Monday, April 29, 2024

MKUTANO WA 24 WA BARAZA LA MAWAZIRI SEKTA YA AFYA EAC WAANZA DAR ES SALAAM


Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa Kawaida wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya unaofanyika jijini Dar es Salaam. 

Mkutano wa Kawaida wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Sekta ya Afya umeanza jijini Dar es Dar es Salaam.

Mkutano huo wa siku tano unaofanyika kwa njia ya mseto (mtandao na ana kwa ana) kuanzia terehe 29 Aprili hadi tarehe 3 Mei 2024 umeanza kwa Ngazi ya Wataalam ukilenga kufanya tathimini ya utekelezaji wa maagizo na makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa 23 wa Baraza hilo. 

Mkutano huo Ngazi ya Wataalam utafuatiwa na Ngazi ya Makatibu Wakuu utakaofanyika tarehe 2 Aprili 2024 na kuhitimishwa na Mkutano Ngazi ya Mawaziri ukaofanyika tarehe 3 Mei 2024. 

Mbali na kufanya tathimini ya utekelezaji wa maagizo na makubaliano yaliyofikiwa katika mkutano wa 23 wa Baraza hilo, agenda zingine zitakazojadiliwa katika katika Mkutano huo ni pamoja na; Kujadili taarifa za Vikundi Kazi (Technical Working Group – TWG) sita (06) vya Sekta ya Afya na pendekezo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la kuanzisha Kituo cha Umahiri cha Upandikizaji Uloto na Sayansi ya Matibabu ya Magonjwa ya Damu chini ya Hospitali ya Benjamin Mkapa. 

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano huo Mganga Mkuu wa Serikali ya Tanzania Prof. Tumaini Nagu, ametoa rai kwa Wataalamu wa Sekta ya Afya wanaoshiriki Mkutano huo, kutoa mchango utakaoisaidia Jumuiya kuimarisha miundombinu ya huduma ya afya ili kukabiliana na matishio ya kiafya ya magonjwa yanayoambukiza na yasiyoambukiza.

“Hatukutani kujadili pekee, bali kutoa suluhisho na majawabu yatakayosaidai kustahimili changamoto za kiafya katika Jumuiya yetu kwa kuzingatia ubunifu na weledi katika mifumo yetu ya afya huku tukiwa wamoja na wenye nguvu zaidi”amesema Prof. Nagu

Amehimiza umuhimu wa Sekta ya Afya ndani Jumuiya kuendelea kufanya kazi kwa ufanisi na umoja katika utekeleza progamu, miradi ya Sekta ya Afya na mikakati mbalimbali inayopangwa ili kufikia mafanikio yanayotarajiwa kwa wakati.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Sekta ya Jamii katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki Dkt. Irene Isaka ameeleza kuwa kupitia mkutano huo nchi wanachama zitapata fursa ya kusikia taarifa zitakazowasilishwa na kila nchi ili kwa pamoja wachangia na kushauri namna bora ya kusimamia na kuendesha programu, miradi, miundombinu ya afya katika Jumuiya.

Mkutano huo Ngazi ya Wataalam unahudhuriwa na Nchi zote Wanachama wa Jumuiya na ujumbe wa Tanzania unaongozwa na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu. 

Wizara ya Mambo ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inawakilishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii Mhandisi Abdillah Mataka. 

