Wednesday, February 28, 2018

Waziri Mahiga akutana na Mabalozi wa Vietnam na Japan waliopo nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Vietnam nchini, Mhe. Kim Nguyen Doanh. Katika mazungumzo yao walisisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizi mbili hususan katika masuala ya biashara na uwekezaji.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Justa Nyange (kushoto) pamoja na Bw. Emmanuel Luangisa (katikati), Afisa Mambo ya Nje na Bw. Magabilo Murobi (kulia), Katibu wa Waziri wakifuatilia mazungumzo kati ya Mhe. Mahiga na Mhe. Kim Nguyen Doanh (hawapo pichani)

.....Mkutano wa Waziri Mahiga na Balozi wa Japan

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Japan nchini, Mhe. Masaharu Yoshida. Mazungumzo yao yalijikita kwenye kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali ya manufaa kwa nchi hizi mbili. 
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Celestine Mushy akifafanua jambo wakati wa mazungumzo kati ya Mhe. Mahiga na Balozi wa Japan nchini, Mhe. Yoshida (hawapo pichani). Wengine katika picha ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Justa Nyange (kushoto)  Bw. Abdallah Kirungu (katikati), Afisa Mambo ya Nje na Bw. Magabilo Murobi (kulia), Katibu wa Waziri.


Mhe. Balozi Simba afunga mafunzo kwa Maafisa wa polisi



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi, ambaye pia alikuwa mgeni rasmi, Mhe. Balozi Hassan Y. Simba akisoma hotuba ya kufunga mafunzo ya siku tatu ya Maafisa wa Polisi, Mafunzo hayo yemetolewa na chuo cha mambo ya usalama cha Naif Arab University for Security Science, hafla hiyo imefanyika tarehe 28 Februari,2018, katika Hotel ya Hyatt Regency, Dar es Salaam.
 Balozi wa Tanzania nchini Saud Arabia, Mhe. Balozi Hemed Mgaza akitoa neno la shukrani kwa niaba ya Wizara ya Mambo ya Nje katika hafla hiyo.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Balozi Hassan Y. Simba (katikati), Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia , Mhe. Balozi Hemed Mgaza (kulia), anayefuata ni Kamishna wa Operesheni na Mafunzo Jeshi la Polisi, Commandor Nsato Marijani. wa pili kutoka mwisho kushoto ni Balozi wa Saudi Arabia nchini Mhe. Balozi Mohamed Ben Mansour Al Malek wakifuatilia shughuli hiyo.
Sehemu ya wageni wakifuatilia ufunguzi huo.
    
Mmoja wa wahitimu wa mafunzo hayo Bw. Hangi Mgaka akipokea cheti katika hafla hiyo
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Ramadhani M. Mwinyi akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa Saudi Arabia nchini, Mhe. Mohamed Ben Mansour Al Malek 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Balozi Hassan Y. Simba akipokea zawadi kutoka kwa Balozi wa Saudi Arabia nchini, Mhe. Mohamed Ben Mansour Al Malek 



Picha ya pamoja

Tuesday, February 27, 2018

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana kwa mazungumzo na Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya MICT

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Olufemi Elias, Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye pia ni Msajili wa Mahakama ya Kimataifa ya Masalia ya kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (Mechanism for International Criminal Tribunals-(MICT) iliyopo Jijini Arusha. Pamoja na mambo mengine Mhe. Elias aliipongeza Serikali ya Tanzania kwa kutoa kiwanja kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama hiyo pia walizungumzia umuhimu wa Mahakama hiyo hapa nchini.
Mkutano ukiendelea.


Monday, February 26, 2018

Wizara ya Mambo ya Nje yaahidi kutekeleza Diplomasia ya Uchumi kwa vitendo

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akitoa taarifa ya ufunguzi katika kikao cha Wizara na wadau kilichofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Februari 2016.

