Thursday, October 30, 2014

IOM yakabidhi vifaa vya Kompyuta Wizarani

Mkurugenzi wa Idara Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza na Mkurgenzi wa Shirika la Kimataifa Ia Uhamiaji (I.O.M), Bw. Damien Thuriaux ofisini kwake alipokuja kukabidhi vifaa vya kompyuta kwa ajili ya Wizara.
Mazungumzo yakiendelea kati ya Balozi Mushy na Damien Thuriaux, huku Bibi Naomi Zegezege, Afisa Mambo ya Nje akinukuu.
Balozi Celestine Mushy akipokea moja ya vifaa hivyo.

Wataalam wa Masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano wa Wizara wakishuhudia makabidhiano hayo
Picha ya pamoja.


Wednesday, October 29, 2014

PRESS RELEASE

H.E. Dilma Rousseff, President of Brazil


PRESS RELEASE

H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to Her Excellency Dilma Rousseff on the occasion of her re-election as President of the Federative Republic of Brazil.

The message reads as follows.

“Her Excellency Dilma Rousseff
  The President of the Federative Republic of Brazil,
  Brasilia,

  BRAZIL.

I have received with great pleasure the news of your re-election to the highest office of your country. On behalf of the Government and people of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, I wish to convey my sincere and warmest congratulations to You and through you to the Government and the people of the Federative Republic of Brazil for your election to the Presidency of Brazil.

Your re-election is a sign of the trust and confidence that the people of Brazil have in your leadership qualities. As you continue discharging the noble duties bestowed upon you, I would like to assure Your Excellency of my continued co-operation in further strengthening the bilateral relations that so happily exist between our two countries.

Please accept, Your Excellency, my personal regards and best wishes for your continued good health and success”.


ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

29TH OCTOBER, 2014

PRESS RELEASE

H.E. Recep Tayyip Erdogan, President of Turkey


PRESS RELEASE

H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to H.E Recep Tayyip Erdogan, President of the Republic of Turkey on the occasion of the National Day of Turkey.

The message reads as follows.

“His Excellency Recep Tayyip Erdogan,
The President of the Republic of Turkey,
Istanbul,
TURKEY.

Your Excellency,

It gives me great pleasure, on behalf of the people and Government of the United Republic of Tanzania and on my own behalf, to extend cordial congratulations to You, and through you to the Government and the people of the Republic of the Turkey on the occasion of the 91st Anniversary of the Proclamation of the Republic of Turkey.

Our historic bilateral relations are multifaceted and cooperate in many areas such as education, agriculture, trade, tourism and transportation.
 
On this special occasion, I wish to cherish and celebrate these bilateral relations that exist between our two countries. Let me also take this opportunity to assure you that the Government of Tanzania remains committed to maintain and consolidating these relations for the mutual benefit of the people of our two countries.

Please accept, Your Excellency, my personal regards and best wishes for your continued good health and success”.


ISSUED BY: THE MINISTRY OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION, DAR ES SALAAM

