Thursday, April 27, 2017

Wabunge wa EALA watoa elimu ya fursa za Mtangano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa Wafanyabiashara wa Dodoma

Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki, Mhe. Adam Kimbisa akizungumza na wajumbe kwenye semina ya kutoa elimu ya mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki sambamba na kuhamasisha fursa zinazotokana na mtangamano huo kwa wafanyabiasahara wa mjini Dodoma. Semina hiyo inayohusisha wafanyabiashara na makundi mbalimbali katika jamii pamoja na mambo mengine inalenga kuongeza urari wa biashara wa Tanzania katika Jumuiya ya Afrika Mashariki; semina hii itaendelea kesho Mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Stephen Mbundi akifafanua jambo kwenye semina hiyo. Bw. Mbundi alitumia fursa hiyo kutolea ufafanuzi masuala mbalimbali yaliyoulizwa na wafanyabiashara na wadau wengine walioshiriki semina hiyo.

Mmoja wa wajumbe akizungumza katika semina hiyo

Semina ikiendelea

Mmoja wa wajumbe kutoka kundi la wafanyabiashara akizungumza


Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania wanaowakilisha Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Mhe. Makongoro Nyerere (kulia) akikabidhi bendera ya Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mwakilishi wa wafanyabiashara mara baada ya semina

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.