Tuesday, April 16, 2024

BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC LAPOKEA MAPENDEKEZO YA KATIBU MKUU MTEULE WA JUMUIYA


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akichangia jambo kwenye Mkutano wa 52 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki

Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) leo tarehe 16 Aprili, 2024 limepokea mapendekezo ya uteuzi wa Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo katika Kikao chake cha 52 cha Dharura kilichofanyika kwa njia ya mtandao.

Ujumbe wa Tanzania katika mkutano huo umeongozwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.) akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi.

Mapendekezo hayo yamewasilishwa kufuatia mabadiliko ya nafasi hiyo yaliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto ambapo amemteua Katibu Mkuu wa Jumuiya hiyo Dkt. Peter Mutuku Mathuki kuwa Balozi wa Jamhuri ya Kenya nchini Urusi.

Hivyo, Mhe. Ruto amempendekeza Bi. Veronica Mueni Nduva kuchukua nafasi ya Katibu Mkuu wa Jumuiya mara baada ya kuthibitishwa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Katibu Mkuu wa Jumuiya huteuliwa na Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki baada ya kupokea mapendekezo kutoka kwa Mkuu wa Nchi husika kulingana na utaratibu wa mzunguko ambao unatoa kipindi cha miaka mitano ya kuhudumu katika nafasi hiyo.

Katibu Mkuu wa sasa Dkt. Peter Mathuki aliteuliwa na Mkutano wa 21 wa Wakuu wa Nchi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 27 Februari, 2021. Hivyo, kulingana na muda wa kuhudumu Jamhuri ya Kenya imebakiwa na miaka miwili kukamilisha kipindi chake cha miaka matano (5).

Mkutano huo wa Baraza la Mawaziri umeamua kuwa, katika kipindi cha mpito majukumu ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yatakaimiwa na Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya Forodha, Biashara na Fedha, Bi. Annette Ssemiwemba kulingana na kifungu 63 (3) cha Mkataba wa Uanzishawaji wa Jumuiyya hiyo.
Mkutano wa 52 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki uliofanyika terehe 16 Aprili 2024 ukiendelea kwa njia ya mtandao
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Mhe. Stephen Byabato (Mb.) na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi wakifuatilia Mkutano wa 52 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki
Mkutano wa 52 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki uliofanyika terehe 16 Aprili 2024 ukiendelea kwa njia ya mtandao
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki, Balozi Stephen Mbundi akifuatilia jambo wakati wa Mkutano wa 52 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.