Friday, November 30, 2018

Dkt. kigwangalla na Dkt. Ndumbaro wafanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) akitoa neno la ufunguzi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Maiasili na Utalii, Mhe. Dkt. Khamis Kigwangalla kuongea na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo. Viongozi hao walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari kuelezea mikakati inayochukuliw na Serikali ya awamu ya tano ya kuvutia utalii nchini. Mikakati hiyo imeanza kuzaa matunda ambapo wnanchi wa Urusi wameichagua Tanzania kuwa eneo bora zaidi kwa utalii duniani na kutoa Tuzo maalum kwa serikali. Aidha, Mikakati iliyofanywa nchini China hivi karibuni imewezesha kuingiwa kwa Mkataba wa kuleta watalii elf 10 kutoka Shangai mwaka 2019. Kushoto ni Balozi wa Urusi nchini, Mhe. Yuri popov.
Dkt. Kigwangalla akizungumza na Waandishi wa Habari hawapo pichani ambapo alitumia fursa hiyo kuwaeleza namna Watalii wanavyoongezeka kuja nchini kwa wingi.  Alisema sekta ya utalii ndiyo inayoongoza kuingizia Taifa hili fedha za kigeni ambapo kitakwimu sekta hiyo inachangia asilimia 25 ya fedha zote za kigeni. Aidha. alitoa pongezi zake za dhati kwa balozi zetu zilizopo nje ya nchi kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kuwa zimekuwa zikifanya jitihada kubwa katika kutangaza Vivutio vilivyopo nchini Tanzania  ambapo kutokana na juhudi hizo Tanzania inapokea watalii wapatao Milioni 1.3 na malengo waongezeke zaidi kila mwaka. 
Balozi wa Urusi naye akizungumza na Waandishi wa Habari
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya naAmerika Wizara ya Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Jestas Nyamanga
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga (kushoto) pamoja na Naibu Balozi wa Urusi wakiwasikiliza kwa makini Mawaziri pamoja na Balozi wa Urusi wakizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari.
Sehemu ya waandishi wa Habari wakisikiliza kwa makini Mawaziri walipokuwa wakiongea.

Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Hassan Mwamweta (wa kwanza kulia), akinukuu yaliyokuwa yakizungumzwa na Mawaziri (hawapo pichani).
Mkutano na waandishi wa habari ukiendelea




Wadau wa maendeleo wana imani na Tanzania, Dkt. Mahiga

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Wadau wa maendeleo wana imani na Tanzania, Dkt. Mahiga

Ziara zinazofanywa nchini na viongozi mbalimbali kutoka nje ya nchi ni ishara ya wazi kuwa nchi rafiki na wadau wengine wa maendeleo wana imani kubwa na Tanzania.

Hayo yalisemwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga baada ya kufanya mazungumzo na viongozi wa nchi nne kutoka Ulaya na Amerika Kusini kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere tarehe 29 Novemba 2018.

Viongozi hao ni Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup; Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura; Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen; Mjumbe kutoka China, Balozi Zhui Yuxiao, anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) na Mkurugenzi wa Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uswisi, Balozi Anne Lugou-Moulin ambaye alikutana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro.

Wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Dkt. Mahiga alieleza kuwa, licha ya Tanzania na Norway kuwa na uhusiano mzuri na imara wa kidiplomasia, kuna umuhimu wa kuongeza nguvu katika ushirikiano wa kiuchumi kwa manufaa ya nchi zote mbili. Dkt. Mahiga alitoa wito kwa Serikali ya Norway kushawishi sekta binafsi ya nchi hiyo kuchangamkia fursa lukuki za uwekezaji zinazopatikana nchini.

Alisema kuna kampuni 33 za kutoka Norway nchini Tanzania ikiwemo kampuni ya Equinor ambayo ipo katika mchakato wa kuwekeza katika gesi asilia mkoani Lindi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kusafirisha nje. “Uwekezaji huu ni mkubwa na unahitaji ardhi kubwa ambayo ishapatikana na utakapokamilika utatoa ajira za maelfu kwa vijana wa Kitanzania”. Balozi Mahiga alisema.

