Wednesday, November 30, 2022

SERIKALI YAZINDUA MFUMO WA KIDIGITALI WA KUAINISHA FURSA ZA UWEKEZAJI






Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwasilisha hotuba ya ufunguzikwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa kidigitali unaoainisha fursa za uwekezaji zinazogusa malengo ya maendeleo endelevu 
Naibu Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Exaud Kigahe akitoa salamu za Wizara katika hafla ya uzinduzi wa mfumo wa kidigitali unaoainisha fursa za uwekezaji zinazogusa malengo ya maendeleo endelevu

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), Bi. Christine Musisi akieleza mkakati wa UNDP katika kuisaidia Tanzania kufikia malengo ya Maendeleo Endelevu


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizindua mfumo wa kidigitali unaoainisha fursa za uwekezaji zinazogusa malengo ya maendeleo endelevu 





 

Tuesday, November 29, 2022

SERIKALI, UNAIDS WAZINDUA RIPOTI YA HALI YA UKIMWI DUNIANI 2022

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya Ukimwi (UNAIDS) wamezindua Ripoti ya Ukimwi Duniani kwa Mwaka 2022 leo Jijini Dar es Salaam.

Hafla ya Uzinduzi wa ripoti hiyo imeongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe. George Simbachawene kwa niaba ya Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa 

Wakati wa uzinduzi huo Mhe. Simbachawene amesema idadi ya maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) nchini yamepungua kwa asilimia 50 kutoka 110,000 mwaka 2010 hadi 54,000 mwaka 2021. 

Waziri Simbachawene amesema pia idadi ya vifo vinavyotokana na Virusi vya Ukimwi kupungua kwa zaidi ya asilimia 50 kutoka 64,000 mwaka 2010 hadi 29,000 mwaka 2021.

“Tanzania imeongeza juhudi za kuzuia maambukizi ya VVU ambapo maambukizi mapya katika miaka minne (2017-2021) iliyopita yalipungua kwa asilimia 38,” alisema Simbachawene. 

“Kama nchi tunaungana na kukubaliana na kaulimbiu ya Siku ya UKIMWI Duniani ya mwaka 2022 ya ‘kukusekana kwa usawa ni hatari’ ili kuhakikisha kuwa kila mtu nchini Tanzania anapata huduma bora za afya na VVU. Ili kukabiliana na tofauti katika upatikanaji na utumiaji wa huduma za afya, Tanzania imeandaa muswada wa bima ya Afya kwa Wote kwa lengo la kuhakikisha Huduma ya Afya kwa Wote. Dhamira ya Mkakati wa Kitaifa wa Afya wa 2021 - 2026 ni kutoa huduma za afya endelevu zenye viwango vinavyokubalika kwa wananchi wote bila vikwazo vya kifedha, kwa kuzingatia usawa wa kijiografia na kijinsia, aliongeza Mhe. Simbachawene.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI (UNAIDS), Bi. Winnie Byanyima amesema kwa mujibu wa ripoti mpya ya UNAIDS iliyozinduliwa inabainisha kuwa hatua za haraka zinahitajika ili kukabiliana na kukosekana kwa usawa katika mapambano dhidi ya UKIMWI duniani. 

“Tunahitaji kushughulikia changamoto ya kukosekana kwa usawa kwa wanawake hasa wenye VVU. Asilimia 50 ya wanawake wanaofanyiwa ukatili wa kijinsia wanauwezekano wa kupata VVU. Katika nchi 33 duniani tangu mwaka 2015 - 2021 sawa na asilimia 41 ya wanawake walioolewa wenye umri wa miaka 15 - 24 wanaweza kufanya maamuzi yao wenyewe juu ya afya ya ngono. Njia pekee yenye ufanisi wa kukomesha unyanyasaji kwa waathirika wa UKIMWI na kufikia malengo ya maendeleo endelevu ni kuhakikisha afya, haki na ustawi wa pamoja vinapatikana kwa wakati,” alisema Bi. Byanyima

Tanzania imekuwa imefanikiwa kupunguza maambukizi na vifo vitokanavyo na ukimwi kwa asilimia 50, jitihada hizo zimeifanya Tanzania kuwa nchi ya mfano duniania katika udhibiti wa ugonjwa huu, ameongeza Bi. Byanyima 

Bi. Byanyima ameongeza viongozi wa mataifa mbalimbali dunia wanapaswa kuhakikisha usawa katika upatikanaji wa haki, huduma, sayansi bora na dawa, kwani kwa kufanya hivyo hakutasaidia tu waliotengwa bali pia kusaidia kila mmoja.

