Wednesday, November 21, 2018

Wawekezaji kutoka Uturuki wajionea fursa za uwekezaji jijini Dodoma



Mkurugenzi wa jiji la Dodoma Bw. Godwin Kunambi akitoa taarifa ya fursa za uwekezaji zinazopatikana jijini Ddodma kwa wafanyabiashara wakubwa kutoka Uturuki ambao wameonesha dhamira ya kuwekeza katika jiji hilo. Fursa zilizoelezwa ni pamoja na ujenzi wa mahoteli yenye hadhi ya nyota tano, ujenzi wa maduka makubwa (shopping malls), masoko makubwa, shule za kimataifa na nyumba za kuishi. Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka Dodoma (DOWASA walikuwepo kuwahakikishia wawekezaji hao kuwa nishati ya umeme na maji sio tatizo jijini Dodoma. wawekezaji hao wamekuja kufuatia jitihada zinazofanywa na Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo.  


Awali Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Maduka Kessy alifungua mkutano kikao hicho kwa kuwahahakishia wawekezaji hao ushirikiano unaohitajika ili dhamira yao iweze kutimia.
Sehemu ya wawekezaji hao wakimsikiliza kwa makini Bw. Kunambi.
Wawekezaji wakimsikiliza kwa makini Bw.  Kunambi aliyekuwa akielezea maeneo mbalimbali ya uwekezaji katika jiji la dodoma.
Juu na Chini ni Sehemu ya watumishi wa Serikali na Ofisi ya Mkurugenzi wa jiji wakimsikiliza Bw. Kunambi.

Wawekezaji kutoka Uturuki walipata fursa ya kuuliza maswali mbali mbali mara baada ya kupata maelezo juu ya maeneo mbalimbali ya uwekezaji katika Mkoa wa Dodoma.


Majadiliano yakiendelea wakati wa mkutano.
Wawekezaji walipata fursa ya kutembelea kwenye maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya uwekezaji katika jiji la Dodoma.
Wawekezaji kutoka Uturuki wakipata maelezo ya ramani ya eneo la uwekezaji kutoka kwa Mchumi na Mratibu wa Maswala ya Uwekezaji katika Halmashauri ya jiji, Bw. Abel Msangi.
Hili ndio eneo la uwekezaji lililotembelewa na wawekezaji hao kutoka uturuki.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Dodoma, Bw. Maduka Kessy akiwaelezea jambo Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya, Bw. Jestas Nyamanga pamoja na Mkurugenzi wa jiji la Dodoma Bw. Godwin Kunambi
Wawekezaji kutoka Uturuki wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa Mkutano wao.













No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.