Friday, December 21, 2018

Katibu Mkuu akutana na Watumishi wa Wizara

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Faraji Kasidi Mnyepe akizungumza kwenye kikao cha kwanza na Watumishi wote wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki (hawapo pichani) tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo. Pamoja na mambo mengine, Dkt. Mnyepe aliwataka Watumishi wa Wizara kufanya kazi kwa kufuata miongozo na kutekeleza majukumu yao kwa bidii, weledi na uzalendo. Mkutano huo umefanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano uliopo kwenye Ofisi za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali uliopo jijini Dodoma tarehe 21 Desemba 2018. Wengine katika picha ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara, Balozi Ramadhan M. Mwinyi (kulia) na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi. Savera Kazaura.
Sehemu ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe (hayupo pichani)


Sehemu ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki wakimsikiliza Katibu Mkuu


Baadhi ya Wakurugenzi na Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe (hayupo pichani)
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Mwinyi akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe na Watumishi wa Wizara


Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu, Balozi Mwinyi (hayupo pichani)
Sehemu nyingine ya Watumishi wakiwa kwenye kikao kati yao na Katibu Mkuu


Baadhi ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia matukio wakati wa kikao kati yao na Katibu Mkuu
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Mnyepe akiwaonesha Watumishi wa Wizara (hawapo pichani) nyaraka ambazo ni miongozo wanayotakiwa kuifuata katika utekelezaji wa majukumu yao.
Watumishi wa Wizara kwenye kikao hicho
Watumishi wengine wa Wizara wakiwa kwenye kikao hicho
Kikao kikiendelea
Kikao kikiendelea


Watumishi wa Wizara wakifuatilia kikao kati yao na Katibu Mkuu 
Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Kikao kikiendelea
Watumishi kutoka Idara na Vitengo mbalimbali wakifuatilia kikao
Sehemu ya watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakiwa kwenye kikao na Katibu Mkuu wa Wizara (hayupo pichani)
Wakurugenzi wa Wizara wakifuatilia kikao kati ya  Katibu Mkuu na Watumishi wa Wizara

Baadhi ya Watumishi wa Wizara wakiwa kwenye kikao

Sehemu nyingine ya Watumishi wa Wizara
Watumishi wa Wizara wakifuatilia kikao
Watumishi wa Wizara wakisikiliza maelekezo 
Kaimu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu, Bi. Savera Kazaura akizungumza wakati wa kikao cha Watumishi wa Wizara na Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe (kulia)
Sehemu ya Watumishi wa Wizara wakimsikiliza Kaimu Mkurugenzi wa Utawala (hayupo pichani) 
Kikao kikiendelea huku Watumishi wa Wizara wakifuatilia kwa makini

Juu na chini ni sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki kikao kati yao na Katibu Mkuu
Katibu Mkuu, Dkt. Mnyepe akiagana na Watumishi mara baada ya kumaliza kikao

Tanzania na Uganda zakubaliana kuimarisha biashara

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda (kulia) na Waziri wa Viwanda, Biashara na Ushirika wa Uganda, Mhe. Amelia Kyabambadde wakiweka saini taarifa ya mkutano wao ambao ulikuwa unajadili namna ya kuondoa vikwazo vya biashara visivyo vya kiforodha kati ya Tanzania na Uganda. waliosimama nyuma kushuhudia uwekaji saini huo ni Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt Aziz Ponary Mlima na Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Kabonero.


Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda (kulia) na Waziri wa Viwanda, Biashara na Ushirika wa Uganda, Mhe. Amelia Kyabambadde wakibadilishana taarifa ya mkutano kati ya Tanzania na Uganda uliojadili namna ya kuimarisha biashara na kuondoa vikwazo vya kibiashara na visivyokuwa vya kiforodha uliofanyika Mutukula, Uganda tarehe 19 Desemba 2018.

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Tanzania na Uganda zakubaliana kuimarisha Biashara

Mkutano kati ya Tanzania na Uganda kujadili namna ya kuimairisha mahusiano ya kibiashara na kiuchumi ulifanyika Mutukula, Uganda kuanzia tarehe 17 hadi 19 Desemba 2018.

Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhe. Joseph Kakunda na Waziri wa Viwanda, Biashara na Ushirika wa Uganda, Mhe. Amelia Kyabambadde waliongoza ujumbe wa nchi zao katika mkutano huo.