Balozi Mahiga aliishukuru Norway kwa misaada ya kimaendeleo inayoipatia Tanzania ikiwemo ya kusaidia kufanya mabadiliko ya kimfumo katika masuala ya ukusanyaji kodi, miundombinu, nishati ya umeme na mbolea.
Aidha, Norway inafadhili mafunzo ya vitendo kwa wahandisi wa kike ili waweze kuwa na sifa ya kusajiliwa na Bodi ya Usajili ya Wahandisi. Kutokana na ufadhili huo ambao kwa miaka minane iliyopita umegharimu Shilingi bilioni 4.2 na kuwezesha wahandisi wa kike 504 kusajiliwa na kupunguza pengo kubwa la uwiano la wahandisi wa kike na kiume ambapo uwiano wao kabla ya ufadhili huo ulikuwa ni 1:27 na sasa ni 1:10.

Waziri huyo kutoka Norway alimdokeza Dkt. Mahiga kuwa Mfalme wa Norway ana panga kufanya ziara nchini Tanzania mwaka 2019.

Wakati wa mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela, wawili hao walisisitiza umuhimu wa Tanzania na Venezuela kubadilishana uzoefu katika sekta ya mafuta na gesi ambapo Venezuela imepiga hatua na sekta ya madini ambapo Venezuela ingependa kujifunza zaidi kutoka Tanzania. Ili kurahisisha utekelezaji wa mazaungumzo yao, Mhe. Naibu Waziri amewasilisha barua rasmi ya maombi ya nchi yake ya kufungua ofisi ya ubalozi nchini jambo ambalo Balozi Mahiga aliahidi litafanyiwa kazi haraka iwezekanavyo.

Katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Dernmark, Waziri Mahiga alijulisha kuwa Kiongozi huyo alitaka kupata ufafanuzi wa hali ya mambo yanavyoendelea nchini badala ya kutegemea taarifa za vyombo vya habari ambazo wakati mwingine zinakuwa sio sahihi. 

Baada ya ufafanuzi ambao ulimridhisha na hivyo kuihakikishia Serikali ya Tanzania kuwa Denmark haijasitisha misaada kwa Tanzania. Ilielezwa kuwa misaada ambayo inakwenda moja kwa moja katika sekta ambayo ina thamani ya Dola za Marekani milioni 550 inaendelea kutolewa. Msaada unaokwenda kwenye bajeti ya Serikali moja kwa moja wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 10 ambao mchakato wake umekamilika,  lakini kwa kawaida huwa unatolewa kwa pamoja na wadau wengine (Umoja wa Ulaya na Sweden) wanasubiriwa wakamilishe michakato yao ya ndani ili uweze kutolewa. Msaada huo kwa upande wa Sweden ni Dola milioni 9 na Umoja wa Ulaya ni Dola milioni 37.

Kuhusu mazungumzo na Balozi Zhui Yuxiao ambayo yalihusu mikakati ya utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa FOCAC uliofanyika Beijing mwei Agosti 2018. Balozi Zhui alishauri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki iteue mtumishi mmoja mwandamizi ili awe mratibu wa masuala ya FOCAC pamoja na kuteua kamati ya utekelezaji yenye wajumbe wa sekta mbali mbali lakini iratibiwe na Wizara ya Mambo ya Nje.

Kwa upande wa mazungumzo kati ya Dkt. Ndumbaro na Katibu Mkuu wa Kusini mwa Jangwa la Sahara kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Uswisi, Balozi Anne Lugou-Moulin, wawili hao waliridhika na uhusiano mzuri uliopo kati ya nchi zao ambao umedumu kwa miaka 98 tokea mwaka 1920.
Dkt. Ndumbaro alihimiza wawekezaji wengi zaidi kutoka Uswisi waje nchini kuwekeza kwa kuwa mazingira ya biashara yameboreshwa kwa kiasi kikubwa. Alisema hakuna mabadiliko ya sheria za uwekezaji isipokuwa mabadiliko ambayo yamelenga kuboresha zaidi yamefanyika katika sheria ya madini. Hivyo, aliwataka wawekezaji wasiwe na hofu yeyote kuhusu Tanzania.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar Es Salaam, Tanzania
Tarehe 30 Novemba 2018


Thursday, November 29, 2018

Dkt. Mahiga akutana na Viongozi kutoka Norway, Denmark, Venezuela na China

Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kushoto ukiwa katika mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam leo. Viongozi hao walijadili namna ya kukuza na kuimarisha ushirikiano hususan wa kibiashara ikiwemo mchakato wa kampuni ya Equinor wa kuzalisha gesi kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na kusafirisha nje ya nchi.
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup wa pili kutoka kulia akisisitiza jambo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kushoto akiongea wakati wa mkutano wake na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup. Wengine katika picha kutoka kulia ni Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga na Afisa Dawati, Bi. Tunsume Mwangolombe


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na mgeni wake, Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup baada ya kufanya mazunguzmo ambayo yalikuwa ya mafanikio makubwa katika mustakabali wa Tanzania na Norway.