Mkutano huo unahudhuriwa na Wizara za Afya (Tanzania Bara na Zanzibar), Hospitali ya Benjamin Mkapa, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Kituo cha Umahiri cha Magonjwa ya Moyo na Mishipa ya Damu cha Afrika Mashariki, Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Mamlaka ya Chakula na Dawa (TMDA), Mpango wa Taifa wa Kudhibiti Ukimwi (NACP), Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi (MUHAS) Bohari ya Dawa (MSD), Maabara Kuu ya Taifa, Mpango wa Kitaifa wa Kudhibiti Malaria (NAMCP) na Mamlaka ya Chakula na Dawa Zanzibar (ZFDA)
Mwenyeki wa Mkutano wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya Ngazi ya Wataalam Dr. Agai K. Akec Mkurugenzi wa Masula ya HIV/AIDS kutoka Jumhuri ya Sudan akiongoza Kikao
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania wakifuatalia Mkutano wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya unaofanyika jijini Dar es Salaam. Tarehe 29 Aprili hadi 3 Mei 2024. 
Mkutano wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya ukiendelea jijini Dar es Salaam
Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Uchumi na Huduma za Jamii katika Wizara ya Mambo ya Nje Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhandisi Abdillah Mataka akifuatilia Mkutano wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya unaoendelea jijini Dar es Salaam
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania wakifuatalia Mkutano wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya unaofanyika jijini Dar es Salaam. Tarehe 29 Aprili hadi 3 Mei 2024. 
Sehemu ya Ujumbe wa Tanzania wakifuatalia Mkutano wa 24 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Afya unaofanyika jijini Dar es Salaam. Tarehe 29 Aprili hadi 3 Mei 2024. 

Thursday, April 25, 2024

BARAZA LA MAWAZIRI EAC LAKUTANA JIJINI ARUSHA.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.).(kulia) akiwa na Naibu Waziri Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb.) wakishiriki Mkutano Maalum wa 53 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika  tarehe 25 Aprili 2024 Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

 



Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.) (katikati) akiwa na Naibu Waziri Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb.) (kushoto) na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi (kulia) wakishiriki Mkutano Maalum wa 53 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika  tarehe 25 Aprili 2024 Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.


Washiriki wa Mkutano Maalum wa 53 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika  tarehe 25 Aprili 2024 Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mkutano huo.



Mkutano Maalum wa 53 wa Baraza la Mawaziri la Jumuiya ya Afrika Mashariki umefanyika leo tarehe 25 Aprili 2024 Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha.

Mkutano huo, pamoja na masuala mengine umejadili na kupitisha Makadrio ya Bajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mwaka wa fedha 2024/2025. 

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo umeongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato (Mb.).

Viongozi wengine walioshiriki mkutano huo ni pamoja na Naibu Waziri Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete (Mb.) na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Balozi Stephen Mbundi.

Mkutano huo umefanyika kufuatia kukamilika kwa kikao cha ngazi ya Makatibu Wakuu kilichofanyika tarehe 24 Aprili 2024 ambacho kilitanguliwa na kikao cha ngazi ya Wataalam cha tarehe 23 Aprili 2024.


Wednesday, April 24, 2024

KATIBU MKUU, CCM AWAPONGEZA MABALOZI WAKIKAMILISHA WARSHA YA SIKU 4 KIBAHA


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani. 

Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amewatembelea Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 ambayo imekamilika mjini Kibaha leo Aprili 24, 2024 kwa kufikia makubaliano mbalimbali ambayo yanalenga kuipaisha diplomasia ya Tanzania duniani.

Dkt. Nchimbi aliwapongeza Mabalozi hao kwa kazi nzuri wanayoifanya ya kuitangaza nchi na kuchangia kwa kiasi kikubwa ongezeko la biashara, uwekezaji na utalii nchini. 

Warsha hiyo ambayo ililazimika kumalizika usiku kila siku ilifanyika chini ya uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe January Makamba (Mb) ilijadili mikakati ya kuboresha utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje na namna ya kutafuta ufumbuzi wa kudumu wa changamoto ambazo zimekuwa kikwazo kufikia ufanisi wa shughuli za Wizara hiyo.

Katika siku zao 4, Mabalozi pamoja na mambo mengine, walipitia mikakati ya Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi, Uendelezaji wa majengo ya ofisi na makazi ya Balozi, Diplomasia ya Umma na Diplomasia ya kidigitali na viashiria vya kupima utendaji (Key Performance Indicators- KPIs).

Mabalozi walieleza kuwa kukamilika kwa nyaraka hizo ambazo hazikuwahi kuwepo Wizarani kabla ni chachu katika mwelekeo mpya wa Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi.