Mkutano huo ulihitimishwa kwa Mawaziri kusaini taarifa ya makubaliano ambayo pamoja na mambo mengine, waliafikiana kuvitafutia ufumbuzi vikwazo vya kibishara na vile visivyo vya kiforodha vinavyozorotesha biashara baina ya nchi hizo mbili.

Mkutano huo ulianza kwa ngazi ya Wataalamu na Makatibu Wakuu ambapo ujumbe wa Tanzania uliongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph R. Buchwaishaija.

Aidha, Balozi wa Tanzania nchini Uganda, Mhe. Dkt Aziz Ponary Mlima na Balozi wa Uganda nchini Tanzania, Mhe. Richard Kabonero walishiriki mkutano huo.


Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Mutukula, Uganda
20 Desemba 2018

Wednesday, December 19, 2018

Ujenzi wa Ofisi ya Wizara Ihumwa, Dodoma washika kasi

Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wametembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Ofisi za Wizara hiyo kwenye Mji wa Kiserikali katika eneo la Ihumwa jijini Dodoma. Ujenzi wa Ofisi hizo zinatarajiwa kumalizika ifikapo mwezi mosi mwakani.
Mkandarasi Mkuu wa Ujenzi wa Ofisi za Wizara ya Mambo ya  Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akielezea maendeleo ya ujenzi huo kwa Wakuu wa Idara na Vitengo walitembelea eneo hilo
Juu na Chini  sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wakimsikiliza kwa makini Mkandarasi Mkuu alipokuwa akiwaelezea maendeleo ya ujenzi huo.
Juu na Chini Wakuu wa Idara na Vitengo wakijionea maendeleo ya ujenzi 









Tanzania na Morocco kuimarisha ushirikiano katika sekta ya afya

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiwa kwenye mazungumzo na Waziri wa Afya wa Morocco, Mhe. Prof. Anas Doukkali yaliyofanyika jijini New Delhi, India wakati wa Mkutano Maalum wa 4 wa Afya ya Mama na Mtoto uliofanyika jijini humo hivi karibuni. Pamoja na mambo mengine Mawaziri hao walikubaliana kuimarisha ushirikiano kwenye sekta ya afya hususan katika kutoa mafunzo kwa madaktari na wauguzi na kubadilishana ujuzi.
Mawaziri wakiendelea na mazungumzo huku wajumbe waliofuatana nao kutoka Tanzania na Morocco wakifuatilia mazungumzo hayo
Mhe. Waziri Ummy akiagana na Mhe. Prof Anas mara baada ya mazungumzo yao.
=======================================================
TANZANIA NA MOROCCO KUIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA YA AFYA

Mhe.Ummy Mwalimu  amekutana na kufanya mazungumzo na Mhe.Prof. Anas Doukkali, Waziri wa Afya wa Falme ya Morocco pembezoni mwa Mkutano Maalum wa 4 wa Afya ya Mama na Mtoto uliofanyika jijini New Delhi hivi karibuni.

Pamoja na mambo mengine, Mawaziri hao walijadili namna ya kukuza na kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Morocco hususan katika Sekta ya Afya ikiwemo uzalishaji wa dawa za binadamu, mafunzo kwa wataalam wa afya, wakiwemo Madaktari, Wauguzi hususan wa idara za wagonjwa mahututi katika Hospitali zote za Mikoa na Wilaya.

Aidha, walijadili namna ya kubadilishana ujuzi wa Wataalam wa Afya kwa ajili ya kuwaongezea ujuzi, kuimarisha huduma za afya katika kukinga magonjwa yasiyoambukiza (NCDs) na yanayoambukiza kama vile VVU/UKIMWI pamoja kuimarisha huduma za mama na motto.

Kwa upande wake, Mhe. Ummy aliiomba Serikali ya Morocco kusaidia kujenga Hospitali ya Wazazi (Maternity Hospital) jijini Dodoma ambapo Mhe. Prof. Anas amesema atapeleka ombi hilo kwa Mfalme wa Morocco, Mtukufu Mfalme Mohamed VI.

Katika kuhakikisha makubaliano hayo, yanatekelezwa mapema, wamekubaliana Wizara kuteua Mtumishi Mwandamizi mmoja awe mratibu wa masuala hayo. Pia, wamekubaliana kuwa uandaliwe Mkataba wa Ushirikiano (MoU) ili waweze kusaini makaubaliano hayo na kuanza kuyatekeleza mapema iwezekanavyo.             