Picha ya pamoja.

Mazungumzo na Mhe. Zhui Yuxiao, Balozi anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano wa China na Afrika (FOCAC)



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga amekutana na Balozi Zhui Yuxiao, Mwakilishi kutoka China anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC). Wawili hao walijadili utekelezaji wa maazimio ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa FOCAC uliofanyika Beijing mwezi Agosti 2018.  Wamekubaliana kuundwa kwa kamati ya utekelezaji ambayo itaratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ambapo Wizara imetakiwa pia kuteua mtumishi mmoja mwandamizi awe mratibu wa masuala ya FOCAC.
Balozi Zhui Yuxiao, Mwakilishi kutoka China anayesimamia masuala ya Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC) akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga. Mwingine ni Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Wang Ke.
Picha ya pamoja.

Mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga katikati akiwa katika mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura hayupo pichani. Wengine ni Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi na Afisa Dawati, Bi. Lillian Kimaro.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura katikati akiwa katika mazungumzo na mwenyeji wake, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga. Mhe. Naibu Waziri pamoja na mambo mengine ameleta ujumbe kuwa Venezuela inataka kufungua ofisi ya ubalozi nchini jambo ambalo Mhe. Mahiga amelikaribisha kwa mikono miwili na kueleza kuwa endapo Venezuela itafungua ubalozi itakuwa nchi ya nne kutoka Latin Amerika kuwa na ofisi ya Ubalozi Tanzania.
Ujumbe wa Venezuela wa kuomba kufungua ubalozi nchini.
Picha ya pamoja 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na mgeni wake, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela anayeshughulikia masuala ya Afrika, Mhe. Yuri Pimentel Moura
Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga wa pili kutoka kushoto ukiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen. Katibu Mkuu alikuja kupata ufafanuzi kuhusu masuala ya haki za binadamu na kuihakikishia Tanzania kuwa haijasitisha msaada wake kwa Tanzania.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiongea wakati wa mkutano wake na Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen. Wengine katika picha kutoka kulia ni Katibu wa Mhe. Waziri, Bw. Magabilo Murobi na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga.
Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen wa kwanza kulia akisisitiza jambo wakati wa mazungumzo yake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akiagana na mgeni wake, Katibu Mkuu anayesimamia Maendeleo na Ushirikiano kwenye Wizara ya Mambo ya Nje ya Denmark, Bi. Trine Rask Thygesen 
Mkutano na Waandishi wa Habari

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga baada ya kumaliza mazungumzo na wageni wake aliongea na waandishi wa habari ili kupitia kwao wananchi waweze kujua masuala yaliyojadiliwa kwa ajili ya manufaa ya nchi yao.
Baadhi ya wanahabari waliohudhuria mkutano na Mhe. Waziri.
Sehemu nyingine ya wanahabari.
Mkutano unaendelea

Wednesday, November 28, 2018

Matukio mbalimbali ya ziara ya Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, Bw. Jestas Nyamanga (kushoto) akizungumza na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ziara ya kikazi ya siku nne. 
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup amekutana na Kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (kulia) katika ofisi za Wizara hiyo leo. Mazungumzo yao yalihusu kukuza na kuimarisha ushirikiano hususan katika programu za kuboresha mifumo ya ukusanyaji fomu kodi Tanzania.
Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup  katikati akiendelea na mazungumzo na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji hayupo pichani. kushoto ni Balozi wa Norway nchini Tanzania, Mhe. Elisabeth Jacobsen
Watumishi walioshiriki mazungumzo hayo, kushoto ni Bi. Tunsume Mwangolombe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisikiliza kwa makini hoja zilizokuwa zinajadiliwa katika mazungumzo hayo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga.

Ziara katika Shirika la Reli Tanzania

Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup akiwa katika Shirika la Reli Tanzania. Mhe. Waziri alienda katika Shirika hilo kutembelea wahandisi wa kike wanaofadhiliwa na Serikali ya Norway. Katika programu hiyo Serikali ya Norway ishafadhili wahandisi wa kike 506 kwa gharama ya zaidi ya Dola za Marekani milioni 4.2 kwa kipindi cha miaka 8. Ufadhili huo umepunguza uwiano wa wahindisi wa kiume na wakike kutoka 1:27 kabla ya programu kuanza na kufikia 1:10 kwa sasa. 