Mabalozi walisisitiza umuhimu wa kumaliza changamoto za kimawasiliano baina yao na wadau ambazo zimekuwa kikwazo za kukamilika kwa wakati kwa fursa na miradi ambayo imekuwa ikiletwa nchini. Changamoto nyingine kubwa ambayo Mabalozi wamesisitiza itafutiwe ufumbuzi ni uwezo mdogo wa nchi yetu wa kuzalisha bidhaa za kukidhi soko katika maeneo yao ya uwakilishi. Waheshimiwa Mabalozi walisema kuna soko kubwa la nyama, maparachichi, korosho, mchele na bidhaa nyingine lakini hakuna bidhaa za kutosha nchini za kulisha soko hilo.

Mabalozi katika warsha hiyo walipata fursa ya kusikiliza nasaha za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa njia ya mtandao ambaye aliwataka kuwa jicho la Tanzania katika maeneo yao ya uwakilishi ili nchi isipitwe na mabadiliko yanayotokea duniani. 

Aidha, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka alifika katika warsha hiyo na kuwambia Mabalozi kuwa wapo katika Wizara iliyokusanya watu wenye taaluma, ujuzi, uzoefu na historia ya kutoka sekta tofauti mchini. Aliwasihi washirikiane kutumia fursa hiyo kuharakisha mabadiliko ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na kutatua changamoto zinazowakabili.

Taasisi kadhaa pia zilialikwa na kuwasilisha mada kuhusu shughuli za ofisi zao ambazo ni Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) na Benki ya Azania. 

Warsha hiyo pia wakati wa ufunguzi, walikaribishwa Mabalozi wastaafu ambao walipata fursa ya kubadilishana uzoefu na Mabalozi wa sasa kwa lengo moja tu la kujengeana uwezo wa kukuza na kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na mataifa mengine, mashirika ya Kikanda na Kimataifa. 

Waziri Makamba ambaye ana muda wa takribani miezi 7 tokea ahamishiwe Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki amesema Wizara inaweza kufanya zaidi kuliko inavyofanya hivi sasa. Hivyo, warsha hiyo iliandaliwa ili kupigana msasa wa kufikia nchi ya ahadi.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani. 
Warsha ikiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mhe. January Makamba akimkaribisha Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Emmanuel Nchimbi kuzungumza na  Mabalozi  kwenye warsha katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akizungumza wakati akiongoza warsha ya siku 4 ya Mabalozi iliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Samwel Shelukindo akielezea jambo kwenye warsha ya Mabalozi iliyofanyika katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani.






Tuesday, April 23, 2024

TUMIENI UZOEFU KUHARAKISHA MADADILIKO, BALOZI KUSILUKA


Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani.

Mabalozi wamehimizwa kutumia taaluma, uzoefu na ujuzi tofauti waliokuwa nao kuharakisha mabadiliko ya kimfumo yanayoendelea ndani ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Kauli hiyo imetolewa leo Aprili 23, 2024 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka wakati anaongea na Mabalozi katika warsha ya siku 4 ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha tokea tarehe 21 Aprili 2024.

"Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki mmebarikiwa kuwa na watu wenye taaluma tofauti na wenye historia ya sekta tofauti, tumieni fursa yenu hii kumsadia Mwanadiplomasia namba moja, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amewarahisishia kazi yenu kwa kuitekeleza diplomasia kwa vitendo", Balozi kusiluka alisema.

Amesema Serikali inazitambua changamoto wanazokabiliana nazo na inazifanyia kazi lakini kutokana na Wizara kuwa na watu wenye uzoefu wa kutoka sekta tofauti, wakishirikiana wanaweza kuzitatua na kuifikisha nchi katika hatua nzuri.

