Wednesday, November 21, 2018

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Balozi wa Iran nchini


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb.) akisalimiana na Balozi wa Iran nchini, Mhe. Mousa Farhang alipofika kwenye Ofisi Ndogo za Wizara jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kumpongeza Mhe. Naibu Waziri kwa kuteuliwa kwenye wadhifa huo na kuzungumzia uhusiano kati ya Tanzania na Iran.
Mhe. Dkt. Ndumbaro akizungumza na Mhe. Balozi Farhang kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu uliopo kati ya Tanzania na Iran.
Ujumbe uliofuatana na Balozi Farhang kutoka Ubalozi wa Iran hapa nchini ukifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Dkt. Ndumbaro na Mhe. Balozi Farhang (hawapo pichani)


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Zainab Angovi (kushoto) kwa pamoja na Katibu wa Naibu Waziri, Bw. Charles Faini na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Kisa Mwaseba wakifuatilia na kunukuu mazungumzo kati ya Mhe. Dkt. Ndumbaro na Mhe. Balozi Farhang (hawapo pichani).

Mazungumzo yakiendelea

Balozi Farhang akimpatia Mhe. Dkt. Ndumbaro zawadi ya sanaa ya kutengenezwa kwa mkono kutoka Iran


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.