Nae mwakilishi wa Baraza la watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi Tanzania (Nacopha), Bi. Bahati Haule amesema kuna umuhimu wa jamii kupewa elimu dhidi ya masuala ya usawa na unyanyapaa kwa waathirika wa VVU kwa kuwa wengi wa walioathirika wamekuwa wakitengwa na kunyanyapaliwa katika jamii zinazowazunguka.

“Ni wakati muafaka kwa dunia na jamii zetu zinazotuzunguka kuungana pamoja katika kupinga unyanyasji dhidi ya waathirika wa VVU pamoja na kuhakikisha usawa katika haki na huduma vinapatikana, alisema Bi. Bahati 

Ripoti ya Siku ya Ukimwi Duniani 2022 inaongozwa na kauli mbiu ambayo ni kukusekana kwa usawa ni hatari.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe. George Simbachawene akizungumza wakati wa uzinduzi wa Ripoti ya Ukimwi Duniani kwa Mwaka 2022 leo Jijini Dar es Salaam. Wengine pichani ni Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel (kulia) na Mkurugenzi Mkaazi wa UNAIDS nchini Tanzania Bw. Martin Odiit 

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI (UNAIDS), Bi. Winnie Byanyima, akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Ukimwi Duniani kwa Mwaka 2022. Kulia ni Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel na kushoto ni mwakilishi wa Baraza la watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi Tanzania (Nacopha), Bi. Bahati Haule.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe. George Simbachawene akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Ripoti ya Ukimwi Duniani kwa Mwaka 2022 Jijini Dar es Salaam

Viongozi mbalimbali wakiongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Mhe. George Simbachawene pamoja naMkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI (UNAIDS), Bi. Winnie Byanyima katika  uzinduzi wa Ripoti ya Ukimwi Duniani kwa Mwaka 2022 Jijini Dar es Salaam









Monday, November 28, 2022

MKURUGENZI MTENDAJI UNAIDS AWASILI NCHINI KWA ZIARA YA KIKAZI

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI (UNAIDS), Bi. Winnie Byanyima amewasili nchini tarehe 27 Novemba , 2022. 

Mkurugenzi huyo atakuwepo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi kuanzia Tarehe 28 Novemba hadi 6 Desemba, 2022.  Mara baada ya kuwasili nchini, Bi. Byanyima alipokelewa na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel

Akiwa nchini Bi. Byanyima atashiriki Maadhimisho ya Siku ya Ukimwi Duniani yatakayofanyika Mkoani Lindi pamoja na kushiriki uzinduzi wa taarifa ya Hali ya Ukimwi nchini pamoja na kukutana na Baraza la watu wanaoishi na VVU (Nacopha). 

Aidha, Bi. Byanyima, anatarajia kukutana kwa mazungumzo na viongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baraza la Mapinduzi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI (UNAIDS), Bi. Winnie Byanyima akiwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Novemba , 2022

Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Godwin Mollel akiongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la UKIMWI (UNAIDS), Bi. Winnie Byanyima baada ya kuwasili nchini kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 27 Novemba , 2022





Saturday, November 26, 2022

DKT. TAX AWAASA VIJANA KUIGA FALSAFA ZA UONGOZI WA NYERERE

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax amewaasa vijana kutumia vyema Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation kujifunza, kubadilishana mawazo juu ya falsafa za Mwalimu Nyerere pamoja na kuimarisha amani na umoja katika jamii. 

Dkt. Tax ametoa wito huo alipokuwa akifungua mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation kwa kundi la kwanza la viongozi vijana 60 kutoka nchi zaidi ya 40 Barani Afrika tarehe 25 Novemba, 2022 usiku Jijini Dar es Salaam. Pamoja na mambo mengine, Dkt. Tax aliwasisitiza vijana hao kutumia mafunzo hayo kuinufaisha jamii inayowazunguka.

“Napenda kutumia fursa hii kuwasihi vijana wa kizazi kipya cha Viongozi wa Afrika na watu wa Afrika, kufanya kazi kwa umoja, ushirikiano, na imani thabiti, kwani bila kufanya hivyo ni vigumu kuwa na mustakabali wa Afrika tunayoitaka,” alisema Dkt. Tax.

Dkt. Tax aliongeza kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya Uongozi Imara wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, imejipanga kuhakikisha vijana wanawezeshwa ili kuendeleza amani, usalama na maendeleo ya kijamii na kiuchumi. 

“Katika kuenzi mchango mkubwa wa Mwalimu Nyerere katika kukuza umoja, amani na maendeleo ya watu nchini Tanzania na Afrika kwa ujumla, Serikali inaendelea kuunga mkono mipango ya amani kwa kuchangia Misheni za ulinzi wa amani Barani Afrika na Kikanda. Leo hii Tanzania ni nchi ya 13 kwa ushiriki katika Operesheni za Ulinzi wa Amani za Umoja wa Mataifa Duniani,” aliongeza Dkt. Tax

Bara la Afrika limebarikiwa rasilimali nyingi, tuchanganye maarifa, ujuzi wa uongozi, na maliasili ilizonazo ili kupeleka bara la Afrika katika ngazi za juu zaidi. Kwa kufanya hivyo, vijana mtakuwa mmeenzi falsafa za uongozi za Mwalimu Nyerere, aliyeongoza mapambano ya kupigania uhuru, umoja, na kujenga misingi imara ya Tanzania na Afrika kwa ujumla.

Awali akizungumza kabla ya ufunguzi wa mafunzo hayo, Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Bw. Joseph Butiku alisema kuwa programu ya Mafunzo ya Uongozi kwa Vijana yanayotolewa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere ni mpango unaolenga kushirikisha viongozi vijana katika kutoa mafunzo, changamoto, kufafanua na kubadilisha mtazamo wa kizazi kipya cha Afrika kuwa viongozi wanaowajibika, wanaojitolea na wapenda amani. 

“Malengo ya taasisi yetu ni kutafiti na kueneza falsafa ya uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere, amani, umoja na maendeleo ya watu. viongozi wazuri na wenye tija wa sasa na wa siku zijazo wa bara hili,” alisema Bw. Butiku.

Mafunzo hayo yametolewa kwa vijana 60 kutoka mataifa mbalimbali ambayo ni Botswana, Burundi, Cameroon, Djibouti, Misri, Ethiopia, Gabon, Guinea, Kenya, Libya, Liberia, Namibia, Nigeria, Rwanda, Sudani, Sudani Kusini, Afrika Kusini, Tanzania, Uganda, na Zambia.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwasilisha hotuba ya ufunguzi katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwasilisha hotuba ya ufunguzi katika hafla ya ufunguzi wa mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Jijini Dar es Salaam

Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Bw. Joseph Butiku akielezea mkakati wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere wa kuwaendeleza na kuwajengea vijana viongozi uwezo 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea tuzo ya heshima kutoka kwa Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Bw. Joseph Butiku baada ya kufungua mafunzo kwa viongozi vijana. Mafunzo hayo yanayotolewa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Jijini Dar es Salaam  

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation, Bw. Joseph Butiku na baadhi ya viongozi vijana walioshiriki katika mafunzo yanayotolewa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere Foundation Jijini Dar es Salaam   



Thursday, November 24, 2022

DKT. TAX AFANYA MAZUNGUMZO NA MENEJIMENTI YA UDOM

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) ambaye pia ni Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) leo tarehe 24 Novemba 2022 amefika chuoni hapo na kufanya mazungumzo na Menejimenti.

Akiwa chuoni hapo pamoja na masuala mengine Dkt. Tax amepokea taarifa kuhusu maendeleo ya maandalizi ya shughuli mbalimbali zinazotarajiwa kufanyika chuoni hapo katika kipindi cha mwisho wa mwaka huu 2022. Taarifa hiyo ilihusisha maendeleo ya maandalizi ya Sherehe ya Mahafali ya 13 ya Chuo hicho yanayotarajiwa kufanyika tarehe 1 na 2 Disemba 2022, na kufanyika kwa Mkutano wa Wanazuoni wa Chuo hicho. 

Akizungumza muda mfupi baada ya Dkt. Tax kuwasili chuoni hapo, Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Lughano Jeremy Kusiluka ameeleza kuwa ni utaratibu wa kawaida wa utendaji wa Menejimenti kutoa taarifa kwa Mkuu wa Chuo kila mara kuhusu maendeleo ya shughuli mbalimbali zinazoendelea Chuoni hapo. 

Mhe. Waziri Dkt. Tax aliteuliwa kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan tarehe 16 Juni 2021.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na Mkuu wa Chuo cha Dodoma akisaini kitabu cha wageni alipowasili katika Chuo Kikuu cha Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Mkuu wa Chuo cha Dodoma akiwa na Manejimenti ya UDOM muda mfupi baada ya kuwasili chuoni hapo kwa mazungumzo na Menejimenti ya Chuo.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) na Mkuu wa Chuo cha Dodoma akiagana na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Lughano Jeremy Kusiluka (kushoto), Naibu Makamu wa Chuo Taaluma, Utafiti na Huduma kwa Jamii Prof. Razack Bakari Lokina (katikati) na Naibu Makamu wa Chuo Mipango, Fedha na Utawala Prof.Wineaster Anderson Saria (haonekani pichani) 

MABALOZI WARIDHISHWA NA MIPANGO YA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA

Mabalozi wa Tanzania wameahidi kufanya kazi kwa karibu na Hospitali ya Benjamin Mkapa ya jijini Dodoma ili iweze kutekeleza mpango mkakati iliyojipangia wa kutoa huduma bora za afya nchini
.
Mabalozi walitoa kauli hiyo wakati wa kikao cha pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo, Dkt. Alphonce Chandika kilichofanyika leo jijini Dar Es Salaam kujadili namna Mabalozi watakavyoweza kuvutia wadau watakaoshirikiana na hospitali hiyo kutekeleza mpango mkakati huo.

"Umeongea mengi na yote uliyoyaongea unaonekana unayaishi na umedhamiria yatokee, ni jambo jema kuwa na dira inayoonesha hospitali inapoelekea katika kuimarisha huduma za afya nchini", Mwakilishi wa Kudumu kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Geneva, Balozi Maimuna Tarishi alisema.  

Dkt. Chitanda aliwaeleza Mabalozi hao mipango ya hospitali hiyo ya kuanzisha huduma mbalimbali za kibingwa na kuimarisha zilizopo, hivyo aliwomba mabalozi kutafuta wadau kwenye maeneo yao ya uwakilishi ili washirikiane na hospitali hiyo kuimarisha huduma za afya nchini.

Baadhi ya maeneo ambayo Mkurugenzi aliomba Mabalozi washirikiane ni pamoja na huduma za matibabu ya magonjwa ya mfumo wa mkojo, saratani, moyo, upandikizaji wa figo na uboho na upasuaji wa nyonga na mishipa ya fahamu. Misaada inayohitajika ni pamoja na mafunzo ya kibingwa, ujenzi wa majengo na ununuzi wa vifaa tiba. 

Mabalozi wa Tanzania wapo nchini wakiendelea na ratiba mbalimbali baada ya kushiriki Mkutano na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan uliofanyika Zanzibar kuanzia tarehe 14 hadi 21 Novemba 2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika akiongea na Mabalozi wa Tanzania kuhusu mipango ya hospitali hiyo yenye lengo la kutoa huduma bora kwa jamii. Mwingine katika picha ni Mkurugenzi wa Mafunzo na Utafiti, Dkt. Monica Kessy.


Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Amidi wa Mabalozi, Mhe. Dkt. Asha-Rose Migiro (katikati), Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kwenye Ofisi za Umoja wa Mataifa, Genrva, Balozi Maimuna Tarishi (kushoto) na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afruka Mashariki, Bslozi Swahiba Mndeme wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika

Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania katika nchi za Ufaransa, Japan na Brazil wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika

Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania katika nchi za Urusi na Austria wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika

Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania wakiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika akiwa katika picha ya pamoja na Waheshimiwa Mabalozi wa Tanzania





Wednesday, November 23, 2022

DKT.TAX AFANYA MAZUNGUMZO NA BALOZI WA URUSI NA IRAN


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax leo tarehe 23 Novemba 2022 kwa nyakati tofauti amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini Mhe. Andrey Levonovich Avetisyan na Balozi wa Iran nchini Mhe. Hossein Alvandi Bahineh yaliyofanyika jijini Dodoma. 

Katika mazungumzo hayo mbali na kudumisha na kuendeleza uhusiano wa kidiplomasia, vilevile yalijikita katika kujadili masuala mbalimbali yenye maslahi mapana kwa pande zote mbili na kimataifa ikiwemo biashara na uwekezaji, utalii, amani na usalama na kuendeleza sekta ya uvuvi na kilimo nchini. 

Dkt. Tax akizungumza na Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini Mhe. Andrey Levonovich Avetisyan ameeleza kuwa licha uhusiano wa muda mrefu wa kidiplomasia uliopo kati ya mataifa haya mawili, Urusi imeendelea kuwa mshirika muhimu wa maendeleo ya sekta mbalimbali nchini. Hivyo serikali itaendelea kudumisha na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo na kuangalia maeno mapya ya ushirikiano kwa manufaa ya pande zote mbili.

