Tuesday, April 30, 2019

Prof. Kabudi akutana na Naibu Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki na Sudan


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi(Mb.),(kulia) akiwa katika mazungumzo na Naibu  Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika  Mashariki na Sudan, Balozi Makila James, katika Ofisi ndogo za Wizara Dar es salaam leo tarehe 30 Aprili, 2019. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Palamagamba John Kabudi(Mb.), akimuonesha Naibu  Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika  Mashariki na Sudan, Balozi Makila James (katikati) maeneo  mbalimabali katika ramani alipokuwa akielezea historia ya Tanzania.Kushoto kwake ni kaimu Balozi wa Marekani Mhe. Imni Patterson.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe.Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) akimuelezea Naibu  Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika  Mashariki na Sudan, Balozi Makila James kuhusu uhuru wa vyombo vya habari nchini  Kushoto kwake ni Kaimu Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Imni Patterson.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini (DGCU),  cha Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Emmanuel Buhohela (wa kwanza kulia) na Afisa Mambo ya Nje wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Albert Philipo, wakifuatilia mazungumzo baina ya Mhe. Prof Palamagamba John Kabudi na Balozi  Makila James.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Palamagamba John Kabudi(Mb.) akiwa katika picha ya pamoja na Naibu  Msaidizi wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani anayeshughulikia masuala ya Afrika  Mashariki na Sudan, Balozi Makila James (wa pili kushoto), kulia kwake ni Kaimu  Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Imni Patterson. Wengine ni afisa wa Wizara wa Mambo ya Nje, Albert Philipo (wa kwanza kulia) na afisa wa Uchumi katika ubalozi wa Marekani nchini Ann Marie Warmenhoven (wa kwanza kushoto).

Joint Communique



Monday, April 29, 2019

Ubalozi wa Tanzania nchini India waadhimisha miaka 55 ya Muungano

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda  akiwahutubia washiriki wa hafla ya kuadhimisha miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar iliyofanyika katika Hoteli ya Leela Palace jijini New Delhi, India tarehe 26 Aprili 2019. Katika hotuba yake, Balozi Luvanda alieleza kuwa, Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni wa kihistoria na wa kupigiwa mfano duniani kote. Pia alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na India ambao umedumu kwa miaka 58.
Mhe. Balozi Luvanda (wa pili kushoto) kwa pamoja na mgeni rasmi Mhe. Shri Sanjiv Arora ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa India anayeshughulikia Masuala ya Kikonseli, Paspoti, Visa na Diaspora wa (kushoto) na wageni waalikwa wakionesha jarida kuhusu miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lililoandaliwa na Ubalozi wa Tanzania nchini India na kuzinduliwa rasmi katika hafla hiyo.
Mhe. Balozi Luvanda (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na mgeni rasmi Mhe. Shri Sanjiv Arora ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa India anayeshughulikia Masuala ya Kikonseli, Pasipoti, Viza na Diaspora wa India wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 55 ya Muungano.
Mhe. Balozi Luvanda akiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wa nchi mbalimbali walioudhuria hafla ya kuadhimisha miaka 55 ya Muungano.
Mhe. Balozi Luvanda (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania, New Delhi wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 55 ya Muungano.

Mhe. Schreiber asisitiza Tanzania kutosaini mkataba wa EPA


Mbunge na Mwenyekiti wa Kamati inayohusika na Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo ya Ujerumani Mhe.  Eva-Maria Schreiber amefanya ziara ya siku saba hapa nchini. Mhe. Schreiber amepata fursa ya kutembelea mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma na Kigoma, ambapo pia amekutana na wenyeviti wa Kamati mbalimbali za Bunge.


Akiwa nchini  Mbunge huyo ametembelea mradi wa maji ujulikanao kama “Seven Towns Urban Upgrading Programme/ Kigoma Urban Water Supply and Sanitation”. Mradi unafadhiliwa na Umoja wa Ulaya na Serikali ya Ujerumani kupitia Benki ya Maendeleo ya Ujerumani (KfW). 

Aidha, mradi huo unahusisha mikoa ya Kigoma, Shinyanga na Lindi. Kwa upande wa Kigoma, utekelezaji wa mradi huu ulianza mwezi Machi 2013 na utakamilika mwezi Oktoba, 2019.
Mhe. Schreiber amekutana na kufanya mazungumzo na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo hayo na waandishi wa habari Mhe. Schreiber amesisitiza umuhimu wa Tanzania kutokusaini Mkataba wa Makubaliano ya Kuichumi (EPA) kati ya Jumuiya ya Umoja wa Ulaya na nchi za Afrika.
 Pia alieleza kuwa endapo Tanzania na nchi nyingine za Afrika hazitofaidika na Mkataba huo kwakuwa zitapoteza mapato.  
Sehemu ya waandishi wakimsikiliza kwa makini Mhe. Schreiber
Mhe. Schreiber akiendelea kuzungumza na waandishi wa Habari.





Saturday, April 27, 2019

Ubalozi wa Urusi waadhimisha Muungano kwa Kutangaza bidhaa za Tanzania

Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mhe. Maj. Jen. Mstaafu Simon Mumwi akitoa neno la ukaribisho kwa wageni mbalimbali walioalikwa kushiriki kilele cha kuadhimisha Siku ya Taifa ya Tanzania (Maadhimisho ya miaka 55 ya Muungano) yaliyofanyika jijini Moscow tarehe 26 Aprili 2019. Maadhimisho hayo yalipambwa na shughuli mbalimbali zikiwemo Maonesho ya bidhaa na vivutio vya utalii vya Tanzania; kukabidhi vyeti kwa wadau mbalimbali ili kutambua mchango wao katika maendeleo ya uchumi wa Tanzania, hususan katika sekta ya utalii, uwekezaji, sanaa, lugha na utamaduni pamoja na kutoa fursa ya kubadilishana mawazo baina ya Mabalozi na taasisi za Urusi zinazojihusisha na masuala ya uwekezaji. Mwingine katika picha ni Naibu Mkurugenzi wa Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi, Bw. George Cherpisk.


Naibu Mkurugenzi wa Afrika kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi, Bw. George Cherpisk akisoma hotuba katika maadhimisho hayo.
Wageni waalikwa wakiwemo Waheshimiwa Mabalozi wa nchi mbalimbali zenye uwakilishi Urusi wakisikiliza hotuba.

Mhe. Balozi Mumwi na Waheshimiwa Mabalozi wa mbalimbali wa nchi za Afrika zenye uwakilishi nchini Urusi wakikata keki ya kuadhimisha miaka 55 ya Muungano wa Tanzania.

Balozi wa Tanzania nchini Urusi, Mhe. Maj. Jen. Mstaafu Simon Mumwi akikabidhi cheti kwa mmoja wa wadau wanaochangia maendeleo na ukuaji wa uchumi nchini Tanzania.

Mdau akipokea cheti chake ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wake katika maendeleo ya Tanzania.

Picha ya pamoja ya baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi, wageni, maafisa wa ubalozi na wanafunzi wa Kitanzania wanaosoma Urusi walioshiriki katika maadhimisho hayo.


Thursday, April 25, 2019

Vacancy announcement


PRESS RELEASE

Vacancy notice
The Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation has received Vacancy Notice for the post of Director General available at the African Development Bank (AfDB) for qualified individuals to apply. 


Application details can be found through the following website: http://www.afdb.org. Closing date for application is 1st May, 2019.


The Ministry encourages qualified Tanzanians to apply.


Issued by:
Government Communication Unit,
Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation,
Dodoma.
25th April, 2019.


Tanzania na China zaadhimisha miaka 55 ya ushirikiano

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako (Mb.) akitoa hotuba kama mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya miaka 55 ya Ushirikiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China yaliyofanyika kwenye ukumbi uliopo kwenye Maktaba  ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam tarehe 24 Aprili, 2019.

 Katika hotuba yake, Prof. Ndalichako ameipongeza China kwa kuimarisha ushirikiano  na  Tanzania hususan katika sekta za Elimu, Biashara na Ujenzi wa miundombinu. Aidha,   amesema kuwa mahusiano kati ya Tanzania na China ni ya muda mrefu na mchango wa nchi hiyo kwenye maendeleo ya Tanzania ni dhahiri akitolea mfano  ujenzi wa Reli ya TAZARA pamoja na ujenzi wa viwanda mbalimbali vya nguo nchini. Vilevile China imeendelea kushirikiana na Tanzania kwenye Sekta ya Afya kwa kubadilishana uzoefu.

Maadhimisho hayo yamehudhuriwa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo  Pinda, Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.), Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bw. Caesar Waitara, na viongozi mbalimbali kutoka Taasisi  za umma na binafsi nchini. 
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo  Pinda akiwa na mke wake Mhe. Tunu Pinda (kushoto)  pamoja na viongozi mbalimbali kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakifuatilia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Prof. Ndalichako (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya miaka 55 ya ushirikiano kati ya Tanzania na China.
Juu na Chini ni sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia hotuba hiyo.

Prof. Ndalichako akiendelea kuhutubia kwenye maadhimisho hayo.
Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini, Mhe. Wang Ke naye akihutubia kwenye maadhimisho hayo. 
Wageni waalikwa wakifuatilia maadhimisho hayo.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo  Pinda pamoja na mke wake Mhe. Tunu Pinda (kushoto) pamoja na viongozi wengine kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakipitia kitabu chenye kuonyesha ushirikiano wa Tanzania na China kwenye sekta mbalimbali.
Mkurugenzi wa Ofisi ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Zanzibar, Balozi Mohammed Hamza (kushoto) kwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia Bw. Caesar Waitara (kulia) wakipitia kitabu kinachoonesha namna Tanzania na China zinavyoshirikiana kwenye sekta mbalimbali.
Maafisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakijadiliana jambo wakati wa maadhimisho hayo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akitambulishwa kwa wageni walioshiriki maadhimisho hayo.
Mshehereshaji, Bi. Bertha Makilagi akitoa mwongozo wa ratiba ya maadhimisho hayo kwa wageni waalikwa.
 Juu na chini ni maonyesho mbalimbali yakiendelea kuonyeshwa na vikundi mbalimbali kwenye maadhimisho hayo


Mgeni Rasmi pamoja na wageni waalikwa wakiwa wamesimama wakati nyimbo za  mataifa ya Tanzania na China zikiimbwa.
Kikundi chenye mchanganyiko wa wanafunzi kutoka Tanzania na China wakiongoza kuimba wimbo wa Taifa wa Tanzania na China kabla maadhimisho hayo kuanza.
Naibu Waziri, Mhe. Dkt. Ndumbaro akimpa mkono wa pongezi mmoja wa wasanii aliyekuwepo kwenye maadhimisho hayo
Mhe. Prof. Ndalichako na wageni waalikwa wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa maadhimisho hayo.
Mgeni rasmi pamoja na Viongozi mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja.

















 















Wednesday, April 24, 2019

PUBLIC NOTICE




Nafasi za Ajira Katika Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali


Dodoma, 24 Aprili 2019

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Nafasi za Ajira

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuwahimiza Watanzania wenye sifa kuomba fursa ya ajira iliyotangazwa na Sekretarieti ya Shirika la Kuzuia Silaha za Kemikali (Organization for the Prohibition of Chemicals Weapons-OPCW) iliyopo The Hague, Uholanzi. Nafasi hiyo ni ya Technical Support Officer-P3 ambapo mwisho wa kufanya maombi ni tarehe 06 Juni 2019.

Wenye sifa zinazohitajika, wanashauriwa kufanya maombi kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya sekretarieti; www.opcw.org

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,

Thursday, April 18, 2019

Fursa ya Ajira.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

NAFASI YA AJIRA KATIKA SEKRETARIETI YA JUMUIYA YA UKANDA WA MAZIWA MAKUU (ICGLR).

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, inawahamasisha Watanzania wenye sifa, kuomba nafasi ya ajira katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Ukanda wa Maziwa Makuu (ICGLR).

Ajira hiyo ni Mtaalam wa Uhakiki wa Nyaraka. Taarifa zote muhimu kuhusu fursa hiyo ya ajira zinapatikana kwa kupitia tovuti www.icglr.org.

Maombi yote yatumwe kwenda katika barua pepe jobs@icglr.org na nakala itumwe katika barua pepe gerard.nayuburundi@icglr.org  yakiwa na kichwa cha habari Maombi ya nafasi ya Mtaalam wa Uhakiki wa Nyaraka.

Mwisho wa kutuma maombi kwa nafasi hiyo ni  tarehe 25 Aprili, 2019.

    Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
      Dodoma.