Saturday, April 29, 2017

Wabunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki watoa elimu ya Mtangamano kwa Wanachuo



Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki na Mwenyekiti wa Wabunge wa Watanzania katika Bunge hilo Mhe. Makongoro Nyerere (aliyesimama) akizungumza wakati wa semina ya kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya Mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliyofanyika katika Chuo cha Mipango cha Mjini Dodoma. 
Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akijibu maswali yaliyoulizwa na wajumbe waliohudhuria semina hiyo.

Meza kuu wakifuatilia semina 
Mbunge Mhe. Makongoro Nyerere (wapili kushoto) akikabidhi machapisho kwa Kaimu Mkuu wa Chuo cha Mipango Prof.Hozen Mayaya. wengine ni baadhi ya Bunge wa Bunge walioshiriki semina hiyo


Sehemu ya wanafunzi wa Chuo cha Mipango wakifuatilia semina

Wanafunzi wakifuatilia semina

Picha ya pamoja

Friday, April 28, 2017

Tanzania na Jamhuri ya Korea zaadhimisha miaka 25 ya Ushirikiano wa Kidiplomasia

Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maadhimisho ya miaka 25 ya Mahusiano ya Kidiplomasia kati ya Tanzania na Korea. Katika hotuba hiyo Tanzania iliishukuru Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kuwa marafiki wakubwa wa Tanzania na kushirikiana kwenye kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali zikiwemo kujenga miundombinu muhimu kama barabara na madaraja.
Rais wa Taasisi ya Sera ya Sayansi na Teknolojia ya Jamhuri ya Korea, Dkt. Jong Guk Song  naye akizungumza katika maadhimisho hayo,
Sehemu ya wageni waalikwa kutoka taasisi mbalimbali wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo
Sehemu nyingine ya wageni kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Korea nchini
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi Mindi Kasiga akitoa ufafanuzi wa ratiba na mpangilio wa matukio wakati wa maadhimisho hayo.
Sehemu ya Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki maadhimisho hayo.
Balozi Mteule wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea, Mhe. Matilda Masuka naye alihudhuria maadhimisho hayo
Picha ya pamoja.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Mkurugenzi wa IFAD Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Mkurugenzi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Kilimo-IFAD wa Kanda ya Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bw. Sana Jatta alipofika Wizarani tarehe 28 Aprili, 2017. Pamoja na mambo mengine walizungumzia namna ya kuendeleza miradi ya kilimo na ufugaji hapa nchini kwa ajili ya kujihakikishia usalama wa chakula na lishe bora kwa maendeleo.
Sehemu ya ujumbe kutoka Ofisi za IFAD hapa nchini alioambatana nao Bw. Jatta. Kulia ni Bw. Francisco Pichon, Mwakilishi na Mkurugenzi wa IFAD nchini akiwa na Bi. Mwatima Juma Afisa Miradi Mwandamizi wa IFAD nchini.
Bw. Jatta nae akimweleza jambo Mhe. Dkt. Susan wakati wa mazungumzo yao.


Sehemu ya ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Jestas Nyamanga, Bi. Eva Ng'itu, Afisa Mambo ya Nje na Bw. Charles Faini, Msaidizi wa Naibu Waziri.
Mhe. Dkt. Kolimba katika picha ya pamoja na wageni wake.

Thursday, April 27, 2017

Wabunge wa EALA watoa elimu ya fursa za Mtangano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Wafanyabiashara wa Dodoma

Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Adam Kimbisa akizungumza na wajumbe kwenye semina ya kutoa elimu ya mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki sambamba na kuhamasisha fursa zinazotokana na mtangamano huo kwa wafanyabiasahara wa mjini Dodoma. Semina hiyo inayohusisha wafanyabiashara na makundi mbalimbali katika jamii pamoja na mambo mengine inalenga kuongeza urari wa biashara wa Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki; semina hii itaendelea kesho Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Stephen Mbundi akifafanua jambo kwenye semina hiyo. Bw. Mbundi alitumia fursa hiyo kutolea ufafanuzi masuala mbalimbali yaliyoulizwa na wafanyabiashara na wadau wengine walioshiriki semina hiyo.

Mmoja wa wajumbe akizungumza katika semina hiyo

Semina ikiendelea

Mmoja wa wajumbe kutoka kundi la wafanyabiashara akizungumza


Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania wanaowakilisha Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kulia) akikabidhi bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mwakilishi wa wafanyabiashara mara baada ya semina

Uingereza na Tanzania kushirikiana katika uboreshaji wa huduma za jamii.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano  wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. Sarah Cooke alipomtembelea leo katika ofisi za Wizara. Katika mzungumzo yao Mhe. Kolimba alieleza nia ya Serikali ya Tanzania katika kuimarisha ushirikiano na Serikali ya Uingereza sambamba na kuzungumzia miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali yake katika kuwaletea maendeleo na kuboresha maisha ya watanzania.
 Mhe. Sarah akimweleza Mhe. Kolimba malengo ya Serikali ya Uingereza katika kuimarisha maeneo ya ushirikiano hususan katika sekta ya kilimo, elimu, afya sambamba na ujenzi wa miundombinu.

Mazungumzo yakiendelea, kulia ni maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo hayo.

Picha ya pamoja.

Tuesday, April 25, 2017

Serikali yamuondoa Mkurugenzi wa UNDP nchini


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali yamuondoa Mkurugenzi wa UNDP nchini 

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeliagiza Shirika la Umoja wa Mataifa la Programu ya Maendeleo (United Nations Development Programs – UNDP) kwa upande wa Tanzania kumuondoa nchini Mkurugenzi wa Shirika hilo Bi Awa Dabo.
Serikali ilifikia uamuzi huo kutokana na  Bi Dabo kutokuwa na maelewano mazuri na baadhi ya Watumishi wenzake na Menejimenti ya Shirika hilo, hivyo kupelekea kuzoretesha utendaji wa shirika hilo nchini na kupunguza kasi ya kuleta maendeleo kwa Watanzania endapo hatua za haraka zisingechukuliwa.
Baada ya kuthibitishiwa kuondoka nchini, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imetoa rai kwa UNDP kuwakumbusha Watumishi wake kuwa kipaumbele chao ni kufanya kazi na Serikali ili kufikia malengo yaliyoainishwa kwenye Dira ya Maendeleo ya Mwaka 2025, Mpango wa Maendeleo wa Miaka mitano na Malengo ya Maendeleo Endelevu ambayo yamefafanuliwa katika Agenda ya Mwaka 2030.  

Mwisho.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasili ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dodoma, 25 Aprili 2017.


Saturday, April 22, 2017

Naibu Waziri afanya mazungumzo na Mabalozi Wateule

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba amekutana na kufanya mazunguzo na Mabalozi Wateule wanaoenda kuiwakilisha Tanzania maeneo mbalimbali Duniani.Mazungumzo hayo yaliyofanyika ofisini kwake Makao Makuu ya Nchi mjini Dodoma, yalijikita katika kujadili namna bora ya kuiwakilisha Tanzania ughaibuni kwa kuzingatia sera ya nchi ya mambo ya nje,  kwa lengo la kuboresha mahusiano ya Kidiplomasia baina ya Tanzania na nchi hizo, na kwa kuzingatia maslahi mapana ya kiuchumi ya nchi yetu ikiwemo kutangaza shughuli za utalii zinazopatikana nchini.

Naibu Waziri Mhe. Dkt. Susan Kolimba akisisitiza jambo

Balozi Mteule Baraka H. Luvanda akichangia jambo wakati wa mazungumzo.

Punde baada ya mazungumzo na Mhe. Naibu Waziri, Mabalozi walikutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 

Katibu Mkuu Wizara Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt.Aziz P Mlima akiongea na Mabalozi ofisini kwake mjini Dodoma


Mazunguzo yakiendelea

Thursday, April 20, 2017

Wizara yajidhatiti kukarabati miundombinu ya Ofisi za Balozi

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba akijibu swali la Mhe. Raisa Adallah Musa Bungeni katika kipindi cha maswali na majibu mapema leo asubuhi, amesema kuwa Wizara kwa kutumia bajeti ya maendeleo ya Serikali na vyanzo vingine vya mapato inaendelea kutekeleza mkakati wa kurekebisha na kuboresha miundombinu ya Ofisi za Balozi na makazi ya watumishi wa ubalozini katika maeneo mbalimbali yenye uwakilishi Duniani. Mkakati huu unahusisha ukarabati wa majengo yaliyopo, ujenzi wa majengo mapya, sambamba na ununuzi wa majengo mapya. Mkakati huu unaanza kutekelezwa katika mwaka wa fedha ujao 2017/2018.  

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba akijibu maswali kutoka kwa Waheshimiwa Wabunge katika  Kikao cha Bunge kwenye kipindi cha maswali na majibu 

Thursday, April 13, 2017

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Watanzania waliokuwa wanashikiliwa nchini Malawi waachiwa huru

Mahakama Kuu ya Mzuzu nchini Malawi jana tarehe 12 Aprili 2017 iliwaachia huru Watanzania wanane waliokuwa wanashikiliwa nchini humo kwa kosa la kuingia kinyume cha sheria kwenye mgodi wa urani wa Kayerekera. 

Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Mzuzu, Bw. Texious Masoamphambe alitoa hukumu ya kifungo cha mwezi mmoja kwa kosa la kuingia kinyume cha sheria kwenye mgodi wa urani wa Kayerekera (trespass) na kifungo cha miezi mitatu kwa kosa la kufanya ujasusi (reconnaissance).

Makosa hayo mawili, kifungo chake kinakwenda pamoja na kwa mujibu wa Hakimu huyo watuhumiwa tayari wameshatumikia kifungo hicho na kuamuru waachiliwe huru. Aidha, Hakimu aliamuru Wizara ya Mambo ya Ndani na Usalama wa Ndani kuhakikisha kuwa Watanzania hao wanasafirishwa na kurejeshwa makwao haraka iwezekanavyo.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Malawi, Watanzania hao wamesafirishwa leo tarehe 13 Aprili 2017, kutoka Mzuzu hadi Mpaka wa Songwe/Kasumulu kati ya Tanzania na Malawi.  

Watanzania hao ambao ni Walasa Mwasangu, 30, Binto Materinus, 32, Ashura Yasiri, 63, Christian Msoli, 38, Layinali Kumba, 47, Maliyu Mkobe, Gilbert Mahumdi, 32, na Martin Jodomusole, 25 walikuwa wamekamatwa na kushikiliwa na vyombo vya usalama vya Malawi tokea tarehe 20 Desemba 2016.
Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dar es Salaam, 13 Aprili  2017.



Balozi Asha-Rose Migiro awasilisha hati za utambulisho kwa Rais Michael D. Higgins wa Ireland

 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro mapema mwezi huu aliwasilisha hati za utambulisho (letter of credence) kwa Rais wa Ireland, Mhe. Michael D. Higgins.

Akiwasilisha hati hizo katika Ikulu ya Ireland, Balozi Migiro alimfikishia Rais Higgins salamu za Mhe. Rais John Magufuli na wananchi wa Tanzania pamoja na kumuahidi kufanya kazi itakayoimarisha uhusiano wa kihistoria baina ya Serikali za Tanzania na Ireland pamoja na kuanzisha maeneo mapya ya ushirikiano kwa kuzingatia vipaumbele vya Serikali ya awamu ya tano ya kujenga uchumi wa viwanda.

Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt Asha-Rose Migiro  akimkabidhi Rais Michael D. Higgins hati ya utambulisho kutoka kwa Mhe.Rais John Pombe Magufuli. 
Mhe. Balozi Migiro akikagua gwaride rasmi lililoandaliwa na kikosi cha Jeshi la Anga la nchi hiyo.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza na Ireland, Dkt. Asha-Rose Migiro  akiagana na Rais Higgins.
Mhe. Migiro  alitumia fursa hiyo pia kukutana na kuzungumza na wanadiaspora wa Tanzania waishio katika miji mbalimbali ya Ireland ambapo waliweza kujadili masuala mbalimbali kwa ajili ya ujenzi na maendeleo ya Taifa, hususan masuala ya uwekezaji na kutumia nafasi walizopata kuwa mabalozi wazuri katika kutangaza fursa zilizopo nchini sambamba na kudumisha utumaduni wetu.Pia Balozi Migiro aliwasihi wanadiaspora kushikamana, kuwa wamoja na kuunda Jumuiya ya Watanzania waishio Ireland akiwakumbusha kauli ya wahenga isimayo kuwa 'Umoja ni nguvu, utengano ni udhaifu'.