Monday, November 19, 2018

Rais Mkapa awasili Uganda kuwasilisha ripoti ya Usuluhishi ya mgogoro wa Burundi kwa Rais Museveni

Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt. Aziz Mlima (kushoto) akimsikiliza Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa ambaye ni  msuluhishi wa mgogoro wa Burundi. Rais Mkapa aliwasili katika Uwanja wa Ndege wa Entebbe asubuhi ya tarehe 19 Novemba 2018 kwa ajili ya kuwasilisha ripoti ya mkutano wa upatanishi uliofanyika hivi karibuni jijini Arusha kwa Mpatanishi Mkuu wa mgogoro huo Rais wa Uganda, Mhe. Yoweri Kaguta Museveni.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mhe. Benjamin William Mkapa ambaye ni msuluhishi wa mgogoro wa Burundi akiwa katika chumba cha wageni maalum katika uwanja wa Ndege wa Entebbe leo. kulia ni Mwambata Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Uganda, Brig Gen. Mkumbo, kushoto ni Msaidizi wa Rais Mkapa katika utatuzi wa mgogoro huo, Balozi David Kapya na anayemfuatia ni Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt. Aziz Mlima.  


Mhe. Mkapa akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mlima, Balozi Kapya na Bw. Makocha Tembele ambaye ni Katibu wa Rais Mkapa.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.