaji, utalii kupitia Filamu ya The Royal Tour na kuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili.
 Mhe. Chithyola akifurahia chakula cha kitanzania alipotembelea banda la Tanzania wakati wa  Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika yaliyofanyika jijini Lilongwe hivi karibuni. Wengine katika picha ni Mhe. Balozi Kayola na wageni wengine waliotembelea Banda la Tanzania.

   
Picha ya pamoja
Picha ya pamoja

========================================

Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  nchini Malawi umeshiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Umoja wa Afrika yaliyofanyika jijini Lilongwe tarehe 9 Septemba, 2023. 

 

Katika kutangaza Diplomasia ya Uchumi, Ubalozi wa Tanzania ulitumia fursa hiyo kutangaza fursa za Uwekezaji, kuhamasisha matumizi ya Lugha ya Kiswahili na kutangaza vivutio vya Utalii kwa kuonesha Filamu ya The Royal Tour. 


Kadhalika Ubalozi ulishirikiana na Watanzania Diaspora wanaoishi Malawi kuonesha  Utamaduni wa Tanzania ikiwemo vyakula vya asili. 



Banda la Ubalozi wa Tanzania lilitembelewa na wageni wengi ambao walipendezwa na vyakula vya asili kutoka Tanzania. 

 

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo alikuwa  Waziri wa Viwanda na Biashara wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Simplex Chithyola.