 Lengo la kikao hicho ni kujadili maandalizi ya maonesho ya bidhaa za viwanda vya Tanzania yanayotarajia kufanyika Nairobi, Kenya kuanzia tarehe 25 hadi 28 Aprili 2018 ambayo yanatarajiwa kwenda sambamba na sherehe za Siku ya Tanzania (Tanzania day) ambayo husherehekewa tarehe 26 Aprili 2018 siku ya Muungano. Maonesho hayo ni njia mojawapo za kutekeleza Diplomasia ya Uchumi inayosisitiza katika kukuza biashara, utalii na uwekezaji.
Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Chana akizungumza. Balozi Chana alieleza kuwa Ofisi za Ubalozi zimejidhatiti kuhakikisha zinasimamia fursa zote za Watanzania hususan masuala ya biashara ili kuweza kuleta mageuzi ya kiuchumi kwa Taifa na Watanzania kwa ujumla.
Wajumbe wa meza kuu wakifuatilia taarifa ya ufunguzi kuhusiana na maonyesho iliyokuwa ikiwasilishwa na Prof. Adolf Mkenda (hayupo pichani). Kutoka kulia ni Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Bw. Juma Ali Juma, Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Pindi Chana na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo  ya Biashara (TANTRADE), Bw.  Edwin Rutageruka.
Sehemu nyingine ya Wajumbe wa meza kuu wakifuatilia taarifa ya ufunguzi. Kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Prof. Joseph Buchweishaija, Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega, Mkurugenzi Mtendaji-Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF), Bw. Godfrey Simbeye na Mwakilishi kutoka Chama cha Wafanyabiashara, Wakulima na wenye Viwanda Tanzania (TCCIA), Bw. Godfrid Muganda.
Wajumbe kutoka Serikalini na sekta binafsi wakifuatilia kikao. Waliokaa mstari wa kwanza  ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Suleiman Salehe. 
Wajumbe wakifuatilia kikao. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Mindi Kasiga na nyuma yake ni Afisa Mambo ya Nje, Bi. Bertha Makilagi.
Wajumbe wakifuatilia kikao.

Sehemu nyingine ya wajumbe wakifuatilia kikao.

Naibu Katibu Mkuu afungua mafunzo ya Maafisa wa Polisi

 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani M. Mwinyi, akifungua mafunzo ya Maafisa wa Polisi yaliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency, Dar es salaam, mafunzo hayo yanaendeshwa na Wataalam kutoka chuo cha sayansi ya masuala ya Ulinzi Cha Naif Arab University cha Saud Arabia. Mafunzo hayo ni ya siku tatu(3), yaliyoanza tarehe 26-28 Februari,2018
Naibu Katibu Mkuu Balozi Mwinyi, kushoto kwake  ni Balozi Mohamed M. Al Malek , Balozi wa Saudi Arabia Nchini, kulia kwake ni , Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Balozi Hemedi Mgaza na mwisho ni Kamishna wa Operesheni na mafunzo wa Jeshi la Polisi Commissioner Nsato M. Marijani  wakifuatilia mafunzo hayo.


Mafunzo yakiendelea
 
Sehemu ya washiriki kutoka Wizarani wakifuatilia mafunzo hayo

 Sehemu ya washiriki  na Wakufunzi wa mafunzo wakifuatilia mafunzo hayo
    Picha ya Pamoja.

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Mwakilishi wa Taasisi ya Aga Khan

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mkurugenzi wa masuala ya Diplomasia katika Taasisi ya Aga Khan, Balozi Arif Lalani.Katika mazungumzo yao walijadili kuhusu ushirikiano kati ya Serikali ya Tanzania na Taasisi hiyo katika sekta ya Elimu na Afya. Mazungumzo hayo ambayo yalihudhuriwa na Bw. Amin Kurji alieambatana na Balozi Lalani yalifanyika katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Jijini Dar es Salaam.   
Balozi Lalani akimweleza jambo Prof. Mkenda.
Mazungumzo yakiendelea.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Mkenda akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Lalani (wa tatu kushoto), Bw. Kurji (wa tatu kulia), Kaimu Mkurugenzi Kitengo cha Sheria, Bibi Caroline Chipeta (wa pili kulia), Katibu wa Katibu Mkuu, Bi. Bertha Makilagi (wa kwanza kushoto) na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Elisha Suku.

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Balozi wa Palestina

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Prof. Adolf Mkenda akisalimiana na Balozi wa Palestina hapa nchini, Mhe. Hazem Shabat alipokuja kumtembelea na kufanya nae mazungumzo katika Ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Jijini Dar es Salaam
Prof. Mkenda akimweleza jambo Balozi Shabat walipokutana na kufanya mazungumzo.
Balozi Shabat naye akifafanua jambo kwa Prof. Mkenda 
Mazungumzo yakiendelea. Kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bi. Kisa Doris Mwaiseba.




