Saturday, November 5, 2022

WIZARA KUSHIRIKIANA NA VYUO VIKUU KUONGEZA WIGO WA ELIMU

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imeahidi kuendelea kushirikiana na vyuo vikuu nchini ili kupanua wigo wa kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu fursa mbalimbali zinazotolewa na wahisani yakiwemo mashirika ya Kikanda, Kimataifa na nchi marafiki.

Ahadi hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga alipokutana na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo Mhe. Henry James na baadhi ya Viongozi wa Serikali za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jana katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Ubungo.

“Fursa za Masomo Nje ya Nchi na ajira zimekuwa zikitangazwa na kuratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje kwa kushirikiana na wadau wengine ili kuendelea kupanua wigo wa kutoa elimu kwa wanafunzi kuhusu fursa mbalimbali zinazotolewa na Wizara Kikanda na Kimataifa.,” Alisema Balozi Mindi

Naye Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Bw. Kheri James amepongeza jitihada zinazotekelezwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki katika kuhakikisha watanzania wanapata fursa mbalimbali za masomo na kazi Nje ya nchi kwani jambo hilo ni la kizalendo.

“Wizara ina fursa ya ziada ya kuviunganisha vyuo vikuu nchini na Vyuo Vikuu Nje ya nchi kwa ufadhili wa masomo, mahusiano kati ya vyuo vya Tanzania na vya Nje na kubadilishana wanafunzi katika taaluma mbalimbali ili kuwajengea uwezo na ufanisi katika masomo,”Alisema Bw. James.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bw. Spencer Minja na Rais wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Bw. Mark Makaranga ambapo pamoja na mambo mengine wanafunzi hao wameipongeza na kuiomba Wizara kuandaa Kongamano la wanafunzi wa Elimu ya Juu kuhusu Mtangamano wa Jumuiya ya Kikanda na Kimataifa. 

Halmashauri ya Wilaya ya Ubungo ina vyuo vitano ambavyo ni, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), Shule Kuu ya Sheria, Chuo cha Maji na Chuo cha Mtakatifu Joseph.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akieleza jambo wakati wa kikao na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Henry James na baadhi ya Viongozi wa Serikali za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jana katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Henry James akimsikiliza Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga wakati wa kikao na baadhi ya Viongozi wa Serikali za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jana katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akifafanua jambo wakati wa kikao na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Henry James na baadhi ya Viongozi wa Serikali za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) jana katika Ofisi za Mkuu wa Wilaya ya Ubungo

Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Bw. Mark Makaranga akieleza jambo wakati wa kikao

Kikao kikiendelea 

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Mhe. Henry James katika pichaa ya pamoja na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga, Rais wa Serikali ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (kulia), Bw. Spencer Minja na Rais wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji Bw. Mark Makaranga (kushoto)


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.