Monday, November 26, 2018

Watanzania wajengewa uwezo wa kupata ajira kwenye Umoja wa Mataifa

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Mwinyi Muombwa amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi kutoka Umoja wa Mataifa, Bi. Huda Hanina ambaye yupo nchini kwa ajili ya kutoa Semina ya kuwajengea uwezo Watanzania kuhusu mbinu za kuomba ajira kwenye Umoja wa Mataifa. Balozi Mwinyi alipongeza hatua hiyo  kwa kuwa Tanznaia licha ya kuwa ni miongoni mwa nchi zinazoongoza kuchangia vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa duniani, lakini idadi ya Watanzania waliojairiwa katika Sekretarieti ya umoja huo ni ndogo mno. 
Sehemu ya Uongozi wa Jeshi la Ulinzi wa Tanzania pamoja Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Hellen Maduhu wakifuatilia mazungumzo
Sehemu nyingine ya watumishi wa Serikali wakifuatilia kwa makini mazungumzo kati ya Balozi Mwinyi na Bi. Hanani 
Mazungumzo yakiendelea.
Balozi Mwinyi na Bi. Hanani wakiwa katika picha ya pamoja na watumishi kutoka serikalini na Umoja wa Mataifa.




Majadiliano katika Meza Duara


Bi. Hanani akielezea mambo mbalimbali kwenye Mkutano na Viongozi wa Serikali na Jeshi la Ulinzi Tanzania, kabla ya kufunguliwa kwa semina za kuwajengea uwezo Watanzania ili kuweza kuchangamkia fursa zinazotolewa na Umoja wa Mataifa.  
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalumu za SMZ - Zanzibar, Mhe. Radhia Haroub Rashid (wa kwanza kulia) akichangia jambo katika semina ya kuwajengea uwezo wa Watanzania wa kuomba nafasi za ajira kwenye Umoja wa Mataifa. 
Juu na Chini sehemu ya viongozi wa vyombo vya Ulinzi na Usalama nchini wakimsikiliza kwa makini Bi. Hanani



Mazungumzo yakiendelea.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.