Sambamba na hilo, Waziri wa Afya wa Morocco, Mhe. Prof. Anas ameahidi kuitembelea Tanzania mwishoni mwa mwezi Februari, 2019 ili kujionea utoaji wa huduma za afya nchini, ambapo ameahidi kuja na Wataalam wa Wizara yake pamoja na Wawekezaji kutoka Morocco hususan kwenye eneo la viwanda vya dawa.

-Mwisho-


Saturday, December 15, 2018

Waziri Ummy Mwalimu aiwakilisha Tanzania mkutano maalum wa mama na mtoto, India

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza kwenye Mkutano Maalum wa 4 wa Mawaziri wa Afya kuhusu Afya ya Mama na Mtoto (Partnership for Maternal, Newborn and Child Health Forum 2018) uliofanyika New Delhi, India kuanzia tarehe 12 hadi 14 Desemba, 2018. 


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akisalimiana na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi wakati wa ufunguzi wa Mkutano Maalum wa Mawaziri wa Afya uliofanyika katika jiji la New Delhi, India kuanzia tarehe 12 hadi 14 Desemba, 2018.
Picha ya pamoja ya Mawaziri wa Afya pamoja na Waziri Mkuu wa India, Mhe. Narendra Modi wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo


Picha ya pamoja ya Mhe.Waziri Ummy Mwalimu na ujumbe wa Tanzania unaoshiriki Mkutano Maalum wa Afya ya Mama na Mtoto jijini New Delhi, India. Wa pili kukia ni Mhe. Baraka Luvanda, Balozi wa Tanzania nchini India


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee naWatoto, Mhe. Ummy Mwalimu akijadiliana jambo na Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda (kushoto} wakati wa Mkutano Maalum wa 4 wa Mawaziri wa Afya kuhusu Afya ya Mama na Mtoto


Mhe. Ummy Mwalimu akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa UNFPA, Marekani, Bibi Natalia Kanem wakati wa Mkutano Maalum wa Mawaziri wa Afya kuhusu Afya ya Mama na Mtoto uliofanyika New Delhi, India
====================================================
WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO ASHIRIKI MKUTANO MAALUM WA MAWAZIRI WA AFYA KUHUSU AFYA YA MAMA NA MTOTO ULIOFANYIKA JIJINI NEW DELHI, INDIA KUANZIA TAREHE 12-14 DISEMBA, 2018.

Tanzania imeshiriki katika Mkutano Maalum unaojadili Afya ya Mama na Mtoto unaojulikana kama "4th Partnership for Maternal,Newborn and Child Health 2018" uliofanyika katika jiji la New Delhi, India kuanzia tarehe 12 hadi 14 Desemba,2018. 

Katika Mkutano huu,Tanzania imewakilishwa na Mhe.Ummy Mwalimu,Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.

Mkutano huu ulifunguliwa na Mhe.Shri Narendra Modi, Waziri Mkuu wa India tarehe 12 Desemba, 2018. Mkutano huu unawakutanisha pamoja Mawaziri wa Afya kutoka nchi mbalimbali duniani kwa lengo la kujadili changamoto zilizopo katika eneo la Afya ya Mama na Mtoto na kuweka mikakati ya pamoja ya kuzitatua changamoto hizo ili kuboresha upatikanaji wa huduma za Afya ya Mama na Mtoto.

Katika hotuba yake ya ufunguzi, Waziri Mkuu wa India alieleza mafanikio yaliyopatikana katika kupunguza vifo vya mama mjamzito na watoto wachanga kufuatia mikakati mizuri iliyowekwa na Serikali ya India na kuzitaka nchi washiriki kuweka mipango thabiti itakayotekelezeka katika kupunguza vifo vya mama na mtoto.

Kwa upande wake, Mhe.Ummy Mwalimu alieleza hatua mbalimbali zilizochukuliwa katika kupunguza vifo vya mama na motto nchini Tanzania ikiwemo kuboresha utoaji wa huduma za afya katika ngazi za chini kwa kuboresha vituo vya Afya na kuajiri watumishi wapya kwenye maeneo yenye upungufu. Pia, ameeleza hatua nyingine zinazochuliwa na serikali ni kumlinda mwanamke kutokana na unyanyasaji wa jinsia ambapo madawati ya jinsia yamezinduliwa katika majeshi ya polisi na magereza ili kuhakikisha mwanamke analindwa wakati wote. 