29TH OCTOBER, 2014

Tuesday, October 28, 2014

TANZANIA YAKATAA RASMI NDOA ZA JINSIA MOJA KWENYE AGENDA ZA MAENDELEO YA MILENIA

Mkurugenzi wa Idara Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy akizungumza kwenye warsha ya siku moja kuhusu Malengo ya Milenia kwa washiriki mbalimbali na kwa kiasi ngani Tanzania imeweza kufikia malengo hayo.
“Watanzania na Afrika kwa ujumla inataka malengo ya millennia na haki za binadamu zizifike mahali kuwadharirisha watu kutoka bara hili kwa kuruhusu mambo yanayokwenda kinyume na historia yao, mila na desturi za mwafrika,”aliongeza.
Kwa upande wake, Mhadhiri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Osward Mashindano amesema kwamba malengo ya milenia kwa kiasi kikubwa yamefikiwa na Tanzania hasa katika upande wa elimu na kupunguza vifo vya wakinamama na watoto wakati wa kujifungua.
“leo tumekutana hapa kuzungumza ni kwa kiasi ngani nchi yetu ya Tanzania imefikia malengo ya milenia na changamoto ni zipi katika malengo mapya ambayo ni 17 badala ya 8 ya awali,” aliongeza
Dkt Mashindano alifafanua kwamba ni lazima sasa serikali kutazama katika Nyanja za ubora katika huduma hizi muhimu kwa jamii baada ya kufikia lengo la kuandikisha watoto wenye umri wa kwenda shule kwa asilimia 85.
Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa, Wanawake, Anna Collins akitoa hotuba yake wakati akifungua warsha ya siku moja kuhusu Malengo ya Milenia kwa washiriki mbalimbali na kwa kiasi ngani Tanzania imeweza kufikia malengo hayo.iliofanyika Makao Makuu ya Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii nchini (ESRF) Oktoba 27, 2014 jijini Dar es Salaam.
Na Mwandishi wetu
SERIKALI ya Tanzania imekataa rasmi kutambua ndoa za jinsia moja (ushoga) kama moja ya agenda za maendeleo katika malengo ya milenia 2015 mpaka 2030 katika mkutano wa Umoja wa Mataifa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam kwenye mkutano wa majadiliano ya malengo ya milenia yanayotazamiwa kumalizika mwakani na kuanza malengo mapya, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy amesema serikali ya Tanzania imekataa kutambua ushoga kama moja ya agenda za maendeleo.
“tunatambua haki za binadamu, usawa wa kijinsia kati ya wanaume na wanawake na hata katiba yetu pendekezwa imetoa haki za sawa kati ya wanaume na wanawake lakini katika swala la kutambua ndoa za jinsia moja hilo tumekataa,” amesema Balozi Mushy
Amesema kwamba tumewaambia nchi zilizoendelea na wahisani wa maendeleo katika Umoja wa Mataifa kwamba swala la ndoa za jinsia moja (ushoga) si agenda ya watanzania na si agenda ya maendeleo.
Wadau mbalimbali walioudhuria wakifuatilia mada mbalimbali.

Mhadhiri wa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Osward Mashindano akifafanua umuhimu wa kuwashirikisha wananchi wa ngazi ya chini kuhusu maswala ya malengo ya milenia ili yaweze kufikiwa kwa urahisi zaidi.
Aliongeza kwamba Tanzania na dunia kwa ujumla wameona ni muhimu kuweka agenda ya ubora katika kila agenda za malengo ya milenia kwa nchi zote ambao ni wanachama wa Umoja wa Mataifa.
Dkt Tausi Kida, Mkurugenzi wa Programu wa Taasisi ya Uchumi na Utafiti wa Kijamii, amesema kwamba malengo haya ya milenia ni lazima yaguse maisha ya watu katika ngazi ya chini ili matokeo chanya yaweze kuonekana kwenye jamii
Amesema kwamba ni lazima nchi zilizoendelea ziweke mkazo katika kuhakikisha kwamba nchini zinazoendelea zinajengewa uwezo wa kutafuta fedha za kutimiza malengo ya milenia.

Monday, October 27, 2014

Rais Kikwete atembelea Shirika la Simu la VIETTEL, Hanoi Vietnam

Wafanyakazi wa Shirika la Simu la VIETTEL wakiwa wamejipanga tayari kumpokea Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania muda mfupi kabla ya kuwasili kwenye Makao Makuu ya Shirika hilo Jijini Hanoi, Vietnam Jumatatu Oktoba 27, 2014 



Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Rais Kikwete kwenye mazungumzo na viongozi wa shirika hilo la simu linalomilikiwa na Serikali ya Vietnam. Kutoka kushoto ni Mhe. Lt. Gen. (Mstaafu) Abdurahman Shimbo, Balozi wa Tanzania nchini China na Vietnam; Mhe. Bernard Membe, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Katibu Mkuu Hazina Bw. Servicius Likwelile.

Mhe. Musa Azzan Zungu, Mbunge na pia Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje ya Bunge akijitambulisha wakati wa maongezi rasmi baina ya ujumbe wa Rais Kikwete na viongozi wa Shirika la VIETTEL.






PRESIDENT KIKWETE'S TWO DAYS STATE VISIT TO VIETNAM

H.E Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania is being received by his Vietnamese counterpart and host H.E. Truing Tan Sang, President of the Socialist Republic of Vietnam earlier today. 


H.E. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania in official talks with Secretary General of the Vietnamese Communist Party, Hon. Nguyen Phun Trong at the party's headquarters in Hanoi, Vietnam on Monday October 27, 2014

Friday, October 24, 2014

Sherehe za kuadhimisha miaka 69 UN zafana.

Mgeni rasmi Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka akiwasili kwenye viwanja vya Karimjee huku akiwa ameongozana Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez.
Pichani juu na chini ni Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akimtambulisha mgeni rasmi Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi Profesa Anna Tibaijuka kwa baadhi ya wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini mara baada ya kuwasili kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka akipokea heshima ya wimbo wa taifa kabla ya kuanza rasmi kwa sherehe za maadhimisho miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka akipokea heshima ya wimbo wa taifa kabla ya kuanza rasmi kwa sherehe za maadhimisho miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Wakwanza kushoto ni Mkuu wa Mabalozi nchini na ni Balozi wa Kongo nchini Tanzania, Balozi Juma Mpango, na katikati ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Balozi Rajab Gamah, na wakwanza kulia ni Brigadia Jeneral Dominic Basil Mrope wa JWTZ wakiwa wamesimama wakati Mgeni rasmi akikagua gwaride. 
Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka akikagua gwaride maalum kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake zilizofanyika leo jijini Dar
Mgeni rasmi Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka akisoma risala kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar.
Mkurugenzi Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Mambo ya Nje Balozi Celestine Mushy akimpongeza Mhe. Waziri Tibaijuka mara baada ya kumaliza kusoma hotuba yake.
Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akisoma ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa zilizofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar.
Wageni mbalimbali wakisikiliza hutoba ya Mratibu Mkazi wa mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez


Mshehereshaji wa sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa Maulida Hassan kutoka Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akitoa mwongo wa hotuba mbalimbali kwa meza kuu.
Waziri wa Ardhi , Nyumba na maendeleo ya makazi, Profesa Anna Tibaijuka akishuhudia bendera ya Umoja wa Mataifa ikipandishwa kama ishara ya kuadhimisha miaka 69 ya Umoja wa Mataifa tangu kuanzishwa kwake.
Makamu Mwenyekiti wa Asasi ya Umoja Mataifa (UNA), Bw. Benedict Kikove akizungumza kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 69 ya Umoja wa Mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee jijini Dar.
Viongozi mbalimbali wa Jeshi wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa 
Kikundi cha watoto walemavu wakitoa burudani wakati wa maadhimisho ya miaka 69 ya UN
Viongozi walioko meza kuu wakiwapongeza watoto hao walipo kuwa wakionyesha onyesho lao.
Wadau kutoka Mambo ya Nje nao walikuwepo.


Picha na Reginald Philip

Warsha kuhusu Amani na Usalama Barani Afrika yahitimishwa Jijini Arusha

Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Mnasa Nyerembe akitoa hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mhe. Magese Mulongo ya kufunga Warsha ya siku tatu kuhusu Amani na Usalama Barani Afrika iliyoandaliwa na Umoja wa Afrika na kufanyika katika Hoteli ya Mount Meru Jijini Arusha.
Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Afrika na nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz kwa pamoja na Balozi wa Ethiopia katika Umoja wa Afrika Mhe. Konjit Sinegiorgis wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Nyerembe (hayupo pichani) alipokuwa akifunga Warsha hiyo ya Amani na Usalama Barani Afrika iliyowakutanisha Mabalozi, Wataalam wa masuala ya Amani na Wasuluhishi.
Sehemu nyingine ya Wajumbe wakimsikiliza Mhe. Nyerembe (hayupo pichani) akiwemo Rais Mstaafu wa Cape Verde, Mhe. Pedro Pires (kulia)
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Zuhura Bundala akifuatilia kwa makini hotuba ya kufunga warsha ya amani na usalama iliyokuwa ikitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Nyerembe (hayupo pichani).
Wajumbe waliokuwepo wakati wa kufunga warsha ya amani na usalama.
Kamishna wa Amani na Usalama katika Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Balozi Smail Chergui akitoa neno la shukrani kwa Uongozi wa Mkoa wa Arusha na kwa Serikali ya Tanzania kwa ujumla kwa kuwa mwenyeji wa warsha hiyo ya siku tatu ambapo wajumbe wamenufaika na masuala yote yalijadiliwa pamoja na huduma nzuri.
Balozi Mstaafu, Prof. Joram Biswaro (kulia) akifuatialia hotuba  ya Balozi Chergui (hayupo pichani)

Bi. Shella Mbita, Mtoto wa Balozi Hashim Mbita nae pia alikuwa mmoja wa wajumbe waliohudhuria warsha ya amani na usalama jijini Arusha (Picha zote na Rosemary Malale)

===============================================

Na.  Ally Kondo, Arusha

Warsha ya siku tatu kuhusu Amani na Usalama Barani Afrika iliyoandaliwa na Umoja wa Afrika (AU) imehitimishwa jijini Arusha siku ya Alhamisi tarehe 23 Oktoba 2014. Warsha hiyo ambayo kaulimbiu yake ilikuwa “Silaha zisitumike kuuwa watu Barani Afrika ifikapo mwaka 2020” ilimalizika kwa wajumbe kutoa Rasimu ya Tamko la Arusha (Arusha Declaration). 

Katika Tamko hilo, kumebainishwa asili ya migogoro inayohusu nchi moja au baina ya nchi na nchi nyingine, vitu vinavyochochea migogoro na ukosefu wa utulivu Barani Afrika, wanaochochea na kudhamini migogoro pamoja na athari za maendeleo ya dunia kwa Bara la Afrika.

Aidha, Tamko hilo limeainisha juhudi zinazofanywa katika kukabiliana na vitendo vya siasa kali, uhalifu wa kimataifa na athari za mabadiliko ya tabianchi katika amani na usalama.

Tamko limebainisha pia kuwa migogoro mingi katika nchi za Afrika inasababishwa na ukosefu wa utawala bora katika Serikali, uwajibikaji, uwazi, uongozi shirikishi pamoja na kushindwa kutatua changamoto za umasikini na ukosefu wa usawa.

Kwa mujibu wa Tamko hilo, wajumbe kwa kauli moja walikubaliana na hoja kuwa ili nchi za Afrika ziondokane na matatizo hayo, hazina budi kutekeleza miongozo na maamuzi yanayotolewa na AU kuhusu amani, usalama na uongozi. Walisema kuwa maamuzi hayo yanatoa dira nzuri ya namna ya kukabiliana na changamoto za usalama Barani Afrika, isipokuwa nchi za Afrika hazina utamaduni wa kuyatekeleza.

Hivyo, wajumbe walisisitiza umuhimu kwa nchi wanachama wa AU kutekeleza maamuzi yote yanayofanywa na kuridhiwa na AU, Jumuiya za Kikanda na wadau wengine.

Aidha, walitoa wito kwa nchi wanachama wa AU, Kamisheni ya AU, Jumuiya za Kikanda, Baraza la Amani na Usalama la AU na wadau wengine kulipa kipaumbele suala la kuweka utaratibu wa kufanya tathmini ya utekelezaji wa maamuzi hayo.

Sanjari na hayo, wajumbe walipongeza mabadiliko chanya yanayotokea Barani Afrika ikiwa ni pamoja na kupungua kwa migogoro ya kutumia silaha, kuongezeka kwa chaguzi za kidemokrasia, kukua kwa uchumi na ongezeko la kasi ya kupambana na vitendo vya ufisadi katika nchi nyingi za Afrika.

Licha ya maboresho hayo, wajumbe walielezea wasiwasi wao   kuhusu tishio linalotokana na changamoto mpya katika amani na usalama wa Bara la Afrika. Walihimiza umuhimu wa kutumia mbinu za kibunifu kukabiliana na changamoto hizo ambazo ni; uhalifu wa kimataifa kama vile ugaidi, uharamia, biashara haramu ya binadamu, biashara ya silaha na dawa za kulevya na biashara ya fedha haramu.

Wakati wa kufunga warsha hiyo ambayo iliwakutanisha Mabalozi, wasuluhishi, wajumbe maalum, wawakilishi wa Jumuiya za Kimataifa na wasomi mbalimbali, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, Mhe. Mnasa Nyerembe alielezea matumani yake kuwa, washiriki walipata fursa nzuri ya kujadili kwa kina chanzo cha migogoro Barani Afrika na kupendekeza njia muafaka za kukabiliana nayo. Alisisitiza umuhimu wa mapendekezo hayo kuingizwa katika sera za kitaifa, kikanda na kimataifa ili yaweze kuwa na manufaa.

-Mwisho-


President Kikwete accorderd rousing Karibu, as China's President Xi Jinping formaly welcomes him to Beijing

President Xi Jinping of China welcomes President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete to the Great Hall of the People in Beijing this evening during the official formal reception at the climax of the State visit at the invitation of the Chinise Leader
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and the First Lady Mama salma Kikwete pose for an official photograph with their  host China's President Xi Jinping and his wife China's First Lady Peng Liyuan shortly after they arrived for an official formal reception at the Great Hall of the People in Beijing this evening

President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and his host Chinese President Xi Jinping inspects a guard of honor mounted China's People Defense force in Beijing this evening during a formal reception at the Great Hall of the people. President Kikwete is on a State Visit to China invitation of  President Xi Jinping.
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete and his host President Xi Jinping waves to the cheering crowd during a formal reception for the President and his delegation held at the Great Hall of  the People in Beijing at the climax of his State visit today 
President Dr. Jakaya Mrisho Kikwete introduces former OAU/AU Secretary General Salim Ahmed Salim to China's President Xi Jinping during the formal reception held at the Great Hall of the People in Beijing this evening Left is the Minister for Foreign Affairs Mr Bernard Membe and second left is CCM Secretary General Abdulrahman Kinona.





