Tuesday, April 16, 2024

WAZIRI MAKAMBA AWASILI UTURUKI KUELEKEA ZIARA YA KITAIFA YA MHE. RAIS SAMIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba amewasili Ankara, Uturuki leo tarehe 16 Aprili 2024 na kukutana kwa mazungumzo na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Mhe. Hakan Fidan.


Pamoja na mambo mengine viongozi hao wamejadili kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya ziara ya kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan itakayofanyika nchini humo kuanzia tarehe 17 hadi 21 Aprili 2024.


Wakati wa ziara ya Mhe. Rais Samia ambayo inafanyika kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Uturuki, Mhe. Recep Tayyip Erdoğan viongozi hao watashuhudia kusainiwa kwa Hati za Makubaliano nane (8) katika sekta za Elimu, Utalii, Utunzaji Nyaraka na ushirikiano katika masuala ya Diaspora. 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba akisalimiana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe.  Hakan Fidan baada ya kuwasili nchini Uturuki kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya ziara ya kitaifa ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan nchini humo
Mhe. Makamba akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, Mhe. Hakan Fidan


Mhe. Waziri Makamba na Mhe. Waziri Fidan wakiwa na ujumbe walioongozana nao wakati wa mazungumzo yao. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Iddi Bakari. Wa pili kulia ni Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Mehmet Gulluoglu







 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.