Friday, October 1, 2021

WAZIRI MULAMULA AWAAGA MABALOZI WALIOMALIZA MUDA WA UWAKILISHI NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) kwa nyakati tofauti amewaaga Balozi wa Indonesia Mhe. Prof. Ratlan Pardede na wa Ethiopia Mhe.Yonas Yosef Sanbe ambao wamemaliza muda wao wa uwakilishi hapa nchini.

Waziri Mulamula akiongea katika hafla ya kuwaaga Mabalozi hao iliyofanyika kwa nyakati tofauti katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam, amewapongeza kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kudumisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na nchi wanazoziwakilisha (Indonesia na Ethiopia).

Akizungumza na Balozi wa Indonesia Waziri Mulamula amemuahidi Mhe.Balozi Prof. Pardede kuwa licha ya mahusiano mazuri ya Kidiplomasia yaliyopo, Tanzania itaendelea kushirikiana na Indonesia katika sekta za elimu, kilimo na tehama kwa maslahi ya Nchi zote mbili. 

“Kwa niaba ya Serikali, naishuru Indonesia kwa kuunga mkono jitihada za Serikali ya Tanzania za kuendeleza kilimo kwa kutoa fursa za masomo kwa vijana wetu, kusomea musuala mbalimbali katika Kilimo na Teknolojia, jambo ambalo litachangia kuleta mapinduzi makubwa kwenye sekta ya Kilimo hapa nchini” Waziri Mulamula. 

Kwa upande wake Balozi wa Indonesia Mhe. Prof. Pardede licha ya kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa kumpa ushirikiano wa kutosha wakati akitekeleza majukumu yake katika kipindi chote alichokuwepo hapa nchini. Vilevile ameelezea kufurahishwa kwake na mahusiano mzuri yaliyopo baina ya Indonesia na Tanzania.

Wakati huohuo Balozi wa Ethiopia hapa nchini Mhe. Sanbe amepongeza hatua mbalimbali ambazo Serikali ya Tanzania imeendelea kuzichukua katika kutekeleza diplomasia ya uchumi sambamba na kutoa msukumo wa matumizi ya lugha ya Kiswahili barani Afrika. Aidha ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuendelea kudumisha na kukuza mahusiano ya Kidiplomasia na Ethiopia.

Tanzania na Ethiopia zimeendelea kuwa na uhusiano na ushirikiano mzuri wa muda mrefu. Nchi hizi mbili zimeendelea kushirikiana katika maeneo mbalimbali ikiwemo kukuza lugha ya Kishwahili, utalii, ulinzi na usalama, na usafiri wa anga.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Indonesia hapa nchini Mhe. Prof. Ratlan Pardede yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akimsikiliza Balozi wa Indonesia Mhe. Prof. Ratlan Pardede ambaye anamaliza muda wake wa uwakilishi hapa nchini. Wa kwanza kulia ni Balozi Caesar Waitara Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia akifuatilia mazungumzo
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifafanua jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Indonesia hapa nchini Mhe. Prof. Ratlan Pardede yaliyofanyika jijini Dar es Salaam
Mazungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Ethiopia anayemaliza kipindi cha uwakilishi wake hapa nchini Mhe.Yonas Yosef yaliyofanyika jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Balozi wa Ethiopia anayemaliza kipindi cha uwakilishi wake hapa nchini Mhe. Yonas Yosef wakati wa mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza Balozi wa Ethiopia anayemaliza kipindi cha uwakilishi wake hapa nchini Mhe.Yonas. Wa kwanza kulia ni Balozi Naimi Azizi Mkurugenzi wa Idara ya Afrika akifuatilia mazungumzo
Mazungumzo yakiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula na Balozi wa Indonesia Mhe. Prof. Ratlan Pardede wakiwa katika mazungumzo. 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.