Saturday, October 11, 2014

Waziri Membe Aongoza Matembezi ya Hisani Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mhe. Bernard Kamilius Membe (Mb.) (wa pili kushoto mstari wa mbele) akishiriki matembezi ya kuchangisha fedha kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mwokovu ya Kanisa Katoliki Sinza, Dar es Salaam mapema leo asubuhi..Wa kwanza kushoto ni  Paroko, Father  Cuthbert Maganga Sasagu, na wa tatu kushoto ni  Mwenyekiti wa Parokia hiyo, Bw. Arnold Mwasumbi Makamu Mwenyekiti wa Parokia, Prof. Alfonce Kyessi, alieleza kuwa awamu ya kwanza ya jengo hilo la gorofa tatu litagharimu shilingi milioni 500, ambapo milioni 250 zimeshafika. Katika matembezi ya leo waamini wa Parokia wamechanga milioni 32.8 na Mhe. Membe na marafiki zake 49 wamechanga shilingi milioni moja moja. 
Matembezi ya hisani yaliyoanzia Parokia ya Mtakatifu Maximilian Kolbe Mwenge yakielekea Parokia ya Sinza kupitia barabara ya Shekilango. Matembezi hayo ya kilomita mbili yaliongozwa na Mhe. Membe.
Waziri Membe akizungumza na waamini wa Parokia ya Bikira Maria Mama wa Mwokovu Sinza (hawapo pichani)
Baadhi ya waamini wa parokia ya Bikira Maria Mama wa Mwokovu Sinza wakimsikiliza Waziri Membe 
Waziri Membe akiendelea kuzungumza na waamini wa parokia hiyo.
Waziri Membe akipokea Zawadi ya picha kutoka kwa Paroko Sasagu
Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na viongowa wa parokia ya Sinza.
Waziri Membe akiwa katika picha ya pamoja na wapuliza Tarumbeta

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.