Saturday, October 30, 2021

WAZIRI MULAMULA ASHIRIKI MAADHIMISHO UHURU WA TAIFA LA UTURUKI NA INDIA.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) ameshiriki hafla ya maadhimisho ya miaka 70 ya Uhuru wa India na miaka 98 ya Uhuru wa Uturuki. Hafla hizo zilizoandaliwa na Ofisi za Ubalozi wa Mataifa hayo hapa nchini zimefanyika kwa nyakati tofauti jijini Dar es Salaam.   

Waziri Mulamula kwa nyakati tofauti akizungumza katika maadhimisho hayo amesifu mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Mataifa hayo na Tanzania na ushirikiano katika maeneo mbalimbali ikiwemo sekta ya elimu, Afya, Kilimo, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, utalii, biashara na uwekezaji. Vilevile alielezea dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi mahiri wa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jumhuri ya Muungano wa Tanzania wa kuendelea kuimarisha mahusiano mazuri yaliyopo na Mataifa hayo (India na Uturuki). 

“Tunashukuru Serikali ya India kwa msaada wa mradi wa usambazaji wa maji safi na salama katika miji 17 ya Tanzania ikiwemo katika maeneo ya jiji la Dar es Salaam na Chalinze. Vilevile kwa mradi wa upanuzi, ukarabati na uboreshaji wa huduma ya maji Zanzibar. Tanzania inaichukulia India kama moja ya washirika muhimu wa kimkakati kati ya Nchi za Asia” Alisema Waziri Mulamula

Kwa miaka mingi Vyuo Vikuu vingi vya nchini Uturuki vimetia saini Mikataba ya Makubaliano na Vyuo Vikuu vya nchini Tanzania ya kushirikiana katika kubadilishana programu, mafunzo na utafiti. Aidha, zaidi ya wanafunzi 400 wa Kitanzania wanaendelea na masomo yao nchini Uturuki katika fani mbalimbali ikiwemo udaktari, uhandisi na Sayansi. Ushirikiano huu umechangia kwa kiasi kikubwa kuendeleza mahusiano ya watu wa Mataifa haya mawili. 

Mwisho Waziri Mulamula alieleza kuwa Serikali ya Tanzania inaendelea na jitihada za kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kwa kufanya marekebisho mbalimbali ya kisera na kisheria. Ametoa wito kwa Wafanyabiashara na Wawekezaji kutoka India na Uturuki na Mataifa mengine duniani kuja kuwekeza hapa nchini.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akihutubia kwenye maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (wa pili kushoto) akifuatilia onesho ya sanaa (hayapo pichani) yaliyokuwa yakiendelea kwenye maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam.
Balozi wa Uturuki hapa nchini Mhe. Dr. Mehmet Gulluoglu akihutubia kwenye maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Uturuki hapa nchini Mhe. Dr. Mehmet Gulluoglu wakiwa na mshindi wa tiketi ya ndege ya Turkish Airlines katika bahati nasibu iliyochezeshwa kwenye maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) na Balozi wa Uturuki hapa nchini Mhe. Dr. Mehmet Gulluoglu wakiwa na mshindi wa tiketi ya ndege ya Turkish Airlines katika bahati nasibu iliyochezeshwa kwenye maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam.
Hafla ya maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam ikiendelea.
Balozi wa Comoron na Kiongozi wa Mabalozi hapa nchini Mhe. Ahamada El Badaoui Mohamed Fakih akihutubia kwenye maadhimisho ya 98 ya Uhuru wa Taifa la Uturuki yaliyofanyika kwenye Ubalozi wa Taifa hilo jijini Dar es Salaam.

BALOZI MULAMULA ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO UBALOZI WA JAMHURI YA KOREA JIJINI DAR ES SALAAM

 

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula alipowasili katika Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Korea na kulakiwa na Balozi wa Korea nchini  Mhe. Tae-ick Cho kwa ajili ya kusaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi huo jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa nchi hiyo Tae-woo ROH aliyefariki dunia tarehe 26 Oktoba 2021
                                                                                 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Jamhuri ya Korea jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa nchi hiyo Tae-woo ROH aliyefariki dunia tarehe 26 Oktoba 2021

                                                                                

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Jamhuri ya Korea jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa nchi hiyo Tae-woo ROH aliyefariki dunia tarehe 26 Oktoba 2021
                                                                                                                                                                     
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini  Mhe. Tae-ick Cho baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi huo jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa nchi hiyo Tae-woo ROH aliyefariki dunia tarehe 26 Oktoba 2021  
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Korea baada ya kusaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi huo jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa nchi hiyo Tae-woo ROH aliyefariki dunia tarehe 26 Oktoba 2021

                                                          

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini  Mhe. Tae-ick Cho baada ya mazungumzo na kusaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi huo jijini Dar es Salaam kufuatia kifo cha Rais wa zamani wa nchi hiyo Tae-woo ROH aliyefariki dunia tarehe 26 Oktoba 2021

                                                                             


 

 

TANZANIA UMOJA WA ULAYA ZAKUBALIANA KUIMARISHA UHUSIANO


 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula  na Mkurugenzi mwendeshaji wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Mhe. Balozi Rita Laranjinha wakibadilishana hati ya pamoja waliyosaini kufuaatia kumalizika kwa majadiliano ya pamoja kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2021


    

