Wednesday, April 10, 2019

Prof. Kabudi akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Belarus nchini


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, tarehe 9 Aprili, 2019, alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Belarus nchini Tanzania mwenye makazi yake Nairobi, Kenya, Mheshimiwa Dmitry Kuptel. Balozi Kuptel yupo nchini kwa ziara ya siku nne kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya Tanzania na Belarus.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akimuonesha  Balozi Dmitry Kuptel ulipo mkoa wa Dodoma  wakati alipokuwa akimuelezea Balozi huyo kuhusu uamuzi wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuhamia Dodoma.

Ujumbe wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashiriki ambao unaohusisha Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Bw. Emmanuel Buhohela (wa kwanza kulia),  Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria, Bibi Caroline Chipeta (kushoto kwa Waziri) na Afisa Mambo ya Nje, Bw. Mohamed Kamal (katikati)  wakimsikiliza Mhe. Waziri Kabudi wakati wa  mazungumzo yake na  Balozi wa Belarus (hayupo pichani)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Prof. Palamagamba John Kabudi, akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe  wa Tanzania na Belarus ulioshiriki katika mazungumzo hayo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.