Wednesday, April 10, 2019

Waziri Kabudi akutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akimkaribisha Balozi wa Ufaransa nchini, Mheshimiwa Frédéric Clavier alipomtembelea ofisini kwake  jijini Dodoma tarehe 10 Aprili 2019.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo baina yake na Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Frédéric Clavier. Katika mazungumzo hayo Tanzania na Ufaransa wamekubaliana kushirikiana katika kilimo cha zabibu, uzalishaji na uuzaji wa mvinyo katika nchi mbalimbali duniani na usafiri wa anga.
Mazungumzo yakiendelea.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Palamagamba John Kabudi akiagana na Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Frédéric Clavier baada ya mazungumzo baina yao.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.