Wenyeviti wenza wa majadiliano ya pamoja kati ya  Tanzania na Umoja wa Ulaya ambao ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Mhe. Balozi Liberata Mulamula  na Mkurugenzi mwendeshaji wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Mhe. Balozi Rita Laranjinha wakizungumza kitu baada ya kubadilishana hati ya pamoja waliyosaini kufuaatia kumalizika kwa majadiliano yao  yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2021


           
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula  akionesha hati ya makubalino ya pamoja  aliyokabidhiwa na Mkurugenzi mwendeshaji wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Mhe. Balozi Rita Laranjinha huku Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt. Stagomena Tax (kulia) akishuhudia baada ya kumalizika kwa majadiliano ya pamoja kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2021


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula  na Mkurugenzi mwendeshaji wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Mhe. Balozi Rita Laranjinha wakionesha hati ya makubalino ya pamoja baada ya kumalizika kwa majadiliano ya pamoja kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2021

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula  akimkabidhi zawadi  Mkurugenzi mwendeshaji wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Mhe. Balozi Rita Laranjinha  baada ya kumalizika kwa majadiliano ya pamoja kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2021

                        

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula  na Mkurugenzi mwendeshaji wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Mhe. Balozi Rita Laranjinha  wakionesha zawadi ya picha baada ya kumalizika kwa majadiliano ya pamoja kati ya Tanzania na Umoja wa Ulaya yaliyofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 29 Oktoba 2021


Na mwandishi wetu, DSM

Tanzania, Umoja wa Ulaya na nchi wanachama wa Jumuiya hiyo zimekubaliana kuendeleza uhusiano baina yao ambao umekuwepo kwa miongo kadhaa ya urafiki, ushirikiano na kwa maslahi ya pande zote.

Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya kukamilika kwa majadiliano ya pamoja kati ya Tanzania , Umoja wa Ulaya na Nchi wanachama wa Umoja huo yaliyofanyika jijini Dar es salaam tarehe  29 Oktoba 2021.

Katika majadiliano hayo Tanzania na nchi wanachaama wa Umoja wa Ulaya wamekubaliana kuendelea kufanya kazi kwa pamoja katika kukuza demokrasia, haki za msingi na utawala wa sheria na kuunga mkono sera zinazolenga kuleta maendeleo endelevu.

Pande hizo pia zimeelezea umuhimu wa nafasi ya wanawake na vijana katika maendeleo endelevu pamoja na kuwawezesha na kujadiliania juu ya taarifa ya Tanzania ya mwaka ya haki za binadamu itakayowasilishwa katika Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa hivi karibuni.

Aidha Umoja wa Ulaya na Tanzania umekubaliana juu ya umuhimu wa maendeleo ya sekta binafsi na uwekezaji kama chachu ya ukuzaji wa uchumi na kutoa ajira kwa watu wengi na wamekubaliana kufanya kazi kwa pamoja ili kufanya mazingira ya biashara nchini yaweze kuvutia zaidi wawekezaji na kukuza biashara za nje kwa pande zote mbili. Pande hizo pia zimeelezea utayari wao wa kujadili masuala yanayoihusu Tanzania katika Mkataba wa ubia wa kibiashara kati ya Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Kuhusu kuimarisha uhusiano zaidi katika siku za usoni pande hizo zimekubaliana juu ya umuhimu wa mpango wa ujirani, maendeleo na nyenzo ya ushirikiano wa kimataifa kama nyenzo mpya za kupata ufadhili wa Jumuiya ya Ulaya na kusisitizia umuhimu wa Serikali ya Tanzania kusimamia na kutekeleza kikaamilifu miradi yote iliyo chini ya mpango huo

Pande hizo pia zimekubaliana kubadilishana taarifa juu ya mipango yao ya kisiasa na kijeshi  katika jimbo la Cabo Delgado na kujadili juu ya madhara ya kibinadamu na kujadili mipango ya maendeleo katika nchi za Maziwa Makuu na zile za Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC).

Pia wamejadiliana kuhusu janga la ugonjwa wa Covid 19 katika maeneo yao na Umoja wa Ulaya umepongeza mwelekeo mpya wa sera ya afya ya Serikali ya Tanzania hasa katika hatua inazochukua za kutoa taarifa na kuchanja raia wake. Kikao hicho pia kimeeleza kutambua mpango wa Serikali ya Tanzania kutengeneza dawa zake yenyewe ikiwa ni pamoja na chanjo yake.

Kuhusu suala la ulinzi katika ukana wa bahari pande hizo zimejadiliana aina mbalimbali za uhalifu wa majini ambazo zikiwemo uvuvi haramu na kuelezea utayari wao juu ya kuchukua hatua za pamoja katika kutatua tatizo hilo.

Wamekubaliana kukutana na kufanya majadiliano ya pamoja angalau mara moja kwa mwaka ili kujadili masuala yanayowakabili wote kwa pamoja.

Majadiliano hayo ya Pamoja yamefanyika chini ya uenyekiti wenza wa Mkurugenzi mwendeshaji  wa Umoja wa Ulaya anayeshughulikia masuala ya Afrika Balozi Rita Laranjinha na Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na kuhudhuriwa Mawaziri na Makatibu Wakuu kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Majadiliano hayo pia yamehudhuriwa na Balozi wa Umoja wa Ulaya nchini Alfredo Fanti na mabalozi kutoka nchi za Ubelgiji, Jamhuri ya Czech, Denmark, Finland, Ufaransa, Ujerumani, Ireland, Italia, Uholanzi, Poland, Hispania na Sweden.