Thursday, November 22, 2018

Mhe. Dkt. Ndumbaro awa mgeni rasmi maadhimisho ya Mshikamano na Taifa la Palestina


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) ambaye pia alikuwa mgeni rasmi kwenye maadhimisho ya Siku ya Mshikamano na Taifa la Palestina akitoa hotuba yake kwenye maadhimisho hayo ambayo yalifanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 21 Novemba, 2018.  Katika hotuba yake, Mhe. Naibu Waziri alisisitiza umuhimu wa kuendelea kushirikiana na Taifa la Palestina ili kuhakikisha taifa hilo linaondokana na hali zote za kuonewa na kugandamizwa na kuwa huru.
Sehemu ya wageni waalikwa wakifuatilia hotuba ya Mhe. Dkt. Ndumbaro (hayupo pichani).
Sehemu nyingine ya wageni waalikwa akiwemo Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Dkt. Bashiru Ali (wa pili kushoto) wakifuatilia hotuba ya Mhe. Dkt. Ndumbaro wakati wa maadhimisho ya siku ya mshikamano na Taifa la Palestina.
Wageni waalikwa wakiwemo watoto ambao ni raia wa Palestina wanaoishi nchini wakiwa kwenye maadhimisho hayo


Balozi wa Palestina nchini, Mhe. Hamdi Abu Ali akitoa hotuba yake wakati wa maadhimisho ya siku ya mshikamano na Taifa la Palestina yaliyofanyika kwenye Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam

Mhe. Naibu Waziri, Dkt. Ndumbaro kwa pamoja na Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim, Waziri Mkuu Mstaafu wakifuatilia hotuba ya Balozi Abu Ali (hayupo pichani).


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ali naye akizungumza wakati wa maadhimisho hayo

Afisa Habari kutoka Kitengo cha Habari cha Umoja wa Mataifa (UNIC) nchini, Bi. Stella Vuzo nae akitoa salamu za Ofisi hiyo kuhusu maadhimisho hayo


Mhe. Dkt. Ndumbaro akimsikiliza Mhe. Dkt. Salim alipokuwa akimweleza jambo wakati wa maadhimisho ya siku ya mshikamano na Taifa la Palestina


Mhe. Dkt. Ndumbaro akimsikiliza Mhe. Dkt. Salim. Pembeni ni Balozi wa Palestina nchini, Mhe. Hamdi Abu Ali


Viongozi wa meza kuu wakiwa wamesisima kwa heshima wakati nyimbo za Taifa la Tanzania na Palestina zikiimbwa wakati wa maadhimisho hayo

Katibu Mkuu wa CCM, Mhe. Dkt. Bashiru Ali (kulia) akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi (katikati) na mmoja wa wageni waalikwa kwenye maadhimisho ya siku ya mshikamano na Taifa la Palestina

Balozi Mwinyi akimweleza jambo  Katibu wa Naibu Waziri, Bw. Charles Faini wakati wa maadhimisho hayo

Sehemu ya Maafisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki maadhimisho hayo

Mhe. Naibu Waziri akimkabidhi zawadi Bi. Zaheeda Alishan ambaye ni mshindi wa kwanza wa shindalo la uchoraji wa picha zinazoelezea matukio mbalimbali kuhusu  Palestina

Viongozi wakiwa kwenye picha ya pamoja na Bw. Jaykesh Rathod (mwenye mfuko) ambaye ni mshindi wa pili wa  shindano la kuchora picha zinazoelezea matukio mbalimbali ya Palestina

Mhe. Dkt. Ndumbaro akizungumza na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Alvaro Rodriguez ambaye nae alishiriki maadhimisho ya siku ya mshikamano na Taifa la Palestina


Mhe. Dkt. Ndumbaro akipata maelezo ya picha kutoka kwa mshindi wa kwanza, Bi. Alishan

Mshindi wa kwanza, Bi.Alishan (kulia) akiwa pamoja na wageni waalikwa kwenye picha yake iliyompatia ushindi.

Mhe. Dkt. Ndumbaro akipata maelezo kutoka kwa mshiriki mwingine wa shindano la kuchora

Mhe. Dkt. Ndumbaro akimsikiliza mshiriki wa maonesho hayo ya picha kuhusu Palestina

Mhe. Dkt. Ndumbaro akipata maelezo kutoka kwa mshiriki mwingine
Mhe. Dkt. Ndumbaro akikaribishwa na Mhe. Balozi Hamdi mara alipowasili kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya siku ya mshikamano na Taifa la Palestina

Mhe. Dkt. Ndumbaro akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maadhimisho hayo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.