Balozi Kusiluka alimaliza hotuba yake kwa kuwapongeza Mabalozi kwa kazi nzuri wanayofanya na kuwaahidi kuwa Serikali itapokea mawazo yote mazuri na ya kibunifu yatakayotokana na warsha hiyo na kuyafanyia kazi.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani.
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akifuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea kwenye warsha ya Mabalozi ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani
Kutoka Kushoto; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses, Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato wakifuatilia warsha ya Mabalozi ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani

Monday, April 22, 2024

RAIS SAMIA ARIDHISHWA NA KAZI YA MABALOZI NA KUWATAKA KUONGEZA JUHUDI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje

Rais wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan amewapongeza Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani kwa kazi nzuri ya uwakilishi ambayo inaonekana kwa kuongezeka kwa masoko ya bidhaa za Tanzania, biashara, uwekezaji, utalii na teknolojia nchini.

Mhe. Rais Samia ametoa pongezi hizo leo Aprili 22, 2024 alipokuwa anawahutubia Mabalozi hao kwa njia ya mtandao ambao wamekusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya siku 4 ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje iliyoanza Aprili 21 na itakamilika Aprili 24, 2024.

Mhe. Rais Samia amesema kuwa nchi inawategemea sana Mabalozi katika utekelezaji wa majukumu yao Ili iweze kusonga mbele kiuchumi na kwa kuliona hilo, Rais Samia amesema amechukua hatua mbalimbali ili kuibadilisha Wizara ya Mambo ya Nje iwe ya kisasa zaidi na kuwa na uwezo wa kuitangaza nchi.

Lengo la Mabadiliko hayo ni kuifanya nchi iendelee kuheshimika na kuwa na ushawishi zaidi duniani kama ilivyokuwa katika miaka ya nyuma wakati wa harakati za ukombozi na baada ya ukombozi.

Hatua ambazo Mhe. Rais Samia alizitaja kuwa ni pamoja na kuteua Naibu Waziri na Katibu Mkuu wanaoshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, kuanzisha Idara ya Diplomasia ya Uchumi, kusaini mikataba ya Kuzuia Utozaji wa Kodi mara Mbili na Kulinda Vitega Uchumi na nchi mbalimbali duniani, kuridhia mkakati wa uendelezaji wa majengo ya ofisi za Mabalozi na makazi na mchakato wa uboreshaji wa Sera ya Mambo ya Nje na Hadhi Maalum kwa raia wenye asili ya Tanzania wanaoishi Nje ya nchi ambao umefikia hatua nzuri.

Mhe. Rais aliwasihi Mabalozi kuwa jicho la Tanzania kwenye maeneo yao ya uwakilishi ili nchi isipitwe na mabadiliko makubwa yanayotokea duniani. 

Mhe. Rais pia alizungumzia misingi sita ya Sera ya Mambo ya Nje ambayo Nchi yetu inaisimamia tangu ilipopata uhuru na kutufikisha hapa tulipo. Aliitaja misingi hiyo kuwa ni pamoja na kulinda uhuru wa kujiamulia, kuheshimu mipaka ya nchi; kulinda uhuru, haki za binadamu na usawa wa kidemokrasia; kudumisha ujirani mwema; kuunga mkono Umoja wa Mataifa, kuendeleza mshikamano wa Umoja wa Afrika na kuunga mkono Sera ya kutofungana na Upande Wowote.

Rais Samia aliwambia mabalozi katika maboresho ya Sera ya Mambo ya Nje yanayoendelea, amependekeza kuongeza msingi wa saba ambao ni kulinda maslahi ya kiuchumi na maadili ya watu. Katika msingi huu, Mhe. Rais alisisitiza umuhimu wa kulinda rasilimali za nchi yetu na utamaduni wake. Alisema nchi yetu imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi ikiwemo madini hadimu. Alisema endapo nchi haitakuwa na mpango madhubuti wa kulinda rasilimali hizo na kunufaifika nazo, basi badala ya kuwa fursa kwa Taifa zinaweza kugeuka kuwa janga.

Aidha, alisisitiza umuhimu wa kulinda Utamaduni wetu kwani kuna juhudi za makusudi zinazoendelea duniani za kulazimishwa tamaduni zilizo kinyume na maadili yetu.