Kadhalika, Mhe.Ummy ameueleza mkutano huo mikatikati iliyopo nchini ya kuhakikisha uboreshaji na utoaji wa huduma za Afya ya Mama na Mtoto unakuwa endelevu, ambapo aliweka bayana mipango hiyo ni pamoja na Kuongeza bajeti ya fedha katika sekta ya Afya, kuimarisha huduma za afya ya Mama na Mtoto kuanzia ngazi ya jamii. 

Mipango mingine ni kuimarisha huduma kwa kuboresha vituo vya afya na kuajiri watumishi wanaohitajika, kutoa elimu ya uzazi wa mpango kwa walengwa pamoja na kutoa huduma stahiki ili kupunguza na kumlinda motto kutokana na maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.

Suala jingine la msingi zaidi ni kuilinda jamii kwa kutoa elimu ya kutosha kuhusu magonjwa ya saratani hususani saratani ya mlango wa kizazi ambayo sasa ni tatizo kubwa kwa akina mama duniani kote.

-Mwisho-



































Wednesday, December 12, 2018

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Viongozi kutoka nchini Cuba na Umoja wa Mataifa wanafanya ziara za kikazi nchini Tanzania zenye lengo la kuimarisha uhusiano na ushirikiano baina ya Tanzania na mamlaka hizo.

Naibu Waziri wa Kilimo wa Cuba, Mhe. Jose Miguel Rodriguez de Armas na ujumbe wake waliwasili nchini tarehe 12 Desemba 2018 na watakuwepo hadi tarehe 19 Desemba 2018.

Ziara ya Mhe. Naibu Waziri wa Cuba na ujumbe wake hailengi tu kukuza na kuimarisha ushirikiano wa kihistoria kati ya Cuba na Tanzania, bali  inalenga pia kufanya majadiliano na wadau husika, ya namna ya kuondoa changamoto zinazokikabili kiwanda cha Labiofam ili kiweze kufanya kazi kwa ufanisi.  

Wakati wa ziara hiyo, Mhe. Naibu Waziri anatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi wa juu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Wizara ya Kilimo na Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC).

Kiwanda cha Labiofam kimejengwa Kibaha mkoani Pwani kwa msaada wa Serikali ya Cuba kwa ajili ya kutengeneza viuadudu vya kuua viluwiluwi wa mbu wanaosababisha ugonjwa wa malaria.

  Kwa upande wa Umoja wa Mataifa, ujumbe wa Umoja huo ukiongozwa na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa masuala ya Misheni za Ulinzi na Amani, Bw. Jean- Pierre Lacroix na Mwakilishi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa MONUSCO utafanya ziara nchini tarehe 13 na 14 Desemba 2018.

Ziara hiyo ni sehemu ya kuadhimisha mwaka mmoja tokea shambulizi lililofanywa na waasi wa Allied Democratic Forces dhidi ya kombania ya Tanzania katika maeneo ya Simulike, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Askari 14 wa Tanzania walipoteza maisha katika shambulizi hilo.

Ujumbe huo unatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi wa Serikali na vyombo vya ulinzi na usalama akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga kuhusu kuboresha ushiriki wa Tanzania katika vikosi vya kulinda amani.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma
 12 Desemba 2018


Tuesday, December 11, 2018

Maonesho ya Jua Kali/Nguvu Kazi yamalizika kwa mafanikio kwa Tanzania


Seneta wa Kaunti ya Uasin Gishu, Mhe. Profesa Magrate Kamar akifunga Maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi jana yaliyofanyika kwa muda wa siku kumi katika Kaunti ya Uasin Gishu mjini Endoret Kenya. Kwenye hotuba yake Prof. Kamar aliwataka wajasiriamali kuongeza mawasiliano miongoni mwao ili kukuza soko la bidhaa zao ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo zimekuwa na viwango bora

 Naibu Katibu wa Wizara ya Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto wa Zanzibar,  Bi. Mau Makame Rajab akitoa neno la shukrani katika sherehe ya kufunga  maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi jana zilizofanyika katika Kaunti ya Uasin Gishu mjini Eldoret, Kenya.
Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Hassan Mnondwa akipokea cheti cha pongezi jana kwa mchango wake wa kufanikisha kufanyika kwa maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi yaliyofanyika katika kaunti ya Uasin Gishu, Eldoret nchini Kenya

Afisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi na Ajira, Bi. Sara Daudi akipokea cheti cha pongezi jana  kwa mchango wake wa kufanikisha kufanyika kwa maonesho ya 19 ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Jua Kali/Nguvu Kazi yaliyofanyika katika kaunti ya Uasin Gishu, Eldoret.