Saturday, October 4, 2014

Mada mbalimbali za uelimishaji zawasilishwa kwenye Mkutano wa DICOTA

Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Mhe. Liberata Mulamula akiwasilisha mada kuhusu Nafasi ya Ubalozi wa Tanzania katika kutoa Huduma kwa Watanzania waishio ughaibuni (Diaspora). Katika mada hiyo Balozi Mulamula alizungumzia umuhimu wa mawasiliano kati ya Ubalozi na Diaspora na matumizi ya Teknolojia katika kurahisisha mawasiliano hayo.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue katika meza kuu na Balozi Mulamula na wajumbe wengine waliohudhuria mkutano wa DICOTA akiwemo Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Rosemary Jairo.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo akiwasilisha mada wakati wa Mkutano wa DICOTA kuhusu Nafasi ya Wizara katika kuwashirikisha Diaspora kuchangia Maendeleo ya Nchi".
Bi. Susan Mzee kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Diaspora akiwasilisha Mada kuhusu  Serikali katika kuwashirikisha Diaspora na nini kimefanyika hadi sasa.
Kamishna Msaidizi wa Nishati anayeshughulikia Gesi Asili katika Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Norbert Kahyoza akiwasilisha Mada kuhusu Usimamizi wa Gesi katika kukuza Uchumi wa nchi wakati wa Mkutano wa DICOTA
Bi Jamila Ilomo kutoka Uhamiaji, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akiwasilisha mada kuhusu Uraia ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Dkt. Mariam Ongara kutoka Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii akiwasilisha mada kuhusu Hali ya sasa nchini kuhusu Afya ya kina Mama Wajawazito na Watoto wakati wa Mkutano wa DICOTA mjini Durham
Bw. Kofi Anani kutoka Benki ya Dunia nae akiwasilisha mada wakati wa Mkutano wa DICOTA.
Bi. Lulu Mengele, Afisa Mwandamizi kutoka Mfuko wa PPF akiwasilisha mada kuhusu Mfuko huo na umuhimu wake kwa Diaspora wakati wa mkutano wa DICOTA
Dkt. Joe Masawe kutoka Benki Kuu ya Tanzania akiwasilisha mada kuhusu Uchumi na umuhimu wa fedha zinazotumwa na Diaspora katika kuchangia uchumi wa nchi.
Bw. Dickson Ernest kutoka Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa DICOTA
Bw. Charles Singili kutoka Benki ya Azania nae akiwasilisha mada wakati wa mkutano wa DICOTA
Afisa kutoka EPZA, Bi. Grace Lemunge akiwasilisha mada kuhusu Fursa za Uwekezaji ndani ya EPZA wakati wa mkutano wa DICOTA.
Wajumbe wakifurahia jambo wakati wa mkutano wa DICOTA

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.