Saturday, April 13, 2019

Wizara ya Mambo ya Nje yashiriki uzinduzi wa mji wa serikali

Leo tarehe 13 Aprili, 2019, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, imeshiriki katika hafla ya kuuzindua Mji wa Serikali iliyofanyika katika eneo la Mtumba, Dodoma. Mgeni rasmi katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.Pichani:Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi (Mb.) (wa nne kutoka kulia) akifurahia jambo wakati wa uzinduzi huo.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa(Mb.), (aliye katika mimbari) akisisitiza jambo wakati wa kutoa taarifa fupi ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa  Mji wa Serikali.



Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na viongozi wa dini wakifurahia jambo wakati wa hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimwa Dkt. John Pombe Magufuli (hayupo pichani).




Umati ulioshiriki katika uzinduzi wa Mji wa Serikali ukifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli.


Kanali Mbuge akipiga saluti kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe  Magufuli, kwa kumpandisha cheo kuwa Brigadia Jenerali baada ya kushiriki kwa ufanisi na weledi wa hali ya juu katika ujenzi wa miradi mbalimbali  ya serikali ikiwemo ujenzi wa ukuta wa Mererani na  ukuta wa Ikulu ya Chamwino na nyumba za watumishi wa umma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Mheshimiwa Dkt John Pombe Magufuli, akikata  utepe katika jengo la Ofisi ya Rais, Utumishi, kuashiria uzinduzi wa jengo hilo.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akibadilishana mawazo na baadhi ya mawaziri walioshiriki katika uzinduzi wa Mji wa Serikali.


Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akiteta jambo na Waziri wa Katiba na Sheria, Mheshimiwa Dkt. Augustine Mahiga, wakati wa hafla ya uzinduzi wa Mji wa Serikali.

Waziri wa Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi,akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Mtera, Mheshimiwa Livingstone Lusinde, kulia kwa waziri ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Kasidi Faraji Mnyepe.


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, akibadilishana mawazo na Mwanasheria wa Serikali, Prof. Adelaus Kilangi.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.