Monday, November 19, 2018

Wawekezaji kutoka Uturuki wajipanga kuja kuwekeza nchini mwakani


Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo akifungua mkutano kati ya ujumbe kutoka Makampuni 7 makubwa ya Uturuki na  wadau muhimu wa masuala ya uwekezaji  jijini Dar es Salaam ambao  ni Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Chama cha Wafanyabiashara, wenye Viwanda na Wakulima (TCCIA), Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Mamlaka ya Ukanda Maalum wa Uwekezaji Tanzania (EPZA), Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Katika mkutano huo ambao ulifanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) tarehe 19 Novemba 2018, Prof. Kiondo alieleza kuwa wawekezaji hao kutoka Uturuki wana nia ya dhati ya kuwekeza hapa nchini kwa kuanzia na mikoa ya Dodoma na Simiyu katika sekta za viwanda vya nguo, uongezaji thamani bidhaa za kilimo, ujenzi wa maduka makubwa ya biashara na ujenzi wa hoteli za kimataifa.
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Ali Davutoglu nae alitumia fursa hiyo kuwahakikishia wawekezaji hao mazingira rafiki ya uwekezaji yaliyopo hapa nchini kutokana na uzoefu wake wa kuwepo nchini.
Sehemu ya ujumbe kutoka Makampuni hayo ya Uturuki wakifuatilia mkutano. Kulia ni kiongozi wa msafara wa wawekezaji hao Bw.Cengiz Ertas
Sehemu nyingine ya wawekezaji hao kutoka Uturuki


Mkutano ukiendelea

Sehemu ya wadau kutoka sekta muhimu za Tanzania nao wakifuatilia mkutano huo

Afisa kutoka TIC, Bi. Diana Ladislaus akiwasilisha mada kuhusu Uwekezaji nchini Tanzania kwa wawekezaji hao kutoka Uturuki

Wadau wakifuatilia kwa makini mada ya uwekezaji iliyokuwa ikiwasilishwa

Wadau kutoka sekta mbalimbali za Tanzania ikiwemo EPZA, TCCIA, TANESCO nao wakifuatilia mkutano

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Jestas Nyamanga (katikati) nae akiwa kwenye mkutano huo. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi wa TIC, Bw. John Mnali

Bw. Nyamanga nae akichangia jambo wakati wa mkutano huo ambapo aliwakaribisha wawekezaji hao nchini

Kiongozi wa Msafara wa Wawekezaji hao, Bw. Cengiz Ertas nae akizungumza na kueleza nia yao ya kuja kuwekeza nchini ambapo alisema kwa ujumla wametenga kiasi cha Dola za Kimarekani milioni 100 kwa ajili ya uwekezaji huo ambao wanatarajia kuuanza mwaka 2019. Pia alieleza kufurahishwa na taarifa kuhusu mazingira mazuri ya uwekezaji hapa nchini.


Mwakilishi kutoka TPSF akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kwa wawekezaji hao
Mhe. Prof. Kiondo akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya mkutano na wawekezaji hao. Kulia ni Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Davutoglu.
Bw. Nyamanga (katikati) na Bw. Mnali (kulia) wakimsikiliza Mhe. Prof. Kiondo (hayupo pichani) akizungumza na waandishi wa habari


Picha ya pamoja
Mhe. Balozi Ali Davutoglu akisalimiana na Bw. Hassani Mwamweta, Afisa Mambo ya Nje mara baada ya mkutano kati ya wadau muhimu wa uwekezaji wa hapa nchini na ujumbe wa Makampuni ya uwekezaji kutoka Uturuki


Wakati huohuo wawekezaji hao wakiongozwa na Balozi Ali Davutoglu walihudhuria maadhimisho ya miaka 30 ya TCCIA yaliyofanyika kwenye Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam

Wadau kutoka Uturuki na Tanzania kwenye maadhimisho ya miaka 30 ya TCCIA

Kina mama ambao walikuwepo kwenye maadhimisho hayo

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.