==========================================================================

China ya yamwaga neema kubwa kwa Tanzania

Jamhuri ya Watu wa China leo, Ijumaa, Oktoba 24, 2014, imetangaza neema kubwa kwa Tanzania, ikiwa ni pamoja na kutoa dola za Marekani milioni 85 kwa ajili ya shughuli za maendeleo na kusaidia Tanzania kufanya mageuzi ya viwanda.

Neema hiyo kwa China kwa Tanzania imetangazwa na Rais Xi Jinping wa nchi hiyo katika mazungumzo rasmi ya Kiserikali kati yake na ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ambaye yuko katika ziara rasmi ya siku sita katika China

Mazungumzo hayo kwenye jumba la The Great Hall of the People yamefanyika baada ya Rais Kikwete kukaribishwa rasmi katika Jamhuri ya Watu wa China kwa kupokelewa na Rais Xi Jinping katika eneo la East Plaza ya Jumba hilo.

Katika mapokezi hayo yakuvutia na kusisimua, Rais Kikwete amepigiwa mizinga 21 na kukagua gwaride la ukakamavu la Jeshi la Ukombozi la Wananchi wa China la People's Liberation Army.
Katika mazungumzo hayo, Rais Xi Jinping alitangaza kuwa China itaipatia Tanzania kiasi cha dola milioni 85 ikiwa ni mchanganyiko wa msaada na mkopo usiokuwa na riba, fedha ambazo Tanzania itaamua yenyewe jinsi gani yakuzituma.

"Katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania kuboresha maisha ya wananchi wake, napenda kutangaza kuwa Jamhuri ya watu wa China itatoa kiasi cha RMB milioni 200 ikiwa ni msaada na RMB 200  milioni nyingine zikiwa ni mkopo ni mkopo usio kuwa na riba kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kiasi cha RMB 100 milioni za msaada kwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambazo zitatumika kwa kadri Serikali hizo mbili zitakavyoamua,'' amesema Rais Jinping.

Rais huyo wa China pia ametangaza kuwa nchi hiyo itaisaidia Tanzania katika uendelezaji wa maeneo ya uwekezaji ya EPZ, uendelezaji wa miundombinu itaharakisha ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo na itaingia katika shughuli za kutafuta gesi na mafuta katika ukanda wa Bandari ya Hindi katika eneo la Tanzania.

Rais Jinping pia ametangaza kuwa Serikali ya China imefanya uamuzi wa kuikarabati Reli ya Uhuru ya TAZARA inayounganisha Tanzania na Zambia na yenye urefu wa Kilometa 1,860 na kusaidia uendeshaji wa reli hiyo. "Ili kutekeleza uamuzi huu kwa haraka, napendekeza kuundwa kwa kamati ya pamoja ya wataalam kuandaa ramani ya namna ya kuitoa reli hiyo katika matatizo yake ya sasa.''

Rais Jinping ametangaza kuwa Serikali yake itatoa nafasi 100 za masomo ya elimu ya juu kwa wanafunzi kutoka Tanzania katika miaka mitano ijayo, itaongeza idadi ya madaktari ambao China inapeleka Tanzania, itahimiza makampuni zaidi ya China kuwekeza katika Uchumi wa Tanzania na kuzishawishi taasisi za kifedha za China kuanzisha shughuli zake katika Tanzania.

Kiongozi huyo wa China pia ametangaza kuwa nchi yake itajenga Chuo kikubwa cha mafunzo ya ufundi katika Tanzania na itaendeleza kushirikiana na Tanzania katika eneo la uimarishaji wa ulinzi na usalama.

Rais Jinping amesema kuwa urafiki na uhusiano kati ya China na Tanzania ni mfano unaong'ara wa uhusiano mzuri na mwema duniani na kuwa china iko tayari kutoa uzoefu wake wa maendeleo kwa Tanzania bila wasiwasi wowote.

Rais Kikwete amemshukuru sana Rais Jinping na Jamhuri ya watu wa China kwa misaada yake ambayo baadhi yake haikutarajiwa.

Imetolewa na: 
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikuli - Dar es salaam