Thursday, October 23, 2014

Fly Dubai yazindua rasmi safari zake nchini.

Ndege ya Shirika la Ndege la Fly Dubai ikiwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere ikiwa katika uzinduzi wake uliofanywa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe. Samia Suluhu, Ndege hiyo itafanya safari zake za moja kwa moja kutokea Dubai mpaka Dar es Salaa, Kilimanjaro, Mwanza na Zanzibar.
Watatu kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe. Samia Suluhu, na wapili kutoka kushoto ni Balozi mdogo wa Tanzania, Dubai Omar Mjenga, wakwanza kushoto ni Spika wa Bunge Mstaafu Mhe. Pius Msekwa na wakwanza kulia ni Bajeti meneja wa Fly Dubai wa nchini Tanzania Bw. Riyaz Jamal wakiitazwa Ndege ya Fly Dubai ilipokuwa inawasili.  
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe. Samia Suluhu akisalimiana na Makamu wa Mkuu wa kampuni hiyo, Sudhir Screedharan mara baada ya kuwasili na Ndege hiyo katikati ni Bajeti meneja wa Fly Dubai Tanzania Bw. Riyaz Jamal.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Simba Yahaya akisalimiana na Bw. Screedharan   
Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai Omar Mjenga akisalimiana na Bw. Screedharan
Mhe. Suluhu akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Ndege hiyo itakayoanzisha safari zake moja kwa moja kutokea Dar es salaam mpaka Dubai 
Wakwanza kushoto ni Bw. Shabani Baraza akimwakilisha Balozi wa Tanzania UAE, wa pili kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Kituo cha Biashara katika Ubalozi Mdogo wa Tanzania, Dubai, Bw. Cleophas Luhumbika Watatu kutoka Kushoto ni Afisa Mambo ya Nje Bw. Hangi Mgaka pamoja na wajumbe wengine wakimsikiliza Mhe. Suluhu
Makamu Mkuu Bw. Screedhana (wakwanza kulia), wa kwanza kushoto Balozi Mdogo Mhe. Mjenga na (katikati) ni Bw. Riyaz Jamal wakimsikiliza Mhe. Waziri alipokuwa akizungumza.  
 Makamu wa Mkuu wa kampuni hiyo, Sudhir Screedharan akizungumza katika hafla hiyo mara baada ya uzinduzi wa safari za Ndege ya Shirika lake la Fly Dubai, alisema safari za ndege zao zinatumia ndege mpya za kisasa aina ya Boeing zipatazo 100.  
Wajumbe mbalimbali wakimsikiliza Bw. Screedharan alipokuwa akizungumza
Balozi Mdogo wa Tanzania, Dubai akizungumza na kuushukuru uongozi wa Fly Dubai kwakukubali kuanzisha safari za moja kwa moja kutokea Dar es salaam mpaka dubai, Balozi mdogo Mjenga alisema kwa kuanza kwa safari ya ndege hiyo inategemewa kuongezeka kwa idadi ya Watalii nchini kutokea Milioni 1 kwa mwaka mpaka Milioni 2, fursa za ajira kwa Watanzania.
Sehemu ya wajumbe wengine wakimsikiliza Balozi Mdogo.
Picha ya pamoja

Picha na Reginald Philip


==============================================================


Na Reginald Philip

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Mhe. Samia Suluhu (Mb.) ameupongeza Uongozi wa Shirika la Flydubai la Dubai kwa kuanzisha safari za ndege za moja kwa moja kati ya Dubai na Dar es Salaam, Kilimanjaro, Mwanza na Zanzibar kwa gharama nafuu.

Akizindua huduma hiyo kwa niaba ya Makamu wa Rais, Dkt. Mohamed Gharib Bilal, jijini Dar es Salaam, Jumatano tarehe 22 Oktoba, 2014, Mhe. Suluhu alimwambia Makamu Mkuu wa Shirika la Flydubai, Bw. Sudhir Sreedharan, kuwa  kuja kwao Tanzania kutafungua njia za kiuchumi na nchi nyingine za Kiafrika.

Alisema kuanzishwa kwa huduma hiyo pia kutatoa fursa ya ajira kwa watanzania, na akawahimiza wananchi kuchangamkia fursa hizo.

Shirika hilo, ambalo ndege zake zina bei nafuu- kutokea Dar es salaam kwenda dubai na kurudi (DSM-DXD-DSM) kwa bei ya dola za Kimarekani 399 tu (budget Airline) litafanya safari zake kati ya Dar es salaam, KIA na Zanzibar. Baadae, shirika hilo litaongeza safari zao kutokea Mbeya kuelekea Dubail.

Katika hafla hiyo ya uzinduzi iliyoandaliwa na shirika la Flydubai kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere, Mhe. Suluhu aliipongeza Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kwa kuratibu uanzishwaji wa safari za bei nafuu kupitia kwa Balozi  Mdogo wa Tanzania nchini Dubai, Mhe. Omar Mjenga, ambaye alihudhuria hafla ya uzinduzi.

Baada ya Dar es Salaam, hafla nyingine ya uzinduzi ilifanyika Zanzibar baadaye hiyo jana, Mgeni rasmi alikuwa Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi.

-Mwisho-

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.