Friday, April 12, 2019

Prof. Kabudi afungua rasmi Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma. Ufunguzi wa ofisi hizo umefanyika tarehe 12 Aprili 2019 na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwemo Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Joseph Kakunda, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri anayeshughulikia uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki, Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, Mhe. Mussa Azan Zungu, Mzee Job Lusinde na Meya wa Jiji la Dodoma, Mhe. Prof. Davis Mwamfupe. Katika hotuba yake, Mhe. Prof. Kabudi ameupongeza Ubalozi wa China hapa nchini kwa uamuzi wa kufungua ofisi hizo na kuwataka wakazi wa Dodoma na wananchi kwa ujumla kuzitumia ofisi hizo kwa ajili ya kujiimarisha kibiashara na uwekezaji.
Sehemu ya viongozi waliohudhuria ufunguzi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi (hayupo pichani) alipohutubia hafla hiyo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi akitoa hotuba yake

Sehemu ya wageni waalikwa nao wakifuatilia hotuba ya Prof. Kabudi (hayupo pichani wakati wa ufunguzi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma. Katikati ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Caesar Waitara na kushoto ni Bw. Charles Mbando, Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Sehemu ya ujumbe wa China wakifuatilia hotuba ya Mhe. Prof. Kabudi (hayupo pichani)
Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke akizungumza wakati wa ufunguzi wa Ofisi za Ubalozi huo jijini Dodoma. Mhe. Wang Ke alisema kuwa ufunguzi wa Ofisi hizo ni kuunga mkono kwa dhati mpango wa Serikali ya Tanzania wa kuhamia makao makuu ya nchi uliotangazwa na Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania
Wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Balozi wa China nchini (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa wakifuatilia hafla ya ufunguzi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma
Hafla ikiendelea
Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia hotuba ya Balozi Wang Ke (hayupo pichani)
Aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini China kuanzia mwaka 1975 hadi 1984  Balozi Mstaafu, Mzee Job Lusinde akizungumza machache kuhusu ushirikiano kati ya Tanzania na China wakati wa hafla ya ufunguzi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma
Mhe. Mussa Azan Zungu, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ambaye alimwakilisha Spika wa Bunge kwenye hafla hiyo naye akipongeza uamuzi wa China wa kufungua ofisi za Ubalozi jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Prof. Palamagamba John Kabudi kwa pamoja na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke wakifunua kitambaa kuashiria ufunguzi rasmi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma
 Mhe. Prof. Kabudi na Mhe. Balozi Wang Ke pamoja na viongozi wengine wakifurahia baada ya ufunguzi rasmi wa Ofisi za Ubalozi wa China jijini Dodoma.





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.