Friday, February 23, 2018

Naibu Waziri akutana na Mjumbe Maalum kutoka Poland

Naibu Waziri  wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki  Mhe. Dkt. Suzan Kolimba akiwa katika mazungumzo na Mjumbe maalum kutoka Nchi ya Poland Mhe. Krzysztof Szczerki alipomtembelea Wizarani, tarehe 22 Februari, Dar es salaam. Mazungumzo yao yalilenga zaidi jinsi ya kuboresha mahusiano kati ya Tanzania na Nchi ya Poland katika maeneo mbalimbali ya maendeleo.

  Mhe. Dkt Kolimba na Mhe. Szczerki wakiendelea na mazungumzo, wanaofuatilia   wa kwanza kushoto ni Balozi wa Poland nchini Mhe. Krzysztof Buzalski pamoja na wajumbe waliombatana nao kutoka Ubalozini na wa kwanza  kulia ni Bw. Salvatory Mbilinyi, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika  na Maafisa kutoka Wizarani.
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Mkurugenzi wa masuala ya Afrika kutoka Canada


Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi akizungumza na Mkurugenzi Mkuu anayeshughulikia masuala ya Kusini na Mashariki mwa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Canada, Bw. Marc-André Fredelte. Katika mazungumzo yao walijadili masuala ya ushirikiano katika masuala ya diplomasia, biashara na maendeleo. Bw. Fredelte yupo nchini kwa ziara ya kikazi.
Ujumbe kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ukifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mwinyi na Bw. Fredelte (hayupo pichani). Kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Bw. Salvator Mbilinyi, Bw. Mustafa M. Ussi, Afisa Mambo ya Nje na Bi. Lilian Kimaro, Afisa Mambo ya Nje
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Mwinyi akiagana na Bw. Fredelte baada ya kumaliza mazungumzo yao
Picha ya pamoja

Kaimu Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje akutana na Mbunge kutoka Uturuki

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiriano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhan M. Mwinyi akiwa katika mazungumzo na Mhe. Zehra Taskesenlioglu, Mbunge na Mwenyekiti wa Umoja wa Wabunge wa Bunge la Uturuki wanaounda Kundi la Wabunge Marafiki na Wabunge wa Bunge la Tanzania alipofika Wizarani tarehe 23 Februari, 2018. Katika mazungumzo yao walizungumzia umuhimu wa kukuza na kuimarisha mahusiano kati ya Tanzania na Uturuki katika nyanja mbalimbali ikiwemo elimu.
Balozi wa Uturuki nchini, Mhe. Ali Davutoglu (kulia) akiwa pamoja na Bw. Aytak Dincer, Mwekezaji na Mwenyekiti wa Baraza la Biashara la Tanzania na Uturuki wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mwinyi na Mhe. Zehra (hawapo pichani)
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Salvator Mbilinyi (kulia) akiwa na Bw. Hassan Mwamweta, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo
Kikao kikiendelea

Naibu Waziri Kolimba aongoza maadhimisho ya siku ya Taifa la Kuwait

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Suzan Kolimba (Mb.) akizungumza katika hafla ya kuadhimisha siku ya Taifa la Kuwait. Katika hafla hiyo Dkt.Kolimba ambaye alikuwa mgeni rasmi alitumia fursa hiyo kulipongeza taifa hilo na kuahidi kuendeleza ushirikiano  uliopo kati ya Tanzania na Kuwait.Pia alimpongeza Balozi wa Kuwait hapa nchini Mhe. Jasem Ibrahim Al Najem kwa juhudi zake za kuboresha na kukuza ushirikiano kati ya Tanzania na Kuwait hususan kwa kuchangia  sekta mbalimbali zikiwemo huduma za kijamii kama elimu na afya. Hafla  hiyo iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya Mabalozi walio hudhuria hafla hiyo wakimsikiliza kwa makini Dkt. Kolimba (hayupo pichani).
Dkt. Kolimba akiendelea kuzungumza huku wageni waalikwa wakimsikiliza.

Balozi wa Kuwait nchini Tanzania Mhe. Jasem Ibrahim Al Najem naye akizungumza wakati wa hafla hiyo.
Sehemu nyingine ya Mabalozi wakimsikiliza kwa makini Mhe. Najem akihutubia.
Dkt. Kolimba akishiriki katika zoezi la kukata keki kwenye hafla hiyo.
Dkt. Kolimba akipokea picha iliyochorwa kwa Mkono kutoka kwa Balozi Najem.
Dkt. Kolimba akisalimiana na Mhe. Dkt. Salim Ahmed Salim walipokutana kwenye hafla hiyo.
Dkt. Kolimba akisalimiana na Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Mhe. Monica Patricip Clemente Mussa. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Suzan Kolimba.