Wahandisi wa kike ambao wapo katika mafunzo ya vitendo wakitoa maelezo ya shughuli wanazofanya katika Shirika la Reli Tanzania.



Ziara katika Viwanja vya Gymkhanas

Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Norway, Mhe. Nikolai Astrup akipiga mpira akiwa katika viwanja vya Gymkhanas. Mhe. Waziri alienda katika viwanja hivyo kujumuika na kuongea na watoto wa kike walioshindwa kumaliza masomo kwa sababu mbalimbali na kwa sasa Serikali ya Norway inatoa msaada wa fedha kwa ajili ya kuwafundisha watoto hao stadi za maisha. 

Baadhi ya watoto waliopo katika programu inayofadhiliwa na Norway ya kuwapatia stadi za maisha ijulikanayo Bonga Programu inayoendeshwa na Mfuko wa OCODE.






Tuesday, November 27, 2018

Dkt. Ndumbaro atembelea Chuo cha Diplomasia

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (kulia) akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Archiula mara baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika chuo hicho. Mhe. Naibu Waziri aliweza kutembelea maeneo mbalimbali ya chuoni hapo pamoja na kufanya mkutano na Uongozi wa chuo na Wakufunzi. Katika mkutano huo, uongozi wa chuo pamoja na Wakufunzi walitumia fursa hiyo kumwelezea Dkt. Ndumbaro changamoto wanazokabiliana nazo chuoni hapo ikiwa ni pamoja na ufinyu wa majengo kulingana na mahitaji ya chuo na uchache na uchakavu wa miundombinu ya kufundishia.
Aidha, Mhe. Naibu Waziri alitumia ziara hiyo kujua mikakati mbalimbali waliyojiwekea chuoni hapo ikiwa ni pamoja na dhamira ya kujenga majengo mapya ambayo ramani ya mchoro wa majengo hayo iliwasilishwa kwa Mhe. Naibu Waziri.

Kwa Upande wa Dkt. Ndumbaro alitumia fursa hiyo kuupongeza Uongozi pamoja na Wakufunzi wa chuo cha Diplomasia kwa kufanya kazi kwa bidii pamoja na changamoto wanazokumbana nazo. Aidha, alitoa rai kwa Uongozi wa Chuo pamoja na Wakufunzi wawe wabunifu zaidi. 
Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Archiula akimwelezea jambo Dkt. Ndumbaro huku Naibu Mkurugenzi wa Masomo Prof. Kitojo Wetengere akisikiliza kwa makini.
Balozi Charles Sanga akisalimiana na Dkt. Ndumbaro
Dkt. Ndumbaro akisalimiana na mmoja wa wahasibu wa Chuo cha Diplomasia, Bw. Daniel Kaguo. 
Dkt. Ndumbaro akizungumza kwenye mkutanao na Uongozi pamoja na Wakufunzi wa Chuo cha Diplomasia hawapo pichani.
Sehemu ya watumishi wa Chuo cha Diplomasia wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri, Dkt. Ndumbaro hayupo pichani alipokuwa akizungumza nao.
Sehemu ya Wakufunzi wa Chuo cha Diplomasia, wa kwanza kulia ni Katibu wa Naibu Waziri, Bw. Charles Faini
Mkutano ukiendelea
Dkt. Ndumbaro akionyeshwa na kuelezewa ramani yenye mchoro wa majengo ya kisasa yatakayo jengwa katika eneo la Chuo cha Diplomasia kilichopo Kurasini jijini Dar es Salaam  









Dkt. Ndumbaro akutana na Mwakilishi wa Aga Khan

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbarom (kulia) akimsikiliza Mwakilishi wa Mfuko wa Aga Khan nchini, Bw. Amin Kurji walipokutana katika Ofisi ndogo ya Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Novemba 2018.

Mazungumzo kati ya Dkt. Ndumbaro na Bw. Kurji yalijikita katika kujadili masuala ya ushirikiano na shughuli za maendeleo ambazo zimekuwa Mfuko wa Aga Khan nchini katika kuhudumia wananchi hususan katika sekta ya Afya na Elimu.

Mazungumzo yakiendelea

Dkt. Ndumbaro akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Kurji 
Dkt. Ndumbaro akiagana na Bw. Kurji mara baada ya kumaliza mazungumzo.