Mhe. Rais Samia alihitimisha hotuba yake kwa kuwakumbusha Mabalozi kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni pande mbili, Tanzania Bara na Zanzibar, hivyo katika majukumu yao ya uwakilishi, wakumbuke vipaumbele vya Zanzibar, hususan kukuza utalii na uchumi wa buluu.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje wakifurahia jambo wakati Rais wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwahutubia kwa njia ya mtandao.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
Mabalozi wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan
Sehemu ya Mabalozi na Viongozi wa Wizara wakifurahia jambo wakati Rais wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwahutubia kwa njia ya mtandao.

Sehemu ya mabalozi wa wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kwa njia ya mtandao.
Sehemu ya mabalozi wa wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kwa njia ya mtandao.
Sehemu ya mabalozi wa wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kwa njia ya mtandao.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwasilisha mada kwenye warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwasilisha mada kwenye warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani kwanjia ya mtandao waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwasilisha mada kwenye warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwasilisha mada kwenye warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje







Saturday, April 20, 2024

MABALOZI WA TANZANIA WAJIFUNGIA KIBAHA KUTAFAKARI NA KUJIPANGA UPYA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na Mabalozi kuelekea warsha inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani

Mabalozi wanaowakilisha Tanzania katika nchi mbalimbali duniani na Wakuu wao wa utawala wamejifungia katika Chuo cha Uongozi Cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha kwa siku 4 kuanzia tarehe 20 hadi 24 Aprili 2024. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) ametaja sababu za kujifungia huko kuwa ni pamoja na kukutana kama familia ya wanadiplomasia wa zamani na wa sasa ili kubadilishana uzoefu wa namna bora ya kutekeleza Sera ya Mambo ya Nje ambayo imejikita katika diplomasia ya uchumi.

Mhe. Makamba alisema kazi ya diplomasia ni moja ya kazi muhimu duniani na kupitia kazi hiyo Tanzania imejitangaza na kusikika, hasa kupitia misimamo yake na umahiri wa wanadiplomasia iliyokuwa nao.

Hivyo, vikao hivyo ni muhimu kwa ajili ya kupata mwendelezo huo, kwani vinatoa fursa ya kutafakari upya na kupanga mikakati ya namna bora zaidi ya kutekeleza majukumu ya Wizara hiyo ambayo ni moja ya nguzo muhimu ya ukuaji wa uchumi nchini.

Alisema mfumo wa kikao hicho ambao ni tofauti kabisa na mifumo ya vikao vilivyofanyika miaka ya nyuma ni kwamba wanadiplomasia watapewa fursa ya kubadilishana kinaga ubaga changamoto wanazokabiliana nazo katika utekelezaji wa majukumu yao, kutafakari kwa pamoja namna bora ya kuzitafutia ufumbuzi na baadaye kuweka mpango kazi wa utekelezaji. 

Aliwahakikishia kuwa Serikali itajitahidi kutoa nyenzo ilizo nazo ili kazi hiyo muhimu iweze kutekelezwa na kuleta matokeo chanya yanayotarajiwa.

"Tutafakari majukumu yetu, masuala mahususi ya kuzingatia pamoja na kutathimini nyenzo zetu za utekelezaji ili wote tuwe katika uelewa na mwelekeo mmoja wa kufanikisha malengo ya Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mama yetu, Mwana diplomasia namba moja, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan". Mhe. Makamba alisema.

Warsha hiyo ya Mabalozi inajumuisha pia Makatibu na Naibu Makatibu Wakuu wa Wizara wakiongozwa na Balozi Dkt. Samwel Shelukindo, Wakurugenzi, Wakurugenzi Wasaidizi, Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara na baadhi ya wadau wanaoshirikiana kwa karibu na Wizara katika utekelezaji wa majukumu ya Diplomasia.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) akizungumza kwenye kikao kazi kuelekea warsha ya Mabalozi inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani
Sehemu ya Mabalozi wakifurahia jambo wakati Waziri Makamba akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kuelekea warsha ya Mabalozi inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani
Mwenyekiti wa Umoja wa Mabalozi Wastaafu Mhe. Balozi Aziz Ponary Mlima akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kuelekea warsha ya Mabalozi inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani