Wednesday, April 5, 2017

Rais Magufuli awaapisha Mabalozi wa Tanzania nchini India na Afrika Kusini.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Sylivester M. Ambokile. Hafla za uapisho huo zimefanyika leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Mhe. Ambokile.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka H. Luvanda . Hafla za uapisho huo zimefanyika leo Ikulu jijini Dar es Salaam.
Rais Magufuli akimkabidhi vitendea kazi Mhe. Luvanda
Sehemu ya viongozi waandamizi wa Serikali na wageni waalikwa waliohudhuria  hafla za uapisho wakiwapongeza viongozi wateule mara baada ya kuapishwa.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufili (mstari wa mbele katikati), Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan (wa pili kushoto), Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi (wa pili kulia) wakiwa katika picha ya pamoja na waheshimiwa Mabalozi walioapishwa na uongozi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.