Friday, April 28, 2017

Tanzania na Jamhuri ya Korea zaadhimisha miaka 25 ya Ushirikiano wa Kidiplomasia

Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwenye maadhimisho ya miaka 25 ya Mahusiano ya Kidiplomasia kati ya Tanzania na Korea. Katika hotuba hiyo Tanzania iliishukuru Jamhuri ya Korea kwa kuendelea kuwa marafiki wakubwa wa Tanzania na kushirikiana kwenye kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali zikiwemo kujenga miundombinu muhimu kama barabara na madaraja.
Rais wa Taasisi ya Sera ya Sayansi na Teknolojia ya Jamhuri ya Korea, Dkt. Jong Guk Song  naye akizungumza katika maadhimisho hayo,
Sehemu ya wageni waalikwa kutoka taasisi mbalimbali wakifuatilia kwa makini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiendelea kutolewa kwenye maadhimisho hayo
Sehemu nyingine ya wageni kutoka Ubalozi wa Jamhuri ya Korea nchini
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi Mindi Kasiga akitoa ufafanuzi wa ratiba na mpangilio wa matukio wakati wa maadhimisho hayo.
Sehemu ya Watumishi kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki walioshiriki maadhimisho hayo.
Balozi Mteule wa Tanzania nchini Jamhuri ya Korea, Mhe. Matilda Masuka naye alihudhuria maadhimisho hayo
Picha ya pamoja.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.