Monday, February 12, 2018

Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Uingereza nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Adolf Mkenda akisalimiana na Balozi wa Uingereza nchini Tanzania Mhe. Sarah Cooke, alipomtembelea Wizarani tarehe 12 Februari,2018, Dar es Salaam
Prof. Mkenda akizungumza na Mhe. Balozi Cooke,katika mazungumzo hayo Prof. Mkenda  alisema Mahusiano ya Uingereza na Tanzania yana historia ndefu, nchi hizi mbili zimekuwa zikishirikiana katika maeneo mbalimbali kama vile biashara, uwekezaji, utalii na elimu.

Naye Mhe. Balozi Cooke alimweleza Prof Mkenda namna yeye na Wanadiplomasia wenzake  walivyofurahishwa na maandalizi ya hafla ya mwanzo wa mwaka kwa Mabalozi (Sherry Party), vilevile Mhe. Cooke alisema Serikali yake inaunga mkono Serikali ya Tanzania kwa juhudi inazofanya ili kufikia uchumi wa viwanda, alisema Uingereza  itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo. 

Balozi Cooke naye akielezea jambo kwa Prof. Mkenda
Mazungumzo yakiendelea, wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika na Ulaya Bw. Salvatory Mbilinyi, na wa kwanza kushoto ni Naibu Balozi Ubalozi wa Uingereza Bw. Matt Sutherland 



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.