Monday, April 15, 2019

Wizara ya Mambo ya Nje yafanya kikao cha kwanza cha Menejimenti katika Mji wa Serikali Mtumba

Leo tarehe 15 Aprili, 2019, Wizara  ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imefanya kikao cha kwanza cha Menejimenti katika Mji wa Serikali uliopo Mtumba jijini Dodoma uliosimikwa rasmi na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 13 Aprili 2019. Pichani: Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Kasidi Faraji Mnyepe, akiongoza kikao hicho.
Baadhi ya wakuu wa Idara na Vitengo wakiwa katika kikao hicho.

Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bibi Caroline Chipeta, akifuatilia kikao hicho.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika  Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashiriki, Bibi Agnes Kayola, akifuatilia kikao hicho.
Mhasibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Paul Kabale akifuatilia kikao hicho.
Kikao kikiendelea
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Kasidi Faraji Mnyepe (wa tano kutoka kushoto) akiwa katika picha ya pamoja Wakuu wa Idara na Vitengo vya Wizara mara baada ya kumaliza kikao chao cha kwanza cha Menejimenti kilichofanyika kwenye Mji wa Serikali uliopo Mtumba jijini Dodoma.
Kaimu Mkurugenzi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Deus Kaganda kwa pamoja na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bibi Mona Mahecha na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bw. Caesar Waitara wakibadilishana mawazo mara baada ya kikao.
Balozi Mteule, Dkt. Mpoki Ulisubisya kwa pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Siasa, Ulinzi na Usalama, Bw. Stephen Mbundi na Mkurugenzi wa Idara ya Miundombinu ya Kiuchumi na Huduma za Jamii, Bw. Eliabi Chodota wakibadilishana mawazo mara baada ya kikao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.