Kwa upande wake Balozi Avetisyan ameeleza kuwa Urusi itaendelea kushirikiana na Tanzania ikiwemo kuongeza msukumo katika masuala ya uwekezaji, biashara, na utalii. Vilevile aliongeza kusema kuwa katika siku za usoni Urusi inatarajia kuongeza kiwango cha ufadhili wa masomo kwa vijana wa Tanzania kwenda kusoma nchini humo. 

Sambamba na hayo, Balozi Avetisyan alisisitiza utayari wa Urusi kushirikiana na Tanzania katika masuala ya utamadumi ikiwemo kuendeleza lugha ya Kiswahili nchini humo. Amebanisha juhudi mbalimbali zinazofanywa na Urusi katika kuendeleza lugha hiyo nchini humo, ambapo ameeleza kuwa hadi sasa kuna takriban Vyuo Vikuu vitano vinavyofundisha Kishwahili nchini humo. 

Kwa upande wake Balozi wa Irani nchini Mhe. Hossein Alvandi Bahineh akizungumza na Waziri Dkt. Tax ameeleza kuwa Iran inaingalia Tanzania kama mbia muhimu wa uwekezaji katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku akielezea nia ya Iran ya kuwekeza nchini katika sekta ya kilimo, uvuvi na uendelezaji wa makazi.

Aidha Waziri Dkt. Tax ameeleza utayari wa Serikali ya Tanzania katika kuendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji na biashara nchini. Alieleza kuwa juhudi hizo zinahusisha hatua mbalimbali zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali katika kufanya maboresho ya kanuni, sera na sheria mbalimbali kwa lengo la kuboresha mazingira ya bishara na uwekezaji nchini. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Balozi wa Shirikisho la Urusi nchini Mhe. Andrey Levonovich Avetisyan wakiwa katika mazungumzo yaliyofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akielezea jambo wakati wa mazungumzo na Balozi wa Iran nchini Mhe. Hossein Alvandi Bahineh yaliyofanyika jijini Dodoma. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimkaribisha Balozi wa Iran nchini Mhe. Hossein Alvandi Bahineh wakati wa mazungumzo yaliyofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Balozi wa Iran nchini Mhe. Hossein Alvandi Bahineh wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika jijini Dodoma.

Sunday, November 20, 2022

MABALOZI WAHIMIZWA KUBIDHAISHA KISWAHILI

 


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu akizungumzia umuhimu wa wadau wa lugha ya Kiswahili kushirikian katika kutekeleza Mkakati wa kubidhaisha lugha ya Kiswahili wakati wa mkutano wa Mabalozi wa Tanzania uliomalizika Zanzibar tarehe 20 Novemba 2022

Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Tanzania (BAKITA), Bi. Consolata Mushi akiwasilisha mada ya mkakati wa kubidhaisha lugha ya Kiswahili katika mkutano wa Mabalozi wa Tanzania uliomalizika Zanzibar tarehe 20 Novemba 2022

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu akimkabidhi tuzo maalum Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa, Mhe. Samwel Shelukindo kwa kutambua mchango wake wa kuipigania lugha ya Kiswahili kwenye medani za kimataifa na kupelekea Unesco kutangaza Julai 7 ya kila mwaka kuwa siku ya Kiswahili 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipokea vitabu vya lugha ya Kiswahili kutoka kwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu kwa ajili ya kutumiwa na Balozi za Tanzania Nje kufundishia lugha ya Kiswahili katika maeneo yao ya uwakilishi 





Saturday, November 19, 2022

RAIS SAMIA AWATAKA MABALOZI KUENDANA NA MABADILIKO YA DUNIA

 



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Mabalozi wa Tanzania Nje ya Nchi wakati wa mkutano uliofanyika Zanzibar tarehe 19 Novemba, 2022 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwatambulisha Mabalozi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wakati wa Mkutano wa mabalozi wa Tanzania Nje ya Nchi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akitoa neno la shukrani kwa niaba ya wizara wakati wa mkutano kati ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Mabalozi wa Tanzania

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akitoa neno la utangulizi  wakati wa mkutano kati ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Mabalozi 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga  ambaye pia alikuwa mshereheshaji akizungumza wakati wa mkutano wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan na Mabalozi 

Sehemu ya Mabalozi wakifuatilia mkutano kati yao na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan uliofanyika Zanzibar 19 Novemba 2022

Meza kuu ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja

Meza kuu ikiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika picha ya pamoja na uongozi wa Wizara ya mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki